< San Marcos 10 >

1 YA cajulo güije, mato qui oriyan Judea, gui otro bandan Jordan; ya manalo y linajyan taotao mandaña guiya güiya; ya jatalo fumanagüe, taegüije, y costumbreña.
Yesu alitoka hapo akaenda mkoani Yudea na hata ng'ambo ya mto Yordani. Umati wa watu ukamwendea tena, naye akawafundisha tena kama ilivyokuwa desturi yake.
2 Ya manmato y Fariseo sija guiya güiya, ya mafaesen güe cao tunas y laje uyute y asaguaña? matietienta güe.
Basi, Mafarisayo wakamwendea, na kwa kumjaribu wakamwuliza, “Je, ni halali mtu kumpa talaka mkewe?”
3 Lao güiya manope, ilegña nu sija: Jafa mantinago jamyo as Moises?
Yesu akawajibu, “Mose aliwapa maagizo gani?”
4 Ya sija ilegñija: Si Moises japetmite na umatugue papet inapattan umasagua ya uyute.
Nao wakasema, “Mose aliagiza mume kumpatia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
5 Ya si Jesus manope, ilegña nu sija: Pot y majetog corasonmiyo na mantiniguie jamyo ni este na tinago.
Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia amri hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
6 Lao desde tutujon y jiniyong, Laje yan palaoan fumatinas sija Yuus.
Lakini tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu aliumba mwanamume na mwanamke.
7 Pot este na rason y laje udingo si tataña yan si nanaña, ya udaña yan y asaguaña.
Hivyo mwanamume atawaacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe,
8 Ya y este y dos, umana unoja na catne; ya esta ti udos mas, na unoja na catne.
nao wawili watakuwa mwili mmoja. Kwa hiyo, wao si wawili tena bali mwili mmoja.
9 Jafaja si Yuus munadaña, y taotao ti unadesapatta.
Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe.”
10 Ya y jalom guma, y disipulo sija mafaesen güe talo ni ayoja.
Walipoingia tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake walimwuliza juu ya jambo hilo.
11 Ya ilegña nu sija: Jayeja y yumute y asaguaña, ya umasagua yan otro, jafatinas y adulterio contra y palaoan.
Naye akawaambia, “Anayemwacha mkewe na kuoa mwingine, anazini dhidi ya mkewe.
12 Ya yaguin y palaoan yumute y asaguaña, ya umasagua yan otro, jafatinas adulterio.
Na mwanamke anayemwacha mumewe na kuolewa na mwingine anazini.”
13 Ya machulie guato guiya güiya diquique na famaguon para upacha: ya y disipulo sija jalalatde ayo sija.
Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
14 Ya anae jalie si Jesus, sen ti ninamagof ya ilegña nu sija: Polo y diquique na famaguon ya ufanmamaela guiya guajo; chamiyo chumochoma; sa iyon este sija y raenon Yuus.
Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa.
15 Magajet jusangane jamyo, na y ti rumesibe y raenon Yuus calang un patgon, ti ujalom gui jalom ayo.
Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia katika Ufalme huo.”
16 Ya jajogüe sija ya japolo y canaeña gui jiloñija, ya jabendise sija.
Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.
17 Ya anae jumanao gui chalan, mato uno malalago ya dinimuye güe gui menaña ya finaesen güe: Mauleg na Maestro, jafa jufatinas para juereda y taejinecog na linâlâ? (aiōnios g166)
Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja alimjia mbio, akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanyeje ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
18 Si Jesus ilegña nu güiya: Jafa na ilegmo nu guajo mauleg? Taya mauleg, na unoja, si Yuus.
Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
19 Untungo y tinago sija: Chamofamumuno; chamo fumatinas adulterio; chamo fañañaque; chamo sumanganñaejon y ti magajet na testimonio; chamo chumu y ti iyomo; onra si tatamo yan si nanamo.
Unazijua amri: Usizini; Usiue; Usiibe; Usitoe ushahidi wa uongo; Usidanganye; Waheshimu baba na mama yako.”
