< Ibraniyawa 4 >

1 Bara nani, uso tiba su seng, nworu na umong bite wa dira uduru nli nbun nalikawali npiru nshinu Kuttelle ba.
Mungu alituahidia kwamba tutaweza kupata pumziko hilo alilosema. Basi, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo.
2 Bara tina se uliru ucine kitene nshinu Kutelle ulle na iwa bellin nari nafo na an Isiraila wandi, nin nani na kani kadure wan kpin imomon kiti nale na ina lanza, sa uwuro imuni uyinnu sa uyenu ku ba.
Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
3 Bara arike, allenge na tiwa yinin - arikere alenge na tiba piru ushinu une, nafo na ina bellin “nafo na nna sillo nanya tinana nayi nighe, na inu nghe ba piru nshinu ni nghe, ba”. Awa bellin nani ko nin nworu makeke katuwa me nmalla unuzu ncizinu nnyi.
Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
4 Bara ana bellin nkan kiti, ubellen liyiri nasabar “Kutelle wa shin vat katuwa me liyiri nasabar”.
Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.”
5 Tutun amini wa woro “na inug ba piru ushinu nighe ba.
Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.”
6 Bara nani, tunda na iwa ceo ushinu Kutelle, among nan pira, tunda na an Isiraila gbardang na lanza uliru ucine, kitene nshinu una ipira ba bara usalin ndortu Kutelle:
Wale waliotangulia kuhubiriwa Habari Njema hawakupata pumziko hilo kwa sababu hawakuamini. Wapo, basi, wengine ambao wangejaliwa kulipata.
7 Kutelle nakuru nlon liyiri na idin yicu “kitomone” ana kele liyiri lole kubi na awa liru kiti Dauda, ulenge na awa bellin uworsu kube na iwadi imal bellu”. “Kitimone asa ulanza liwui me, na uwa ti gbas nin kibinayi fe ba”.
Jambo hili ni wazi, kwani Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo”. Miaka mingi baadaye Mungu alisema juu ya hiyo siku kwa maneno ya Daudi katika Maandiko yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu.”
8 Bara andi Joshuwa wa ni nani ushinu, na Kutelle wasu uliru kitene nlon liyiri ba.
Kama Yoshua angaliwapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.
9 Bara nani, udak nene nlon liyiri na sabar duku na ina ceo bara annit Kutelle.
Kwa hiyo, basi, bado lipo pumziko kwa watu wa Mungu kama kule kupumzika kwake Mungu siku ya saba.
10 Ame ulenge na apira nshinu Kutelle, ata litime tutun ashino nanya nadadu me, nafo Kutelle nanya kan me.
Maana, kila anayepata pumziko aliloahidi Mungu atapumzika baada ya kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika baada ya yake.
11 Bari nani, na tiyita nin nayi npiru nshinu une, bara umong wa dira nanya nsalin dortu Kutelle na idin su.
Basi, tujitahidi kupata pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwenu atakayeshindwa, kama walivyofanya wao kwa sababu ya ukosefu wao wa imani.
12 Tigbullang Kutelle ti duku, nin likara akatin litan kileou, asa a wuso nin kosu kidowo nanya nruhu, anin munu gbolgbok, amini nwansa a yinno ukpilizu kibinayi nin nniya.
Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali zaidi kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na mafuta. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.
13 na imon makeke nyeshin nyenju Kutelle ba, bara nani, imon vat di fisere nin fong kiti niyizi ame ulle na tiba ni kibatiza kitime.
Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake. Kwake, sisi sote tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
14 Tidi mun npirist udia, ulenge na ana katah udu kitene, Yisa gono Kutelle, na ti min uyinnu bite nin likara gangang.
Basi, tunapaswa kuzingatia kwa uthabiti imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka kwa Mungu mwenyewe—Yesu, Mwana wa Mungu.
15 Na tidimun npirist udia ulenge na a sali sa ulanzu nkunekune bite bara usali likara ba, ame ulenge nanya vat tibau ina dumun nghe nafo arike, ame cas di sa kulapi.
Huyu Kuhani Mkuu wetu si mmoja ambaye hawezi kutuunga mkono katika unyonge wetu, ila ni Kuhani Mkuu ambaye alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
16 Na arike kuru ti dak nin yinnu kibinayi, kiti kutet tigo naliheri, tinan sere ntop nin se naliheri udu nbunu kubi ndamuwa.
Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu, palipo na neema, ili tukajipatie huruma na neema ya kutusaidia wakati wa lazima.

< Ibraniyawa 4 >