< Katwa Nono Katwa 14 >

1 Nyan min Iconiun Paul nin Barnabas iwa piro kutii lira na Yawudawa, i belle tipipin Yise nin likara me. amini wa ti, a yahudawa nin na Greek i yinna nin tipipin Yesu.
Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
2 Vat nin nanin among a Yhudawe wa yinin ba, inin belle anan salin yinu Kutelle ba inari, ita nibinai nanan salinyinu Kutelle nan.
Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
3 Nin nan Paul nin Barnabas i ya don-don kite ne kan imini wa lira tipipin Kutelle sa fiu, amini wa ninani kaduran bolu Kutelle kana ti kamata ti se ba
Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
4 Vat nin nanin anite i wawuchu kidaw, among ima dofunu among nin belle indofunu nono kata Y bellin esu.
Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
5 Nin nanin anan salin yiri Kutelle, nin na yahudawa, i wa tinin risu na dida mine, inan taasu an Paul nin Barnabas,
Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
6 Dana ulire daa kutuf nan Bulus nin barnabas imini iwa chun ka gbire udu nmin [Kagbiri] Liconia, Listra nin Derba a usauran niti naana nidi pit ba.
Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
7 kikanare tutung an Paul nin barnabas iwa tinin bellu nani nin dursuzu ani tipipin Kutelle,
wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
8 Nan Listra umong unit wa diku salikara nabunu. Kubi kona uname wa marighe, na a sa tabina u sun chinba.
Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
9 Unit une wa lanza paul ku inliru, dana paul yeneghe, paul yinno, yinnume sau yenume matighe ashin.
Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
10 Amini wa belinghe nin liwui kan “fita nin nabunufe, “Ninnanin unite ghina nin nabunume atinan chinu.
akasema kwa sauti kubwa, “Simama wima kwa miguu yako!” Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
11 Dana anite yene ile imon na Bulus in su, ittunna ighantinna tiwui mine in belu nin tilem Nikoniyum “atelle abebene danari nafo anit.”
Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: “Miungu imetujia katika sura za binadamu!”
12 Inin naa an paul nin Barnabas tisa, barnabase inaghe lisa “zeus”ame paul iyichilaghe nin lisa“harmas”bar ame wadi unanliru udiawe.
Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
13 Kutin prist zeus wadik kibulun kagbiri, ame nin anite, itina i nuzu kap udas nin nin Ninamine a tifulawa amomoagigimeichizina unakwizu usakirfais.
Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
14 Tutun Paul nin Barnabas lanza nanin inuzu nin kibinain kibibit nin jartina
Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
15 inin woro anite bar yanghari imasu ilaimone? bar nanin na iwa molu inamine ba, arikima anitari nafo anighe, tida mini nin liru uma, tidimun su ichin imon inazan ine idak kiti Kutelle un nan la, amare ulena anake kitene nin kutin ah kuli kubgardan
“Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
16 Nayirin burne, vat mine alenge na idi Ayahudawa ba wadin dortu namong atelle na iwa dinin suwe. Kutelle wa yinnin idortu nani bara na iwa yirughe ba.
Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
17 Ama awa durso nari nworu adin sunari katwa kacine. Amere asa ata uwuru ju, akuru ata imuse kunjo. Asa aamere tutung nafi imoli, ukuru akulo nibinayi mine nin nayi abo.
Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha.”
18 Anite wa lanza imon ilenge na Paul nbelle, vat nin nani iwa yita nin su inakpiza ina ididya ine isu Paul nin Barnabas ku usujada. Ama udu nimalighe, anite kpiliza na isu ba.
Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
19 among a Ayahudawa, da unuzu Antiyok nin Ikoniyum, iwa dak ida risa anite gbardang nin nanan Listira inin nworu ilemon na Paul din bellu mimnu kinuwaridi. Anite na iyinna nin lire na Yahudawe tunna ilanza ayi nin Paul. Ita a Yahudawa tinnan filisu pau, inin kuru wunughe udu das kagbir, kikane iwa chiso aku
Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
20 Among na iwa yinni nin liru Kutelle Listira wa tinin iyisina ku popo Paul, kikane na awanonku kutinghe. Paul tunna azinto. Anin fita nya nin nanan yinnun nin liru Yesu inin pira ka gbire.
Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
21 Iwa so ita ayiri kikane ka, ile ubun bellu tipipin Yes, aniti gbardan wa yinin nin tipipinghe, nin kidu Paul nin Barnabas ita ubellen kwilu. inin kuru ida u Listira. inani wa kuru ikata udu Ikoniyum ini kuru ikata udu ka gbiri Antiyok nanya Pisidiya
Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
22 Vat kika na ipira iyatinin nizu linana likara nayi, na iwa lanza fiu ba, imini wa balin nanin yinu mine nin salin yenu itere kibinai mine nan ny, bar nanin nan nya tikanchi tona tinare matinari tipiru kitekane[kilari Kutelle]
Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, “Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu.”
23 Paul nin Barnabas wa fere adidya nanya ligozin nanite. Nin tin bellen gniu nan nya nite Paul nin Barnabas inanin wa pitirin anite, i ta ayiri nan ghinu i nin ta ilira nin kifin unu[sauli ninmunli] nin nanin Paul nin Barnabas ininnakwa nanin kiti Kutelle udia urkana iwa yinin ninghe ama bunu nanin,
Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
24 Unuzu kidun, an Paul nin Barnabas, wa kata udu pisidiya inin da Upampiliya.
Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
25 Nanya kusa kone, inin lirina tipipin Kutelle nan ghe ka gbiri Perga innin kata udu Attalia.
Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
26 Kikanner, iwa nin pira ujirgi mmen intina i kwiila udu Antakiya, nanghe kagbiri in Siriya. Kagbiri kanere iwa fere Paul nin Barnabas do nnan niti idi su uwaze ku, tutung niti nanga anan yinnu nin Yesu wasu nlira Kutelle bun Paul nin Barnabas nanya katwawe na ina malu nene.
Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
27 Kubikono iwadak nanya Antiyok inin yichila anan yinnu sa uyenu kitikirum, inin belle elemon na Kutelle nasu nin punu kibulun udu iktinanan salin yinu Kutelle ini selibou lirika longo na lima du nin ghinu kitene nin yinnu yesu
Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
28 Nin nanin Paul nin Barnabas wa dodon nin nono kata Kutelle
Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.

< Katwa Nono Katwa 14 >