20 Güiya manope ilegña: Maestro, todo este juadadaje desde nae patgonyo.
Naye akamjibu, “Mwalimu, hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
21 Ayo nae matan güe as Jesus, güinaeya güe, ya ilegña nu güiya: Fatta jao uno: Janao ya ufajan todo y güinajamo, ya unnae y mamobble sija, ya uguaja güinajamo gui langet: ya maela, ya undalalag yo.
Yesu akamtazama, akampenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja: nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.”
22 Lao güiya ninamatolaeca y mataña ni este na sinangan ya mapos ninatriste; sa guaja megae güinajaña.
Aliposikia hayo, alisikitika, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.
23 Ayo nae si Jesus manatan gui oriya, ya ilegña ni disipuluña sija: Na minapot manjalom gui raenon Yuus ayo sija y mangaegüinaja!
Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
24 Ya y disipulo sija ninafanmanman ni sinanganña: Lao si Jesus manope ilegña talo: Famaguon, na minapot manjalom, gui raenon Yuus y umangongoco sija gui güinaja!
Wanafunzi walishangazwa na maneno yake. Yesu akawaambia tena, “Watoto wangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25 Mas guse malofan un cameyo gui matan un jaguja, qui y gaegüinaja ujalom gui raenon Yuus.
Ni rahisi zaidi ngamia kupenya katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 Ya sija ninagos fanmanmanman, ya ilegñija nu güiya: Ayo nae, jaye siña satbo?
Wanafunzi wake wakashangaa sana wakaulizana, “Ni nani basi, atakayeweza kuokoka?”
27 Ayo nae si Jesus jaatan sija, ya ilegña: Para y taotao sija, este ti siña, lao para si Yuus ti taegüine; sa para si Yuus todo ninasiña.
Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo, maana kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
28 Ayonae si Pedro jatutujon ilegña nu güiya: Estagüejamja na indingo todo, ya indadalalagjao.
Petro akamwambia, “Na sisi je? Tumeacha yote, tukakufuata!”
29 Inepe as Jesus ilegña. Magajet jusanganejao: Taya ni un taotao ni y dumingo gumaña, pat mañeluña lalaje, pat mañeluña famalaoan, pat nanaña, pat tataña, pat famaguonña, pat fangualuaña, pot guajo, yan y ibangelio;
Yesu akasema, “Kweli nawaambieni, kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au mama, au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema,
30 Na ti uresibe pagoja sienbiaje: guma sija, yan mañeluña lalaje, yan mañeluña famalaoan, yan nanaña, yan famaguonña, yan fangualuan sija, yan umapetsigue; ya y mámamaela na siglo, taejinecog na linâlâ. (aiōn g165, aiōnios g166)
atapokea mara mia zaidi wakati huu wa sasa nyumba, ndugu, dada, mama, watoto na mashamba pamoja na mateso; na katika wakati ujao atapokea uzima wa milele. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lao megae na manfinenana, ufanuttimo, ya y manuttimo, ufanfinenana.
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
32 Ya anae mangaegue gui chalan, mangajulo guiya Jerusalem; ya si Jesus malag y menañija; ya ninafanmanman: ya y dumadalalag mangosmaañao. Ya jacone talo y dose, ya jatutujon sumangane sija jafa ususede güe.
Basi, walikuwa njiani kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa anawatangulia. Wanafunzi wake walijawa na hofu, na watu waliofuata waliogopa. Yesu akawachukua tena kando wale kumi na wawili, akaanza kuwaambia yale yatakayompata:
33 Ylegña: Estagüejit na mangajulo guiya Jerusalem, ya y Lajin taotao umaentrega gui magas mamale, yan y escriba sija, ya umasentensia para umapuno, ya umaentrega gui Gentiles.
“Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe na kumkabidhi kwa watu wa mataifa.
34 Ya umamofea, yan umatolae, yan umasaulag, yan umapuno; ya y despues di tres na jaane ucajulo talo.
Nao watamdhihaki; watamtemea mate, watampiga mijeledi na kumwua. Na baada ya siku tatu atafufuka.”
35 Ya si Santiago yan si Juan, lalajin Sebedeo, manmato jijot guiya güiya ya ilegñija nu güiya: Maestro, manmalagojam na unfatinas guiyajame jafa y malagomame.
Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.”
