< Yakubu 4 >

1 Nweri kabung nin diru yinnu nin nati ku nanya mine? na kudin fitizu nan nya mine unucu nlip nibinai ni nanzang na udin su likum nan nya mine ba, linuwa anan yinnu nin kutellẹ ba?
Ugonvi na migogoro miongoni mwenu vyatoka wapi? Haviinuki kutoka katika tamaa zenu mbaya zinazoleta vita ndani ya washirika wenu?
2 Idin nlip nimon ille na idumun ba, idin molsu ikuru ipizira imon ile na i wasa ise ba. Idin su nnun.
Mnatamani kile msichokuwa nacho. Mnauwa na mnafukuzia kile msichoweza kuwa nacho. Mnapigana na kugombana, na bado hampati kwa sababu hamumwombi Mungu.
3 Isu kabung ku, vat nani na isebabura na itirino kutellẹ ba. Idin tiru a na i sare ba, bara idin ntiru imon inanzang, inan moluso libau nsu nibinai mine.
Mnaomba na hampokei kwa sababu mnaomba kwa ajili ya mambo mabaya, ili kwamba muweze kuvitumia kwa tamaa zenu mbaya.
4 Anung anam zina! akilaki, Na iyiru nwoni lidondong nin yih ulele nshinari nin kutellẹ ba? Bara nani ulle na ayinna asu lidondon nin yih a durso litime unan shina Kutellẹ.
Enyi wazinzi! Hamjui kwamba urafiki na ulimwengu ni uadui dhidi ya Mungu? Kwa hiyo, yeyote aamuaye kuwa rafiki wa ulimwengu hujifanya mwenyewe adui wa Mungu.
5 Sa idin cissu uliru Kutellẹ naso lem na unaworo uruhu Kutellẹ na ina ti nan nyo bite ukulun nin lip liyarin na?
Au mnadhani maandiko hayana maana yasemapo kwamba Roho aliyoweka ndani yetu ana wivu sana kwa ajili yetu?
6 Nan nya nani Kutellẹ na nani ubolu me gbardang, bara na uliru Kutellẹ na woro, “Kutellẹ nari anan tikunang liti, ana niza ubelu me kiti nale na itoltuno uti mine”.
Lakini Mungu hutoa neema zaidi, ndiyo maana maandiko husema, “Mungu humpinga mwenye kiburi, lakini humpa neema mnyenyekevu.”
7 Bara nani, nan ati mine kiti Kutellẹ, taan shakk nin nshaitan, a nan nya pit nan ghinu.
Hivyo, jitoeni kwa Mungu. Mpingeni ibilisi na yeye atakimbia kutoka kwenu.
8 Dan susut nin Kutellẹ, amac wang ma daksusul nan ghinu, kusun achare mine lau anung anan nalapi, wesen nibincu mine, anung anan nibinayi nibaba.
Sogeeni karibu na Mungu, na yeye atakaribia karibu nanyi. Safisheni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na takaseni mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.
9 Sun liburi lisirne a tiyom nin kuculu. Kpilliyan tisina mine ti tinana nayi, so ulanzun nmang mine lawa liburi lisirne.
Huzunikeni, ombolezeni, na kuria! Geuzeni kicheko chenu kuwa huzuni na furaha yenu kuwa maombolezo.
10 Toltunon atimine nbun Ncikilari Ame ma ghantin minu.
Jinyenyekezeni wenyewe mbele za Bwana, na atawainua juu.
11 Na iwansu kubellum natimine ba, linuana, unit ulle na asu kubellum ngwana sa ushariya ngwana, adin su ushara nan nyan nshara Kutellẹ. Asa usu uduka ushara fe wang na una dortu nsharawere ba, fe nso sharan nin nari.
Msineneane kinyume ninyi kwa ninyi, ndugu. Mtu anenaye kinyume na ndugu yake, au kumhukumu ndugu yake, hunena kinyume na sheria na huihukumu sheria ya Mungu. Mkiihukumu sheria, hamuitii sheria, bali mnaihukumu.
12 Unit urumari cas unan nizun duka nin shariyawe, ame Kutellẹ, ulle na amere wasa asu utucu nin molsu, fe ghari, unan su ndọ lissan fe ushara?
Ni mmoja tu ambaye ni mtoa sheria na hakimu, Mungu, yeye ambaye ana uwezo wa kuokoa na kuangamiza. Wewe ni nani ambaye unamhukumu jirani yako?
13 Lanza fe ulle na udin bellu, “Kitimone sa udun kwoi tiba du nanya kipin, ti duru likus kikans, ti di su kujauna tise uriba”.
Sikilizeni, ninyi msemao, “Leo au kesho tutakwenda katika mji huu, na kukaa mwaka huko, na kufanya biashara, na kutengeneza faida.”
14 Ghari yiru imon ille na ina se ninkwui, iyaghari ulai mine? Idi nafo ulonna3i na sas unuzu nin kubiri bat umala kiti.
Ni nani ajuaye nini kitatokea kesho, na maisha yenu ni nini hasa? Kwa kuwa mnafanana kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi na kisha hupotea.
15 Bara nani mbara iworo nengbe “asa cikilari inyinna tiba yitu nin lai tisu ilenge sa ileli.
Badala yake mngesema, “kama ni mapenzi ya Bwana, tutaishi na tutafanya hiki au kile.”
16 Nene idin fo figiri nin zkpilizu mine, vat ulle ufo figire unanzanghari.
Lakini sasa mnajivuna juu ya mipango yenu. Majivuno yote hayo ni uovu.
17 Bara nani kitin nle na ayiru usu nimon icine amini nari usue, kitime kulapiyari.
Kwahiyo, kwake yeye ajuaye kutenda mema lakini hayatendi, kwake huyo ni dhambi.

< Yakubu 4 >