< المَزامِير 116 >
إِنِّي أُحِبُّ الرَّبَّ لأَنَّهُ يَسْمَعُ ابْتِهَالِي وَيَسْتَجِيبُ إِلَى تَضَرُّعَاتِي. | ١ 1 |
Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
أَمَالَ أُذُنَهُ إِلَيَّ لِذَلِكَ أَدْعُوهُ مَادُمْتُ حَيّاً. | ٢ 2 |
Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
طَوَّقَتْنِي حِبَالُ الْمَوْتِ. أَطْبَقَ عَلَيَّ رُعْبُ الْهَاوِيَةِ. قَاسَيْتُ ضِيقاً وَحُزْناً. (Sheol ) | ٣ 3 |
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol )
فَدَعَوْتُ الرَّبَّ: آهِ يَارَبُّ نَجِّ نَفْسِي! | ٤ 4 |
Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
الرَّبُّ حَنُونٌ وَبَارٌّ. إِلَهُنَا رَحِيمٌ. | ٥ 5 |
Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
الرَّبُّ حَافِظُ الْبُسَطَاءِ. تَذَلَّلْتُ فَخَلَّصَنِي. | ٦ 6 |
Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
عُودِي يَانَفْسِي إِلَى طُمَأْنِينَتِكِ، لأَنَّ الرَّبَّ قَدْ أَحْسَنَ إِلَيْكِ. | ٧ 7 |
Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
لأَنَّكَ يَارَبُّ أَنْقَذْتَ نَفْسِي مِنَ الْمَوْتِ، وَعَيْنِي مِنَ الدَّمْعِ، وَقَدَمَيَّ مِنَ التَّعَثُّرِ، | ٨ 8 |
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
لِذَلِكَ أَسْلُكُ بِطَاعَةٍ أَمَامَ الرَّبِّ فِي دِيَارِ الأَحْيَاءِ. | ٩ 9 |
ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
آمَنْتُ لِذَلِكَ تَكَلَّمْتُ. أَنَا عَانَيْتُ كَثِيراً. | ١٠ 10 |
Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
وَقُلْتُ فِي حَيْرَتِي: «جَمِيعُ الْبَشَرِ كَاذِبُونَ». | ١١ 11 |
Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
مَاذَا أَرُدُّ لِلرَّبِّ مُقَابِلَ كُلِّ مَا أَبْدَاهُ نَحْوي مِنْ حُسْنِ الصَّنِيعِ؟ | ١٢ 12 |
Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
سَأَتَنَاوَلُ كَأْسَ الْخَلاَصِ، وَأَدْعُو بِاسْمِ الرَّبِّ. | ١٣ 13 |
Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
أُوْفِي نُذُورِي لِلرَّبِّ أَمَامَ كُلِّ شَعْبِهِ. | ١٤ 14 |
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
عَزِيزٌ فِي عَيْنَي الرَّبِّ مَوْتُ قِدِّيسِيهِ. | ١٥ 15 |
Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
آهِ يَارَبُّ أَنَا عَبْدُكَ. أَنَا عَبْدُكَ وَابْنُ أَمَتِكَ. أَنْتَ حَلَلْتَ قُيُودِي. | ١٦ 16 |
Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
لَكَ أُقَدِّمُ ذَبَائِحَ الشُّكْرِ، وَأَدْعُو بِاسْمِكَ. | ١٧ 17 |
Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
أُوْفِي نُذُورِي لِلرَّبِّ أَمَامَ كُلِّ شَعْبِهِ. | ١٨ 18 |
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
فِي دِيَارِ بَيْتِ الرَّبِّ، فِي وَسَطِكِ يَاأُورُشَلِيمُ. هَلِّلُويَا. | ١٩ 19 |
katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.