< San Lucas 13 >

1 YA mangaegue güije na tiempo taotao sija, ni masangane güe pot y Galileo sija, ni si Pilatos janadaña y jâgâñija yan y inefresenñija.
Wakati huo watu fulani walikuja, wakamweleza Yesu juu ya watu wa Galilaya ambao Pilato alikuwa amewaua wakati walipokuwa wanachinja wanyama wao wa tambiko.
2 Ya si Jesus manope ya ilegña nu sija: Jinasonmiyo na este sija na Galileo, mas manisao qui todo Galileo sija na japadese ayo sija?
Naye Yesu akawaambia, “Mnadhani Wagalilaya hao walikuwa wahalifu zaidi kuliko Wagalilaya wengine, ati kwa sababu wameteseka hivyo?
3 Jusangane jamyo na aje; sa yanguin ti manmañotsot jamyo, manparejoja jamyo manáchamalingo.
Nawaambieni hakika sivyo; lakini nanyi, hali kadhalika, msipotubu, mtaangamia kama wao.
4 Pat ayo sija y diesiocho ni y podong y tore gui jiloñija guiya Siloe ya manpinino, jinasonmiyo na mas manisao ayo sija qui todo y taotao ni y mañasaga Jerusalem?
Au wale kumi na wanane walioangukiwa na mnara kule Siloamu wakafa; mnadhani wao walikuwa wakosefu zaidi kuliko wengine wote walioishi Yerusalemu?
5 Jusangane jamyo na aje; sa yanguin ti manmañotsot jamyo, manparejoja jamyo manáchamalingo.
Nawaambieni sivyo; lakini nanyi msipotubu, mtaangamia kama wao.”
6 Ya jasangan este na acomparasion: Un taotao guaja y trongcon igos na matanme gui fangualuanña; ya anae mato para uegaga cao guaja tinegchaña, ti mañoda.
Kisha, Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini katika shamba lake. Mtu huyu akaenda akitaka kuchuma matunda yake, lakini akaukuta haujazaa hata tunda moja.
7 Ya ilegña ni y lancheruña: Esta guaja tres años ni matoyo güine na trongcon igos, manegagayo tinegcha, ya taya nae mañodayo; utut papa; para jafa na jaocucupa y tano?
Basi, akamwambia mfanyakazi wake: Angalia! Kwa miaka mitatu nimekuwa nikija kuchuma matunda ya mtini huu, nami nisiambulie kitu. Ukate! Kwa nini uitumie ardhi bure?
8 Ya manope ilelegña nu güiya: Señot, polo pago na año ya juguadog y oriyaña, ya junaye estietcot:
Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
9 Ya yanguin ufanogcha, mauleg; yanguin aje, siempre, unutut.
Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata.”
10 Ya estaba na mamananagüe gui un sinagoga, gui sabado na jaane.
Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
11 Ya estagüe un palaoan, na guaja un espiritun malango guiya güiya esta diesiocho años, ya esta ninaojlo, ya tisiña tumacho.
Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
12 Ya anae linie as Jesus, inagang ya ilegña nu güiya: Palaoan, libre jao gui malangumo.
Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umeponywa ugonjwa wako.”
13 Ya japolo y canaeña gui jiloña; ya enseguidas ninatunas, ya jaalaba si Yuus.
Akamwekea mikono, na mara mwili wake ukawa wima tena, akawa anamtukuza Mungu.
14 Lao y magas sinagoga lalalo sa si Jesus, numanajomlo gui sabado na jaane, ya manope ilegña nu y linajyan taotao sija: Guaja saes na jaane para ufanmachocho y taotao sija: ya este nae mauleg mato para numajomlo; lao ti y sabado na jaane.
Lakini mkuu wa sunagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo akawaambia wale watu walikusanyika pale, “Mnazo siku sita za kufanya kazi. Basi, fikeni siku hizo mkaponywe magonjwa yenu; lakini msije siku ya Sabato.”
15 Ayonae inepe ni y Señot, ya ilegña: Hipocrita jamyo, ada ti siña cada uno guiya jamyo upula y gaña guaca, pat asno gui pesebre, ya ucone ya unaguimen gui sabado na jaane?
Hapo Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Nani kati yenu hangemfungua ng'ombe au punda wake kutoka zizini ampeleke kunywa maji, hata kama siku hiyo ni ya Sabato?
16 Ya ti siña este na palaoan, ni y jagan Abraham, ni guinede as Satanas diesiocho años, manalibre gui magodeña, gui sabado na jaane?
Sasa, hapa yupo binti wa Abrahamu ambaye Shetani alimfanya kilema kwa muda wa miaka kumi na minane. Je, haikuwa vizuri kumfungulia vifungo vyake siku ya Sabato?”
17 Ya anae jasangan estesija, todo y enemiguña ninafan mamajlao; ya todo y taotao sija ninafanmagof, pot todo y sennamagof na güinaja ni y machogüe pot güiya.
Alipokwisha sema hayo, wapinzani wake waliona aibu lakini watu wengine wote wakajaa furaha kwa sababu ya mambo yote aliyotenda.