36 Ya ilegña nu sija: Jafa malagonmiyo na jufatinas guiya jamyo?
Yesu akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
37 Ilegñija nu güiya: Nafanmatachongjam, y uno gui agapamo, ya y otro gui acagüemo, gui minalagmo.
Wakamjibu, “Uturuhusu tuketi mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wa Ufalme wako.”
38 Si Jesus ilegña nu sija: Ti intingo jafa ingagagao. Siña jamyo manguimen gui copa anae gumiguimenyo? yan infanmatagpange ni y matagpangeco?
Yesu akawaambia, “Hamjui mnachoomba! Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa, au kubatizwa kama nitakavyobatizwa?”
39 Ya ilegñija nu güiya: Mansiñajam. Ayonae ilegña si Jesus nu sija: infanguimen gui copa anae gumiguimenyo, yan infanmatagpange ni y ma tagpangeco;
Wakamjibu, “Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokunywa mtakinywa kweli, na mtabatizwa kama nitakavyobatizwa.
40 Lao y infanmatachong gui agapajo, yan y acagüeco; ti guajo jufannae; lao para ayo sija ufanmanae y manmapreparaye.
Lakini ni nani atakayeketi kulia au kushoto kwangu si wajibu wangu kupanga, bali nafasi hizo watapewa wale waliotayarishiwa.”
41 Ya anae majungog este ni y dies, ninafanlalalo as Santiago yan Juan.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, walianza kuchukizwa na Yakobo na Yohane.
42 Lao maninagang as Jesus ya ilegña nu sija: Intingo na ayo y manmanafanmagas gui Gentiles, jafatinas minagas gui jiloñija; ya y manmagas, jafatinas ninasiña gui jiloñija.
Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba wale wanaofikiriwa kuwa watawala wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, na wakuu hao huwamiliki watu wao.
43 Lao ti utaegüenao guiya jamyo; sa jaye y malago dumangculo guiya jamyo; güiya ufañeñetbe.
Lakini kwenu isiwe hivyo, ila anayetaka kuwa mkuu kati yenu, sharti awe mtumishi wenu.
44 Ya jaye guiya jamyo y malago mumagas; utentago para todo.
Anayetaka kuwa wa kwanza, sharti awe mtumishi wa wote.
45 Sa magajet ni y Lajin taotao ti mato para umasetbe, lao para ufañetbe, ya para ufannae y jaaniña ni un rescate para unafanlibre megae.
Maana Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, ila alikuja kutumikia, na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
46 Ya manmato Jerico. Ya anae manjanao gui Jerico, yan y disipuluña yan un dangculon linajyan taotao, si Bartimeo lajin Timeo, na bachet, matatachong gui oriyan chalan, ya umegagao.
Basi, wakafika Yeriko, naye Yesu alipokuwa anatoka katika mji huo akiwa na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mwombaji aitwaye Bartimayo mwana wa Timayo alikuwa ameketi kando ya barabara.
47 Ya anae jajungog na si Jesus Nasareno, jatutujon umagang ilegña: Jesus, Lajin David, gaease nu guajo.
Aliposikia kwamba ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita mahali hapo, alianza kupaaza sauti, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
48 Ya megae mumomye para ufamatquilo: lao mas umagang gosagang: Jago ni y Lajin David, gaease nu guajo.
Watu wengi walimkemea ili anyamaze, lakini yeye akazidi kupaaza sauti, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
49 Ya si Jesus tumojgüe ya ilegña: Agang güe. Ya maagang y bachet ilegñija nu güiya: Magofjao; cajulo sa inaagangjao.
Yesu alisimama, akasema, “Mwiteni.” Basi, wakamwita huyo kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Simama, anakuita.”
50 Ya janasuja y capaña, y cajulo, ya malag as Jesus.
Naye akatupilia mbali vazi lake, akaruka juu, akamwendea Yesu.
51 Ya si Jesus manopegüe ya ilegña: Jafa malagomo jufatinas guiya jago? Y bachet ilegña nu güiya: Raboni, nafanliiyo.
Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Huyo kipofu akamwambia, “Mwalimu, naomba nipate kuona.”
52 Si Jesus ilegña: Janao, y jinengguemo munajomlojao. Ya enseguidas manlie, ya jadalalag si Jesus gui jinanaoña.
Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Mara huyo kipofu akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.

< San Marcos 10 >