< Luka 11 >

1 Na amala nliran nkan kiti, umon nanya nono kadura mye woro, “Cikilari, dursuzo nari usunn nliran nafo na Yohanna wa dursuzo nono kadura mye.”
Ilitokea wakati Yesu alipokuwa anaomba mahali fulani, mmoja wa mwanafunzi wake alimwambia, “Bwana, tufundishe sisi kuomba kama Yohana alivyo wafundisha wanafunzi wake'.
2 Yesu woro nani, “Kubi na iba su nliran woron, 'Ucif na lisafe so lau. Na kipin tigo fe dak.
Yesu akawaambia, Msalipo, semeni, 'Baba, Jina lako litakazwe. Ufalme wako uje.
3 Na nari imonli nkolome liyiri.
Utupe mkate wetu wa kila siku.
4 Shawa nin nalapi bite, nafo na arike din shawuzu nin nalenge na isu nari alapi. Na uwa do ninghirik kiti ndumuzunu ba.'”
Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe wote waliotukosea. Usituongoze katika majaribu.”
5 Yesu woro nani, “ghari nanya mine dimun ndondon, amin ndo kiti mye nin kiyitik, a bellinghe, 'Udon nigh nei ure nakalan nfon gol atat,
Yesu akawaambia, “Ni nani kwenu atakuwa na rafiki, ambaye atamuendea usiku, na kumwambia, Rafiki niazime mikate mitatu.
6 umong udon nigh worin ndak unuzu ncin, na ndinin nile imon na nba nighe ba.'
Kwa sababu rafiki yangu amenijia sasa hivi kutoka safarini, nami sina cha kumuandalia.'
7 Ame ulele nanye ba kawughe, na uwa damei ba, nmal tursu kibulung, meng nan nono nmall noo, nwasu nfita nnafi ufungul ba.
Na yule aliyeko ndani akamjibu, usinitaabishe, Mlango umekwisha kufungwa, na watoto wangu, pamoja nami tumekwisha kulala kitandani. Siwezi kuamka na kukupa wewe mikate.
8 Meng nbellin munu, ko na aba fitu a nighe ufungule ba bara fe udon mere, bara uciu kibinai fe nin salin nlanzu ncing, aba fitu anifi ile imon na udinin su we gbardang.
Nawaambia, japo kuwa haamki na kukupatia mikate kama rafiki yake, kwa sababu ya kuendelea kumgongea bila aibu, ataamka na kukupatia vipande vingi vya mikate kulingana na mahitaji yako.
9 Meng tutun nbellin munu, tirinon iba nii munu, piziran iba se, reyon kibulu aba punu, munu mun.
Nami pia nawaambieni, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata, pigeni hodi nanyi mtafunguliwa.
10 Bara vat nle na atirino aba seru, unan piziru ba se unan nrizu kibulun iba punghe mun.
Kwa kuwa kila mtu aombaye atapokea, na kila mtu atafutaye atapata, na kila mtu apigaye hodi, mlango utafunguliwa kwake.
11 Ghari nanya mine ulenge na adi ikifi gono mye ntiringhe ufungul aba nighe litala, sa fibo anaghe fiyii ya?
Ni baba yupi miongoni mwenu, mwanaye akimuomba samaki atampa nyoka badala yake?
12 Sa atirin likpai, ana naghe finagha?
Au akimuomba yai atampa nge badala yake?
13 Bara nani anung na idi anan maggunta, iyiruufilizinu nimmon icine kiti nono mine, iyaghari ngbardang na ucif mine kitene kani ba nii Uruhu Ulau nale na itiringhe?”
Kwa hiyo, ikiwa ninyi mlio waovu mnajuwa kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, je si zaidi sana Baba yenu wa mbinguni kwamba atawapa Roho Mtakatifu hao wamuombao?”
14 Nin kidughee, Yesu wa di nutuzunu nagbergenu, nan naturi, uso kubi nna agbergenu wa nuzu, unit uture lirina, ligozi nanit kiffo tinu!
Baadaye, Yesu akawa anakemea pepo, na mtu mwenye pepo alikuwa bubu. Ikawa pepo lilipomtoka, mtu huyo aliweza kuongea. Umati wakastaajabu sana.
