< San Marcos 6 >

1 YA anae jumanao güije mato gui tanoña; ya y disipuluña sija madalalag güe.
Yesu aliondoka hapo akaenda katika kijiji chake, akifuatwa na wanafunzi wake.
2 Ya anae mato y sábado na jaane, jatutujon mamanagüe gui sinagoga; ya megae ni jumungog güe ninafanmanman, ya ilegñija: Mano nae guaja este taotao este sija na güinaja? Yan jafa este na tiningo y esta manae güe? ya jaftaemano este sija na ninámanman ni mafatinas ni canaeña?
Siku ya Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika sunagogi. Wengi waliomsikia walishangaa, wakasema, “Je, ameyapata wapi mambo haya? Ni hekima gani hii aliyopewa? Tena, anatendaje maajabu haya anayoyafanya?
3 Ada ti este y catpintero, lajin Maria, chelun Santiago, yan si Joses, yan si Juda, yan si Simon? Ada ti manjijita yan y mañeluña famalaoan güine? Ya maninefefende nu güiya.
Je, huyu si yule seremala mwana wa Maria, na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simoni; Je, dada zake si wanaishi papa hapa kwetu?” Basi, wakawa na mashaka naye.
4 Lao si Jesus ilegña nu sija: Taya profeta sin onraña lao y tanoñaja, yan entre y parientesña sija, ya y guimaña.
Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima isipokuwa katika nchi yake, kwa jamaa zake na nyumbani mwake.”
5 Ya ti siña jafatinas güije jafa na námanman, na japolo y canaeña gui jilo palo manmalango sija, ya janajomlo.
Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache, akawaponya.
6 Ya güiya ninámanman ni ti manmanjongguenñija; ya malilicue gui y sengsong sija mananagüe.
Alishangaa sana kwa sababu ya kutoamini kwao. Kisha Yesu alivitembelea vijiji vya pale karibu akiwafundisha watu.
7 Ya jaagang y dose sija, y jatutujon tumago dos en dos, ya janae ninasiñañija gui jilo manáplacha na espiritu sija;
Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawiliwawili. Aliwapa uwezo wa kuwatoa pepo wachafu,
8 Ya jatago sija na chañija fanmañuñule ni jafa para y chalan, na un bastoñija; ni costat, ni pan, ni salape gui betsanñija;
na kuwaamuru, “Msichukue chochote mnapokwenda isipokuwa fimbo tu. Msichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni.
9 Lao ufanchenancleta; ya munga manminagago dos na magago.
Vaeni viatu lakini msivae kanzu mbili.”
10 Ya ilegña nu sija: Manoja na guma nae manjalom jamyo; fañaga güije, asta gui manjanao jamyo güije na lugat.
Tena aliwaambia, “Popote mtakapokaribishwa nyumbani, kaeni humo mpaka mtakapoondoka mahali hapo.
11 Ya todo ayo sija y ti rumesibe jamyo, ni ti maninecungog jamyo, fanjanao güije, sacude y petbos ni gaegue gui papa adengmiyo para testimonio contra sija. Magajet jusangane jamyo, na mas sungunon na castigon Sodoma, yan Gomora gui jaanin y sentensia, qui ayo na sidua.
Mahali popote ambapo watu watakataa kuwakaribisheni au kuwasikiliza, ondokeni hapo na kuyakung'uta mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao.”
12 Ya manmapos jasetmon na y taotao sija ufanmañotsot.
Basi, wakaondoka, wakahubiri watu watubu.
13 Ya jayute juyong megae na anite sija, ya japapalae laña megae na manmalango sija, ya janafanjomlo.
Waliwafukuza pepo wengi wabaya; wakawapaka mafuta wagonjwa wengi, wakawaponya.
14 Ya jajungog y ray Herodes y faman Jesus (sa afamao y naanña), ya ilegña: Si Juan Bautista cajulo guine y manmatae sija; ya pot este mangaeninasiña na chocho, esta fumatinas nu güiya.
