< Luka 6 >

1 Na iwa di lirin Nassabath na Yesu wadin cin nanya kunen ni leu acurmye wadin nkulu nati ni leu, ipara na cara mene ituna nlee.
Sasa ilitokea kwenye Sabato kwamba Yesu alikuwa akipita katika ya shamba la nafaka na wanafunzi wake walikuwa wakichuma masuke, wakayasuguasugua kati ya mikono yao wakala nafaka.
2 Amon nanya na Farisiyawa woro, “Inyari ita idin nsu nilemong le na i caun isu liri na Sabbth ba?”
Lakini baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Kwa nini mnafanya kitu ambacho si halali kisheria kukifanya siku ya sabato”?
3 Yesu kauwa nani a woro, “Na anung na karanta imung ile na Dauda wasu kube na wa lazan kukpong, ligowe nan nanit na iwa di nanghe?
Yesu, akawajibu, akisema, “Hamkuwahi kusoma kile Daudi alifanya alipokuwa na njaa, yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye?
4 Awa piru kilari Kutelle, ayira uburodi ule na iwa ceu a leu umon nanya ukuru ama alenge na imadi ligo we nan ghe un na priestari cas ile.”
Alikwenda katika nyumba ya Mungu, na akachukuwa mikate mitakatifu na kuila baadhi, na kuitoa baadhi kwa watu aliokuwa nao kuila, hatakama ilikuwa halali kwa makuhani kuila.”
5 Anin woro nani, “Gono nit Ucifari un na Sabath.”
Kisha akawaambia, “Mwana wa Adamu ni Bwana wa Sabato.”
6 Uda among Asabar na awa piru nanya kutii nlira adin dursuzu anite kikane umong unit wa diku nin ku girin cara.
Ilitokea katika Sabato nyingine kwamba alikwenda ndani ya sinagogi na kuwafundisha watu huko. Palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kulia ulikuwa umepooza.
7 Anan niyert nang na Farisiyawa wadin yenju susut sa a ba shinu nin mung unan konu lirin na Sabath, inan se imong ile na inna Vuruzughe mung.
Waandishi na Mafarisayo walikuwa wanamwangalia kwa makini kuona kama angemponya mtu siku ya Sabato, ili waweze kupata sababu ya kumshtaki kwa kufanya kosa.
8 Bara nani ayino ile imung na idin kpilizue nibinai myene a woron nle na ucara di kuger, “Fita, uyisin kitill nanite.” Unite fita a yisina kitene.
Lakini alijua nini walikuwa wanafikiri na akasema kwa mtu aliyekuwa amepooza mkono, “Amka, simama hapa katikati ya kila mmoja.” Hivyo huyo mtu akanyanyuka na kusimama pale.
9 Yesu woro nani, natirin minu, ucaun isu imong icine liri na Sabatha sa isu inanzang i tucu ulai ya sa inanza unin?”
Yesu akasema kwao, “Nawauliza ninyi, ni halali siku ya Sabato kufanya mema au kufanya madhara, kuokoa maisha au kuyaharibu?” Kisha aliwaangalia wote na kumwambia yule mtu,
10 A yenje nani vat anin woro anite, “Nakpa ucara fe.” Ata nani ucara mye kpilaku.
“Nyoosha mkono wako.” Akafanya hivyo, na mkono wake ulikuwa umeponywa.
11 Bara nani ayi mine nana ilira nanya natimine, kitene nile imon na ibasu Yesu ku.
Lakini walijawa na hasira, wakaongeleshana wao kwa wao kuhusu nini wanapaswa wafanye kwa Yesu.
12 Uso nani, nanya nayiri ane a ghana kitene liikup asu nliran, a leo ubun nin kiitike vat nlira kiti Kutelle.
Ilitokea siku hizo kwamba alikwenda mlimani kuomba. Aliendelea usiku mzima kumuomba Mungu.
