< Uruyan Yuhana 1 >

1 Ulelere upunu mbeleng Yesu Kristi na Kutelle wa nighe, a duro achin me imon ncin dak nan nya nayiri baat. A taa iyinno inin nan nyan ntuu ngono kadura me udu nkiti kuchin mye Yohanna.
Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo ni lazima yatukie hivi karibuni. Alijulisha mambo haya kwa kumtuma malaika wake kwa Yohana mtumishi wake,
2 Yohanna belle uliru ulele vat nin likara imon ile na awa yene ubeleng nliru Kutelle nin nimon inyenu idya na iwa belin kitenen Yesu Kristi.
ambaye anashuhudia kuhusu kila kitu alichokiona, yaani, Neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo.
3 Unan mmariari ame na adin bellu inyerti nin liwui li kang nin vat nalenge na idin lanzu tigwulan nlenge na adin su uliru nin nuu Kutelle a yinna nimon ile na ina nyertin nan nye, bara kuben daa susut.
Amebarikiwa yeye asomaye maneno ya unabii huu, na wamebarikiwa wale wanaoyasikia na kuyatia moyoni yale yaliyoandikwa humo, kwa sababu wakati umekaribia.
4 Yohanna, udu ni anan dortu Kutelle kuzor nan nyan Asiya: Ubolu Kutelle udu anun nin nmang unuzu ngye na adi, nin awa di, nin le na a din cinu, nin nnuzu kiti nanan kiti ti ruhu kuzor na i di nnbun kutet tigo me,
Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: Neema na amani iwe kwenu kutoka kwake aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi,
5 nin nuzu kitin Yesu Kristi, na amere iyizi mba kiden, unan burnu maru, unan burnu nfitu nanya na nan kul, nin na nan tigo kitene nago in yii. U du kitime na adinin su bite, amini na bunku nari nanya nnye na adin suu bite amini nati i suun nari ti nuzu nnanya na lapi bit lar nnmii me,
na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni yule shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, mtawala wa wafalme wa dunia. Kwake yeye anayetupenda na ambaye ametuweka huru kutoka dhambi zetu kwa damu yake,
6 amini ntari anan kipin tigo, apriests ucindu kiti Kutelle nin Ncif me, kitime ngongong nin na agang saligang. Usonani. (aiōn g165)
akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen. (aiōn g165)
7 Yenen, a din cinu nin na wut, vat nizi baa yenu nghye, ligowe nin na le na iwa jotugye. Ti lem vat inyi ba su lidurun bar ame. Eh, Usonani.
Tazama! Anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona, hata wale waliomchoma; na makabila yote duniani yataomboleza kwa sababu yake. Naam, ndivyo itakavyokuwa! Amen.
8 Cikilari Kutelle inworo, “Mere Ucizune nin Malzine,” “ule na adi, a wa di, nin nghe na a din cinu, ame unan Likalin.”
“Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.”
9 Meng, Yohanna-gwana mine ule na indi sonu nniu nin teru kibinai urume ligo nan ghinu nan nya kipin tigo Kutelle alenge na idi nanya Yesu na nwadi kitine Fikuru fongo na idin yicu fining Patmos bara uliru Kutelle nin shaida Yesu.
Mimi, Yohana, ndugu yenu ninayeshiriki pamoja nanyi mateso katika Yesu na katika ufalme na uvumilivu katika saburi, nilikuwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu.
10 Meng wa di nan Ruhu lirin Cikilari. Nlanza liwui nafo lin kulantung kang kimal nighe.
Katika siku ya Bwana, nilikuwa katika Roho na nikasikia sauti kubwa kama ya baragumu nyuma yangu
11 Li wuiye woro, “Nyertine nan nya kugbundulung kufa ninyerte imong ile na uyene, utuumung udu nilarin lira kuzor, in Uafisawa, Usamaruna, Upagamus, Utiyatira, Usadis, Ufiladelfiya nin cin du Ulaudikiya.”
ikisema, “Andika kwenye kitabu haya yote unayoyaona, kisha uyapeleke kwa makanisa saba, yaani: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”
12 Ngitirno nnan yene sa liwui nghaari din liru nin mi, nan gitirno in yene tica nla nizinaria kuzor yisin.
Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Nami nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,
13 Kiyitik tica nlee, umong wa diku nafo Usaun Nnit, awa shoon kulutuk ijakaka ku duru abunu me, nin likpa na liwa kilin figiri me.
na katikati ya vile vinara vya taa, alikuwamo mtu kama Mwana wa Adamu, akiwa amevaa joho refu, na mkanda wa dhahabu ukiwa umefungwa kifuani mwake.
14 Litie nin titi me wadi pau nafo uwulu, nafo nkalkali, a iyizi me nafo lilem nla.
Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
15 Afa nabunu me wadi, nafo uwaltu fikoro fishine, nafo fikoro fishine fongo na ijuju ikpelte fining kuwetel, a liwui me nafo uduu mmyen kurawa.
Nyayo zake zilikuwa kama shaba inayongʼaa, katika tanuru ya moto, nayo sauti yake ilikuwa kama mugurumo ya maji mengi.
16 Awa miin iyini kuzor ncara ulime me, a kusangali kileo nasari aba nucu nnuu me. Umuro me walta nafo uwui ugberere.
Katika mkono wake wa kuume alishika nyota saba, na kinywani mwake ulitoka upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa kama jua likingʼaa kwa nguvu zake zote.
17 Nan yene ghe, ndeo nabunu me nafo ule na akuu. A tarda ucara ulime me kitene ning a woro, “Na uwa lanza fiu ba. Merie unan cizunu nin ni maline,
Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akauweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope, Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho.
18 nin lenge na adi nin lai. Meng wa ku, vat nani yene, ndi nin lai sa ligang! Mmini di nin nimon nnpun nkul nin nisek. (aiōn g165, Hadēs g86)
Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Barnani nyertine ile imon na uyene, ile na idi, nin nile na iba yitu kimal nilele.
“Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yale yatakayotukia baada ya haya.
20 Uyinu nbeleng niyini kuzor ine na unyeshine na uwa yene nchara ulime nighe, a tica inla nizinariya kuzore: iyini kuzore nono kadura Kutelle ndu nilari nlira kuzorari, a tica nla kuzore nilari nlira kuzorari.
Kuhusu siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume na vile vinara saba vya taa vya dhahabu ni hii: Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, navyo vile vinara saba ni hayo makanisa saba.

< Uruyan Yuhana 1 >