< Luhka 10 >

1 Acunkäna, Jesuh naw akce khyühkip la nghngih jah mcawn lü, a cehnak vaia mlüh la hmun avana, a maa, nghngih ci a jah tüih.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 Acunüng Jesuh naw, “Cang ah vai khawjah awmki, cunsepi atki ngcek ve; acunakyase, cang at khai a jah tüih law vaia, cangmah kthäh u lü ktaiyü ua.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 “Cit u; he hea ksunga to hea kba ka ning jah tüiki.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 “Ngui ip, kthäheinaka ngja, khawdawke ä nami jah cehei vai, lama khyang ä nami hnukset vai.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 “Nami luhnak im avana, akma säiha, ‘Hina im üng dim'yenak pha law se’ nami ti vai.
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 “Acuna im üng dim'yenak ngjahlüki a awm üng nami pyena dim'yenak acunüng ani üng awm khai, ngjahlüki am a ve üng nami hnuksetnak nami lakin be vai.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 “Acuna im üng awm laih laih u lü, ami ning jah pet nami eiawk vai; khüiki cun ngkheng khawiki ni. Im avan üng ä nami kai hü vai.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 “Nami luhnaka mlüh avan üng ami ning jah pet nami ei vai,
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 “Ami mlüha am phetki he nami jah m’yai be vai, ami veia, ‘Pamhnama khaw naw ning jah k'et law ve’ nami ti vai.
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 “Mlüh nami luhnaka am ami ning jah cäinak üng, ami lam üng cit hü u lü,
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 ‘Nami mlüh üngka mvut, kami khawpha üng kawpki pi nami khana kami khawki; cunsepi Pamhnama khaw naw ning jah k’et law ve’ nami ti vai.
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 “Ka ning jah mthehki, ngthumkhyanaka mhmüp üng, Pamhnam naw acuna mlüha kthaka Sodom mlüh m'yenei bawk khai.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 “Korazin mlüh aw, na jo se ve! Bethsaida mlüh aw, na jo se ve! Nangmi üng mdana kba müncankse he Turah la Sidon mlüha mdan vai sü ta, ajan denga jihkpyawn sui ni lü, mvut üng ngaw ni lü, ngjut päng khai sü xawi.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 “Cunsepi, ngthumkhyanaka mhmüp üng Pamhnam naw nanga kthaka ta Turah la Sidon mlüh jah m'yenei hlü bawk ve.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 “Nang Kapenawm mlüh, khankhaw däa mhlünmtaia kya lü pi, mulai mei däa ning khyaka na kya khai” a ti. (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 Jesuh naw, “Upi, nami ngthu ngaiki cun, keia ngthu ngaikia kyaki; upi nami ngthu ä ngaiki cun keia ngthu ä ngaikia kyaki ni; upi keia ngthu ä ngaiki cun kei na tüi lawkia ngthu ä ngaikia kyaki ni,” a ti.
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 Acunüng, khyühkip la nghngihe jekyainak am nghlat law be u lü, “Bawipa aw, na ngming am khawyai he kami jah ksäta kba awmki he,” ti u se,
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 Jesuh naw, “Khawyam mkeka kba khankhaw üngka naw kya law se ka hmuh.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 “Ngai u, kphyukse he, jawngk’ai hea khana ngleheinak la, ye he jah nängnaka khyaihnak ka ning jah peki, i naw am ning jah lembawisak khai.
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 “Cunsepi khawyai he nami ti tia ami awma phäha ä jekyai ua; khankhawa nami ngming he angyuka phäha jekyai ua,” a ti.
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 Acunüng, Jesuh Ngmüimkhya Ngcim üng jekyainak am be lü, “Mce la khankhaw Bawipa, ka Pa aw! khyang ktheme la ngtheingthangki hea veia hina ngthu mjih lü, ä ngtheingthangki hea veia na ngdangsaka phäha ning jekyai na veng; ka Pa aw, acun cun na ngaiha dawki ni.