15 Among nanya nanite woro, “Nin Bazelbula, ugo nagbergenu adin nutuzunu agbergenu.”
Lakii watu wengine wakasema, huyu anaondo mapepo kwa Beelzebul, mkuu wa mapepo
16 Among dumunghe idin piziru nalama unuzu kitene kani.
Wengine walimjaribu na kumtaka awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
17 Yesu yinno ukpilizu mine, a woro nani, “Vat tigo tongo na tidi nivira nati mine ti ba so hem, Kilari ka na kidi nivira nati mine kiba di.
Lakini Yesu aliyatambua mawazo yao na kuwaambia, “Kila ufalme utakaogawanyika itakuwa ukiwa, na nyumba iliyo gawanyika itaanguka.
18 Asa Sheitan di nivira nin liti mye Iyiziyari tigo mye ba yisina? Bara anung nworo ndin nutuzunu agbergenu nin Balzebul.
Kama Shetani atakuwa amegawanyika, ufalme wake utasimamaje? Kwa sababu mwasema natoa mapepo kwa Belzebuli
19 Andi ndin nutuzunu agbergenu nin Balzebul, nin iyanghari anan dortu din nutuzunu muna? Bara nani inung ba so munu anan sharaa.
Kama mimi natoa mapepo kwa Belzebuli, je wenzenu wanatoa mapepo kwa njia gani? Kwa sababu hii, wao watawahukumu ninyi.
20 Ama asa ndin nutuzunu agbergenu nin liyicin Kutelle, kipin tigo Kutelle nda kiti mine.
Lakini, kama natoa mapepo kwa kidole cha Mungu, basi uflame wa Mungu umewajia.
21 Kubi na unan likara, kullun nin na soja idin ncaa kilari mye, imon mye ba so cai,
Mtu mwenye nguvu aliye na silaha akilinda nyumba yake, vitu vyake vitakaa salama.
22 bara kubi ba unan likara nsu inasara a bollo imon likum kit nnite, aba pitirinu imon nacara nnit une.
Lakini akivamiwa na mtu mwenye nguvu zaidi, Yule mtu mwenye nguvu atamnyang'anya silaha zake, na kuzichukua mali zake zote.
23 Ulenge na adi nin mye ba, adi nivira nin mye ame ulenge na apitirno nin mye ba ashagilina.
Yeye asiye pamoja nami yuko kinyume nami, na yeye asiyekusanya pamoja nami hutapanya.
24 Kubi kongo na uruhu inanzang nnuzu kiti nnit, asa akatiza kiti nmyen, adin piziru nshinu, asa na ase ba, a woro, 'Nba kpillu kilari kanga na nna nuzu ku.'
Pepo mchafu amtokapo mtu, huenda na kutafuta mahali pasipo na maji ili ajipumzishe. Atakapokuwa amekosa, husema, 'nitarudi nilipotoka.
25 Na akpilla, aba se kilari ikuzu kinin inin ceo kinin gegeme.
Akirudi na kukuta nyumba imefagiliwa na imekaa vizuri.
26 Aba nuzu adi yiru nton tiruhu kuzor, tongo nati katinghe nin magunta, vat mine ba dak ida so kikane, imali lisosin nnit une ba katinu uburne nin nanzang.
Hivyo huenda na kutafuta mapepo saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe na kuwaleta waje wakae mahali pale. Na hali ya mtu huyo huwa mbaya kuliko ilivyokuwa mara ya kwanza.”
27 Uso kubi na abelle ileli Imone vat, umon uwani ghantina liwui mye nbun ligozi nanit, a woro, “Nmarari liburi longo na lina marufi, nin nayazin ale na una mazin ku.”
Ilitokea kwamba alipokuwa akisema maneno hayo, mwanamke fulani alipasa sauti yake zaidi ya wote kwanye mkutano wa watu na kusema “Limebarikiwa tumbo lililo kuzaa na matiti uliyoyanyonya”
28 Bara nani ame woro, “Anan nmariari alenge na idin lanzu tugbulan Kutelle, inani myin tinin.”
Lakini yeye akasema, wamebarikiwa wale wasikio neno la Mungu na kulitunza.
29 Na ligozi din pitiru anit gbardang, acizina ubellu, ko kuje, kuji magunta ri, idin piziru alama, na amon duku alenge na iba nii nani ba, se an Yunana.
