< San Lucas 24 >

1 LAO y finenana na jaane gui semana, gui taftataf gui egaan, manmato gui naftan, mapmañuñule guato paopao ni y finamaulegñija.
Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.
2 Ya masoda y acho na esta managalileg gui pettan y naftan.
Walikuta lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.
3 Ya anae manjalom ti masoda y tataotao y Señot Jesus.
Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.
4 Ya anae manmajngang nu este, dos taotao tumotojgue gui oriyanñija, na minagagago ni y lamlam na magago.
Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung'aa sana, wakasimama karibu nao.
5 Ya anae ninafanmaañao ya manecon papa gui eda, ilegñija nu sija: Jafa muna inaliligao y lâlâ gui entalo y manmatae?
Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?
6 Taegüe güine, lao esta cajulo: jaso y mansinangane jamyo, anae estataba Galilea,
Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:
7 Ylegña: Na nesesita na y Lajin taotao umaentrega gui canae y taotao sija ni manisao, y umaatane gui quiluus, ya ucajulo talo gui mina tres na jaane.
Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka.”
8 Ayonae jajaso sija y sinanganña,
Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,
9 Ya manalo guato gui naftan ya jasangane y onse nu este sija, yan todo y pumalo.
wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.
10 Ya sija si Maria Magdalena yan si Juana, yan si Maria nanan Santiago; yan y pumalo palaoan ni mangachongñija, sumangane y apostoles nu estesija.
Hao waliotoa habari hizo kwa mitume ni: Maria Magdalene, Yoana na Maria mama wa Yakobo, pamoja na wanawake wengine walioandamana nao.
11 Lao sija japolo na taetiningo, y sinanganñija ya ti majonggue.
Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.
12 Ayonae cajulo si Pedro, ya malago asta y naftan: ya anae ñumejon ya jaatan jalom, jalilie y sabanasja gui un lugat, ya mapos güe iyasija ya ninamanman nu este y manmalofan.
Lakini Petro alitoka, akaenda mbio hadi kaburini. Alipoinama kuchungulia ndani, akaiona tu ile sanda. Akarudi nyumbani huku akiwa anashangaa juu ya hayo yaliyotokea.
13 Ya, estagüe, dos guiya sija na jumajanao, güijeja na jaane, para un songsong ni naanña Emmaus, sesenta estadios desde Jerusalem.
Siku hiyohiyo, wawili kati ya wafuasi wake Yesu wakawa wanakwenda katika kijiji kimoja kiitwacho Emau, umbali wa kilomita kumi na moja kutoka Yerusalemu.
14 Ya cumuecuentos y dos mona pot todo estesija y masusede.
Wakawa wanazungumza juu ya hayo yote yaliyotukia.
15 Ya susede anae cumuecuentos y dos, ya manafaesen entre sija, mato si Jesus ya mañisija manjanao.
Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akatokea, akatembea pamoja nao.
16 Lao y atadogñija calang manmatampe, para chañija tumutungo güe.
Walimwona kwa macho, lakini hawakumtambua.
17 Ya ilegña nu sija: Jafa na cuentosmimiyo uno yan otro, anae manajanao jamyo, ya mañaga ya ninafantriste?
Akawauliza, “Mnazungumza nini huku mnatembea?” Nao wakasimama kimya, nyuso zao wamezikunja kwa huzuni.
18 Inepe ni ayo y uno ni y naanña si Cleofas ya ilegña nu güiya: Ada sumagaja jao guiya Jerusalem, ya ti untungo jafa manmalofan güine sija na jaane?
Mmoja, aitwaye Kleopa, akamjibu, “Je, wewe ni mgeni peke yako Yerusalemu ambaye hujui yaliyotukia huko siku hizi?”
19 Ayonae ilegña nu sija: Jafa sija? Ya ilegñija nu güiya: Ayo sija iyon si Jesus Nasareno, ni profeta güe ni gaeninasiña gui checho yan y sinangan gui menan Yuus yan todo y taotao sija;
Naye akawajibu, “Mambo gani?” Wao wakamjibu, “Mambo yaliyompata Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye uwezo wa kutenda na kufundisha mbele ya Mungu na mbele ya watu wote.
20 Ya maentrega, gui magas mamale yan y magalajenmame para umasentensia ni y finatae, ya maatane gui quiluus.
Makuhani na watawala wetu walimtoa ahukumiwe kufa, wakamsulubisha.
21 Lao jame innanangga sa güiya y para unafanlibre y Israel. Junggan, yan mas qui todo este, pago esta mina tres na jaane desde que masusede estesija.
Lakini sisi tulitumaini kwamba yeye ndiye angeikomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotendeka.
22 Yan locue palo famalaoan ni mangachongmame janamanman jam sa manmato gui naftan gui taftataf gui egaan;
Tena, wanawake wengine wa kwetu wametushtua. Walikwenda kaburini mapema asubuhi,
23 Ya anae ti masoda y tataotaoña, manmato guiya jame ilegñija na manmanlie sija y liniin angjet sija, ni y jasnangane na lâlâgüe.
wasiukute mwili wake. Wakarudi wakasema kwamba walitokewa na malaika waliowaambia kwamba alikuwa hai.
