< Luka 15 >

1 La yuwak nob merangkab kange nob yoka kemer doreko bouti Yeecu nen cin nuwacoti.
Siku moja, watoza ushuru na wahalifu wengi walikwenda kumsikiliza Yesu.
2 Farisawa kange nob mulangka bo cima fwenati bwitici ciki” Niwo yo nob bwirangkebti ci ca caitoti waritak.
Mafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunung'unika: “Mtazameni mtu huyu! Anawakaribisha wenye dhambi, na tena anakula nao.”
3 Yeecu tok danke wo yici.
Yesu akawajibu kwa mfano:
4 Canno kange kume ki kwame kumi kwo lawin more ce lem, mani ca dob kwini Teer culombo teere ti naci bwanten meka wuro win lemeu naci fiyam.
“Hivi, mtu akiwa na kondoo mia, akigundua kwamba mmoja wao amepotea, atafanya nini? Atawaacha wale tisini na tisa mbugani, na kwenda kumtafuta yule aliyepotea mpaka ampate.
5 Tano ci fiyam ri naci tuu ci yaken Lagwamcem ci no fuwor nerer tiye.
Akimpata, atambeba mabegani kwa furaha.
6 No ci yilaudi naci cwo farubcebo kange nubo biom kange ceu, naci yici, kom ti kanye fuwor nerer min fiya kwame mi lemeu.
Anapofika nyumbani, atawaita rafiki zake akiwaambia, Furahini pamoja nami, kwa sababu nimempata yule kondoo wangu aliyepotea.
7 Miyikomti nyo a ma fuwor nerer tiye dii kwama don ni bwiranker win kange nobo kiner luma kwini taar culombo teereu wuro dobo ywelka bwirange keu cereu.
Kadhalika nawaambieni, ndivyo kutakavyokuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya kutubu kwa mwenye dhambi mmoja, kuliko kwa ajili ya watu tisini na tisa wanaojiona kuwa wema, wasiohitaji kutubu.
8 Kaka we nawiye, ki kemer nai nyo kwob no lemdi manica wentalkire ti ci nyina yum mor kuwe la citi doi naci fiyam me?
“Au mwaonaje? Tuseme mwanamke fulani ana sarafu kumi za fedha, akipoteza moja, atafanya nini? Atawasha taa, aifagie nyumba na kuitafuta kwa uangalifu mpaka aipate.
9 Noci fiyam laci mwer farubcebo kange nubo bidom kange ceu ciyicii kom tikanye fuwor nerer min fiyam kwame meu.
Akiipata, atawaita rafiki na jirani zake akisema, Furahini pamoja nami, kwa sababu nimeipata ile sarafu yangu iliyopotea.
10 Nyo mi yi komtiye, diker fuwer nerer nob tomangeb kwamab cano, ni bwinrangke winn dob bwirangkerori.
Kadhalika nawaambieni, ndivyo watakavyofurahi malaika wa Mungu kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja anayetubu.”
11 La Yeecu yici “Ni kange wi ki bibei bayilob yob.
Yesu akaendelea kusema, “Kulikuwa na mtu mmoja mwenye wana wawili.
12 La bi duwareu yi teece Tee neye miu kwalito mor cuweka mwekonin. Dila Tee ce kabkamm cinen kwalito.
Yule mdogo, alimwambia baba yake: Baba, nipe urithi wangu. Naye akawagawia mali yake.
13 Ki Kumeni kilabori dila bwe biduware murance kwalito yaken biti kange katangi. cin yakcangum kwalito tie nen bikulentiti yakcangum kemero cero noranka diker.
Baada ya siku chache, yule mdogo aliuza urithi wake, akasafiri na fedha aliyopata, akaenda nchi ya mbali ambako aliitumia ovyo.
14 Kambo ci yakcangum kwalitori la cin ma wura kambo ken bitine con ni lam doken bwini.
Alipomaliza kutumia kila kitu, kukatokea njaa kali katika nchi ile, naye akaanza kuhangaika.
15 Yacin neken dorcero nangen ni kange bitineco, la twamom mor tangini ce nacinen Bilerce cariti.
Akaomba kazi kwa mwananchi mtu mmoja wa huko naye akampeleka shambani mwake kulisha nguruwe.
16 La cin cari ca do dike bilerece a catiyeu, wori ni kange mani neco cariti.
Alitamani kula maganda waliyokula wale nguruwe, ila hakuna mtu aliyempa kitu.
