< Matiyu 18 >

1 Nanya kubi kurume nono katwa me da kitin Yisa iworo ghe, “Ghari udiawe nanya kipin tigo Kutellẹ?”
Wakati huo, wanafunzi wakamjia Yesu na kumuuliza, “Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?”
2 Yisa yicila gono kibene adak kitime, ayisa ghe kiyitik mine,
Yesu akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao.
3 anin woro, “Kidegene ndin belle munu se anung nsuna alapi mine iso nafo nono nibebene, anung ghe nan nya nkolome libau na iwasa ise upiru kipin tigo Kutellẹ ba.
Naye akasema: “Amin, nawaambia, msipookoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni.
4 Bara nani vat ulle na a toltuno litime nafo gono, kibene kane unit une amere udiawe nan nya kipin tigo Kutellẹ.
Kwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni.
5 Nin ullenge na asere nkang gono kibene nan nya lisa nighe, asere mereku.
“Yeyote amkaribishaye mtoto mdogo kama huyu kwa Jina langu, anikaribisha mimi.
6 Vat nle na ata warum nan nya nibebene nane na iyinna nin mi, ita kulapi, uba katinghe iyaun litala lidia iterighe nto, inin turunghe nan nya kuli kudia kiti kicacam.
Lakini kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa hawa wadogo wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
7 Kash udu uyi bara kubin ntirzuari! bara uso doleari kubi kone ba dak bara ame!
“Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya yale mambo yanayosababisha watu kutenda dhambi! Mambo hayo lazima yawepo, lakini ole wake mtu yule ambaye huyasababisha.
8 Assa ucara sa kubunu fe, bba tifi utiro, werne unin ufilig pit kitife, uba katinfi usee ulai nin kagiisin kidowo, ninworu itufi nan nya nla so ligan uyiita nin ncara sa abunu fe vat. (aiōnios g166)
Ikiwa mkono wako au mguu wako unakusababisha utende dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
9 Assa iyizife bba tiifi utiro, herina linin ufilin kitife, uba katinfi use ulaii nin liyizi lirum, nin woru itufi nan nya nla sa ligun nin niiyizi fe ib. (Geenna g1067)
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe, ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
10 Yenjen na iwa yassu warum nan nya kitene kane nono kadura Kutellẹ mine ko kome kubi idi nyenju nmoru ncif nighe ulle na adi kitene kani.
“Angalia ili usimdharau mmojawapo wa hawa wadogo, kwa maana nawaambia, malaika wao mbinguni daima wanauona uso wa Baba yangu aliye mbinguni. [
11 Bara gono nnit na dak ada tucu nalenge na ina wulu.
Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichopotea.]
12 Iyaghari idi nkpilize? Asa umon unit dinin nakam akalt likure, kurum nanye nwulu, na aba cinu akalt likure udiru kuurume kitene kikup adi piziru kone na kuna wulu ba?
“Mwaonaje? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je, hatawaacha wale tisini na tisa vilimani na kwenda kumtafuta huyo mmoja aliyepotea?
13 Andi ase kunin, kidegen ndi nbellu munu, liburi libo me kitene kukam kurume bba katinu nin gbardang kitene nakam akalt likure udiru kurum na kuna wulu ba.
Naye akishampata, amin, nawaambia, hufurahi zaidi kwa ajili ya huyo kondoo mmoja kuliko wale tisini na tisa ambao hawakupotea.
14 Nan nya nanere, na usun Ncif mine allenge nadi kutenit kane warum nan nya nibebene nai nanna ba.
Vivyo hivyo, Baba yenu wa mbinguni hapendi hata mmojawapo wa hawa wadogo apotee.
15 Asa gwana fine ntafi kulapi, durso ghe utanu me, anung ligan mine, cas, asa a lanza fi, utuucu gwana fine.
“Kama ndugu yako akikukosea, nenda ukamwonyeshe kosa lake, kati yenu ninyi wawili peke yenu. Kama akikusikiliza, utakuwa umempata tena ndugu yako.
16 Andi na a lanzafi ba, yira nuwa na fine unit kiti nwanana urum sa anwaba ido kitime bara iyizi nawaba sa awaatat sa ko lome lugbulang base uyisinu.
Lakini kama hatakusikiliza, nenda na mtu mwingine mmoja au wawili ili kila neno lithibitishwe kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.
17 Asa anari ulanza nanan dortu Yisa, awa nari ulanzu nanan dortu Yisa, na ame so kitife nnafo kulumai sa unan sesen ngandu.
Kama akikataa kuwasikiliza hao, liambie kanisa. Naye kama akikataa hata kulisikiliza kanisa, basi awe kwenu kama mtu asiyeamini au mtoza ushuru.