Basi, mfalme Herode alisikia juu ya hayo yote, maana sifa za Yesu zilienea kila mahali. Baadhi ya watu walikuwa wakisema, “Yohane Mbatizaji amefufuka kutoka wafu, ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake.”
15 Palo ilegñija: Si Elias. Y palo ilegñija: Profeta güe, pat uno gui profeta sija.
Wengine walisema, “Mtu huyu ni Eliya.” Wengine walisema, “Huyu ni nabii kama mmojawapo wa manabii wa kale.”
16 Ya anae jajungog si Herodes, ilegña: Este si Juan ni guine judegüeya: güiya cajulo guine y manmatae sija.
Lakini Herode alipopata habari hizi alisema, “Huyu ni Yohane! Nilimkata kichwa, lakini amefufuka.”
17 Sa güiyaja si Herodes manago na umamantiene si Juan, ya umapreso gui catset pot si Herodias, asaguan y cheluña as Felipe, sa jacone para asaguaña.
Hapo awali Herode mwenyewe alikuwa ameamuru Yohane atiwe nguvuni, akamfunga gerezani. Herode alifanya hivyo kwa sababu ya Herodia ambaye Herode alimwoa ingawaje alikuwa mke wa Filipo, ndugu yake.
18 Sa si Juan ilegña as Herodes: Ti cabales na uncone y asaguan y chelumo.
Yohane alikuwa amemwambia Herode, “Si halali kwako kumchukua mke wa ndugu yako.”
19 Ya pot este si Herodias uninaguaguat contra güiya, ya jadesesao na upuno, lao ti janasiña.
Basi Herodia alimchukia sana Yohane, akataka kumwua, asiweze.
20 Sa si Herodes maañao as Juan, jatungo na tunas yan Santos na taotao ya jaguefadaje. Ya anae jajungog, gosbumuebuente gui corasonña; ya jaecungogjao ni minagofña.
Herode alimwogopa Yohane kwa maana alijua kwamba yeye ni mtu mwema na mtakatifu, na hivyo akamlinda. Herode alipenda kumsikiliza Yohane, ingawaje baada ya kumsikiliza, alifadhaika sana.
21 Ya anae mato un jaane na si Herodes gumupot ni mafañaguña, ya mamatinas sena para y prinsipeña sija yan y capitan sija, yan y manmagas sija guiya Galilea;
Ikapatikana nafasi, wakati wa sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode. Herode aliwafanyia karamu wazee wa baraza lake, majemadari na viongozi wa Galilaya.
22 Ya jumalom y jagan Herodias, ya bumaela, ya janamagof si Herodes, yan ayo sija y mangachochongña gui lamasa; ya y ray ilegña ni patgon na palaoan: Gagaoyo ni malagomo, ya junaejao.
Basi, binti yake Herodia aliingia, akacheza, akawafurahisha sana Herode na wageni wake. Mfalme akamwambia huyo msichana, “Niombe chochote utakacho, nami nitakupa.”
23 Ya manjula: Todo y ungagaoyo, junae asta lamita gui raenoco.
Tena akamwapia, “Chochote utakachoniomba, nitakupa: hata ikiwa ni nusu ya ufalme wangu.”
24 Ya mapos güe, ya ilegña as nanaña: Jafa jugagao? Si nanaña ilegña: Y ilun Juan Bautista.
Hapo huyo msichana akatoka, akamwuliza mama yake, “Niombe nini?” Naye akamjibu, “Kichwa cha Yohane mbatizaji.”
25 Ayo nae jumalom enseguidas gui ray ya jagagao, ilegña: Malagoyo pago na unnaeyo gui un plato ni ilun Juan Bautista.
Msichana akamrudia mfalme mbio akamwomba, “Nataka unipe sasa hivi katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji.”
26 Ya y ray ninagostriste; lao pot y juramentoña, yan ayo sija y mangachongña gui lamasa, ti malago japune.
Mfalme akahuzunika sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake, na kwa ajili ya wale wageni wake karamuni, hakutaka kumkatalia.
27 Ya enseguidas y ray manago uno gui guatdia, jatago na ujanao ya uchinilie ni iluña. Ya mapos, ya jadegüeya gui jalom catset.
