< San Marcos 1 >

1 TUTUJON y ibangelion Jesucristo, Lajin Yuus.
Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 Jaftaemano esta matugue gui profeta Isaias: Estagüe, guajo tumago y tentagojo gui menan matamo, para ufamauleg y chalanmo gui menamo.
Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3 Ynagang ni umaagang gui desierto: Fanmauleg y chalan y Señot: natunas y cayejonña.
Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
4 Si Juan managpange gui desierto, ya jasetmon y tinagpangen minañotsot para inasiin isao sija.
Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5 Ya manjanao guiya güiya guato todo y tano Judea, yan todo sija guiya Jerusalem; ya todo sija mantinagpange gui sadog Jordan, ya jaconfesatñaejon y isaoñija.
Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6 Ya si Juan minagagon pulon cameyo, yan sinturon cuero gui senturaña; ya y naña, apacha yan miet monte.
Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7 Ya mansesetmon, ilegña: Ufato gui tateco uno na masgaeninasiña qui guajo, y coreas y sapatosña, ti digno yo nu jutecon ya jupula.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8 Guajo magajet na jutagpange jamyo yan janom; lao güiya infantinagpange ni Espiritu Santo.
Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 Ya susede ayo sija na jaane, na si Jesus mato guine Nasaret Galilea, ya tinagpange as Juan gui Jordan.
Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10 Ya enseguidas nae cajulo gui janom, jalie na mababa y langet, ya y Espiritu, calang paluma tumunog gui jiloña,
Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11 Ya mato un inagang guine y langet na ilegña: Jago y lajijo ni yajo, iya jago nae gosmagof yo.
Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
12 Ya enseguidas ninafalag y desierto ni Espiritu.
Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13 Ya sumaga güije cuarenta na jaane, ya tinienta as Satanas; yan mañisija y manmachaleg na gâgâ sija; ya y angjet sija masetbe güe.
akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14 Anae munjayan si Juan mapreso, mato si Jesus guiya Galilea, jasesetmon y ibangelion Yuus.
Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15 Ya ilegña: Y tiempo esta macumple; ya y raenon Yuus esta jijot: fanmañotsot, ya injenggue y ibangelio.
“Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
16 Ya mamomocat gui oriyan tasen Galilea, jalie si Simon, yan si Andres chelun Simon, na jayuyute y lagua gui tase, sa sija manpescadot.
Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17 Ya si Jesus ilegña nu sija: Maela dalalagyo, ya junafanpescadot taotao jamyo.
Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
18 Enseguidas japolo y laguañija ya madalalag güe.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Anae malofan talo didide mona, jalie si Santiago, lajin Sebedeo, yan si Juan cheluña, na manestaba locue gui batco na jalememenda y laguañija.
Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Ya enseguidas jaagang; ya jadingo si tatanñija as Sebedeo gui batco yan y manmachocho sija, ya madalalag güe.
Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21 Ya manjalom Capernaum; ya enseguidas, gui sábado na jaane, jumalom gui sinagoga ya mamanagüe.
Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22 Ya sija ninafanmanman ni finanagüeña; sa jafananagüe sija calang uno ni gaeninasiña, ya ti calang y escriba sija.
Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23 Ya enseguidas guaja güije gui sinagogañija un taotao na guaja áplacha na espiritu, ya güiya umagang,
Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24 Ylegña: Parajafa jam nu jago, Jesus taotao Nasaret? Matojao para unnafanaelayejam? Jutungoja jayejao, jago y Santos guine as Yuus.
akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
25 Ya si Jesus jalalatde ilegña: Pacaca, ya maela juyong guiya güiya.
Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
26 Ya anae y áplacha na espiritu tiniteg güe, ya ninaagang gosdangculo na inagang, jumuyong guiya güiya.
Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27 Ya todo sija ninafanmanman, pot este manafaesen entre sija, ilegñija: Jafa este? Jafa na nuebo finanagüe este! yan ninasiña jatago y manáplacha na espiritu, ya maosgueja güe?
Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 Enseguidas y famaña manamamta todo gui tano oriyan Galilea.
Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29 Ya enseguidas anae jumuyong gui sinagoga, mato gui guima Simon yan si Andres, yan si Santiago yan si Juan.
Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30 Ya y suegran Simon estaba na umaason sa malango yan calentura: ya masangane güe enseguidas nu y palaoan.
Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31 Ayo nae mato güe, ya jamantiene canaeña, ya jajatsa julo; ya pinelo ni calentura, ya güiya sumetbe sija.
Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32 Ya anae estaba esta pupuenge, anae machom y atdao, maconiigüe todo ni manmañetnot yan y maninanite.
Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33 Ya todo y siuda mandaña gui petta.
Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34 Ya janafanjomlo megae ni manestaba manmalango todo clasen chetnot sija; ya jayute juyong megae na anite sija; ya ti japolo nu y anite sija cumuentos sa matungo güe.
Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35 Ya y egaan güije, cajulo gostaftaf, jojomjomja trabia, ya jumuyong, ya malag y un lugat desierto, ya manaetae güije.
Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36 Ya tinatiye güe as Simon, yan y mangachochongña.
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37 Ya anae masoda güe, ilegñija nu güiya: Todo umaliligaojao.
Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38 Güiya ilegña nu sija: Nije tafanmalag y otro lugat gui sengsong ni jijot, ya jufansetmon locue güije; sa pot este na matoyo.
Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39 Ya jumalom gui sinagogañija todo Galilea, sesetmon ya jayuyute juyong y anite sija.
Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40 Ya un ategtog mato guiya güiya, tinayuyut güi ya dumimo, ya ilegña: Yaguin malagojao, siña unnagasgasyo.
Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41 Ya si Jesus ninamaase ya jaestira y canaeña, ya japacha, ya ilegña: Malagoyo, ungasgas.
Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
42 Ya enseguidas y chetnot y ategtog mapos guiya güiya ya gasgas güe.
Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43 Ya jagosencatga, ya jatago na ujanao,
Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44 Ya ilegña nu güiya: Atan ya chamo sumangangane ni jaye jafa; lao sigueja gui jinanaomo ya unfanue y pale nu jago, ya unofrese ni guinasgasmo ni si Moises manago, para testimonioñija.
“Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
45 Lao güiya mapos, ya jatutujon munamatungo, yan janagosmamta y checho; pot este, si Jesus ti siña jumalom matungo nu güiya gui siuda; lao sumasagaja gui sumanjiyong gui lugat desierto sija, ya manmato guiya güiya guinin todo y patte sija.
Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.

< San Marcos 1 >