< Roma 2 >

1 Bara nani idimun nimon inbellu ba, anugne anit, anung anan wusu nliru, imon irika na iwuso kitenen nmon, asa imusuzu natimine. Anugne na idinsu katuwan nwusuze anug wang din su imone.
Basi, rafiki, kama unawahukumu wengine, huwezi kamwe kujitetea haidhuru wewe ni nani. Kwa maana, kwa kuwahukumu wengine, unajilaani wewe mwenyewe kwa vile nawe unayafanya mambo yaleyale unayohukumu.
2 Arik nani tiyiru uwusuzu Kutelle kidenere, asa deu kitene nale na idin suzu imon ine.
Tunajua kwamba hukumu ya Mungu kwa wale wanaofanya mambo kama hayo ni hukumu ya haki.
3 Yene ilaimone, anung anit, ale na idin wusuzu among anan suzu nimon inanza anung din suze, ima chum ikata usuzu Kutelle?
Lakini wewe, rafiki, unayewahukumu wale wanaofanya mambo kama hayo bali wewe pia unayafanya, je unadhani utaiepa hukumu ya Mungu?
4 Sa anung din kpilizu imon ichine me chigilin, umolu kubi nin wusuzume, ayi asheume, na anuung yiru imon ichine me din wunu minu uchin dun deu nabunu meh ba?
Au labda unaudharau wema wake mkuu, uvumilivu wake na saburi yake, bila kutambua kwamba wema wake huo una shabaha ya kukuongoza upate kutubu?
5 Nani tutun, bara gbasminere nin salin ndisu nabunu nibinayi mine, idin chisu atimine tinannayi Kutelle liri tinannayi, lirin puzunu nimon ichine mawusuzu Kutelle.
Lakini unao ugumu na ukaidi wa moyo, na hivyo unajilundikia adhabu kwa Siku ile ambayo ghadhabu ya Mungu na hukumu zake za haki vitadhihirishwa.
6 Amma kurtunu kogha ku nin nilaimon na unite nbatamun katuwame:
Siku hiyo Mungu atamlipa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
7 inung ale na kitenen suzu nimon ichine sa ushizunu idin pizurun zazunu, ningogon, a upizuru nimon in salin nanuzu, ulai sa ligan. (aiōnios g166)
Wale wanaozingatia kutenda mema, kutafuta utukufu na heshima ya Mungu na kutokufa, watapata uzima wa milele. (aiōnios g166)
8 Ale tutun na idin pizuru liti, na inari udort kiden, ima di sa ulanzu feu Kutelle, natimine, tinanayi nin nayi ananza ma dak,
Lakini wale wengine wenye ubinafsi, wenye kukataa mambo ya haki na kufuata uovu, wataangukiwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
9 liguburi nin neu, ma yitu litin kogha na adin su imon inanzan, uchizunu nin kuyahudawa udu kiti kuwurmi.
Mateso na maumivu yatampata binadamu yeyote atendaye uovu. Yatawapata Wayahudi kwanza, na watu wa mataifa mengine pia.
10 Harnani uzazunu, ughantinu, nin lisosi limang ma dak kitin kogha na adin su imon ichine, uchizunu nin Kuyahudawa nin du kiti Kuwurmi.
Lakini Mungu atawapa utukufu, heshima na amani wale wanaotenda mema; Wayahudi kwanza, na watu wa mataifa mengine pia.
11 Bari nani, Kutelle din feru umong nbun nmong ba,
Maana Mungu hambagui mtu yeyote.
12 Vat narika na ina tizu alapi sa ushara, vat arika na idintizu nalapi kitenen nshara imasu ani uwusuzu nin shara.
Wale wanaotenda dhambi bila kuijua Sheria ya Mose wataangamia ingawaje hawajui Sheria. Na wale wanaotenda dhambi wakiwa wanaijua Sheria watahukumiwa kisheria.
13 Lanzan, na anan lanzu nliru Kutelleri anan feu me ba, arikana idin dortun nsharawere ma nuzu nan nya tikanchi.
Mtu hafanywi kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuisikia Sheria, bali kwa kuitii Sheria.
14 Adi Awurmi ale na idumun nsharaba, idin dortu bari makeke Kutelle imon irika na usharawen nbele, inung, udirun sharai mine, usharawari natimine.
Mathalan: watu wa mataifa mengine hawana Sheria ya Mose; lakini kila wanapotimiza matakwa ya Sheria wakiongozwa na dhamiri zao, wao wenyewe wanakuwa kipimo cha Sheria ingawa hawaijui Sheria.
15 Nan nya nani, idin dursu nita nirika na ni di nan nya niyerti nin shara nna nibinayi mine; nan nya nibinayin suzu nimon ichine nin ninanza ita iyizi nba nang ghinu, tutun ukpilizumine ma kesunani, sa unaza ani.
