< San Juan 7 >

1 YA despues di manmalofan estesija, si Jesus jumanao para Galilea: ya ti malago mamocat guiya Judea, sa y Judio sija maaliligao güe para umapuno.
Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2 Ya estaba jijot y guipot y Judio sija, na mafanaan gupot tabetnaculo.
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3 Y mañeluña sija pot este na rason ilegñija nu güiya: Falofan güine, ya unjanao para Judea, para y disipulumo sija locue ujalie y chechomo sija ni unfatitinas.
Basi ndugu zake wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4 Sa taya ni uno, mamatitinas jafa na güinaja gui secreto, ya güiyaja mismo ualigao na umatungo gui publico. Yaguin unfatitinas este sija na güinaja, fanuejao gui tano.
Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu.”
5 Sa mañeluña sija locue ti majonggue güe.
(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6 Ayo nae si Jesus ilegña nu sija: Y tiempoco ti mafato trabia, lao y tiemponmiyo siempre esta listo.
Basi, Yesu akawaambia, “Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7 Y tano ti siña manchinatlie jamyo; lao guajo jachatlie, sa mannae yo testimonio pot güiya, na y chechoña manaelaye.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8 Jamyo infangajulo güine na gupot; guajo ti jucajulo güine na gupot; sa y tiempoco trabia ti macumple.
Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika.”
9 Ya anae munjayan jasangane estesija, sumaga trabia guiya Galilea.
Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10 Lao anae y mañeluña sija mangajulo; ayo nae güiya locue cumajulo gui guipot; ti gui publico, lao calang gui secreto.
Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11 Ayo nae y Judio sija maaliligao güe gui guipot; ya ilegñija: Manggue güe?
Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: “Yuko wapi?”
12 Ya guaja un dangculon gonggong entalo y linajyan taotao sija pot güiya; sa guaja ilegñija: Güiya mauleg na taotao; palo, ilegñija: Aje, lao jadadague y taotao sija.
Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.”
13 Lao ni uno umadingan gui publico pot güiya, sa manmaañao ni Judio sija.
Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14 Anae y entalo y guipot, cajulo si Jesus gui templo ya mamanagüe.
Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15 Enao muna y Judio sija manamanman ya ilegñija: Jafa muna jatungo este letra na ti umeeyag?
Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?”
16 Maninepe as Jesus ilegña: Y finanagüeco, ti iyoco lao iyon ayo y tumago yo.
Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17 Yaguin guaja y mumalago fumatitinas y minalagoña, güiya utumungo y finanagüeco, cao güiya iyon Yuus, pat jusangan estesija na güinaja pot guajo namaesa.
Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18 Y umadingan pot güiyaja, ualiligao y minalagña namaesa; lao y umaligao y minalag iyon ayo y tumago güe, güiya magajet ya taya tinaelaye gaegue guiya güiya.
Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19 Ti manninae jamyo as Moises y tinago sija, ya taya uno guiya jamyo cumumple ya tinago sija? Sajafa na inprocucura para inpino yo?
Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
20 Y linajyan taotao manmanope: Anite guaja guiya jago! Jaye promucucuraja pumano jao?
Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
21 Manope si Jesus ya ilegña: Un chocho guajo fumatinas, ya todo jamyo ninafanmanman.
Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22 Pot este si Moises manninae jamyo ni y circunsision (na ti guine as Moises lao iyon y tata sija), ya asta pago gui sabado incircunsida y taotao.
Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23 Yaguin y taotao resibe gui sabado y circunsision, para ti umapoca y tinagon Moises; manbubo jamyo nu guajo, sa junasenguefjomlo un taotao gui sabado na jaane?
Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24 Chamiyo injisga taemanoja y liniinmiyo, lao injisga taemanoja y cabales na juisio.
Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
25 Ylegñija locue palo gui taotao Jerusalem: Ti güiya este y manmaliligao para upuno.
Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26 Ya lie na umadingan jafa malagoña, ya taya sumangan jafa nu güiya. Siña na y magalaje sija jatungo magajet, na este si Cristo?
Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27 Lao jita tumungo este na taotao, guine mano güe: ya anae mato si Jesucristo, taya uno tumungo taotao mano.
Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!”
28 Si Jesus entonses umagang gui. templo anae mamananagüe ilegña: Jamyo intingo yo, jaye yo, yan intingo locue taotao mano yo; ya guajo mamaela ti pot guajoja: lao y tumago yo, güiya magajet, ya jamyo ti intingo güe.
Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29 Guajo tumungo güe, sa guine güiya yo, ya güiya tumago yo!
Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”
30 Japrocura sija para macone güe, lao taya uno mato canaeña guiya güiya, sa y oraña trabia ti mafato.
Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31 Ya megae gui linajyan taotao jumonggue güe, ya ilegñija: Ada yaguin si Cristo mamaela, ujafatinas mas megae na señat qui y fumatiñas este na taotao?
Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”
32 Y Fariseo sija jumungog na y linajyan taotao manafaesen pot estesija, ya y manmagas mamale yan y Fariseo sija manmanago ni ofisiatñija para umacone.
Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33 Enaomina si Jesus ilegña: Trabia didide na tiempo gaegue yo guiya jamyo, ya despues bae falag ayo y tumago yo.
Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34 Ynaligao yo, ya ti inseda yo; ya mano nae gaegue yo, jamyo ti siña manmamaela.
Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika.”
35 Entonses y Judio sija ilegñija entre sijaja: Para mano este, para ti siñajit tasoda güe? Mapos buente para y manmachapon sija anae mangaegue sija gui entalo y Griego sija, ya mamnanagüe ni y Griego sija?
Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36 Jafa na sinangan na ayo y esta masangan: Inaligao yo ya ti inseda yo, ya mano nae gaegue yo, jamyo ti siña manmamaela.
Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?”
37 Y uttimo na jaane, dangculo na jaanin gupot, si Jesus tumojgue, ya umagang ilegña: Yaguin y taotao guaja minajo umamaela guiya guajo, ya uguinem.
Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38 Ya y jumonggueyo, taegüije y sinangan y Tinigue: y sanjalomña manmimilalag y sadog janom na lalâlâ.
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!”
39 Jasangan este na sinangan pot y Espiritu, ni para uresibe ayo sija y manmanjonggue guiya güiya: sa trabia taya mananae ni Espiritu Santo, sa si Jesus ti rumesibe y minalagña,
(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40 Entonses palo gui linajyan taotao, manmanjungog nu este na sinangan, ilegñija: Sumenmagajet na este güiya y ayo na profeta.
Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
41 Y palo ilegñija: Este güiya si ayo na Cristo: Y palo despues ilegñija: Jafa? guinin Galilea umamaela si Cristo?
Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42 Ti ilelegña y Tinigue, na si Cristo mamaela gui semiyan David, yan guinin y sengsong iya Betlehem anae sumaga si David?
Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
43 Ya guaja inaguguat gui entalo linajyan taotao pot güiya.
Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44 Ya guaja guiya sija y manmalago na ujacone, lao taya uno siña minajalom canaeña guiya güiya.
Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45 Ayonae y ofisiat sija manmalag y magas na mamale yan y Fariseo sija; ya ilegñija nu sija: Sajafa muna ti inchile güe mague?
Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”
46 Y ofisiat sija manmanope: Taya na taotao umadingan taegüine.
Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!”
47 Entonses y Fariseo sija maninepe: Jamyo locue manabag gui chalan?
Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48 Ada guaja palo y jumonggue güe gui magalaje sija pat y Fariseo sija?
Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49 Este sija na linajyan taotao ni ti jatungo y tinago sija, manmatdito.
Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!”
50 Ylegña nu sija si Nicodemo (ayo y mato gui as Jesus antes güiya uno guiya sija),
Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51 Manjujusga un taotao y iyota na tinago, yaguin y finenana ti majungog guiya güiya ya matungo jafa y finatinasña?
“Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?”
52 Manmanope ya ilegñija nu güiya: Jago locue taotao Galilea? Aligao, ya unlie, cao guine Galilea taya nae cajulo profeta.
Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!”
53 Manalo guato cada uno gui guimañija.
Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;

< San Juan 7 >