< Filibiya 3 >

1 Umalzunu vat linuana, sun liburi libo nanyan Cikilari. Kitininghe nkurun yerten minu ile imone na imon nkonnu litiari ba. Ilenge imone ma ciu minu gegeme.
Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana! Mimi kuwaandikia mambo yale yale hakuniudhi, kwa maana ni kinga kwa ajili yenu.
2 Yenjen bara ninau. Yenjen anan katwa kananzanga. Yenjen anan molsu nanit.
Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa.
3 Bara arikari ukalzu nacuru mine. Arikere anan sujada nin Ruhu Kutelle. Arikere anan fo nigiri nin Yesu Kristi, alenge na idi nin nayi akone nin katwa kidowo.
Kwa maana sisi ndio tulio tohara, sisi tumwabuduo Mungu katika Roho, tunaona fahari katika Kristo Yesu, ambao hatuweki tumaini letu katika mwili,
4 Nanya nane, meng wang wadi nin nayi akone nin katwa kidowo. Nwa dimun wang gbardang.
ingawa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuutumainia mwili. Kama mtu yeyote akidhani anazo sababu za kuutumainia mwili, mimi zaidi.
5 Iwa kalai kucuru liri lin kutir. Iwa marui nanya kuwunun Israila, nanya likuran Bayamin, Kuyahudawa kidegen nanya na Yahudawa. Kusarin dortun duka, iwa marui ku Farisawa.
Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania. Kwa habari ya sheria, ni Farisayo,
6 Meng wadin lanzun mang ntizu kilari Kutelle uniu kang. Bara katwa kacine nduka, na nwa dinin tanu ba.
kwa habari ya juhudi, nilikuwa nalitesa kanisa, kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria, mimi nilikuwa sina hatia.
7 Ama vat nani inyaghari wadi ukpinu ninghe, nmini na yaun inin imon ihem vat bara Kristi.
Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
8 Kidegene, nene ndin batuzu imone vat udiuwari bara katwa kacine in yirun Kristi Yesu Cikilari ninghe. Bara ame nna filing imon vat. Nna yiru inin vat katwa kanangzanghari bara nnan se Kristi ku,
Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo.
9 inan seyi nanya me tutung. Na nna se katwa kacine litining bara udortu nduka ba. Nna nase katwa kacine kanga na na kadi nanyan yinnu sa uyenu nin Kristi, katwa kacine ka na kadi kiti Kutelle unuzun yinnu sa uyenu.
Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani.
10 Nengene ndi nin su inyininghe nin likaran fitu me nanya kul a ligowe nanyan niu me. Ndi nin suu nse ukpiliu nanya lissosin ninghe bara ukul me.
Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake,
11 nnani men ciro ufitu nnuzu na nan kul.
ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.
12 Na kidegenere nna malu useru ilenge imone ba, sa meng mal se ukulu nimone ba. Ama ndin sho liti nnan kifo ileli imone na mma kifu kitin Kristi Yesu.
Si kwamba nimekwisha kufikia, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha! Bali nakaza mwendo ili nipate kile ambacho kwa ajili yake, nimeshikwa na Kristo Yesu.
13 Linuana, na ndin yenju nafo meng liti ninghe nmal kifu imon ba. Ama imon irum duku meng fillo imon ile na imal katu nmini ceo ayi nimon ile na idin bunnning nanya Kristi Yesu.
Ndugu zangu, sijihesabu kuwa nimekwisha kushika. Lakini ninafanya jambo moja: Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele.
14 Ndin sho liti udi duru kiti kanga na ndi ninsu nduru nnan se uduk in yicu Kutelle nanyan Kristi Yesu.
Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.
15 Vat bite na timal kunju, na ti kpiliza nani. Andi udin kpilizu ugan nbelen nimon imong, Kutelle wang ma dursu fi ining.
Hivyo sisi sote tuliokuwa kiroho tuwaze jambo hili, hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu ataliweka wazi hilo nalo.
16 Vat nani, vat nimon ile na timal duru ining, na timiin inin nin likara.
Lakini na tushike sana lile ambalo tumekwisha kulifikia.
17 Piziran iyita nafo meng, linuana, shonon iyizi iyenje gegeme alenge na idin cinju imusun cin ule na anung nase kiti bite.
Ndugu zangu, kwa pamoja fuateni mfano wangu na kuwatazama wale wanaofuata kielelezo tulichowawekea.
18 Anit gbardng din cinu nanya nalenge na ndin bellu minu ubelen mine kokome kubi, nene tutung ndin belu minu nin mizin, among din cinu masin nafo idi nivira nin kucan kotunung Kristari.
Kwa maana, kama nilivyokwisha kuwaambia mara nyingi kabla, nami sasa nasema tena hata kwa machozi, watu wengi wanaishi kama adui wa msalaba wa Kristo.
19 Imalin mine ukulari. Bara Kutelle mine aburi minere, a tikunan nati mine di nanya ncing mine. Inung din kpilizu ubelen nimon nyii ari.
Mwisho wa watu hao ni maangamizi, Mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu, na mawazo yao yamo katika mambo ya dunia.
20 Kipin bite di kitene kaneri, kiti kanga na tidin ca nnan tucu ku, Cikilari Yesu Kristi.
Lakini uenyeji wetu uko mbinguni. Nasi tunamngoja kwa shauku Mwokozi kutoka huko, yaani, Bwana Yesu Kristo,
21 Ame ma kpiliu nidowo kutyen bite niso nidowo nanga na ana kye nafo kidowon gongong me, kanga na ina kye nin likara lidyya me anan wunno imon vat udak litime.
atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, ili upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote chini yake.

< Filibiya 3 >