13 Kubi na kiti nshanta, ayicila nono katuwa mye, a fere annit likure alenge tutung na iwa ni nani lissa “anan kadura.”
Ilipokuwa asubuhi, aliwaita wanafunzi wake kwake, na akawachagua kumi na wawili kati yao, ambao pia aliwaita “mitume.”
14 Tisa nanan kadura mye inughe Simon (ulenge na iwa nighe lisa Bitrus) nin gwana mye Andrawus, Yakubu, Yohanna, Filibus, Bartamalawus,
Majina ya wale mitume yalikuwa Simoni (ambaye pia alimwita Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartolomayo,
15 Matta, Tomas, Yakubu usaun Alfa, Simon, ulenge na idin yicughe Zaloti,
Mathayo, Tomaso na Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni, ambaye aliitwa Zelote,
16 Yahuda usaun Yakubu, nin Yahuda Iskariyoti ulenge na aba lewughe.
Yuda mwana Yakobo na Yuda Iskariote, ambaye alikuwa msaliti msaliti.
17 Kube Yesu tolo kitene likupe nan ghinu ida yisina kiti kitendelen, ligozi na nan katuwa mye gbardang wa duku, nin ligozi nani gbardang na inuzu Nyahudiya nin Urushelima, nin nbui kurawa Sidoniya a Utaya.
Kisha Yesu alitelemka pamoja nao toka mlimani na kusimama mahali tambarare. Idadi kubwa ya wanafunzi wake walikuwa huko, pamoja na idadi kubwa ya watu kutoka Uyahudi na Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
18 Iwa daka ida lanza ghe, ukuru ise ushinu nin tikonu mine, anit alenge na iwadi nniu nin nruhu unanzang iwa shinn.
Walikuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Watu waliokuwa wakisumbuliwa na pepo wachafu waliponywa pia.
19 Ko gha nanya ligoze wa dinin su a dudo ghe bara likara nshishinu vat.
Kila mmoja kwenye hilo kusanyiko alijaribu kumgusa kwa sababu nguvu za uponyaji zilikuwa zikitokea ndani yake, na aliwaponya wote.
20 Ame yene anan katuwa mye a woro, “Anung anan nmariari ulenge na idi akimon, bara anughere anan kipin tigo Kutelle.
Kisha akawaangalia wanafunzi wake, na kusema, “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa maana ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Anan nmariari unughe na idi lanzu kukpon nene, bara anug ba shittu, anan nmariari anughe na idi kuculu, bara iba su tisina.
Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa maana mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mliao sasa, kwa maana mtacheka.
22 Anan nmariari anughe asa anit nnari munu, kubi na ikoso ligo nan ghinu, isu munu nshina, inani nanza munu lisa nworo anug umuguari, bara upiziru lisa ngono nnit.
Mmebarikiwa ninyi ambao watu watakapowachukia na kuwatenga na kuwashutumu ninyi kwamba ni waovu, kwa ajili ya Mwana Adamu.
23 Suun liburi libo liyiri lole, inyizin bara ulanzu nmang, bara fe base uduk udia nanya kitene kani bara acif mine nanere iwa su anan kadura Kutelle.
Furahini katika siku hiyo na kurukaruka kwa furaha, kwa sababu hakika mtakuwa na thawabu kubwa mbinguni, kwa maana baba zao waliwatendea vivyohivyo manabii.
24 Kash anung anang nimon nacara, barra imal seru uduk mine.
Lakini ole wenu mlio matajiri! Kwa maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Kash anung alenge na ishitin nene, bara kukpon ba da munu nin ndu nbun, kash anung na idi tisina. nene, iba su tiyom nin kuculu nin ndu nbun.
Ole wenu mlio shiba sasa! Kwa maana mtaona njaa baadaye. Ole wenu mnaocheka sasa! Kwa maana mtaomboleza na kulia baadaye.