18 Pot enao ilegña: Jafa parejuña y raenon Yuus? yan jafa nae juacompara?
Yesu akauliza: “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaulinganisha na nini?
19 Parejo yan y granon y semiyan mustasa, ni y jachule y taotao, ya jatanme gui jalom jardinña; ya docó, ya jumuyong trongcon jayo; ya esta y pajaro sija gui langet mañaga gui ramasña.
NI kama mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake; ikaota hata ikawa mti. Ndege wa angani wakajenga viota vyao katika matawi yake.”
20 Ya ilegña talo: Jafa nae juacompara y raenon Yuus.
Tena akauliza: “Nitaulinganisha Ufalme wa Mungu na nini?
21 Parejo yan y libadura, ni jachule un palaoan, ya janaatog gui tres medidan arina, asta qui todo manespongja.
Ni kama chachu aliyoitwaa mama mmoja na kuichanganya pamoja na unga debe moja kisha unga wote ukaumuka wote.”
22 Ya jumajanao gin chalaña, malag y siuda sija, yan y sengsong mamananagüe, ya jumajananao para Jerusalem.
Yesu alindelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri.
23 Ya ilegña uno nu güiya: Señot, didide manmasatba? si Jesus ilegña nu sija,
Mtu mmoja akamwuliza, “Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?”
24 Guefprocura mangejalom gui maiot na potta; sa jusangane jamyo na megae prumocucura mangejalom, lao ti mansiña.
Yesu akawaambia, “Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.
25 Yanguin y magas y guima jayasja cajulo ya jajuchom y petta, ya intitujon jamyo manmanojgue gui sumanjiyong ya inyajo y petta, ya ilegmi miyo: Señot, babayejam: ya ufanope ya ualog nu jamyo: Ti jutungo manguinemano jamyo:
“Wakati utakuja ambapo mwenye nyumba atainuka na kufunga mlango. Ninyi mtasimama nje na kuanza kupiga hodi mkisema: Bwana, tufungulie mlango. Lakini yeye atawajibu: Sijui mmetoka wapi.
26 Ya intitujon umalog: Guinin mañochojam yan manguimenjam gui menamo, yan mamanagüe jam gui cayenmame.
Nanyi mtaanza kumwambia: Sisi ndio wale tuliokula na kunywa pamoja nawe; na wewe ulifundisha katika vijiji vyetu.
27 Lao güiya ualog: Jusangane jamyo, na ti jutungo manguinemano jamyo: fañuja guiya guajo, todos jamyo ni y chumogüe y tinaelaye.
Lakini yeye atasema: Sijui ninyi mmetoka wapi; ondokeni mbele yangu, enyi nyote watenda maovu.
28 Ya ayonae uguaja cumasao, yan chegcheg nifen, yanguin inlie si Abraham, yan si Ysaac, yan si Jacob, yan todo y profeta sija, gui raenon Yuus; ya jamyo infanmachoneg juyong.
Ndipo mtakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo, na manabii wote wapo katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mmetupwa nje!
29 Ya ufanmato manguinen y sancatan yan y sanlichan, yan y sanlago yan y sanjaya; ya ufanmatachong gui raenon Yuus.
Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini, watakuja na kukaa kwenye karamu katika Ufalme wa Mungu.
30 Ya estagüe na guaja manuttimo ya ufanfinenana, y guaja manfinenana ya ufanuttimo.
Naam, wale walio wa mwisho watakuwa wa kwanza; na wale walio wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
31 Ya ayo na ora, manmato Fariseo sija ya ilegñija nu güiya: Janao ya unsuja güine; sa malago si Herodes na unpinino.
Wakati huohuo, Mafarisayo na watu wengine walimwendea Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine, kwa maana Herode anataka kukuua.”
32 Ya ilegña nu sija: Janao, sangane ayo na sora, na estagüe, na juyute juyong y anite sija, yan manaamteyo pago na jaane yan agupa, ya y mina tres na jaane ufonjayanyo.
Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie huyo mbweha hivi: Leo na kesho ninafukuza pepo na kuponya wagonjwa, na siku ya tatu nitakamilisha kazi yangu.
33 Lao nesesita jufamocat pago yan agupa yan y inagpaña, sa ti siña na ufalingo y profeta gui Jerusalem.
Hata hivyo, kwa leo, kesho na kesho kutwa, ni lazima niendelee na safari yangu, kwa sababu si sawa nabii auawe nje ya Yerusalemu.
34 O Jerusalem! Jerusalem! ni y unpuno y profeta sija, yan unfagas ni acho ayo sija y manmatago para güiya! cuanto biaje malagoyo na junafandaña y famaguonmo, taegüije y ponidera janafandaña y poyitasña gui papa papaña, ya timalago jamyo!
“Yerusalemu! We Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, Lakini wewe umekataa.
35 Estagüe na manmapoluye jamyo ni y guimanmiyo taetaotao; ya jusangane jamyo: Ti inliiyo, asta qui mato ayo na tiempo anae inalog: Dichoso ayo y mamamaela ni y naan y Señot.
Haya, utaachiwa mwenyewe nyumba yako. Naam, hakika nawaambieni, hamtaniona mpaka wakati utakapofika mseme: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.”

< San Lucas 13 >