Wakati umati wa watu wanakusanyika na kuongezeka, Yesu akaanza kusema “Kizazi hiki ni kizazi cha uovu. Hutafuta ishara, na hakuna ishara watayopewa zaidi ya ile ishara ya Yona.
30 Nafo na Yunana wa da so alama udu uniniva, nanere tutun gono nnit, ba so alama kiti nko kuje.
Maana kama Yona alivyokuwa ishara kwa watu wa Ninawi, ndivyo na Mwana wa Adamu atakavyokuwa ishara kwa kizazi hiki
31 Uwani ngo Kusari nkudu ba fitu liyiri nwucu kidegen nin nanilime nko kuje ati nani iso anan nca nkul, bara awa duk unuzu nimalin kutyin ada lanza uyiru Solomon, ayene ulenge na akatin Solomon ku kikane.
Malkia wa Kusini atasimama siku ya hukumu na watu wa kizazi hiki na kuwahukumu wao, kwani yeye alitoka katika mwisho wa nchi ili aje asikilize hekima za Solomoni, na hapa yuko aliye mkuu kuliko Solomoni.
32 Nanilime Nninniva ba yisinu liri wucu kidegen, nin nanit kuji kone, iba ti nani iso anan ncaa nkul, bara iwa diu kutyin nin wazi yunana, yene umon duku, akatin Yunana ku adi kikane.
Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki siku ya hukumu watakihukumu, kwani wao walitubu kwa mahubiri ya Yona, na tazama, hapa yuko aliye mkuu kuliko Yona.
33 Na umong duku ulenge na aba ti ulah npitila a nyeshe unin ba, sa kadas kukuzun, se kitene kiti ncise bara alenge na iba piru iyene nkanang.
Hakuna Mtu yeyote, awashaye taa na kuiweka sehemu ya chini yenye giza isiyoonekana au chini ya kikapu, ila huwasha na kuweka juu ya kitu ili kila mtu aingiaye aweze kuona mwanga.
34 Iyizife nnert upitila kiddowo fe ba kullu nin kanag, andi iyizi caun ba, to kidowo fe ba kulu nin Sirti.
Jicho lako ni taa ya mwili. Jicho lako likiwa zuri basi mwili wako wote utakuwa kwenye mwanga. Lakini jicho lako likiwa baya basi mwili wako wote utakuwa kwenye giza.
35 Bara nani su seng, nkanang nanya fe na nsirtiyari ba.
Kwa hiyo, mjihadhari ili mwanga ulio ndani yenu usitiwe giza.
36 Asa nanere, kidowo fe kulun nin nkanang, na nkan kiti di nsirti ba, vat kidowo fe ba so nafo uputila a udin kassu, aba tifi nkanang.”
Hivyo basi, kama mwili wako wote uko kwenye mwanga, na hakuna sehemu iliyo katika giza, basi mwili wako utakuwa sawa na taa iwakayo na kutoa mwanga kwenu.”
37 Kubi na amala utiru, ku Farisiyawa bellinghe au idi lii imonli kilari mye, Yesu do adi lii imonle.
Alipomaliza kuongea, Farisayo alimwalika akale chakula nyumbani kwake, naye Yesu akaingia ndani na kuwa pamoja nao.
38 Kunin Kufarisiya su amamaki nworu atina nlw sa ukusu nacara.
Na Mafarisayo wakashangaa kwa jinsi ambavyo hakunawa kwanza kabla ya chakula cha jioni.
39 Ame Cikilari woroghe, “Anung a Farisiyawa, asa ikusu mamal nkop nin kishik, nanya mine kulun nin ucuci a magunta.
Lakini Bwana akawaambia, “Ninyi Mafarisayo mnaosha nje ya vikombe na bakuli, lakini ndani yenu mmejaa tamaa na uovu.
40 Anung anan sali nati! Na ulenge na ana ke udase, amere na ke nanye ba?
Ninyi watu msio na ufahamu, Je yeye aliyeumba nje hakuumba na ndani pia?
41 na anan sali nimon ile imon na idi nanye, vat nimone bati lau.
Wapeni masikini yaliyo ndani, na mambo yote yatakuwa safi kwenu.
42 Bara nani, kash, anung Afarisiyawa bara idin nizu uzakka nimon kunen vat, inani nsuna imon icine nin su Kutelle. Uso lellei tisu gegeme nin nsu, na tiwa dira usu kagisin nimon ba tutun.
