< المَزامِير 116 >

إِنِّي أُحِبُّ الرَّبَّ لأَنَّهُ يَسْمَعُ ابْتِهَالِي وَيَسْتَجِيبُ إِلَى تَضَرُّعَاتِي. ١ 1
Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
أَمَالَ أُذُنَهُ إِلَيَّ لِذَلِكَ أَدْعُوهُ مَادُمْتُ حَيّاً. ٢ 2
Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
طَوَّقَتْنِي حِبَالُ الْمَوْتِ. أَطْبَقَ عَلَيَّ رُعْبُ الْهَاوِيَةِ. قَاسَيْتُ ضِيقاً وَحُزْناً. (Sheol h7585) ٣ 3
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
فَدَعَوْتُ الرَّبَّ: آهِ يَارَبُّ نَجِّ نَفْسِي! ٤ 4
Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
الرَّبُّ حَنُونٌ وَبَارٌّ. إِلَهُنَا رَحِيمٌ. ٥ 5
Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
الرَّبُّ حَافِظُ الْبُسَطَاءِ. تَذَلَّلْتُ فَخَلَّصَنِي. ٦ 6
Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
عُودِي يَانَفْسِي إِلَى طُمَأْنِينَتِكِ، لأَنَّ الرَّبَّ قَدْ أَحْسَنَ إِلَيْكِ. ٧ 7
Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
لأَنَّكَ يَارَبُّ أَنْقَذْتَ نَفْسِي مِنَ الْمَوْتِ، وَعَيْنِي مِنَ الدَّمْعِ، وَقَدَمَيَّ مِنَ التَّعَثُّرِ، ٨ 8
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
لِذَلِكَ أَسْلُكُ بِطَاعَةٍ أَمَامَ الرَّبِّ فِي دِيَارِ الأَحْيَاءِ. ٩ 9
ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
آمَنْتُ لِذَلِكَ تَكَلَّمْتُ. أَنَا عَانَيْتُ كَثِيراً. ١٠ 10
Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
وَقُلْتُ فِي حَيْرَتِي: «جَمِيعُ الْبَشَرِ كَاذِبُونَ». ١١ 11
Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
مَاذَا أَرُدُّ لِلرَّبِّ مُقَابِلَ كُلِّ مَا أَبْدَاهُ نَحْوي مِنْ حُسْنِ الصَّنِيعِ؟ ١٢ 12
Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
سَأَتَنَاوَلُ كَأْسَ الْخَلاَصِ، وَأَدْعُو بِاسْمِ الرَّبِّ. ١٣ 13
Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
أُوْفِي نُذُورِي لِلرَّبِّ أَمَامَ كُلِّ شَعْبِهِ. ١٤ 14
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
عَزِيزٌ فِي عَيْنَي الرَّبِّ مَوْتُ قِدِّيسِيهِ. ١٥ 15
Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
آهِ يَارَبُّ أَنَا عَبْدُكَ. أَنَا عَبْدُكَ وَابْنُ أَمَتِكَ. أَنْتَ حَلَلْتَ قُيُودِي. ١٦ 16
Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
لَكَ أُقَدِّمُ ذَبَائِحَ الشُّكْرِ، وَأَدْعُو بِاسْمِكَ. ١٧ 17
Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
أُوْفِي نُذُورِي لِلرَّبِّ أَمَامَ كُلِّ شَعْبِهِ. ١٨ 18
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
فِي دِيَارِ بَيْتِ الرَّبِّ، فِي وَسَطِكِ يَاأُورُشَلِيمُ. هَلِّلُويَا. ١٩ 19
katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< المَزامِير 116 >