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 “Ka Pa naw ahmäi na pe pängki. Capa u ni ti cun Pa dänga thea u naw am ksing; Pa u ni ti cun Capa la Capa naw a xüa khyang hea thea u naw am ksing thei u,” a ti.
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 Acunüng, Jesuh axüisaw hea veia nghlat lü, anghmüa, “Atuh hmuh vai he nami jah hmuki he nami jo sen ve;
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 “Ka ning jah mthehki, sahma khawjah la, sangpuxang khawjah naw, nami jah hmuh la nami jah ngjak he, hmu hlü u lü ngja hlü kyawki he, am hmu u lü am ngja hlawt u,” a ti.
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 Acunüng, thumksing mat naw Jesuh a mhnüteinak am, “Saja aw, anglät xünnak ka yahnak vaia i ni ka pawh kawm?” ti se, (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 Jesuh naw, “Cangcim üng i ng’yu se, ihawkba na ksingki ni?” a ti.
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 Ani naw, “Bawipa na Pamhnam cun na mlungmthin avan, na xünnak avan, na kyannak avan la, na ngaikyunak avan am na jawngnak vai, acunüng na impeiloceng namäta kba na jawngnak vai’ tia awmki,” a ti.
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 Acunüng Jesuh naw, “Msang thei veki, acunkba va pawha, na xüng khai ni,” a ti.
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 Acunüng, acuna khyang naw ngnäng khaia bü lü, Jesuh üng, “Acunüng ka impeiloceng he ta u he ni?” a ti.
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 Jesuh naw msang lü, “Khyang mat Jerusalem üngka naw Jerikhoa ju cit khai sü, khyang m'yuk’eie jah sawngei msawk se, acun he naw a suisak jah suh pe u lü, thi khyo khaia kpaiki he naw ami ceh tak.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 “Acunüng, ktaiyü mat, acuna lam bä üng citki naw, a hmuh la lam kpema ngpeng lü a ceh tak.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 “Acukba bäa, Levih khyang mat pi acuna hmun pha law lü, a hmuh la lam kpema ngpeng lü citeiki.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 “Cunsepi, Samarih khyang mat a kdungnak lama, acuna awmnak pha law hngaki naw, a hmuh la m'yenei leng leng lü,
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 a veia va cit lü, a nghma üng situi la capyitui am jah bui lü, hlawpki naw, amäta sangnghngaksaü üng taih lü, khin ima cehpüiki naw, a msümcei.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 “A ngawi üng, denarih tangka nghngih, khin im ngängki üng pe hüt lü, ‘Ana msümceia, hina thea pi na bäihnak, avan pi ka nghlat law be üng ning thung be kawng’ a ti.
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 “Acuna kthum he üng m'yuk’eie jah sawngeikia khyanga khana impei locenga kba biloki cun ua ni na ngaih?” ti se,
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 Thumksing naw, “M'yeneinak taki cen” a ti. Acunüng Jesuh naw, “Nang pi acunkba va pawha,” a ti.
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 Acunüng, Jesuh la axüisaw he ami ceh lama ngnam mat üng lut u se, acuia a ngming Matah naki naw a na khinak.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 Acuna, nghnumia hnunpüi Marih naki nghnumica mat awmki. Acuna nghnumica cun Jesuha khaw kunga ngthu ngai lü ngawki.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 Acunüng, Matah cun khüi lü am ngbüneiki, Jesuha veia law lü, “Bawipa aw, ka na naw ka mät däng ka khüi khaia ana yawkin hin na dawsaki aw? Na kpüi law khaia mtheha,” a ti.
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 Acunüng Jesuh naw, “Matah, Matah, aktäa ngaikyu lü bawngbai veki;
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 “Cunsepi, aktung mat däng awmki. Marih naw akdaw xüei ve, acun cun u naw pi yuhei hlawt vaia am kya ve,” ti lü a msang.
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< Luhka 10 >