Lakini ole wenu Mafarisayo, kwani mnatoa zaka ya mnanaa na mchicha na kila aina ya mboga ya bustani. Lakini mmeacha mambo ya haki na kumpenda Mungu. Ni muhimu zaidi kufanya yaliyo ya haki na kumpenda Mungu, bila kuacha kufanya na hayo mengine pia.
43 Kash anung Afarisiyawa, idinin su lisosin nbun, nanya nkasssa we.
Ole wenu Mafarisayo, kwa kuwa mnapenda kukaa katika viti vya mbele kwenye masinagogi na kuamkiwa kwa salamu za heshima sokoni.
44 Kash udu kiti mine, idi nafo nissek nanga na idin yenju ba anit sa ipalila sa uyiru mine.”
Ole wenu, kwani mnafanana na makaburi yasiyo na alama ambayo watu hutembea juu yake pasipokujua.”
45 Umong unan yiru nanya nduka Nayahudawa kauwa aworoghe, “Unan yira ile imon na ubelle tigozori kiti bite.”
Mwalimu mmoja wa sheria za Kiyahudi akamjibu na kumwambia, “Mwalimu, unachokisema kinatuudhi pia sisi.”
46 Yesu woroghe, “Kash anung anan nyiru nduka! Bara asa anung na anit kutura gbardang kun nijasin in yauna, anung ba dudu kutura kone nin tiyicin mine ba.
Yesu akasema, “Ole wenu, waalimu wa sheria! kwani mnawapa watu mizigo mikubwa wasiyoweza kuibeba, walakini ninyi hamgusi mizigo hiyo hata kwa moja ya vidole vyenu.
47 Kash udu kiti mine, anun din ke niti nlizinu nin na nan nliru nin nnu Kutelle, alenge na acif mine wa mollusu nani.
Ole wenu, kwa sababu mnajenga na kuweka kumbukumbu kwenye makaburi ya manabii' ambao waliuwawa na mababu zenu.
48 Bara anung iyizi inbari, iyinna nin katuwa nacif mine, bara inughere wa molusu anan nliru nin nuu Kutelle, ina ke nisek mine, inan lizino mung.
Hivyo ninyi mwashuhudia na kukubaliana na kazi walizozifanya mababu zenu, kwa sababu hakika waliwauwa manabii ambao mnajenga kumbukumbu katika makaburi yao.
49 Bara nanere tutun uyiru Kutelle a woro, 'Nba tuu nani, anan nliru nin nuu Kutelle, nin na nan kadura, ibati nani ineo, imolsu amon mine.'
Kwa sababu hiyo pia, hekima ya Mungu inasema, 'Nitawatumia manabii na mitume nao watawatesa na kuwaua baadhi yao.
50 Ko kuje, inughere ba yaunu uhaki nmyi nanan nliru nin nnuu Kutelle mongo na iwa gutun, tun uburnu inye,
Kizazi hiki kitawajibika kwa damu ya manabii waliouawa tangu kuanza kwa dunia,
51 Unuzu nmyi Habila udu Zakariya ule iwa mulu kiyitik nbagadi nin kilari nliran, nanere nworo munu ko kuje ba yaunuu uhakke.
Kutoka damu ya Abeli hadi damu ya Zakaria, aliyeuawa katikati ya madhabahu na patakatifu. Ndiyo, nawaambia ninyi, kizazi hiki kitawajibika.
52 Kash anung anan nyiru nduka na Yahudawa, bara ina yaun imon npunu nyiru, na anung ati mine npira ba, inani nwantina anan pire.”
Ole wenu waalimu wa sheria za Kiyahudi, kwa sababu mmechukua funguo za ufahamu; nyie wenyewe hamuingii, na wale wanaotaka kuingia mnawazuia.”
53 Kubi na Yesu nsuna kikane, anan ninyerte nan na Farisiyawa ighana ghe, isu amusunanghe kitene nimon gbardang,
Baada ya Yesu kuondoka pale, Waandishi na Mafarisayo walimpinga na kubishana naye juu ya mambo mengi.
54 Nkukari nwori ikiffo ghe nanya tigbulang mye.
wakijaribu kumnsana kwa maneno yake.

< Luka 11 >