< Lucas 3 >

1 Y andré a berji pansch-decima e imperio de Tiberio Cæsar, sinando Poncio Pilato Chino baro de Judea, y Herodes Tetrarchâ de Galiléa, y desquero plano Philipo Tetrarchâ de Ituréa, y e chim de Trachônite, y Lysanias Tetrarchâ de Abilina,
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
2 Sinando Manclayes es erajais Annás y Caiphas, abilló a varda e Erañoró opré Juan, chaboro de Zacharias, andré o desierto.
nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
3 Y abilló por saro o chim de Jordan garlando o muchobelar de penitencia somia mecos de grecos,
Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
4 Sasta sinela randado andré o embéo de las vardas de Isaias Propheta: Gole de yeque garlando andré ó desierto: Aparejad o drun e Erañoró, Querelad bustarias as sendas de ó.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
5 Saro butron se perelará; y saro bur y plai se pejerá: y o torcido sinará enderezado: y os drunes fragosos allanados:
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
6 Y dicará sari maas a golipen de Debél.
Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
7 Y penó á os manuces, que abillaban somia que los muchobelase: ¿Rati de birbirechas, coin penó á sangue á najar de la ira que ha de abillar?
Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
8 Querelad pues mibao cabalico de penitencia, y na os chitelais penar: Terelamos por batu á Abraham. Porque sangue penelo, que astisarela Debél de oconas barendañías ardiñar chabores á Abraham.
Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
9 Presas acana sinela chibada a tescharí á la raiz es carschtas, pues sari carschta, sos na diñele mibao lacho, sinará velada, y chibada andré a yacque.
Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
10 Y le puchababan os manuces, y penaban! ¿Pues qué querelaremos?
Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
11 Y rudelando les penaba: O manu sos terela duis coneles, díñele al manu sos na terela: y o sos terela que jamar, querele o matejo.
Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Y abilláron tambien á ó os Publicanes, somia que os muchobelase, y le penáron: ¿Duquendio, qué querelaremos?
Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
13 Y ó les penó: Na ustileis butér de ma os sinela penado.
Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
14 Le puchababan tambien os jundunares, penando: ¿Y mu qué querelaremos? Y les penó: Na queraleis choro á cayque, ni le mareleis, y sineleis lacho sat jiré jayere.
Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
15 Y sasta os manuces creyesen, y os sares penchabasen andré desqueres carlochines, si por ventura Juan sinaba o Christo:
Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
16 Rudeló Juan, y penó á os sares: Menda aromali muchobelo sangue andré paní: Tami abillará avér butér silnó que menda, de coin na sinelo cabalico de despandar a correa de desqueres tirajais: ocola muchobelará sangue andré Peniche, y yaque:
Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 De coin o bieldo sinela andré su baste; y alimpiará desquero era, y chibará ó gi andré su malabai, y la pus jachará sat yaque, que na se bedela.
Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
18 Y andiar anunciaba averias baribustrias buchias á la sueti andré sus exhortaciones.
Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
19 Tami Herodes ó Tetrarchâ; sinando reprehendido por ó á causa de Herodias romi de sun planó, y de sarias as buchias chorias que Herodes habia querdi,
Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
20 Anadio á sares tambien ocona de querelar pandar a Juan andré la estaripel.
Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
21 Y anacó, que sasta sari a sueti ustilase o muchobelar, tambien sinaba muchobelado Jesus; y sinando ó manguelando á Debél, se despandó o Tarpe:
Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
22 Y pejó ostely opre ó el Peniche andré trupo, sasta gobaró: y se juneló ocono gole del Tarpe: Tucue sinelas minrió Chaboro camelado; andré tucue menda me alendelo.
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
23 Y o Jesus comenzaba a terelar sasta de sinebo berjis, chaboro y segun se penelaba, de Joseph, chaboro de Heli, chaboro de Mathat,
Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
24 Chaboro de Leví, chaboro de Melchi, chaboro de Janne, chaboro de Joseph,
Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
25 Chaboro de Mathathias, chaboro de Amos, chaboro de Nahum, chaboro de Hesli, chaboro de Nagge,
Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
26 Chaboro de Mahath, chaboro de Mathathias, chaboro de Semei, chaboro de Joseph, chaboro de Judá,
Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
27 Chaboro de Joanna, chaboro de Resa, chaboro de Zorobabél, chaboro de Salathiel, chaboro de Neri,
Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
28 Chaboro de Melchi, chaboro de Addí, chaboro de Cosán, chaboro de Helmadan, chaboro de Her,
Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
29 Chaboro de Jesus, chaboro de Eliezer, chaboro de Jorim, chaboro de Mathat, chaboro de Levi,
Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
30 Chaboro de Simeón, chaboro de Júdas, chaboro de Joseph, chaboro de Jonás, chaboro de Eliakim,
Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
31 Chaboro de Melea, chaboro de Menna, chaboro de Mathatha, chaboro de Nathán, chaboro de David,
Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
32 Chaboro de Jessé, chaboro de Obed, chaboro de Booz, chaboro de Salmon, chaboro de Naasson,
Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
33 Chaboro de Aminadab, chaboro de Arám, chaboro de Esron, chaboro de Pharé, chaboro de Judas,
Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
34 Chaboro de Jacob, chaboro de Isaac, chaboro de Abraham, chaboro de Thares, chaboro de Nachor,
Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
35 Chaboro de Sarug, chaboro de Regau, chaboro de Phaleg, chaboro de Heber, chaboro de Salé,
Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
36 Chaboro de Cainán, chaboro de Arphaxad, chaboro de Sem, chaboro de Noé, chaboro de Lamech,
Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
37 Chaboro de Mathusalé, chaboro de Henoch, chaboro de Jared, chaboro de Malaleel, chaboro de Cainan,
Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
38 Chaboro de Henos, chaboro de Seth, chaboro de Adám, sos fué chaboro de Un-debél.
Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.

< Lucas 3 >