Basi, mfalme akamwamuru askari kukileta kichwa cha Yohane. Askari akaenda, akamkata kichwa Yohane mle gerezani,
28 Ya machule guato y iluña gui un plato, ya manae y patgon palaoan, ya y patgon palaoan janae y nanaña.
akakileta katika sinia, akampa msichana naye msichana akampa mama yake.
29 Ya anae majungog ni disipuluña sija, manmato, ya machule y tataotaoña, ya mapolo gui un naftan.
Wanafunzi wa Yohane walipopata habari, walikwenda wakachukua mwili wake, wakauzika kaburini.
30 Ya y apostoles mandaña gui as Jesus, ya masangane güe todo ni chechoñija, yan y finanagüenñija.
Wale mitume walirudi, wakakusanyika mbele ya Yesu wakamwarifu yote waliyotenda na kufundisha.
31 Ya güiya ilegña su sija: Maela jamyo apatte gui un lugat desierto, ya infandescansa didide; sa megae sija manjajanao, yan manmafato, ya manaelugat mañocho.
Alisema hivyo kwa kuwa kulikuwa na watu wengi mno walikuwa wanafika hapo na kuondoka hata Yesu na wanafunzi wake hawakuweza kupata nafasi ya kula chakula. Basi, Yesu akawaambia, “Twendeni peke yetu mahali pa faragha kula chakula, mkapumzike kidogo.”
32 Ya manmapos gui un batco gui un lugat desierto apatte.
Basi, Wakaondoka peke yao kwa mashua, wakaenda mahali pa faragha.
33 Ya y lumie sija na manjanao megae, ya matungo güe; ya manmalalago para ayo megae manmamomocat gui siuda sija, ya manmato antes qui sija, ya mandaña guiya güiya.
Lakini watu wengi waliwaona wakienda, wakawatambua. Hivyo wengi wakatoka katika kila mji, wakakimbilia huko Yesu na wanafunzi wake walikokuwa wanakwenda, wakawatangulia kufika.
34 Ya anae jumuyong si Jesus jalie y linajyan taotao ya ninamaase nu sija, sa manparejoja yan y quinilo sija ni taya pastotñija; ya jatutujon fumanagüe megae na güinaja.
Waliposhuka pwani, Yesu aliona umati mkubwa wa watu, akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji. Akaanza kuwafundisha mambo mengi.
35 Ya anae estaba pupuenge, y disipuluña sija manmato guiya güiya, ilegñija: Y lugat desierto este, ya esta pupuenge.
Saa za mchana zilikwisha pita. Basi, wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwambia, “Hapa ni nyikani, na sasa kunakuchwa.
36 Najanao sija para ufanmalag y campo yan y sengsong sija gui oriya, ya ujafanmamajan pan para sija.
Afadhali uwaage watu waende mashambani na katika vijiji vya jirani, wanunue chakula.”
37 Lao manope, ilegña nu sija: Nae sija mañija. Ya sija ilegñija nu güiya: Infanjanao ya infanmamajan pan pot dosientos na denario, para innae sija nañija?
Lakini Yesu akawaambia, “Wapeni ninyi chakula.” Nao wakamwuliza, “Je, twende kununua mikate kwa fedha dinari mia mbili, na kuwapa chakula?”
38 Ya güiya ilegña nu sija: Cuanto na pan guaja jamyo? Janao, ya inlie. Ya anae jatungo sija, ilegñija: Sinco, yan dos na güijan.
Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi? Nendeni mkatazame.” Walipokwisha tazama, wakamwambia, “Kuna mikate mitano na samaki wawili.”
39 Ya jatago, sija na ujanafanmatachong todos pot mangachong gui jilo y manbetde na chaguan.
Basi, Yesu akawaamuru wanafunzi wawaketishe watu wote makundimakundi penye nyasi.
40 Ya manmatachong pot mangachong, siento yan siento, yan sincuenta yan sincuenta.
Nao wakaketi makundimakundi ya watu mia moja na ya watu hamsini.
