< San Juan 4 >

1 ANAE y Señot jatungo, na Fariseo sija manmanjungog, na si Jesus jafatinas disipuluña ya jatagpange megaeña qui si Juan.
Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2 (Achogja ti si Jesus namaesa matagpange, lao y disipuluñaja),
(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3 Jadingo guiya Judea, ya mapos talo malag Galilea.
Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4 Ya janesesita na umalofan inanaco Samaria.
na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5 Mato pues gui un siudan Samaria, na mafanaan Sicar, jijot gui fangualuan na si Jacob janae si José, lagiña.
Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6 Ya gaegue güine y tipo Jacob. Enaomina si Jesus, sa yayas güe guinin y chalan, matachong gui oriyan y tipo. Güenao na ora cana a las saes.
Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 Mato un palaoan Samaria para ufanlupog janom; ya si Jesus ilegña nu güiya: Naeyo ya juguinem.
Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.”
8 Sa y disipuluña manmapos para y siuda, para ufanmamajan nengcano.
(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 Ylegña nu güiya y palaoan Samaria: Jaftaemano na jago y Judio jao, ya untagojit najunaguinemjao, ya guajo palaoan Samaria? (Sa y Judio sija ti manatungo yan y taotao Samaria).
Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10 Manope si Jesus, ya ilegña nu güiya: Yaguin untungo y ninaeña si Yuus yan jaye güe y sumangane jao, naeyo ya juguinem: jago ungagao güe ya güiya unninae janom lalâlâ.
Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”
11 Ya y palaoan ilegña nu güiya: Señot, taya siña unlupog, sa y tipo tadong: amano pues nae guaja jao ni y janom lalâlâ.
Huyo mama akasema, “Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12 Ada dangculoña jao qui y tatanmame as Jacob, ni y numaejam nu este na tupo, ya güiya gumiguinem yan famaguonña, yan y gaña gâgâ sija?
Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
13 Manope si Jesus, ya ilegña nu güiya: Jaye y guminem nu este na janom, güiya umajo talo.
Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14 Lao ayo y guminem uje na janom y junae güe, para todo y tiempo ti umajo; ya ayo na janom y guajo junae güe, güiya y janom tupo, ni jumuyong para linâlâ na taejinecog. (aiōn g165, aiōnios g166)
Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 Ylegña nu güiya y palaoan: Señot, naeyo nu este na janom para ti siñayo majo, ni jutalo mague para jufanlupog.
Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
16 Si Jesus ilegña nu güiya: Janao agange y asaguamo, ya unmamaela güine mague.
Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
17 Manope y palaoan ya ilegña nu güiya: Taya asaguajo. Ylegña nu güiya si Jesus: Mauleg sinanganmo na ilegmo. Taya asaguajo.
Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
18 Sa sinco jagas asaguamo; ya pago y gaegue guiya jago, ti güiya y asaguamo: este unsangan pot minagajet.
Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
19 Ya ilegña nu güiya y palaoan: Señot, pineloco nu jago, profeta jao.
Huyo Mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20 Y tatanmame manmanadodora güine gui jalomtano, ya jamyo ilegmiyo, na iya Jerusalem, ayo na lugat, siempre nae umafatinas y adorasion.
Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu.”
21 Ylegña nu güiya si Jesus: Palaoan, jonggue yo sa ufato y ora, na ti este na jalomtano, ni iya Jerusalem, inadora jamyo si Yuus Tata.
Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 Jamyo inadora ti intingo. Jame inadora y tiningomame, sa y satbasion y Judio sija güiya.
Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 Lao y jaane umamaela, ya güiya güe pago, nae y magajet na manmanadododora, uje adodora si Yuus Tata gui espiritu yan y minagajet; sa si Yuus Tata, locue jaaliligao ayo sija y umadodora güe.
Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24 Si Yuus, güiya Espiritu, ya y umadora güe, siempre jaadora güe y espiritu yan y minagajet.
Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake.”
25 Ylegña nu güiya y palaoan: Guajo jutungo na y Mesias umamaela (ayo y naanña si Cristo); yaguin mato güe, güiya ufanagüejit todo.
Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
26 Ylegña nu güiya si Jesus: Guajoyo, ni umadingangane jao.
Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
27 Ya pot este manmato y disipuluña ya ninafanmanman pot y umadingan yan y palaoan: ya ni uno siña umalog: Jafa finaesesenmo? pat, pot jafa uncuentutuse güe?
Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
28 Taegüenao y palaoan japolo y batdeña, ya mapos malag y siuda, jasangane y taotao sija ya ilegña:
Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29 Fanmamaela ya inlie un taotao ni sumangane yo todo y finatinaso! Güiya buente si Cristo?
“Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
30 Manmapos gui siuda, ya manmalag as Jesus.
Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31 Ayo na tiempo magagagao güe ni disipulo sija, ilegñija: Rabi, chocho!
Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
32 Ya güiya ilegña na sija: Guaja najo nengcano na jamyo ti intingo.
Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 Enaomina y disipulo sija ilegñija entre sija: Buente guaja chumulilie naña?
Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
34 Si Jesus ilegña nu sija: Y nengcanojo y jufatinas y minalago ayo y tumago yo, ya magpo chechoña.
Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35 Ya ti ilegmiyo: Guaja trabia cuatro na meses nae ufato y quineco? Estagüe na jusangane jamyo: Fanalagquilo y matanmiyo ya inatan y fangualuan sija, sa esta manapaca para quineco.
Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36 Ya y mangoco uresibe y apasña, ya uchule y tinegcha para taejinecog na linâlâ; para ayo y mangoco, ya ayo y manananom mandaña gui minagof. (aiōnios g166)
Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 Ya pot este macumple y sinangan: uno manananom ya y otro mangongoco.
Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38 Guajo jamyo tumago para infanmangoco ya ti jamyo chumogüe; otro manmachocho ya jamyo manjalom gui chechoñija.
Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
39 Ya megae na taotao Samaria, taotao güije na siuda, manmanjonggue nu güiya pot y sinangan y palaoan, sa manae testimonio na ilegña: Jasangane yo todo ni y finatinasjo.
Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.”
40 Enao mina anae y taotao Samaria manmato guiya güiya, magagao na usaga ya ufandaña; ya güiya sumaga güije dos na jaane.
Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41 Ya y manmanjonggue nu güiya gofmegae pot y sinanganña.
Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42 Ya ilegñija nu y palaoan: Pago ti pot y finomo na injenggue; sa jame mismo injingog güe, ya intingo na este, güiya y magajet na Salvadot y tano.
Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
43 Ya depues di dos na jaane, jumanao güije ya malag Galilea.
Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44 Potjafa na si Jesus mismo manae testimonio, na y profeta gui tanoña taya onraña.
Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.”
45 Ya pot este anae malag Galilea, y taotao Galilea maresibe güe sa malie todo y finatinasña guiya Jerusalem, na jafatinas gui tiempo y guipot; sa sija locue manmalag y guipot.
Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46 Mato, otro biaje, si Jesus, guiya Cana siuda guiya Galilea, nae y jafatinas bino y janom: ya guaja güije un magalaje na y lajiña malango guiya Capernaum.
Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47 Ya anae jajungog na si Jesus, jumanao gui Juda ya tumunog para Galilea, mapos güe malag as Jesus, ya jagagao na utunog guiya Capernaum, ya uamte y lajiña, sa esta cumequematae.
Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48 Enao mina si Jesus ilegña nu güiya: Yaguin ti inlie señat sija, yan y ninamanman sija, ti injenggue.
Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”
49 Ya ilegña y magalage nu güiya: Señot, tunog lasajyao, antes qui umatae y lajijo!
Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.”
50 Ylegña si Jesus nu güiya: Janao, sa y lajimo lâlâ! Jajonggue y taotao y sinangan Jesus ni y sinangane güe, ya mapos.
Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao yu mzima.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51 Ya anae güiya tumutunog, y familiaña matagam güe ya masangane na ilegñija, Na y lajimo lâlâ!
Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52 Mamaesen jafa na ora y lajiña na mumauleg, ya ilegñija: Nigap gui las siete na ora pinelo ni calenturaña.
Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.”
53 Jatungo y tataña enao na ora nae sinangane güe as Jesus, Y lajimo lâlâ; ya güiya namaesa jajonggue yan todo y familiaña!
Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao yu mzima.” Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54 Este y mina dos na señat, na jafatinas si Jesus, anae jinanaoña guiya Judea, para Galilea.
Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.

< San Juan 4 >