< Uruyan Yuhana 18 >

1 Na ile imone wakat vat uwa yene kan gono kadura Kutelle ntulsu cin dak nnuzu kitene kani. A wa di nin likara lidya, uye wa li kanang nin gongon mye.
Baada ya haya nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, akiwa na mamlaka makuu na dunia ikamulikiwa na mngʼao wake.
2 A taa ntyet nin liwui lidya, abenle, “Udewu, udewu ubabalila udiyai a so kitin lisosin na gbergenu, kiti lisosin vat ti ruhu ti nanzang nin kiti lisosin vat kijin kuzenzen.
Naye akalia kwa nguvu kwa sauti kubwa, akisema: “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu! Umekuwa makao ya mashetani na makazi ya kila pepo mchafu, makazi ya kila ndege na kila mnyama achukizaye.
3 Nipinpin ne vat nsono ntoro nzina mye na mina da ninghe tinana nayi. Ago nyii nasu uzina ninghe. Anan malesulesa nanya nyii so anan nimon na cara bara likara lisosin limang mye.”
Kwa maana mataifa yote yamekunywa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake. Nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi nao, nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.”
4 Nlanza nlon liwui nnuzu ketene kani nworo, “Nuzun nanya mene, anit ning, bara i wa seru imemun inanzan mye.
Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: “Tokeni katikati yake, enyi watu wangu, ili msije mkashiriki dhambi zake, ili msije mkapatwa na pigo lake lolote;
5 Alapi mye malkulu udu kitene kani, Kutelle nin katwa ka nanzan mye.
kwa kuwa dhambi zake zimelundikana hadi mbinguni, naye Mungu ameukumbuka uhalifu wake.
6 Kurtunghe ku imon na ame na su anite, kurtwaghe ku tiba iman ile na ana kurtuz anite ku; nanya kakup ka na awa ketelin, ketelenghe ti ba.
Mtendee kama yeye alivyotenda; umlipe mara mbili kwa ajili ya yale aliyotenda. Katika kikombe chake mchanganyie mara mbili ya kile alichochanganya.
7 Nafo na ana ghantin liti mye anin su mang, naghe gbardang uniu nin tunana naye. A woro nanya kibinai mye, 'Nsosin nafo ushono ngo; Na meng unan diru nlisari ba, na iwa yenu kibinai kisirnebai.
Mpatie mateso na huzuni nyingi sawa na utukufu na anasa alizojipatia. Kwa kuwa moyoni mwake hujivuna, akisema, ‘Mimi ninatawala kama malkia; mimi si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.’
8 Bara nani imon inanzan mye ma se ghe: ukull, lisosin nayi asirne, nin kukpon. Ula ma liighe.”
Kwa hiyo mapigo yatampata kwa siku moja: mauti, maombolezo na njaa. Naye atateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana Mungu amhukumuye ana nguvu.
9 Agon yee na ina su uzina ninghe inani na nuzu insalin lanzun niliru ninghe ima gilu nin ghe i wa yene mcin nli nla mye din ghanju.
“Wafalme wa dunia waliozini naye na kushiriki anasa zake watakapoona moshi wa kuungua kwake, watamlilia na kumwombolezea.
10 I ma yisinupiit, idin lanzu fiyu nniyu mye, mbenlu, “Kash, kash udu kipin ki diya, Babila, kipin llikara! Nanyan kube kurun uniu fe ndaa.”
Kwa hofu kubwa ya mateso yake, watasimama mbali na kulia na wakisema: “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, ee Babeli mji wenye nguvu! Hukumu yako imekuja katika saa moja!’
11 Anan malesulesu nye gila nin lisosin nayi asirne bara ame, bara na umong ma kuru asere imon nlesu mye tutung ba-
“Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumwomboleza kwa sababu hakuna anunuaye bidhaa zao tena:
12 Imon lesu ni zinariyanin, nin nazurfa, nin natola nikurfung, nin luu-luu, nin liniw ukpekpet, nin nimon nmyein nafo, nin siliki, nin malufi vat nin naca nikurfuung, nin vat nishik nicaut, nin fikoro fishine, nin fikoro fisirne nin mabil,
Bidhaa za dhahabu, za fedha, za vito vya thamani na vya lulu, kitani safi, nguo za rangi ya zambarau, hariri, nguo nyekundu, aina zote za miti ya udi, na vifaa vyote vya pembe za ndovu, vifaa vyote vya miti yenye thamani kuliko yote, shaba, chuma na marmar,
13 nin fikoro, nin animon, nin turare, nin mai kuya kunang, nin lubar, nin alkama, nin nina, nin nakam, nin nibark, nin karusa, nin nacin, nin ti lai na nit.
bidhaa za mdalasini, vikolezi, za uvumba, manemane, na uvumba wenye harufu nzuri, za divai, na mafuta ya zeituni, za unga mzuri na ngano; ngʼombe na kondoo; farasi na magari; na miili na roho za wanadamu.
