< Лука 2 >

1 О Но ангелът им рече: Не бойте се, защото, ето, благовестявам ви голяма радост, която ще бъде за всичките люде.
Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2 Това беше първото записване, откакто Квириний управляваше Сирия.
Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
3 И всички отиваха да се записват, всеки в своя град.
Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
4 И тъй, отиде и Йосиф от Галилея, от града Назарет, в Юдея, в Давидовия град, който се нарича Витлеем, (понеже той беше от дома и рода Давидов),
Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
5 за да се запише с Мария, която беше сгодена за него и беше непразна.
Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
6 И когато бяха там, навършиха се дните - да роди.
Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
7 И роди първородния си Син, пови Го, и положи Го в ясли, защото нямаше място за тях в страноприемницата.
akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
8 И на същото място имаше овчари, които живееха в полето, и пазеха нощна стража около стадото си.
Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
9 И ангел от Господа застана пред тях, и Господната слава ги осия; и те се уплашиха много.
Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
10 Но ангелът им рече: Не бойте се, защото, ето, благовестявам ви голяма радост, която ще бъде за всичките люде.
Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
11 Защото днес ви се роди в Давидовия град Спасител, Който е Христос Господ.
Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
12 И това ще ви бъде знакът: ще намерите Младенец, повит и лежащ в ясли.
Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
13 И внезапно, заедно с ангела, се намери множество небесно воинство, което хвалеше Бога, казвайки:
Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
14 Слава на Бога във висините. И на земята мир между човеците, в които е Неговото благоволение.
“Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
15 Щом ангелите си отидоха от тях на небето, овчарите си рекоха един на друг: Нека отидем тогава във Витлеем, и нека видим това, що е станало, което Господ ни изяви.
Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
16 И дойдоха бързо и намериха Мария и Йосифа, и Младенеца лежащ в яслите.
Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
17 И като видяха, разказаха каквото им беше известено за това детенце.
Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
18 И всички които чуха, се зачудиха за това, което овчарите им казаха.
Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
19 А Мария спазваше всички тия думи и размишляваше за тях в сърцето си.
Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
20 И овчарите се върнаха, славещи и хвалещи Бога за всичко, що бяха чули и видели, според както им беше казано.
Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
21 И като се навършиха осем дни и трябваше да обрежат Детенцето, дадоха Му името Исус, както беше наречено от ангела преди да е било зачнато в утробата.
Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
22 Като се навършиха и дните за очистването им, според Мойсеевия закон, занесоха Го в Ерусалим за да Го представят пред Господа,
Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
23 (както е писано в Господния закон, че всеки първороден младенец от мъжки пол ще бъде свят на Господа),
Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
24 и да принесат жертва според казаното в Господния закон две гургулици и две гълъбчета.
Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
25 И ето, имаше в Ерусалим един човек на име Симеон; и тоя човек бе праведен и благочестив, и чакаше утехата на Израиля; и Святият Дух беше в него.
Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
26 Нему бе открито от Святия Дух, че няма да види смърт, докле не види Христа Господен.
Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
27 И по внушението на Духа той дойде в храма; и когато родителите внесоха детенцето Исус, за да сторят за Него по обичая на закона,
Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
28 той Го взе на ръцете си и благослови Бога, като каза:
Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
29 Сега, Владико, отпущаш слугата Си в мир, според думата си;
“Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30 защото видяха очите ми спасението,
Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
31 което си приготвил пред всички люде;
ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
32 светлина да просвещава народите. И слава на Твоите люде Израил.
Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
33 А баща Му и майка Му се чудеха на това, което се говореше за Него.
Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
34 И Симеон го благослови, и рече на майка Му Мария: Ето, това детенце е поставено за падане и за ставане на мнозина в Израиля, и за белег, против който ще се говори.
Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
35 Да! И на сама тебе меч ще прониже душата ти, за да се открият помислите на много сърца.
na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
36 Имаше и някоя си Анна, Фануилова дъщеря, от Асировото племе; (тя беше в много напреднала възраст, като бе живяла с мъжа си седем години от девството си.
Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
37 И беше вдовица за цели осемдесет и четири години), която не се отделяше от храма, дето нощем и денем служеше Богу в пост и молитва.
Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
38 И тя, като се приближи, в същия час, благодареше Богу, и говореше за Него на всички, които ожидаха изкуплението на Ерусалим.
Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
39 И като свършиха всичко, що беше според Господния закон, върнаха се в Галилея, в града си Назарет.
Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
40 А Детенцето растеше, крепнеше, и се изпълваше с мъдрост; и Божията благодат бе на Него.
Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
41 И родителите Му ходеха всяка година в Ерусалим за празника на Пасхата.
Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42 И когато Той беше на дванадесет години, като отидоха по обичая на празника,
Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43 и като изкараха дните и се връщаха, Момчето Исус остана в Ерусалим, без да знаят родителите Му.
Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
44 А те, понеже мислеха, че Той е с дружината, изминаха един ден път, като Го търсеха между роднините и познатите си.
Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
45 И като не Го намериха, върнаха се в Ерусалим и Го търсеха.
Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
46 И след три дни Го намериха в храма, седнал между законоучителите, че ги слушаше и ги запитваше.
Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 И всички, които Го слушаха, се учудваха на разума Му и на отговорите Му.
Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
48 И като Го видяха, смаяха се; и рече Му майка Му: Синко, защо постъпи тъй с нас? Ето, баща Ти и аз, наскърбени, Те търсехме.
Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
49 А Той им рече: Защо да Ме търсите? Не знаете ли, че трябва да се намеря около дома на Отца Ми?
Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
50 А те не разбраха думата, която им рече.
Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
51 И Той слезе с тях, и дойде в Назарет, и там им се покоряваше. А майка Му спазваше всички тия думи в сърцето си.
Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
52 А Исус напредваше в мъдрост, в ръст и в благоволение пред Бога и човеците.
Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.

< Лука 2 >