< Ugalantiyawa 1 >

1 Nuwana nilime nan nishono nan nya Kipin tigo in Galantiyawa. Meng Bulussari, unan kadura na unuzu kiti nanit ba, a na unuzu kiti nnit ba, unuzu kitin Yisa Kristiari nin Kutellẹ Uciffe, ulenge na awa fiyaghe nan nya nkul.
Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
2 Nin linuana vat na idi ligowe nin mi udu nilarin nlira in Galatiya.
na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
3 Ubollu Kutellẹ udu kiti mine nin lisosin limang unuzu kiti Kutellẹ Ucifbit nin Cikilari bit Yisa Kristi,
Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
4 na awa ni litime bara alapi bite, anan se a bolo nari nan nya kubiri kunanzang nado ukpilizu Kutellẹ bit nin Ciff bit. (aiōn g165)
aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
5 Kitimerẹ ngongong so saligan Usonani. (aiōn g165)
Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
6 Imonen nayi fiu nin kpillu mine nan nya nliru ntucu uburnẹ na ina seru udu umong ugang. Nin kpillu nati mine kitin lenge na ana yicila minu nin bolun Kristi.
Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
7 Na umong ulirun tuchu duku ugang ba, vat nani among anit din fizu ayi nanit inan musuzu ulirun tuchun Kristi.
ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
8 Sa arike sa Gono kadura Kutellẹ unuzu kitene kani nda minu nin kankadura ugang nin lenge na tina malu ubellin minu na unu kifoghe.
Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
9 Nafo na tiwa bellin minu nin burnẹ, nene wang ndin bellẹ tutung, ''Asa umong bellin minu ulirun ntucu ugan nin le na ina malu useru, tan ghe unu.''
Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
10 Negene meng din pizuru uyinnu nanitari sa un Kutellẹ? sa ndin pizuru npwo anit ayeri? Asa meng nengene ndi ninsu npwo anit ayeri, na meng kuchin Kristari ba.
Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
11 Bara ndinin su iyinin nuana, ulirun ntuchu na ndin bellu na un na nitari ba.
Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
12 Na nna seru kitin nitari ba, a na umon na dursuzai unin ba, una na nadak kitinighe unuzu kitin Yisa Kristari.
Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
13 Iwa lanza lisosin nburu nighe nan nya nadini na Yahudawa na nwa ti butan butang nnanzu nliru Kutellẹ nin na nan ndortu Kutellẹ, ineo kang sa ligang.
Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
14 Meng wadi nlibun pït nan nya nadini na Yahudawa nkatiza adon nighe a Yahudawẹ. Meng wa di nin liyarin kan nbellen dortu matiza naciff ning.
Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
15 Kubi ko na Kutellẹ wa lanza nmang afereyi ndutu nan nya liburin naning. Awa yicilai nan nya me.
Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
16 Adurso Gono me kiti ning, nnan yino ubellun liru me kitik nalumai. Na nwa mala upizuru in yinnu nin kidowo nin mï ba,
alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
17 ana nwa do u Urushalime kiti na lenge na iwa yarni katawa ba. Nwa do Arabiyari, nnin kpilla u Damascus tutung.
wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
18 Na akus atat nnin kata, nnin ghana udu lizi ngan Kefas in Urushalima nta ayiri likure nin na taun ligowe ninghe.
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
19 Vat nayiri ane nan nta, na nwayene umong nan nya nono katwe ba, ma Yakuburi cas gwanan NCikilare nwa yeneghe ku.
Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20 Yenen nbun Kutellẹ wang, na ndimunu kinu nan nya niyerte na nsu minu ba.
Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
21 Nin kiddughe nmini wa do nmin Siriya nin silisiya.
Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
22 Vat nani nan nyan Yahudiya alenge na iwa dortu nan nya nilarin nlira wa di isa yinni ba.
Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
23 Iwa din lanzun belle nighere cas, '' Ulenge na awa nadi unan lantizu nari ukul nengene din su uwazi in yinnu ulenge na ame wadin musuzun unin.''
Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
24 Inani wa tizu Kutellẹ gongong bara mewẹ.
Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.

< Ugalantiyawa 1 >