< Katwa Nono Katwa 26 >

1 Agrippa woro in Bulu ku, “Uwasa usu uliru nin litife” Bulus nakpa ucara me asu uliru nkussu litime.
Ndipo Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujitetea.” Hivyo Paulo akawaashiria kwa mkono wake, akaanza kujitetea, akasema:
2 “In yira liti ning unan ayi abo, ugo Agrippa, nsu uliru nighe nbunfe kimone nbelleng nimon ile ena a Yhudawa na belin liti ning;
“Mfalme Agripa, najiona kuwa na heri kusimama mbele yako leo ninapojitetea kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi,
3 bara fe unan yiraari kitine vat ntanda na Yahudawa nin tiru mine. Ndin tiru fi nworo ulanzai nin nayi ashau.
hasa kwa sababu unajua vyema desturi zote za Kiyahudi na ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na masuala ya mabishano. Kwa hiyo, nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.
4 Kidegere, a Yahudawa vat yiru imusun lissosin longo na nna su a in yita kwanyana nmin nighe nin Ushalima.
“Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu nilipokuwa mtoto, kuanzia mwanzo wa maisha yangu katika nchi yangu na pia huko Yerusalemu.
5 Innung yiru ucizunighe tutung ucaun inin yinin nworu meng ku farisawari, alenge na idin kpilizu imon hem ba.
Wao wamefahamu kwa muda mrefu na wanaweza kushuhudia kama wakipenda, ya kwamba kutokana na misimamo mikali sana ya dhehebu letu kwenye dini yetu, niliishi nikiwa Farisayo.
6 Nene in yissing kikane bara ndin piziru nciu nliru ulenge na kutelle wa ni acifi bite.
Nami sasa ni kwa sababu ya tumaini langu katika kile ambacho Mungu aliwaahidi baba zetu, ninashtakiwa leo.
7 Bara nanere akura nnonon Israila na su Kutelle katwa kitik nin lirin nan nya kidegen, arik ani nceo ayi ti duru kite bara ule uciu nayere a Yahudawa nvuroyi, Ugo!
Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
8 Iyaghari nta idin yenju uma konu Kutelle fya anan kul?
Kwa nini yeyote miongoni mwenu afikiri kwamba ni jambo lisilosadikika Mungu kufufua wafu?
9 Nkon kubi asa nkpilza nsu imon gambalang gbardang kitene lissan Yesu Nnazareth.
“Mimi pia nilikuwa nimeshawishika kwamba imenipasa kufanya yote yale yaliyowezekana kupinga Jina la Yesu wa Nazareti.
10 Nna su in Urshalima; nwa yaccu anan katwa kacine kilari licin gbardang, nwa seru likara nsu nani kiti ndya na priest iwa molusu nani, asa mere yinna isu nani.
Nami hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Kwa mamlaka ya viongozi wa makuhani, niliwatia wengi wa watakatifu gerezani na walipokuwa wakiuawa, nilipiga kura yangu kuunga mkono.
11 Ina tizu nani ineo kang nan nya nilari nlira mine nkuru ntiza nani izoguzu Kutelle. Nwa yita nin tinana nayi nin ghinu kang ndortu nani uduzu mmin das.
Mara nyingi nilikwenda kutoka sinagogi moja hadi ingine nikiamuru waadhibiwe, nami nilijaribu kuwalazimisha wakufuru. Katika shauku yangu dhidi yao, hata nilikwenda miji ya kigeni ili kuwatesa.
12 Na nwa din su nani, Nwa do Udamaska nin yinnu a likara ngo na priest;
“Siku moja nilipokuwa katika mojawapo ya safari hizi nikiwa ninakwenda Dameski, nilikuwa na mamlaka na agizo kutoka kwa kiongozi wa makuhani.
13 libowe ucin due, nin wui gberere, Ugo, in yene imon nkanan unuzu kitene Kutelle mida mala kiti bite vat umunu alenge na iwa din cin ligowe nan mi.
Ilikuwa yapata adhuhuri, ee mfalme, nilipokuwa njiani, niliona nuru kutoka mbinguni kali kuliko jua, ikingʼaa kunizunguka pande zote mimi na wale niliokuwa pamoja nao.
14 na vat bite ndeo kutyen, nlanza liwui nin ti Ibrananci din liru nin mi, 'Shawulu, Shawulu, iyaghari nta udin tizui nneo? Uwa konui men nari.'
Wote tulipokuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, mbona unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.’
15 Ntunna nworo, fe ghari, Cikilaria? Cikilare kawa, ' men Yesu ule na udin funu ghe.
“Nikauliza, ‘Ni nani wewe, Bwana?’ “Naye Bwana akajibu, ‘Ni Mimi Yesu unayemtesa.
16 Nene fita uyissin nin nabunu fe; bara ile imonere ndurso liti nighe kitife, nfere fi uso kucin a unan wazi nbell nimon ile na uyiru inin nin nen nin nimon ile na Mma dursu fi iwa dandaun;
Sasa inuka usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuteue uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeyaona, na yale nitakayokuonyesha.