17 Dila kambo yulancero bwiceri yice ki cnga Tee mi cingile cike cari la cinnen bo dila mi fo ma bwiyati ka ker carity.
Alipoanza kupata akili akafikiri: Mbona kuna wafanyakazi wengi wa baba yangu wanaokula na kusaza, nami ninakufa njaa?
18 Man kweni neken Tee mi in yico “Tee Min ma dikwanin bwirainke min kangmwen.
Nitarudi kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia.
19 Ma datenbo coya muki bibwemiri yokenye min yilam win mor cangabtinim mweb?”.
Sistahili hata kuitwa mwanao. Nifanye kama mmoja wa wafanyakazi wako.
20 Lacin kweni, cibou tecemin. Dila kambo ci kutanneri, la Tee ce tomco cibwini ceto yaki cwak, yan bwabco, lata macinen cuika.
Basi, akaanza safari ya kurudi kwa baba yake. Alipokuwa bado yu mbali, baba yake alimwona, na kwa moyo wa huruma alimkimbilia, akamkumbatia na kumbusu.
21 Bweu inyico Tee, mi ma dii kwama nen bwiranke, min kangum mwen. ma labo coten ye muki bi bwemwe.
“Mwanawe akamwambia: Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia. Sistahili hata kuitwa mwanao.
22 Di la Teece yi cangab cebo, kom bouki bellewo yor yoreu, kom ducinen kon dok cinen keneu kange cek kange ta nacek.
Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: Haraka! Leteni nguo nzuri mkamvike! Mvisheni pete na viatu!
23 la ko bou ki neneu mobiyeu kom biyem bima cenen bilengtum ciko.
Mchinjeni ndama mnono; tule kusherehekea!
24 Na weu bebwemi bwiyam fiyeco dila naweu yilau ki dume. Lem fiyeco dila fiyau. lacin teer cika.
Kwa sababu huyu mwanangu alikuwa amekufa, kumbe yu mzima alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana. Wakaanza kufanya sherehe.
25 Ki kwama co bibwece durko ki kambo dadom loweri cin nuwa ci kwaban dikerti kange nuwetinin.
“Wakati huo kaka yake alikuwa bado shambani. Alipokuwa akirudi na kukaribia nyumbani akasikia vifijo na ngoma.
26 Lacin com kange bwe canage loceu meco dikerowo mati loriyeu. neneu mob mobeu wori cin yilau lo kwamer.
Akamwita mmoja wa watumishi, akamwuliza: Kuna nini?
27 Bwe cangau yico kemwe yilau lowe, Tee mwe biyem neneu cin yilau lo kwamer.
Huyo mtumishi akamwambia: Ndugu yako amerudi nyumbani, na baba yako amemchinjia ndama mnono kwa kuwa amempata akiwa salama salimini.
28 Di la kece bwe durko mam funer ko do kako mor luwe Tee ce ceriu kale kinang co.
Huyo kijana mkubwa akawaka hasira hata akakataa kuingia nyumbani. Baba yake akatoka nje na kumsihi aingie.
29 Bwe durko ciyace Tee ce ki to ka cotiyowo mi ari kange mo ki komwem bo tomange nii wucak kange wo mune yob be nibeni wo ma cati kange farub mibeu.
Lakini yeye akamjibu: Kumbuka! Miaka yote nimekutumikia, sijavunja amri yako hata mara moja. Umenipa nini? Hujanipa hata mwana mbuzi mmoja nikafanye sherehe pamoja na rafiki zangu!
30 Di la bwe wuro ya cutang bicir mwer dor mun biye cinen kalnenero mob mo bo.
Lakini mtoto wako huyu aliyekula mali yako pamoja na makahaba, mara tu alipokuja umemchinjia yule ndama mnono.
31 Di la Teece yico ki “Bibwemi, mu wari kange mo gwam dikero na mi yeri na mwe.
Baba yake akamjibu: Mwanangu, wewe uko pamoja nami siku zote, na kila nilicho nacho ni chako.
32 Di la dong dong cimamwen luma kange fur nerer, wori kemwe wo buyam dila nawori ki dume, fiayco lem la nanweu, bin fiyam.
Ilitubidi kufanya sherehe na kufurahi, kwa sababu huyu ndugu yako alikuwa amekufa, kumbe yu mzima; alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana.”

< Luka 15 >