26 Kash anung alenge na anit di nliru gegeme kitene mine, bara acif wa su anan nliru kinu nin nnu Kutelle nanere.
Ole wenu, mtakaposifiwa na watu wote! Kwa maana baba zao waliwatendea manabii wa uongo vivyohivyo.
27 Bara nani meng di belle munu na idin lanzu, taan usu na nan nivira nanghinu, isu imon icine kiti nalenge na inari munu.
Lakini nasema kwenu ninyi mnaonisikiliza, wapendeni adui zenu na kufanya mema kwa wanao wachukieni.
28 Taan aleenge na itamunu unnu nmari, suun alenge na idin tumunu ineo nliran.
Wabarikini wale wanao walaani ninyi na waombeeni wale wanaowaonea.
29 Ame ulenge na areoufi kuwwau kpiliya ghe kunbe, asa umon bollo ugudum fe munu ghe kulutuk fe ku tutun.
Kwake yeye akupigaye shavu moja, mgeuzie na la pili. Kama mtu akikunyang'anya joho lako usimzuilie na kanzu.
30 Na vat nlenge na atirin fi, asa umon nbollo imomon na idi infe, na uwa tiringhe anifi ba.
Mpe kila akuombaye. Kama mtu akikunyang'anya kitu ambacho ni mali yako, usimuombe akurudishie.
31 Ile imon na fe idinin su anit sufi fe wang su nani.
Kama mpendavyo watu wawatendee, nanyi watendeeni vivyo hivyo.
32 Asa fe din su usu nalenge na idinin su fere cas, iyaghari uduk fe? Vat inung anan kulapi dinin nsu nalenge na idinin su mine.
Kama mkiwapenda watu wawapendao ninyi tu, hiyo ni thawabu gani kwenu? Kwamaana hata wenye dhambi huwapenda wale wawapendao.
33 Asa udin suu imon icine kiti nale na idin su fi imon icine, iyaghari uduk fe? Nanere wang anan kulapi din su we.
Kama mkiwatendea mema wale wanaowatendea ninyi mema, hiyo ni thawabu gani kwenu? Kwa maana hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo.
34 Asa udin yenju iba biufi, iyaghari uduk fe? Inung anan kulapi din nizu ure kiti nalenge na idin yenju iba kpillu ini nani tutun.
Kama mkikopesha vitu kwa watu ambao mnategemea watawarudishia, hiyo ni thawabu gani kwenu? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi, na hutegemea kupokea kiasi hicho hicho tena.
35 Taa usu nnan nivira nin fi, usu ghe gegeme. Niza nani ure na iwa ceo kibinai nworu uba seru ba, uuduk fe ba yitu gbardang, uba so gono nnan kitene kani. Bara ame liti mye din su gegeme kiti nale na idinsu ugodiya ba.
Lakini wapendeni adui zenu na watendeeni mema. Wakopesheni na msihofu kuhusu kurudishiwa, na thawabu yenu itakuwa kubwa. Mtakuwa wana wa Aliye Juu, kwasababu yeye mwenyewe ni mwema kwa watu wasio na shukurani na waovu.
36 Lanza nkune kune, nafo Ucif fe na adin lanzu nkunekune.
Iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 Na uwa ti umon aso unan kulapi ba, bara fe wang iwa su fi nani. Na uwa mollu umon ba. Fewang na iba mollu fi ba, shawa nin kulapi namong, fewang iba shawu nin kunfe.
Msihukumu, nanyi hamta hukumiwa. Msilaani, nanyi hamtalaaniwa. Sameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 Niza anit fewang iba niiti, uni udia na iba zinlinu ukuru ituku bara kuyanga kongo na uguro uman mun, kunere iba guni fe ku mun.”
Wapeni wengine, nanyi mtapewa. Kiasi cha ukarimu - kilichoshindiliwa, kusukwasukwa na kumwagika - kitamwagika magotini penu. Kwa sababu kwa kipimo chochote mnachotumia kupimia, kipimo hicho hicho kitatumika kuwapimia ninyi.”