17 mma tucu fi na cara nanite nin na wurme alenge na mma tuu fi ucindu kitimine;
Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
18 udi pun iyizi mine uti nani ikpilin isun adu nsirti mine udak nan nya nkanang, nan nya likara nshaitan udak likara Kutelle, inan se ukussu nalapi kiti Kutelle, nin gadu ulenge na ina ni ceo nani nin liti nighe nan nya yinnu sa uyenu.'
uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
19 Bara nani, Ugo Agrippa, Na nna dira uyinnu nin anabci Kutelle ba;
“Hivyo basi, Mfalme Agripa, sikuacha kuyatii yale maono yaliyotoka mbinguni,
20 amma, kiti na lenge na idin Damaska tukuna, nin na nan Urshalima, nin na lenge vat na idi nmin in Yhudiya, a ining awurmi, ndi wazi i sun alapi mine ikpilin kiti Kutelle, isu imon ile na ima dak nin sunu nalapi.
bali niliyatangaza kwanza kwa wale wa Dameski, kisha Yerusalemu na katika vijiji vyote vya Uyahudi na pia kwa watu wa Mataifa, kwamba inawapasa kutubu na kumgeukia Mungu na kuthibitisha toba yao kwa matendo yao.
21 Bara ile imonere a Yahudawa na kifo nannya kilari nlira inani pizira imolui.
Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua.
22 Kutelle koni na buni udak nene, in yissin nbelin nbun na talaka nin nanit adidya na umong ubeleng ugan ba se ulenge na anan liru nin nuu Kutelle nin Musa na belin uma se;
Hadi leo nimepata msaada kutoka kwa Mungu, na hivyo nasimama hapa nikishuhudia kwa wakubwa na wadogo. Sisemi chochote zaidi ya yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia:
23 nworu Kristi ma niu gbas, tutng ama yitu unan burnun fitu nan nya nissek anin kuru a durso nkanang kiti na Yahudawa nin na wurmi.
kwamba Kristo atateswa, na kwamba yeye atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, na atatangaza nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.”
24 Na Bulus nmala ukusu litime, Fastos woro nin liwui gberere, “Bulus uta ilaza; uyiru udya fe nta fi ilaza.”
Paulo alipokuwa akifanya utetezi huu, Festo akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, wewe umerukwa na akili! Kusoma kwingi kunakufanya uwe kichaa!”
25 Amma Bulus woro ghe, “Na ndi nin nilaza ba Fastos unit udya; amma nin nayi akone ndin su liru kidegen nin toltenu liti.
Lakini Paulo akajibu, “Mimi sijarukwa na akili, mtukufu sana Festo, bali nanena kweli nikiwa na akili zangu timamu.
26 Bara Ugo yiru ubelleng nilenge imone, bara nani, ndi woas nsu nin ghe, bara meng yiru na imonmong nyeshin kiti me ba, bara na ina su ilenge imone likot ba.
Naam, Mfalme anajua kuhusu mambo haya yote, nami nasema naye kwa uhuru. Kwa sababu nina hakika kwamba hakuna hata mojawapo ya mambo haya asilolijua, kwa kuwa hayakufanyika mafichoni.
27 Uyinna nin na annabawe, Ugo Agrippa? Ina yiru uyinna nin ghinu.”
Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini.”
28 Agrippa woro Bulus ku “nan nya kabiri bar uma kpiliu nso unan dortu Kutelle?”
Agripa akamwambia Paulo, “Je, unanishawishi kwa haraka namna hii niwe Mkristo?”
29 Bulus woro, “Ndi inlira kiti kutelle, sa nin kabiri bat sa nin kubiri gbardang, na fe usanfi ba, amma umunu alenge na idin lanzui kiti mone, iso nafo mewe, amma na nin ninyang kilari licin ba.
Paulo akasema, “Ikiwa ni kwa haraka au la, namwomba Mungu, si wewe peke yako bali pia wale wote wanaonisikiliza leo, wawe kama mimi nilivyo, kasoro minyororo hii.”
30 Ugowe tunna a fita ayissina, a udya mine nin Barniki wang fita umuni alenge na iwa sossin ligowe nan ghinu;
Baada ya kusema hayo, mfalme akainuka pamoja na mtawala na Bernike na wale waliokuwa wameketi pamoja nao.
31 na isuna kudarua, itunna nliru nin nanit mine idin su, “Na unit ulele nati nkon kulapi kongo na ku batina ukul so utecu ba.”
Walipokuwa wakiondoka, wakaambiana, “Mtu huyu hafanyi jambo lolote linalostahili kufa au kufungwa.”
32 Agrippa woro Festus ku, “Iwa sunu unit ulele nda fo na afo acara kitin Kaisar ba.”
Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeachwa huru kama hangekuwa amekata rufaa kwa Kaisari.”

< Katwa Nono Katwa 26 >