< Uruyan Yuhana 1 >

1 Ulelere upunu mbeleng Yesu Kristi na Kutelle wa nighe, a duro achin me imon ncin dak nan nya nayiri baat. A taa iyinno inin nan nyan ntuu ngono kadura me udu nkiti kuchin mye Yohanna.
Huu ni ufunuo wa Yesu Kristo ambao Mungu alimpa ili kuwaonesha watumishi wake mambo ambayo lazima yatokee karibuni. Aliyafanya yajulikane kwa kumtuma malaika wake kwa mtumishi wake Yohana.
2 Yohanna belle uliru ulele vat nin likara imon ile na awa yene ubeleng nliru Kutelle nin nimon inyenu idya na iwa belin kitenen Yesu Kristi.
Yohana alitoa ushuhuda wa kila kitu alichoona kuhusiana na neno la Mungu na kwa ushuhuda uliotolewa kuhusu Yesu Kristo.
3 Unan mmariari ame na adin bellu inyerti nin liwui li kang nin vat nalenge na idin lanzu tigwulan nlenge na adin su uliru nin nuu Kutelle a yinna nimon ile na ina nyertin nan nye, bara kuben daa susut.
Amebarikiwa yeye asomaye kwa sauti na wale wote wanaoyasikia maneno ya unabii huu na kutii kilichoandikwa humo, kwa sababu muda umekaribia.
4 Yohanna, udu ni anan dortu Kutelle kuzor nan nyan Asiya: Ubolu Kutelle udu anun nin nmang unuzu ngye na adi, nin awa di, nin le na a din cinu, nin nnuzu kiti nanan kiti ti ruhu kuzor na i di nnbun kutet tigo me,
Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: neema iwe kwenu na amani kutoka kwake aliyepo, aliyekuwepo, na atakayekuja, na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
5 nin nuzu kitin Yesu Kristi, na amere iyizi mba kiden, unan burnu maru, unan burnu nfitu nanya na nan kul, nin na nan tigo kitene nago in yii. U du kitime na adinin su bite, amini na bunku nari nanya nnye na adin suu bite amini nati i suun nari ti nuzu nnanya na lapi bit lar nnmii me,
na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mtawala wa wafalme wa dunia hii. Kwake yeye atupendaye na ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu yake,
6 amini ntari anan kipin tigo, apriests ucindu kiti Kutelle nin Ncif me, kitime ngongong nin na agang saligang. Usonani. (aiōn g165)
ametufanya kuwa ufalme, makuhani wa Mungu na Baba yake - kwake kuwa utukufu na nguvu milele daima. Amina. (aiōn g165)
7 Yenen, a din cinu nin na wut, vat nizi baa yenu nghye, ligowe nin na le na iwa jotugye. Ti lem vat inyi ba su lidurun bar ame. Eh, Usonani.
Tazama, anakuja na mawingu; kila jicho litamwona, pamoja na wote waliomchoma. Na kabila zote za dunia wataomboleza kwake. Ndiyo, Amina.
8 Cikilari Kutelle inworo, “Mere Ucizune nin Malzine,” “ule na adi, a wa di, nin nghe na a din cinu, ame unan Likalin.”
“Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “Yeye aliyepo, na aliyekuwepo, na ambaye anakuja, Mwenye nguvu.”
9 Meng, Yohanna-gwana mine ule na indi sonu nniu nin teru kibinai urume ligo nan ghinu nan nya kipin tigo Kutelle alenge na idi nanya Yesu na nwadi kitine Fikuru fongo na idin yicu fining Patmos bara uliru Kutelle nin shaida Yesu.
Mimi, Yohana - ndugu yenu na mmoja anayeshiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu thabiti ulio katika Yesu; nilikuwa katika kisiwa kiitwacho Patimo kwa sababu ya neno la Mungu na ushuhuda kuhusu Yesu.
10 Meng wa di nan Ruhu lirin Cikilari. Nlanza liwui nafo lin kulantung kang kimal nighe.
Nilikuwa katika Roho siku ya Bwana. Nilisikia nyuma yangu sauti ya juu kama ya tarumbeta,
11 Li wuiye woro, “Nyertine nan nya kugbundulung kufa ninyerte imong ile na uyene, utuumung udu nilarin lira kuzor, in Uafisawa, Usamaruna, Upagamus, Utiyatira, Usadis, Ufiladelfiya nin cin du Ulaudikiya.”
ikisema, “andika katika kitabu unayo yaona, na uyatume kwa makanisa saba, kwenda Efeso, kwenda Smirna, kwenda Pergamo, kwenda Thiatira, kwenda Sardi, kwenda Philadelphia, na kwenda Laodikia.”
12 Ngitirno nnan yene sa liwui nghaari din liru nin mi, nan gitirno in yene tica nla nizinaria kuzor yisin.
Nikageuka kuona ni sauti ya nani aliyekuwa akiongea nami, na nilipogeuka niliona kinara cha dhahabu cha taa saba.
13 Kiyitik tica nlee, umong wa diku nafo Usaun Nnit, awa shoon kulutuk ijakaka ku duru abunu me, nin likpa na liwa kilin figiri me.
Katikati ya kinara cha taa alikuwemo mmoja kama Mwana wa Adamu, amevaa kanzu ndefu iliyofika chini ya miguu yake, na mkanda wa dhababu kuzunguka kifua chake.
14 Litie nin titi me wadi pau nafo uwulu, nafo nkalkali, a iyizi me nafo lilem nla.
Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe kama theluji, na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
15 Afa nabunu me wadi, nafo uwaltu fikoro fishine, nafo fikoro fishine fongo na ijuju ikpelte fining kuwetel, a liwui me nafo uduu mmyen kurawa.
Nyayo zake zilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama shaba ambayo imekwisha pitishwa katika moto, na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi yanayotiririka kwa kasi.
16 Awa miin iyini kuzor ncara ulime me, a kusangali kileo nasari aba nucu nnuu me. Umuro me walta nafo uwui ugberere.
Alikuwa ameshikilia nyota saba katika mkono wake wa kuume, na kutoka kinywani mwake kulikuwa na upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa uking'aa kama mwanga mkali wa jua.
17 Nan yene ghe, ndeo nabunu me nafo ule na akuu. A tarda ucara ulime me kitene ning a woro, “Na uwa lanza fiu ba. Merie unan cizunu nin ni maline,
Nilipomwona, nikaanguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kulia juu yangu na kusema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa Mwisho,
18 nin lenge na adi nin lai. Meng wa ku, vat nani yene, ndi nin lai sa ligang! Mmini di nin nimon nnpun nkul nin nisek. (aiōn g165, Hadēs g86)
na ambaye ninaishi. Nalikuwa nimekufa, lakini tazama, ninaishi milele! Na ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Barnani nyertine ile imon na uyene, ile na idi, nin nile na iba yitu kimal nilele.
Kwa hiyo, yaandike uliyoyaona, yaliyopo sasa, na yale yatakayotokea baada ya haya.
20 Uyinu nbeleng niyini kuzor ine na unyeshine na uwa yene nchara ulime nighe, a tica inla nizinariya kuzore: iyini kuzore nono kadura Kutelle ndu nilari nlira kuzorari, a tica nla kuzore nilari nlira kuzorari.
Kwa maana iliyojificha kuhusu nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na kile kinara cha dhahabu cha taa saba: nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, na kinara cha taa saba ni yale makanisa saba.”

< Uruyan Yuhana 1 >