14 Ku mat na ca ko na una din nin serwe i wulu fi. Vat mmang fe nin nimon fo figiri i nana kiti fe, na ima kuru ise inin tutung ba.
“Watasema, ‘Yale matunda ambayo roho yako iliyatamani yamekoma. Utajiri wako wote na fahari yako vimetoweka, wala haviwezi kupatikana tena kamwe!’
15 Ale na i wa din nlesu nile imone se ikurfung kang bara usu mye yisina piit ninghe bara fiiyu nniyu mye, kuculu nin tiit nayi asirne.
Wale wafanyabiashara waliotajirika kwa bidhaa hizo kutoka kwake watasimama mbali naye kwa hofu kubwa ya mateso yanayompata. Watalia na kuomboleza wakipiga kelele wakisema:
16 I ma woro, “Kash, kash nin kipin ki diya kane na ki wa su kuyuk nin ni ninoon icene, nanya nimon nmyein nafa, nin kye kidowome nin nizinariya, nin nimoon natuf nikurfung nin luu-luu.”
“‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, uliyekuwa umevikwa mavazi ya kitani safi, ya rangi ya zambarau na nyekundu, ukimetameta kwa dhahabu, vito vya thamani na lulu!
17 Nanya kube kurum vat nilele imoon nikurfunghe nana. Vat nanan con njirgi myeen, vat nanang cin nanya njirgi myeen, nin na le na i din sessu imonli nanyan kurawa ku dundya we, yisina piit.
Katika muda wa saa moja utajiri wote mkubwa kama huu umeangamia!’ “Kila nahodha, na wote wasafirio kwa meli, na wote wapatao kipato chao kutokana na bahari, watasimama mbali.
18 I taa ntest na iyene incin nli nla mye. I woro, “Kiyeme kipinari masin fo ka kipin ki dya?”
Watakapouona moshi wa kuungua kwake watalia wakisema, ‘Je, kulipata kuwako mji mkubwa kama huu?’
19 i tiza lidao nidowo mene, inin taa nteet, ning myiziin mi gbagbai nin lisosin tiyoom, “Kash, kash udu kipin kidya kane ki kaa na vat nale na i di nin tijirgin myen kurawa kudin dya nda se ikurfun ku unuzun dukiya mye. Bara na nanya kubi kurum ida nanza ghe.”
Nao watajirushia mavumbi vichwani mwao, huku wakilia na kuomboleza, wakisema: “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, mji ambao wote wenye meli baharini walitajirika kupitia kwa mali zake! Katika saa moja tu ameangamizwa!
20 “Taan liburi liboo bara ameh, kitene kani, anung anit alau, anang kaduran Yesu, nin nanan liru nin nuu Kutelle, bara na Kutelle nda nin mawucu wuce mye lite mye!”
Furahia kwa ajili yake, ee mbingu! Furahini watakatifu, mitume na manabii! Mungu amemhukumu kwa vile alivyowatendea ninyi.’”
21 Unan katwa Kutelle yira litala nafo litala tiyazung a too linin nanya kurawa kudya we, a benle, “Nanya nlo libau ule, uBabila, kipin kidya, i ma fillu kutyein nin tinana nayi na i ma kuru i yene tutung ba.
Kisha malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe kubwa kama la kusagia akalitupa baharini akisema: “Hivyo ndivyo mji mkubwa Babeli utakavyotupwa chini kwa nguvu wala hautaonekana tena.
22 Ti wui nanang foo nidowo, anang navu, anan pee nishiriya, nin nanang wulsu na langtung na i ma kuru ilanza nani. Nanya fe ba na i ma kuru i se anang makeke nimon nanya fe tutung ba. Na ima kuru i lanzan tiyazun nanya fe tutung ba.
Nyimbo za wapiga vinubi na waimbaji, wapiga filimbi na wapiga tarumbeta kamwe hazitasikika tena ndani yako. Ndani yako kamwe hataonekana tena fundi mwenye ujuzi wa aina yoyote. Wala sauti ya jiwe la kusagia kamwe haitasikika tena.
23 Nkanan nla ma bicu na ima kuru iyene mining tutung ba. Liwui na wanlapese nang na lese na ima kuru ilanza tutun ba, bara na imoon nlesu fe wadi ashoono na goo nyii, nin myin uwa rusuzu nani ning niyuu fe.
Mwanga wa taa hautaangaza ndani yako tena. Sauti ya bwana arusi na bibi arusi kamwe haitasikika ndani yako tena. Wafanyabiashara wako walikuwa watu maarufu wa dunia. Mataifa yote yalipotoshwa kwa uchawi wako.
24 Nanya mye i wa se nmyii nanang liru ning nuu Kutelle nin nanit a lau, ning myii na le na i wa mulsu nani nanya nyii.”
Ndani yake ilionekana damu ya manabii na ya watakatifu na wote waliouawa duniani.”

< Uruyan Yuhana 18 >