Mwenendo wao unaonyesha kwamba matakwa ya Sheria yameandikwa mioyoni mwao. Dhamiri zao zinashuhudia pia jambo hilo, maana fikira zao mara nyingine huwashtaki, na mara nyingine huwatetea.
16 liri lirika na Kutelle masuzu mawusu wusu nyeshizunu na nit, nafo na idin nya lirun nlai Yisa Kirsti.
Hivyo, kufuatana na hii Habari Njema ninayohubiri, ndivyo itakavyokuwa wakati Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya binadamu kwa njia ya Yesu Kristo.
17 Asa udin yichu litife Kuyahudawa, yerdine kidowon shara, su liburi libo kitene Kutelle.
Na wewe, je? Wewe mwenyewe unajiita Myahudi; unaitumainia Sheria na kujivunia kuwa wa Mungu;
18 Yinno usumeh, ukuru umala imon irika na idi ngan gan ninninin, nafo na iwabelufi nan nya shara.
kwa njia ya Sheria unajua matakwa ya Mungu na unaweza kuchagua jambo jema;
19 andi ureu figiri nwo fe wang unan wunu naduwari udu libau lichine, uso nkanan kiti na le na idin sirti,
wewe unajiona kuwa kiongozi wa vipofu na mwanga kwa wale walio gizani;
20 unan kelu nale na idi alala, unan dursuzu nnono, tutun unin dimun nan nya shara uyenju inyiru nin kidegen.
unajiona kuwa mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa wale wasiokomaa bado. Unayo katika Sheria picha kamili ya elimu na ukweli.
21 Asa fe din dursuzu among libauwe, udin dursuzu litife ba? Fena udin bellu among yenje iwasuzu likiri, fe din suzu likire?
Basi, wewe unawafundisha wengine; kwa nini hujifundishi wewe mwenyewe? Unawahubiria wengine wasiibe, lakini kumbe wewe mwenyewe unaiba.
22 Fena uworo yenje iwasu ufunu, fe dinsun fune? Fena udin lanzu infachak inchil, fe din nwo nitin chille?
Unasema: “Msizini,” na huku wewe unazini; unachukia sanamu za miungu hali wewe unajitajirisha kwa kuiba katika nyumba za miungu.
23 Fena udinin na ayi abo nin shara Kutelle, fedin nanzu lisame kitene kugbas fe?
Kwa kujigamba ati unayo Sheria ya Mungu, je huoni kwamba kwa kuivunja Sheria unamdharau Mungu?
24 Yene “lisa Kutelle nnana nan nya Nawurmi bara fe,” nafo na idin nya niyerte.
Kama vile Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Watu wa mataifa mengine wamelikufuru jina la Mungu kwa sababu yenu ninyi Wayahudi!”
25 Bara ubo nono na minu ulinbun asa idin dortun shara, nani tutu adi idin nazu nshara Kutelle, ubomine nso nafo udirun nbo.
Kutahiriwa kwako kutakuwa na maana kama ukiitii Sheria. Lakini kama unaivunja Sheria, basi, ni afadhali ungalibaki bila kutahiriwa.
26 Andi ameh unan nan dirun nbowe din dortu sharawe, na udirun bome so nso ubowa une ba?
Kama mtu wa mataifa mengine ambaye hakutahiriwa akitimiza matakwa ya Sheria, hakika atafikiriwa kana kwamba ametahiriwa.
27 Na ameh urika na bara kumat me di sa ubo, andi a kulo udortu sharame, suminu mawusu wusu, arika na idi nan nya niyerte inliru Kutelle anan nbo nin nanzu sharaba?
Watu wa mataifa mengine watakuhukumu wewe Myahudi kama ukiivunja Sheria, ingawaje unayo maandishi ya Sheria na umetahiriwa, hali wao wanaitii Sheria ingawa hawakutahiriwa.
28 Bara na ame Kuyahudawari ba nan nya yenju ndas; tutun na ame nbowariba urika na udin nan nya kidowoba.
Ndiyo kusema, si kila anayeonekana kwa nje kuwa Myahudi ni Myahudi wa kweli, wala mtu hawi Myahudi wa kweli ati kwa kuwa ametahiriwa kimwili.
29 Ameh Kuyahudawari urika na adi nya kibinayi, tutun ubo uchine unere nya kibinayi, nan nya nfip michine, na nya kidowoba. U zazuna nale anit din dasu kiti Kutelleri na anit asireba.
Myahudi wa kweli ni yule aliye Myahudi kwa ndani, yaani yule ambaye ametahiriwa moyoni. Hili ni jambo la Roho, na si jambo la maandishi ya Sheria. Mtu wa namna hiyo anapata sifa, si kutoka kwa watu, bali kutoka kwa Mungu.

< Roma 2 >