< Matiyu 26 >

1 Kube na Yesu wa malu ubellu nliru une vat, a woro nono katwa me.
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
2 “iyiru upaska nlawa ayiri abari cas, ima nakpu Usau Nnit ikotinghe kitene kuca.”
“Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe.”
3 Ugo na Priest nin nakune nbun nanite wa da pitirin kiti kirum kudaru Ngo na Prieste, ulenge na iwa yirughe nin lissa Kefas.
Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
4 Ligowe ipizira tibau nworu ikifo Yeso ku imolughe likire.
Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
5 Iwa din bellu, “Na kubin idi paska, bara iwa fya anite ayi.”
Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
6 Kube na Yesu wa di in Baitanya ngan Simon ukutulu,
Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
7 na awa sossin kiti nli nimonli, umong uwani da kitime nin libo nnuf kunya kumang min nikurf gbardang, a kpilya minin litime.
mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
8 Na nono katwa me in yene nani, ayi nana nani i woro, “Nyaghari finu nka kimole?
Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Ya nini hasara hii?
9 Iwa lewu mini nin nikurfu gbardaang ikoso nikimon.”
Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha.”
10 Yesu nin yiru nane, a woro iyaghri nta idin bukuru nwani ulele kibinayi? Bara asuyi katwa kacine.
Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
11 Idi ligowe nan nikimone ko kome kubi, na meng ma yitu nan ghinu ko kome kubi ba.
Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
12 Ule ukpilyu nnufe kidowe na asuyi, asu nani a kelei bara ukassu nigha.
Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
13 Nbelin minu kidegen, kiti kanga na ima su ulenge uwaze ku nanya lenge uyeh vat, imon ilenge na uwani ulele nsu ima bellu unin inan lizino nighe.
Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye.”
14 Umong nanya likure, ulenge na iwa yicughe Yahuda Iskaroti, ado kitin Ngo na Priest
Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
15 aworo, “Imashinari ima ni meng nakpa minu ame?” Ibataghe azurfa akut atat.
akawaambia, “Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?” Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
16 Atunna ipizuru ndina ule na ama nakpu nani ame.
na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
17 Lirin ncizunu nli fungal nsalin muccu, nono katwa me da kitime iworoge, “Weri udi nin su tidi kyele bara uli npaske?”
Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, “Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?”
18 Aworo, “Can kitin mon unit nanya kipine iworoghe, 'Cikilari nworo, “kubi nighe nda duru. Meng ba su upaska ngafere ligowe nin nono katwa nighe”
Yeye akawajibu, “Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu.”
19 Nono katwawe su nafo ubellu me, I kyele imonli Npaske.
Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
20 Na kubi kuleleng nta, aso ama li ligowe nin nono katwa me likure.
Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
21 Idi nanya kilewe, aworo, “Ndin bellu minu kidegen umon nanya mine ma lewui.”
Walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti.”
22 Ita aburi asirne kang, kogha nanya mine tiringhe, sameri Cikilari?”
Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, “Bwana! Je, ni mimi?”
23 Akawa aworo, “ulenge na adin sho ncara kishik kirume nin mi amere ma lewui.
Yesu akajibu, “Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
24 Usaun Nnit ma nyiu nafo na ina yerti litime. Kash nnit ulenge na ama liwu Usaun Nnit! Uma katinu unit une nin caut na iwa na marughe ba.”
Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa.”
25 Yahuda ulenge na amere ma lewughe woro, “Sa menghari unan dursusu niyerti?” Aworoghe, ubelle nin litife.”
Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, “Mwalimu! Je, ni mimi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
26 Na iwa di kilewe, Yesu yauna ufungal, ata nlira ku, a pucco unin. Ana nono katwa me unin aworo, “Seren, leon. Kidowo nighari.”
Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni mle; huu ni mwili wangu.”
27 Ayauna kakkuke ata nlira ku, a nakpa nani aworo, “Sonon, vat mine.
Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, “Nyweni nyote;
28 Mone nmii nalikawali nigharibmongo na ina gutun bara gbardang na se ukusu nalapi.
maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
29 Ndin bellu minu, na nma kuru nsono nmyen kumat kuce ba, se loli lire na nma sonu minin mipesse nan ghinu nanya kipin tigo Ncif ning.”
Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30 Na ita avu nimalin, inuzu inya ucindu likup in zaitun.
Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
31 Yesu woro nani, “kyitik kane vat mine ma tiru bara meng, bara ina nyerti,'nma kpui unan libyawe ligo nakame ma malu kiti.'
Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
32 Vat nani asa ifyyi, nma nyiu ubun mine udu nanyan Galili.”
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya.”
33 Bitrus woroghe, “Andi vat min ba diu bara fewe, na meng wasa nma tiro nsunfi ba.”
Petro akamwambia Yesu “Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe.”
34 Yesu woroghe, meng din bellufi kidegen, nin kyitik kane kukulok mayitu kusa kolsino ba, uba woru na uyiri ba so titat.”
Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 Bitrus woroghe, Andi ma mma ku ninfi gbas, na nma narifi ba.” Ngisin nono katwa me vat belle nanare wang.
Petro akamwambia, “Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 Yesu tunna a nya ligowe nanghinu udu nkan kiti na idin yiccu kinin Ugetsemani a woro nono katwa me, “Son kikane meng do kikani ndi ti nlira.”
Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali.”
37 A yira Bitrus ku nin na saun Zabeden ligowe nanghe atunna a cizina usirzu nayi, ayime nana.
Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
38 A tunna a woro nani, “Liburi nin siro bibit, nafo nku. Son kikane i yenje kiti nan mi.”
Hapo akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.”
39 A cancana udu ubun bat, a deo nin nalung ata nlira, a woro, “Ucif ning, andi uwasa uso nani, na kakukkane kata kiti nighe. “Vat nani, na ubellu nighe ba, ubellu fere.”
Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: “Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe.”
40 Ada kiti nnono katwa me ada se nani nmoro, a woro, a woro Bitrus ku, “inyaghar, na uwasa uyenje kiti nin mi kutanki kurumba?
Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
41 Yenjen kiti isu nlira bara iwa piru nanyan dumuzunu. Uruhe yinna, kidowere dinin likara ba.”
Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu.”
42 Ado tutung unba adi ti nlira, aworo, “Ucif ning, andi na uwasa ukata nani ba se nsono uning, na ubellu fere so.”
Akaenda tena mara ya pili akasali: “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike.”
43 Ada tutung ada se nani idin moro, bara iyizi mine wa ti getek nin moro kang.
Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
44 Akuru a nya tutung, adi ti nlira uti un tat a belle uliru urume.
Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
45 Yesu da kitin nono katwa me aworo nani, “Idu nmoro nin shinua? Yeneng, kubi mal da duru, imal lewu Usaun nnit nacara nannan nalapi.
Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, “Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
46 Fitan nari ti nya. Yenen ulenge na aba lewiye nda duru.”
Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti.”
47 A dutun nlirue, Yahuda, umong nanya mine likure da. Ligozin gbardang wa di ligowe ninghe unuzu kiti ngo na priest nan nakune nanite. Ida nin na sangali nan tica.
Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
48 Nene unit ulenge na amere ma lewu Yeseku wa tinani udursu, aworo, “Ulenge na in nyukkunghe, amere kiffonghe.”
Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: “Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni.”
49 Ata mas ada kitin Yesu aworo, Ndin lissufi una dursuzu ninyerte! A nyukunghe.
Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, “Shikamoo, Mwalimu!” Kisha akambusu.
50 Yesu woroghe, “Udondong su imong irika na uda nsue.” Inughe tunna ida, i kiffo Yesu ku, i nya ninghe.
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya ulichokuja kufanya.” Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
51 Umong nanya nalenge na iwa di ligowe nan Yesu tunna a nakpa ucara me, a shuku kusangali, a kowo kucin Ngo na Priest, a weringhe kutuf.
Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52 Yesu tunna aworoghe, kpilla ushon kusangali fe kuparinme, bara vat nalenge na idin molsu nin na sangali iba molsu nani nin na sangali.
Hapo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
53 Udin yenju na meng wasa in yicila Ucif ning, a toyi nin nono kadura me a lenge na ima katunu amui akut atat nin kutocin ba?
Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 Ani iba ti iyizari uliru Kutelle kulo, nworu unan so nani gbas?”
Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?”
55 Kubi kone, Yesu woro ligo nanite, “I da nin na sangiali nan tica ida kifoi nafo ukirya? Ndin sozu ndursuzo anit nanya kutii nlira kolome liri, ana i kiffoi ba.
Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, “Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
56 Vat ilenge imone so nani iyerte nanan liru nin nu Kutelle nan kulo.” Nono katwa me tunna isunghe ico.
Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie.” Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
57 Alenge na i kiffo Yesue ku nya nighe udumun kiti Kefas ugo na Priest kikanga na anan niyerte nin nakune wa pitin ku ligowe.
Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
58 Bitirusa cas wa dortughe kidun piit udu kudaru nwuccu nliru ndya kutii nlirie. A wa piru nanya a so ligowe nin nan ca ayene inyaghari iba su ninghe.
Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
59 Nene udya kutii nlirie nin nanan kpilzu me vat pizira uliru bellu litime na ise Yesu ku nin kulapi, bara inan se finu nliru imolughe.
Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
60 Na iwa se uliru ba, vat nin nan liru kinuwe na iwa da ida su. kimal nani among naba da
lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
61 I woro, “Unit ulele wor, meng wasa npuco kutii nlira Kutelle nkpila nke kunin nanya nayiri atat.”
wakasema, “Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.”
62 Udya kutii nlire fita ayisina, aworoghe, “na udin liru ule na uma kpanu ba? Inyaghari ilele idin bellu litife?”
Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, “Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
63 A Yesu yita nin kutike. Udya kilari nlira woroghe, “Ndifi kucukusu nin Kutellen lai, belle nari sa fere Kriste, Gono Kutelle.”
Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!”
64 Yesu kawaghe, “Ubelle nani litife. Meng bellinfi nene, udu ubun uma yenu Usaun nnit sossin ncara ulime un likara, adin cinu kitene nawut kitene kani.”
Yesu akamwambia, “Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 Udya kilari nlire marya kulutuk me aworo, “A zogo Kutelle. Iyaghari nta tutung ti kuru ti du nin su nmon uliru? Yeneng nene anung lanza tizogoe.
Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
66 Iyaghari idin kpilizue?” Ikawaghe i woro, “Abatina ukul.”
Ninyi mwaonaje?” Wao wakamjibu, “Anastahili kufa!”
67 Itufuzunghe ataf nmoro, ikuru iruzoghe, ifoghe tutung nin nacara mine,
Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
68 I woro, “Sunari anabci fe Kristi. Ame ghari ulenge na a riofi?”
wakasema, “Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!”
69 Kubi kone, Bitrus wa sossin ndas nbun kutii nwuccu nlirue, nkan kabura kucin da kitime a woro. “Fewang di ligowe nin Yesu Ngalili.”
Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, “Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70 Ata amusu kun nbun mine vat, aworo, “Na meng yiru imon ilenge na udin liru kitene ba.”
Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”
71 Na anuzu udu kibulung, nkon kubura kucin ugan tutung yeneghe a woro alenge na iwa di kitene, “Unit ulele wang wa di ligowe nin Yesu Nnazaret.”
Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
72 Akuru ata amusu ku tutun nin nisiling, “Na in yiru unite ba.”
Petro akakana tena kwa kiapo: “Simjui mtu huyo.”
73 Nin kubiri bat, alenge na iwa yissin kitene da ida woro Bitrus ku, “Kidegenere, fe wang umong nanya minere, bara lilemfe ndursofi.”
Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha.”
74 Atunna a cizina izogo nin nisiling, “Na in yiru unitte ba.” Na nin dandaunu ba, kukulok kolsuno.
Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, “Simjui mtu huyo!” Mara jogoo akawika.
75 Bitrus lizino ulire na Yesu nin bellinghe. “Kukulok mayitu kusa kolsuno ba, uma ti umusun yiru nin titat.” A nuzu ado udas adi gilu kang.
Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Basi, akatoka nje akalia sana.

< Matiyu 26 >