< Yuhana 17 >

1 Meng Yesu nbelle ilenge imone, a ghantina iyizi me kitene Kutelle aworo, “Ucif, kube nda; ta Usaunfe gongong-
Yesu alipokwisha sema hayo, alitazama juu mbinguni, akasema, “Baba, saa imefika! Mtukuze Mwanao ili naye Mwana apate kukutukuza.
2 nafo na una nighe tigo kitene nanan tilai vat, bara anan na alenge na una nige ulai nsa ligang. (aiōnios g166)
Maana ulimpa Mwanao mamlaka juu ya watu wote ili awape uzima wa milele wote hao uliompa. (aiōnios g166)
3 Ulai un saligaghere ulele: inan yininfi, fere cas Kutelle kidegen, a ame ulenge na una tuu, Yesu Kristi. (aiōnios g166)
Na uzima wa milele ndio huu: kukujua wewe uliye peke yako Mungu wa kweli, na kumjua Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
4 Meng ntafi gongong in yie, na nna kulo katwa ka na unani nsu.
Mimi nimekutukuza hapa duniani; nimeikamilisha ile kazi uliyonipa nifanye.
5 Nene, Ucif, tye ngogong umunu litife wang nin nimus ngongon mongo na nwa dimun ninfi a uyie dutu sa ukye.
Sasa, Baba, nitukuze mbele yako kwa ule utukufu niliokuwa nao kabla ya kuumbwa ulimwengu.
6 Nna durso lissafe kiti nanit alenge na una ni nanyan yii. Inung anit fere, umini na ni inung, inani din dortu ulirufe.
“Nimekufanya ujulikane kwa watu wale ulionipa kutoka duniani. Walikuwa watu wako, nawe ukanipa wawe wangu; nao wamelishika neno lako.
7 Nene inung yiru vat nimon ile na una nii, inan nuzu kitifere,
Sasa wanajua kwamba kila ulichonipa kimetoka kwako.
8 uliru fe na una nii, nna ni nani uliru une. Ina seru tining, inani na yinin kidegenere nna dak unuzu kitife, inani na yinin fere na tuyi.
Mimi nimewapa ule ujumbe ulionipa nao wameupokea; wanajua kwamba kweli nimetoka kwako, na wanaamini kwamba wewe ulinituma.
9 Ndi nani nlira, na ndi su uyii nlira ba, ama inung alenge na unayi, inung anit fere.
“Nawaombea hao; siuombei ulimwengu, ila nawaombea hao ulionipa, maana ni wako.
10 Vat nimon ilenge na idi inang, in fere, imongfe inanghari. Meng ta gongon nanya ni ning.
Yote niliyo nayo ni yako, na yako ni yangu; na utukufu wangu umeonekana ndani yao.
11 Na meng du nanya nyie ba, ama inung anit ane di nanya nyie. Meng din cinu udak kitife. Ucif ulau mino nani nanya lissafe inung alenge na una nii, inan so unit urum, nafo na arik di urume.
Na sasa naja kwako; simo tena ulimwenguni, lakini wao wamo ulimwenguni. Baba Mtakatifu! Kwa nguvu ya jina lako ulilonipa, tafadhali uwaweke salama ili wawe kitu kimoja kama sisi tulivyo mmoja.
12 Kube na nwa di nan ghinu, nwa ceo nani nanya lissa fe alenge na uwa nii; nwa kesse nani, na unit urum na wolu ba, se ame gonon nnanu, bara ulirufe nan se ukulu.
Nilipokuwa nao, mimi niliwaweka salama kwa nguvu ya jina lako ulilonipa. Mimi nimewalinda, wala hakuna hata mmoja wao aliyepotea, isipokuwa yule aliyelazimika kupotea ili Maandiko Matakatifu yapate kutimia.
13 Nene ndincinu udak kitife; ama ndin bellu ile imone nanya nyi, bara ayiabo mine nan se ukulu nati mine.
Basi, sasa naja kwako, na nimesema mambo haya ulimwenguni, ili waweze kushiriki kikamilifu furaha yangu.
14 Nna ninani ulirufe, uyi na nari inung, bara na inung anan yieri ba, nafo na meng kunan yiere ba.
Mimi nimewapa neno lako, nao ulimwengu ukawachukia, kwa sababu wao si wa ulimwengu kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
15 Na ndi nlira ukala nani nanya inyieba ama u kesse nani nin nanan naburi asirne.
Siombi uwatoe ulimwenguni, bali naomba uwakinge na yule Mwovu.
16 Na inung anan yiere ba, nafo na meng kunan yieri ba.
Wao si wa ulimwengu, kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
17 Kusu wesse nani nin kidegen, ulirufe kidegenghari.
Waweke wakfu kwa ukweli; neno lako ni ukweli.
18 Una tuyi nanya nyii, meng uni na tuu nani nanya yie.
Kama vile ulivyonituma ulimwenguni, nami pia nimewatuma wao ulimwenguni;
19 Bara inung, meng na wesse litinighe, inung atimine wang nan se uwessu nanya kidegene.
na kwa ajili yao mimi mwenyewe najiweka wakfu ili nao pia wafanywe wakfu katika ukweli.
20 Na bara alele cas ndin su nlira ba, umunu alenge vat na ima yinnu unuzun liru mine.
“Siwaombei hao tu, bali nawaombea pia wote watakaoamini kutokana na ujumbe wao.
21 Bara inan so arume vat, nafo nafe Ucif, udi nanya ning, a meng yita nanyafe. Ndin lira inung wang yita nanya bite uyie nan yinna fere na tuyi.
Naomba ili wote wawe kitu kimoja. Baba! Naomba wawe ndani yetu kama vile wewe ulivyo ndani yangu nami ndani yako. Naomba wawe kitu kimoja kusudi ulimwengu upate kuamini kwamba wewe ulinituma.
22 Ngongonghe na una nii, nna nii nani unin, inung wang nan yita urum, nafo na arike di arum-
Mimi nimewapa utukufu uleule ulionipa mimi, ili wawe kitu kimoja kama nasi tulivyo mmoja;
23 Meng nanya mine, a fe nanya ning, inan se ukulu nanyan warume; bara uyie nan yinno fere na tuyi, umini dinin su mine nafo na udinin su ninghe.
mimi niwe ndani yao, nawe uwe ndani yangu; naomba wakamilishwe na kuwa kitu kimoja, ili ulimwengu upate kujua kwamba wewe ulinituma, na kwamba unawapenda wao kama unavyonipenda mimi.
24 Ucif, aleli na una nii wang. Ndin piziru inung yita nan mi kiti kanga na nduku, inan yene ngongong nighe, mongo na uwa nii: bara udi nin su nighe a i ditu sa ucizinun kye in yii.
“Baba! Nataka wao ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili wauone utukufu wangu ulionipa; kwa kuwa ulinipenda kabla ya kuumbwa ulimwengu.
25 Ucif katwa kacine, na uyii yirufi ba, ama meng yirufi, inung alele yiru fere na tuyi.
Baba Mwema! Ulimwengu haukujui, lakini mimi nakujua. Hawa nao wanajua kwamba wewe ulinituma.
26 Nna durso nani lissafe, tutung nba ti nani iyinin bara usuwe na udi mun nan yita nati mine, meng wang nan yita nanya mine.”
Nimekufanya ujulikane kwao na nitaendelea kufanya hivyo, ili upendo ulio nao kwangu uwe ndani yao, nami niwe ndani yao.”

< Yuhana 17 >