< اَلْمَزَامِيرُ 82 >
مَزْمُورٌ لِآسَافَ ٱللهُ قَائِمٌ فِي مَجْمَعِ ٱللهِ. فِي وَسْطِ ٱلْآلِهَةِ يَقْضِي: | ١ 1 |
Mungu amesimama katika kusanyiko la mbinguni; katikati ya miungu anahukumu.
«حَتَّى مَتَى تَقْضُونَ جَوْرًا وَتَرْفَعُونَ وُجُوهَ ٱلْأَشْرَارِ؟ سِلَاهْ. | ٢ 2 |
Hata lini mtahukumu bila haki na kuonesha upendeleo kwa waovu? (Selah)
اِقْضُوا لِلذَّلِيلِ وَلِلْيَتِيمِ. أَنْصِفُوا ٱلْمِسْكِينَ وَٱلْبَائِسَ. | ٣ 3 |
Wateteeni maskini na yatima; dumisheni haki kwa aliyetaabishwa na fukara.
نَجُّوا ٱلْمِسْكِينَ وَٱلْفَقِيرَ. مِنْ يَدِ ٱلْأَشْرَارِ أَنْقِذُوا. | ٤ 4 |
Muokoeni maskini na muhitaji; watoeni mkononi mwa waovu.
«لَا يَعْلَمُونَ وَلَا يَفْهَمُونَ. فِي ٱلظُّلْمَةِ يَتَمَشَّوْنَ. تَتَزَعْزَعُ كُلُّ أُسُسِ ٱلْأَرْضِ. | ٥ 5 |
Hawajui wala hawaelewi; hutembea gizani; misingi yote ya nchi imebomoka.
أَنَا قُلْتُ: إِنَّكُمْ آلِهَةٌ وَبَنُو ٱلْعَلِيِّ كُلُّكُمْ. | ٦ 6 |
Mimi nilisema, “Ninyi ni miungu, na ninyi nyote wana wa Mungu aliye Juu.
لَكِنْ مِثْلَ ٱلنَّاسِ تَمُوتُونَ وَكَأَحَدِ ٱلرُّؤَسَاءِ تَسْقُطُونَ». | ٧ 7 |
Hata hivyo mtakufa kama wanadamu na mtaanguka kama mmoja wa wakuu.”
قُمْ يَا ٱللهُ. دِنِ ٱلْأَرْضَ، لِأَنَّكَ أَنْتَ تَمْتَلِكُ كُلَّ ٱلْأُمَمِ. | ٨ 8 |
Uinuke, Ee Mungu, uihukumu nchi, maana unaurithi katika mataifa yote.