< Matiyu 3 >

1 Na yiri ane Yohanna unan Shitizinu nanit nmyen wa dak adin bellu nliru ntucu nan nya ntene in Yahudiya a woro,
Katika siku zile Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Yuda akisema,
2 “Sunan alapi, bara kipin tigo Kutellẹ nda duru.”
“Tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni u karibu.”
3 Bara amere ulele ulenge na iwa bellin ubelen me nnu Ishaya unan liru nin nuu Kutellẹ, a woro, “Liwui umong din yiccu nan nya ntene, 'Kelen libau ncikilari, kelen ulin mine nan-ghe.'”
Kwa maana huyu ndiye aliyenenwa na nabii Isaya akisema, “sauti ya mtu aitaye kutoka jangwani; 'wekeni tayari njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.”'
4 Imon kidowo in Yohanna wa di kukpa kuron komiari a likpa na liwa terin kutino me. Imonli me wa di acin ni titong.
Sasa Yohana alivaa manyoya ya ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
5 Anan Urushalima, nin Yahudiya a vat nigbiri nkilinu kurawan urdun wa nuzu idọ kitime.
Kisha Yerusalemu, Yuda yote, na eneo lote linalozunguka mto Yorodani wakaenda kwake.
6 Awa shintu nani nan nyan nmyen kurawan urdun, a icin bele alapi mine.
Walikuwa wakibatizwa naye katika mto Yorodani huku wakitubu dhambi zao.
7 Kube na awa yene liigo na Farisawa nin na Saddukiyawa ucinfak kitime a shintu nani nmyen, a woro nani, “Anung kumat niyii timung, gharin wunung minu atuf ina ni din cum kiti tinana nayi na ti din ciinu?
Lakini alipowaona wengi wa mafarisayo na masadukayo wakija kwake kubatizwa, akawaambia, ''Enyi uzao wa nyoka wenye sumu nani aliye waonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
8 Nutunong kumat ko na ku batiina usunuu na lapi.
Zaeni matunda yaipasayo toba.
9 Ana iwa kpiliza i woro nan nya mine, 'Tidi nin Ibrahim ucif bit.' Bara ndin belu minu Kutellẹ wasa ana Ibrahim ku nnan nono ko kiti na tala alele.
Na msifikiri na kusemezana miongoni mwenu, 'Tunaye Ibrahimu kama baba yetu.' Kwa kuwa nawaambieni Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutoka katika mawe haya.
10 Nene imali ciu gidowo litino naca. Vat kuca kongo na ku mara kumat kucine ba ima kowu kunin iti kunin nan nya nla.
Tayari shoka limekwisha kuwekwa kwenye mzizi wa miti. Kwahiyo kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa kwenye moto.
11 Meng din shintu minu nmyen i sun alapi mine. Ame ulenge na adin cinu kidun nighe a di nin likara a katini, na meng wang batin in yaun akpatak me ba. Ame ma shintu minuu nin Ruhu Ulau a ula.
Ninawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba. Lakini yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi nami sistahili hata kubeba viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
12 Ku puruk me di nacara me, ama shintulu a nutun alkama nan nya kusheri lan, ama nin ciu alkame nan nya filai. Nani ama nin juju kusheri nin la ule na uma so ubico ba.”
Na pepeto lake li mkononi mwake kusafisha kabisa uwanda wake na kuikusanya ngano yake ghalani. Lakini atayachoma makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
13 Yisa tunna a fita a da kurawan urdun unuzun in Galili kitin Yohanna ada shintin ghe nmyen.
Kisha Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka mto Yorodani kubatizwa na Yohana.
14 Ame Yohanna ta usu nworo a nantinghe, a woro, “Meng din piziru fe shintini nmyen, fe uni nna da kiti nigha?”
Lakini Yohana alitaka kumzuia akisema, “Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?''
15 Yisa kpana a woro ghe, “Yinna nani nene, bara udi gegeme kiti bite tikulo katwa kacine vat.” Yohanna yinnin ghe mun.
Yesu akajibu akasema, ''Ruhusu iwe hivi sasa, kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote.'' Kisha Yohana akamruhusu.
16 Kimal nshintin ghe kule, Yisa nuzu nan nyan nmyene mas, na nin molu kubi ba, i punghe kitene kani. A yene Uruhu Kutellẹ utolu kadas nafo kuwullung udak kitime.
Baada ya kuwa amebatizwa, mara Yesu alitoka kwenye maji, na tazama, Mbingu zikafunguka kwake. Na alimuona Roho wa Mungu akishuka kwa mfano wa njiwa na kutulia juu yake.
17 Itunna liwui nuzu kitene Kutellẹ liworo, “Ggono nsu kibinai Nighari kane. Ndin lanzu mmang me kang.”
Tazama, sauti ilitoka mbinguni ikisema, “Huyu ni mwanangu mpendwa. Ninaye pendezwa sana naye.''

< Matiyu 3 >