39 Akuru a belle nani tinan tigoldo. “Unan uduu waansa adursu umon unit uduu libauwa? Asa asu nani vat mine ba diu nanya kuwu, su nani ba?
Kisha akawaambia mfano pia. “Je mtu aliye kipofu aweza kumwongoza mtu mwingine kipofu? Kama alifanya hivyo, basi wote wangalitumbukia shimoni, je wasingetumbukia?
40 Unan nmasu nyinnu nimon wasa akata unan dursuzu mye ba, bara kogha kubi ko na amala umase, aba so nafo unan dursuzu mye.
Mwanafunzi hawi mkubwa kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu akiisha kufundishwa kwa ukamilifu atakuwa kama mwalimu wake.
41 Ani iyaghari nta udin yenju limoo nanya niyizin gwana fine, na idin yenju kukunti na ku di niyizifi ba?
Na kwa nini basi wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti lililo ndani ya jicho lako huliangalii?
42 Iyizirari uba bellu gwana fine, 'Gwana nan nkala limoo longo na lidi nanya niyizi,' fe litife na uyene kukunti na ku di nanya niyizife? Fe unan rusuzu liti! Burno ukala kukunti nanya niyisife, nin nani unin yene gegeme limoo longo na lidi niyizin gwana fine.
Utawezaje kumwambia ndugu yako, 'Ndugu, naomba nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,' nawe huangalii boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Kwanza itoe boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utaona vizuri kutoa kibanzi katika jicho la ndugu yako.
43 Bara na kon kutca kucine wansa anaa kumat kunanzang ba, sa kutca kunanzan nii kumat kucine ba.
Kwa sababu hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
44 Bara ko kuyemu kutca idin kunin bara kumat mere. Bara na anit wasa ikala kupu kidowo fimart ba, nanere iwasa ikala inabi nanya fimart kusho.
Kwa sababu kila mti hutambulika kwa matunda yake. Kwa sababu watu hawachumi tini kutoka kwenye miba, wala hawachumi zabibu kutoka kwenye michongoma.
45 Unit ucine nanya nile imon na adin cisu kibinai mye, asa abelle imon ile na idi icine, unan magunta nutuno imon inanzang ile na idi kibinai mye nin nnu mye.
Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu. Kwa sababu kinywa chake husema yale yaujazayo moyo wake.
46 Iyaghari nta idin yicie, 'Cikilari, Cikilari,' nin nani na idin dortu imon ile na nbellen munu ba?
Kwanini mnaniita, 'Bwana, Bwana', na bado hamyatendi yale nisemayo?
47 Vat ulenge na ada kiti nighe, a lanza tigbulang adofino tinin a di nafo.
Kila mtu ajaye kwangu na kuyasikia maneno yangu na kuyatendea kazi, nitawaonyesha jinsi alivyo.
48 Adi nafo unit ule na akee kilari amini nwuzu kiteen anin tuno kutyi ata atata ku. Kubi na uwuru nda kang nmyen nda kilari kane wasa kizillino ba, bara kidinin litino licine.
Anafanana na mtu ajengae nyumba yake, ambaye huchimba chini sana, na kujenga msingi wa nyumba juu ya mwamba imara. Mafuriko yalipokuja, maporomoko ya maji yaliipiga nyumba, lakini hayakuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
49 Bara nani, ulenge na a lanza tigbulang ninghe na adofino tinin ba, aba so nafo unite ulenge na kidiin sa litino licine, aswu uwuru ntolo, nmyen ndofino kilari kane, deddei ki diu, na udiu wa ba caunuu ba.”
Lakini yeyote asikiaye neno langu na hakulitii; mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ulipoishukia kwa nguvu, nyumba ile ilitopata maangamizi makubwa.

< Luka 6 >