18 Kidegene re ndin bellu minu, vat nile imon na itere nan nya nnye, iba teru kitene kane, nin vat nile imon na ibunku nnye nanere iba bunku kitene kane.
“Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.
19 Ukpiine ku ndi bellu munu asa an wada nwa yinin nin nimon ule na iba tirrinu menku nan nya nnyi ucif nighe ulle na adi kitene kane bba su nani mun.
“Tena nawaambia, ikiwa wawili wenu watakubaliana duniani kuhusu jambo lolote watakaloomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
20 Bara kiti ka na awaba sa an watat nzuro nan nya lisa nigh, ndi nanghinu.”
Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa Jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.”
21 Nin nani Bitrus da ada belle Yisa ku, “Cikilari, udu timashinari gwana nighba sui kulapi meng shawa muna? udu so kuzora?”
Ndipo Petro akamjia Yesu na kumuuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?”
22 Yisa bellinghe, “Nna meng na bellinfi udu kuzor ba, uduru akalt kuzorii sau kuzor.
Yesu akamjibu, “Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
23 Bara nani, kipin tigo Kutellẹ di nafo umon ugo, na awa dinin su asu kibatiza nan nacin me.
“Kwa hiyo Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme aliyetaka kufanya hesabu zake za fedha na watumishi wake.
24 Kubi ka na awa acizina kibatize, ida nin nkon kucin me ulle na ame din dortughe titalent amui likure.
Alipoanza kufanya hesabu zake, mtu mmoja aliyekuwa anadaiwa talanta10,000, aliletwa kwake.
25 Bara na awa idinin libau nbiuwe ba, Cikilari me na uduka idi lewuughe nin nwane a none umunu vat nile iimon na adumun, ida biyaghe.
Kwa kuwa alikuwa hawezi kulipa deni hilo, bwana wake akaamuru kwamba auzwe, yeye, mkewe, watoto wake na vyote alivyokuwa navyo, ili lile deni lipate kulipwa.
26 Ame kucine dio kutyin, atumuno nbuun me aworo, 'Ccikilari, tursui limuri meng ba biyufi imonẹ vat.'
“Yule mtumishi akampigia magoti, akamsihi yule bwana akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
27 Nin nani, Cikilari kucine, atinna alanza nkunekune me, bunkun ghe, shawan nin nre me.
Yule bwana wa huyo mtumishi akamwonea huruma, akafuta deni lake lote, akamwacha aende zake.
28 Ame kucin kone nuzu ase umon udone licin me ulle na ame din dortu ghe idinari likalt akifo ghe kusholshok, a woroghe, 'Blayi imon ile na ndi ndortu fi.'
“Lakini yule mtumishi alipokuwa anatoka nje, akakutana na mtumishi mwenzake aliyekuwa amemkopesha dinarimia moja. Akamkamata, akamkaba koo akimwambia, ‘Nilipe kile ninachokudai!’
29 Ame udone licinne dio kutyin, adi fo ghe nacara aworo, 'Ta ayi ashau nin mi nba biufi.'
“Yule mtumishi mwenzake akapiga magoti akamsihi akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
30 Ame kucin nburne nari, nin nani, ayiraghe atoghe licin, udu kubi ko na aba biughe ule imon na adin dortu ghe.
“Lakini akakataa. Badala yake, alienda akamtupa gerezani hata atakapolipa hilo deni.
31 Kubii na adone licin nyene ile imon na asu, ayi mine nana. Ida idi belle Cikilari mine vat nile imon na asu.
Watumishi wenzake walipoona haya yaliyotukia wakaudhika sana, nao wakaenda na kumwambia bwana wao kila kitu kilichokuwa kimetukia.
32 Cikilari kucin kone yicila ghe, a bellinghe, 'Fe vat bara uwa sui kuculu.
“Yule bwana akamwita yule mtumishi akamwambia, ‘Wewe mtumishi mwovu! Mimi nilikusamehe deni lako lote uliponisihi.
33 Na fe nwasa ulanza nkunekune ndofine kucine ba? Nafo na meng na lanza nkunekune fe?'
Je, haikukupasa kumhurumia mtumishi mwenzako kama mimi nilivyokuhurumia wewe?’
34 Cikilarri me wa nanna ayi ninghe, a nakpa ghe nacara nanan nfo nanit udu kubi ko na aba biu imon ile na idi ndortu ghe.
Kwa hasira, yule bwana wake akamtia yule mtumishi mikononi mwa askari wa gereza ili ateswe mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa.
35 Nanere wang ucif nighe kitene kani, ba su anunku, asa na anug ba shawa nin nalapi nuana nan nya nibinai mine ba.
“Hivi ndivyo Baba yangu wa mbinguni atakavyomfanyia kila mmoja wenu ikiwa hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.”

< Matiyu 18 >