24 Ya mamjanao guato gui naftan palo gui mangachongmame ya masoda taemanoja y sinangan y famalaoan; lao ti malie güe.
Wengine wetu walikwenda kaburini wakashuhudia yale waliyosema hao wanawake; ila yeye hawakumwona.”
25 Ya ilegña nu sija: O taotao manaetiningo jamyo, yan y ñateng y corasonmiyo para injenggue todo y sinangan y profeta sija!
Kisha Yesu akawaambia, “Mbona mu wapumbavu kiasi hicho na mioyo yenu ni mizito hivyo kusadiki yote yaliyonenwa na manabii?
26 Ada ti nesesita na si Cristo ufamadese nu este sija ya taegüine nae ujalom gui minalagña?
Je, haikumpasa Kristo kuteswa, na hivyo aingie katika utukufu wake?”
27 Ya jatutujon desde as Moises, yan y profeta sija, y jasangangane claro todo ni tinigue ni y pot güiya.
Akawafafanulia mambo yote yaliyomhusu yeye katika Maandiko Matakatifu kuanzia Mose hadi manabii wote.
28 Ya manmato gui sengsong ni jajananagüe güije; ya jasigue para mas chago jinanaoña.
Walipokikaribia kile kijiji walikokuwa wanakwenda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea na safari;
29 Lao sija janasaga fuetsao, ilegñija: Maela tafañaga sa este puenge ya jocog y jaane; ya jumalom para usaga mañisija.
lakini wao wakamsihi wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia.” Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.
30 Ya susede, anae matachong gui lamasa yan sija, jachule y pan ya jabendise, ya jaipe ya manninae.
Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.
31 Ayonae manmababa atadogñija ya matungo güe; lao güiya jamalingoja gui inatanñija.
Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.
32 Ya ilegñija entre y dos: Ada ti sinenggue y corasonta gui sumanjalomta mientras jacuentutusejit gui chalan, yan anae jababayejit ni y tinigue?
Basi, wakaambiana, “Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?”
33 Ya cumajulo y dos güije na ora, ya tumalo guato Jerusalem: ya masoda y onse mandadaña, yan y manestaba mangachongñiñija,
Wakaondoka saa ileile, wakarudi Yerusalemu: wakawakuta wale mitume kumi na mmoja na wale wengine waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
34 Ya ilelegñija: Magajet, esta cajulo y Señot, na umalie yan si Simon.
wakisema, “Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni.”
35 Ayonae sija jasangane nu este sija y masusede gui chalan; yan jafa taemano, tungoñija anae jaipe y pan.
Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.
36 Ya mientras manguecuentos nu este sija, güiya tumojgueja gui entaloñija, y ilegña nu sija: Pas guiya jamyo.
Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia “Amani kwenu.”
37 Ayonae manmaañao ya manmajngang ya jinasonñija na manmanlie sija un espiritu.
Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.
38 Lao güiya ilegña nu sija: Jafa na ninafanestotba jamyo? Ya jafa na cumajulo y jinasonmiyo gui corasonmiyo?
Lakini yeye akawaambia, “Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?
39 Atanja y canaejo yan y adengjo, sa guajo mismoyo: pacha yan inlie sa y espiritu taecatne ni tolang, taegüije inliija na guajayo,
Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo.”
40 Ya anae jasangan este, manfinanue ni y canaeña yan y adengña.
Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.
41 Ya anae ti jajonggue sija pot minagofñija, ya ninafanmanman, güiya ilegña nu sija: Guaja güine jafa para utacano?
Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, “Mnacho chakula chochote hapa?”
42 Ya sija janae un pedason güijan na mapeja.
Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.
43 Ya jachule ya jacano gui menanñija.
Akakichukua, akala, wote wakimwona.
44 Ya ilegña nu sija: Este sija na sinangan ni y jusangangane jamyo anae manjijita: taemanoja na nesesita na umacumple todo y esta matugue gui lay Moises yan y profeta sija, yan y Salmos pot guajo.
Halafu akawaambia, “Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi.”
45 Ayonae manbinaba y jinasoñija para ujatungo y tinigue;
Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.
46 Ya ilegña nu sija: Taegüine esta matugue, na si Cristo ufamadese ya ucajulo talo guinin y manmatae gui mina tres na jaane;
Akawaambia, “Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,
47 Ya umapredica gui naanña y sinetsot yan inasiin isao, gui todo y nasion sija, umatutujon desde Jerusalem.
na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.
48 Ya jamyo testigo nu estesija na güinaja.
Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.
49 Ya, estagüe, na bae jutago y promesan y Tatajo gui jilo miyo: lao jamyo fañaga gui siuda guiya Jerusalem, asta que manminagago jamyo ni y ninasiña guinin iya jululo.
Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu.”
50 Ya manquinene juyong asta Betania; ya jajatsa y canaeña ya manbinendise sija.
Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.
51 Ya susede anae manbinendise, jaapatte güe guiya sija ya machule julo gui Langet.
Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.
52 Ya sija jaadora ya manalo guato Jerusalem yan y dangculon minagofñija;
Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:
53 Ya mangaegue siempre gui templo, manmanbendidise as Yuus. Amen.
wakakaa muda wote Hekaluni wakimsifu Mungu.

< San Lucas 24 >