< Yakubu 2 >

1 Nuwana ning, na iwa dortu uyinnu sa uyenu un Cikilari bite Yisa Kristi, Cikilari ngongon, nin su liti sa maferu feru ba.
Ndugu zangu, mkiwa mnamwamini Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwabague watu kamwe.
2 Asa umong npira ada se minu nan nya lisosin mine nin ficancan fin zinariya nin nimon igegeme, umong tutun pira kikimon unan diru nimon nacara nin nimọn ndinong,
Tuseme mtu mmoja ambaye amevaa pete ya dhahabu na mavazi nadhifu anaingia katika mkutano wenu, na papo hapo akaingia mtu maskini aliyevaa mavazi machafu.
3 anung ani nceo ayi mine kiti nnit unan nimon igegeme, inin woroghe ''cikusu da so kiti kigegeme'' inin woro unan diru nimon nacare, ''Yisina kikani'' sa ''So nabunu ning,''
Ikiwa mtamstahi zaidi yule aliyevaa mavazi ya kuvutia na kumwambia: “Keti hapa mahali pazuri,” na kumwambia yule maskini: “Wewe, simama huko,” au “Keti hapa sakafuni miguuni pangu,”
4 na anughe din su ushara nan nya nati mine, iso anan shara nin kpilizu unanzan ba?
je, huo si ubaguzi kati yenu? Je, na huo uamuzi wenu haujatokana na fikira mbaya?
5 Lanzan nuwana nayi ningh, na Kutellẹ na fere anan sali nimon nacara in yih ulele iso anan nimon nan nya yinnu sa uyenu nin sen gadu tigoh na awasu likawali udu kiti nale na idumun su me ba?
Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni! Mungu amechagua watu ambao ni maskini katika ulimwengu huu ili wapate kuwa matajiri katika imani na kupokea Utawala aliowaahidia wale wanaompenda.
6 Anunghe nin di yassu anan diru nimon nacara! Na anan nimon nacarere din yoh minu bå, na inunghere din cin ninghinu kutẹin nsharawe bå?
Lakini ninyi mnawadharau watu maskini! Je, matajiri si ndio wanaowakandamizeni na kuwapeleka mahakamani?
7 Na anan nimon nacarere din nanzu lisa ligegeme longo na iwa yicila minu mun ba?
Je, si haohao wanaolitukana hilo jina lenu zuri mlilopewa?
8 Vat nin nani asa ukulo uduka tigowe nafo na ina yertu nan nya liru Kutellẹ, ''Uma su usü nnan lisosin kupofe nafo litife,'' usu gegeme.
Kama mnaitimiza ile sheria ya Utawala kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Mpende binadamu mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe”, mtakuwa mnafanya vema kabisa.
9 Nin nani asa ufere among usu nani imon icine, udin su kulapi, ushara nkifofi ina nin so anan nalapi.
Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo Sheria inawahukumu ninyi kuwa mna hatia.
10 Ulenge na adoffino uduka vat, aminin tana nan nya nrum cas, aso unan tanu nan nyan duke vat.
Anayevunja amri mojawapo ya Sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja Sheria yote.
11 Ame Kutellẹ na ana woro “Na uwa su uzina ba,'' amere kuru aworo ''na uwa molsu anit ba,'' andi na usu uzina, umini na molo unit, uso unan kalin duka Kutellẹ.
Maana yuleyule aliyesema: “Usizini,” alisema pia “Usiue”. Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini lakini umeua, wewe umeivunja Sheria.
12 Nani imon ile na idin bellẹ na iso innare idin sue, nafo na ale na iba sunani ushara nbuntu.
Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.
13 Bara ushara din dasu sa nkune-kune kiti nalenge na idin dursu nkune- kune ba. Nkune-kune din li likaran shara.
Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.
14 Iyaghari gegeme nuwana nin assa umonn nworo adumun nin yinnu sa uyenu a na ayita nin katwa kacine ba, uleli u yinnu sa uyene wasa utuchu-ghe?
Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?
15 Asa gwana kilime sa kishono din pizuru nimon shonu kidowo nin nimonli liyirin,
Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.
16 umaong nan nya mine woro nani ''cang idi so mang, ilanza momo illi ishito, a na anung in nin nani imonle na idin pizure bara kidowo ba, iyaghari ngegeme?
Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: “Nendeni salama mkaote moto na kushiba,” bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?
17 Nanere wang unin uyinnu sa uyenu andi na katwa kacine duku ba, libiari.
Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.
18 Vat nani asa umong woro, ''Fe dumun yinnu sa uyenu, a meng yita nin katuwa kacine,'' dursai uyinnu sa uyenu fe sa katuwa, meng ba dursu fi uyinnu sa yenu ninghe nan nya katwa nighe.
Lakini mtu anaweza kusema: “Wewe unayo imani, mimi ninayo matendo!” Haya! Nionyeshe jinsi mtu anavyoweza kuwa na imani bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
19 Uyinna Kutellẹ kurumari nanere. Agbergenu wang in yinna nani ketuzu.
Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.
20 Udi nin su uyinin wangha unit ulala, nworu uyinnu sa uyenu sa katuwa uso hem.
Mpumbavu wee! Je, wataka kuonyeshwa kwamba imani bila matendo imekufa?
21 Ndunsu ame Ibrahimẹ, uciff in yinnu sa uyenu bite wa se useru kiti Kutellẹ bara katuwa kacine na awa nakpa gono me Ishaku kiti Kutellẹ?
Je, Abrahamu baba yetu alipataje kukubalika mbele yake Mungu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa mwanae Isaka sadaka juu ya madhabahu.
22 Uyene uyinnu sa uyenu me na cinu nin katuwa me, nanere wang katuwa me na kulo nan nya yinnu sa uyenu me.
Waona basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.
23 Nanere uliru Kutellẹ wa kulo na uwa woro “Ibrahim wa yinnin nin Kutellẹ, unnere iwa bataghe unan fiu Kutellẹ.” Bara nani iwa yicughe udondon Kutellẹ.
Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki wa Mungu.”
24 Uyenẹ, kiti katuwari unit nse usurtu, na kitenen yinnu sa uyenu chas ba.
Mnaona basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake na si kwa imani peke yake.
25 Nanere wang Rahap ukilaki wase usurtu bara katwa kacine, kubẹ na awa seru anan kadura, a duro nani long libau ugang?
Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.
26 Nafo kidowa sa nfip libbiari, Nanere wang uyinnu sa uyeni sa katuwa libbiari.
Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.

< Yakubu 2 >