41 Ya jachule y sinco na pan yan y dos na güijan, ya manatan julo gui langet, ya jabendise, ya jaipe y pan sija; ya janae y disipuluña sija para ujaplanta gui sanmenañija; ya y dos na güiyan manmapatte todos.
Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu, akaimega mikate, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu. Na wale samaki wawili pia akawagawia wote.
42 Ya mañocho todos, ya manjaspog.
Watu wote wakala, wakashiba.
43 Ya jajatsa y pedaso sija dose na canastra manbula; yan pedaso y güijan sija locue.
Wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
44 Ya ayo sija y mañocho ni pan, sinco mit na lalaje sija.
Nao waliokula hiyo mikate walikuwa wanaume elfu tano.
45 Ya enseguidas jaapura y disipuluña sija na ufangajulo gui batco, ya ufanjanao gui menaña gui otro banda guiya Betsaida, mientras janajanao y linajyan taotao.
Mara Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie kwenda Bethsaida, ng'ambo ya ziwa, wakati yeye anauaga umati wa watu.
46 Ya despues, anae munjayan janajanao sija, mapos malag y egso para ufanaetae.
Baada ya kuwaaga watu alikwenda mlimani kusali.
47 Ya anae esta pupuenge, y batco estaba gui talo gui tase, ya güiyaja namaesa gui tano.
Ilipokuwa jioni, mashua ilikuwa katikati ya ziwa, naye alikuwa peke yake katika nchi kavu.
48 Ya jalie sija na manmachochocho mapot manmamómogsae, sa y manglo contrario para sija; ya jijot gui mina cuatro na guatdia gui puenge, mato güe guiya sija, mamómocat gui jilo tase; ya malago na ufalofan gui oriyañija.
Basi, akawaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kupiga makasia, maana upepo ulikuwa unawapinga. Karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea akitembea juu ya maji. Alitaka kuwapita.
49 Ya anae malie nu sija, na mamómocat gui jilo tase, jinasoñija na pantasma, ya managang;
Lakini walimwona akitembea juu ya maji, wakadhani ni mzimu, wakapiga yowe.
50 Sa todos lumie güe, ya ninafañatsaga. Lao enseguidas jacuentuse sija, ya ilegña nu sija: Angoco jamyo, guajoyo; chamiyo fanmaaañao.
Maana wote walipomwona waliogopa sana. Mara Yesu akasema nao, “Tulieni, ni mimi. Msiogope!”
51 Ya cajulo guiya sija gui batco, ya y manglo mapos: ya sija ninafangosmanman;
Kisha akapanda mashuani walimokuwa, na upepo ukatulia. Nao wakashangaa sana.
52 Sa sija ti jatungo y milagron y pan sija; sa y corasonñija estaba mangosmajetog.
maana hawakuwa bado wameelewa maana ya ile mikate. Akili zao zilikuwa bado zimepumbazika.
53 Ya anae manmalofan para y otro banda, manmato gui tano Genesaret, ya manmalag y puetto.
Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti, wakatia nanga.
54 Ya anae manjuyong sija gui batco, enseguidas matungo güe.
Walipotoka mashuani, mara watu wakamtambua Yesu.
55 Ya manmalago gui oriyan todo ayo na tano, ya matutujon mañule gui todo y patte, manmalango sija gui cama, mano nae majungog na estaba güije.
Basi, kwa haraka wakazunguka katika nchi ile yote, wakaanza kuwachukua wagonjwa wamelala juu ya mikeka yao, wakawapeleka kila mahali waliposikia Yesu yupo.
56 Ya manuja nae jumalom, songsong, pat suida, pat fangualuan, mapolo papa y malango sija gui chalan, y matayuyut güe na upacha y canton y magaguña, ya todo ayo sija y japacha, manjomlo.
Kila mahali Yesu alipokwenda, vijijini, mijini, au mashambani, watu waliwaweka wagonjwa uwanjani, wakamsihi waguse walau pindo la vazi lake. Nao wote waliomgusa walipona.

< San Marcos 6 >