< Matiyu 2 >

1 kubẹ na iwa maru Yisa ku in Baitalami un Yahudiya nayiri tigoh in Hiridus, amon anitt anan yiru yenju niyini kusari kitene nin Urushalima da ida woro,
Baada ya Yesu kuzaliwa katika mji wa Bethlehemu huko Uyahudi, wakati wa utawala wa Mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu
2 Adin weri ulenge na ina marughe ugoh na Yahudawe? Tina yene fiyini mere kusari kitene unnare ti da tida zazinghe.”
wakiuliza, “Yuko wapi huyo aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tumeona nyota yake ikitokea mashariki, nasi tumekuja kumwabudu.”
3 Na ugoh Hiridus in lanza nani, ayi me nin na nitin Urushalima fita vat.
Mfalme Herode aliposikia jambo hili aliingiwa na hofu sana pamoja na watu wote wa Yerusalemu.
4 Hiridus pitirino a didya na Priest nin na nan ninyerte nanit vat kiti kirum, anin tirino nani, “Nweri ima Kristi ku?”
Herode akawaita pamoja viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, akawauliza ni mahali gani ambapo Kristo angezaliwa.
5 I woro ghe nenge, “In Baitalamin Yahudiya, bara imon ile na nyan lirun nuu Kutullẹ na nyertin nari ine,
Nao wakamwambia, “Katika Bethlehemu ya Uyahudi, kwa maana hivyo ndivyo ilivyoandikwa na nabii:
6 'A fe, ubaitalami, in myin Yahudiya, na fere ubene nan nya na nan bun Yahudiya, nani nan nya fere unan tigo ba nuzukuulenge na ama su libya nanit nig Israila.'”
“‘Nawe, Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si mdogo miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana kutoka kwako atakuja mtawala atakayekuwa mchungaji wa watu wangu Israeli.’”
7 Hiridus tunna ayicila anan yiru vat likire a tirino nani in dert kubi kongo na fiyine na nuzu.
Ndipo Herode akawaita wale wataalamu wa nyota kwa siri na kutaka kujua kutoka kwao uhakika kamili wa wakati ile nyota ilionekana.
8 A to nani udu ubaitalahmi, a woro, “Can idi piziru ubeleng gono seng. Asa i se ghe, dan ida belli, bara meng wang nan do in di zazinghe.”
Kisha akawatuma waende Bethlehemu akiwaambia, “Nendeni mkamtafute kwa bidii huyo mtoto. Nanyi mara mtakapomwona, mniletee habari ili na mimi niweze kwenda kumwabudu.”
9 Na i lanza ugowe ku, i kiffo libau i nya, fiyine na ini yene kusari kitene tunna ncin nbun mine fidi duru fiyisina kiti kirum dert kiti kanga na gọnọ diku.
Baada ya kumsikia mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaenda zao, nayo ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama mahali pale alipokuwa mtoto.
10 Na iyene fiyinie, isu ayi abo nin liburi libo kang.
Walipoiona ile nyota wakajawa na furaha kubwa mno.
11 Itunna ipira nan nya kilare iyene gone nin nene Maryamue. Itumuno izazin ghe. Itunna i puzuno tika mine i nakpaghe imon ile na i ming mun, izinariya, lubban a kwul.
Walipoingia ndani ya ile nyumba, wakamwona mtoto pamoja na Maria mama yake, wakamsujudu na kumwabudu yule mtoto Yesu. Ndipo wakafungua hazina zao, wakamtolea zawadi za dhahabu, uvumba na manemane.
12 Na ise uwannu nataf kiti Kutellẹ nan nya namorona iwa kpilin kitin Hiridus ba, ifita i yira nlong libau ugang ukpillu kipin mine.
Nao wakiisha kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Herode, wakarudi kwenda katika nchi yao kwa njia nyingine.
13 Na inung nna nya, Gono kadura Kutellẹ tun na a da kitin Yusufu nan nya namoro, a woroghe, “Fita uyiru gono, kinesse nin nene urum udu uMasar, udi so kikane se kubi kongo na mbellin fi uliru bara na Hiridus ma pizuru gone a molu kining.”
Walipokwisha kwenda zao, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kumtafuta huyu mtoto ili amuue.”
14 A tunna nin kitik ka ne afita a yauna ggono kinesse nin nene inya mun ucindu umasar.
Kisha Yosefu akaondoka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake wakati wa usiku, nao wakaenda Misri
15 Awa di so kikane udi duru kubin nkul in Hiridus, ulire nan kulo na cikilare wa bellin kitin nnan liru nin nuu Kutellẹ, “Unuzun nan nyan Masar nna yicila usaun ning ku.”
ambako walikaa mpaka Herode alipofariki. Hili lilifanyika ili litimie lile lililonenwa na Bwana kwa kinywa cha nabii kusema: “Nilimwita mwanangu kutoka Misri.”
16 Na Hiridus iyene anitt ayinjing ane nrusuzo ghe, ayi nana ghe kang, ato idi molusu nnono ni lirine vat na niwadi in Baitalahmi, udu ligan nminne vat, ucizunu na kus aba utolu kadas nalenge na idurun ba, nafo kubatino kube na awa lanza Ubeleng nan nyan tinu na nit ajinjin ghe.
Herode alipongʼamua kwamba wale wataalamu wa nyota wamemshinda kwa akili, alikasirika sana, naye akatoa amri ya kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kurudi chini katika mji wa Bethlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda alioambiwa na wale wataalamu wa nyota.
17 Ulirue u ni wa kulo vilengwe na iwa bellin kitin Irimiya unan liru nin nuuKutellẹ.
Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia.
18 “I wa lanza liwani nan nyan rama, kuculu nin tiyom a liburi lisirne, Rahilla di kuculu nnono me.”
“Sauti ilisikika huko Rama, maombolezo na kilio kikubwa, Raheli akilia kwa ajili ya wanawe, akikataa kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”
19 Na Hiridus nku gono kadura Kutellẹ da kitin Yusufu nan nya namoro in masar.
Baada ya Herode kufa, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto huko Misri
20 “Aworo, Fita, yauna gono kinesse nin nene, udo nan nyan nmin Israila.”
na kusema, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mwende, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliokuwa wanatafuta uhai wa mtoto wamekufa.”
21 Yusufue fita, a yauna gone nin nene, ada nan nya nmin Israila.
Basi Yosefu, akaondoka akamchukua mtoto na mama yake wakaenda mpaka nchi ya Israeli.
22 Na alanza Arkila usari di tigon yahudiya kudarun ncife, Hiridus, fiu kiffo ghe na ado ba, vat nin woru Kutellẹ nwununghe kutuf nan nya namoro, ana lassina udu nmin ngalili.
Lakini aliposikia kwamba Arkelao alikuwa anatawala huko Uyahudi mahali pa Herode baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye akiisha kuonywa katika ndoto, akaenda zake sehemu za Galilaya,
23 Amini ana wa dak ada da so nkan kipin na idin yiccu kinin unazarati, inan kulo uliru na iwa bellin tinu na nan nliru nnu Kutellẹ ima yiccu ghe kunan Nazarat.
akaenda akaishi katika mji ulioitwa Nazareti. Hivyo likawa limetimia neno lililonenwa na manabii, “Ataitwa Mnazarayo.”

< Matiyu 2 >