< Katwa Nono Katwa 13 >

1 Nene nanya ligozi na kagbirin Antakiya, anan liru nin nnu Kutelle nin nanan dursuzu yita ku. Tisa mine wa di Barnaba, Simeon (na iwa yicughe Niger), Lukiyus unitin Karita, Manain (unan liwalin gwanan Hiridus kukune me), nin Shawulu.
Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
2 Kube na ndin zazinu Kutelle nin sun kotu nayi, Uruhu Ulau woro, “Feren ni Barnabas ku nin Shawulu, isu katwa kanga na nna yicila nani bara kanin.”
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
3 Na ligozen mmala ukotu nayi nin lira, i wunno nani likoot inin tarrda nani acara.
Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
4 Ame Barnabas nin Shawulu suu ubiyayya nin Ruhu Ulau itunna i nyi udu kusarin kilikiya; unuzu kikane idi tunun udu nlong lidan nanya kurawan kubrus.
Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
5 Kubi na iwa di nanya kagbir salamis, ibelle uliru Kutelle nanya kutyi nlirag, na Yahudawa, inung tutun yita nan Yohanna Markus nafo unan buunu mine.
Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
6 Kubi na inya udu vat lidan kiyitik nmyen, udu Bafusa, idi se umong unan nizu tikanlang, ku Yahudawa, unan su kinu nin nnu Kutelle, ulenge na lisa me Bar Yesu.
Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
7 Unan nizu tikankane munu liti min mukadas, Sargis, nin Bulus unit ujinjin, unit une wasu manyardang nin Barnabas a Bulus, bara adinin su alanzauliru Kutelle.
Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
8 Ame Alima unan “nizu tikankang” (nanere lisa me di) asu ivira nanghinu, asa likum nworu a kpiliya Sarijiyus ku nanya nyinnu sa uyenu me.
Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
9 Ame Shawulu, ulenge na idin yicu Bulus, awa kullun nin Ruhu Ulau a borioghe iyizi
Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
10 anin woro, “Fe gono shaitan, ukulun nin kinu a karusuzo, nin magunta, fe unan nivira nin vat ko iiyeme imon icine, na uba sunu ukpilizu nimon idert in Cikilari ba sa iba sunu?
na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
11 Nene yene ucara Cikilari di kitene fe, uba da lawu uduu. na iba yenu uwui ba nin kubi baat.” Dedei luwutun nin nsirti, a cizina kiti, intiri nanut ikifo ghe ucara.
Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
12 Kubi na ame Sarjisu nyene ile imon na idi, ame yinna, bara awa kifo unuu nin ndursuzu kitene Cikilari.
Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
13 Nene Bulus nan nadondon me, kaffina unuzu Bafus udu Perga nanya Pamfiliya, ame Yohanna suuna nai a kpila Urushelima.
Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
14 Bulus nan nadondon me, cinna unuzu Bafos udak Antakiya Nbisidiya. Kikane inya udu kutyi nlirag liyiri nassabar idi soo kikane.
Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
15 Kubi na ibelle inyerte nduka, nin na nan nliru nin nnu Kutelle, udia kutyi nlirag too nani nin kadura a woro, “Linuana, andi idinin nkan kadura, kan kpinu nagang kiti nanite kikane, bellen kanin.”
Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
16 Bara Bulus fita ayisina a zillino liti me, a woro, “Annit Israila nin nalenge na idin zazinu Kutelle, lanzan.
Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
17 Kutelle nanit ale Israila wa feer acif bite ata nani anit gbardang, kubi na iwa so nmyin masar, nin nacara nakara awa nutun nani kitee.
Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
18 Udu akus akut anas, ayita nanghinu nanya kusho.
Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
19 Kubi na awa mallu nin nipin kuzor, nanyan nmyin kaana, anaa anit bite nmyin mine miso nani ugadu.
Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
20 Vat nile imone iwasu inin ukatu nakus akalt anas nin nakut ataun, kubi nile imone vat, Kutelle na nani unan wucu kidegen udu Samaila unan nliru nin nnu Kutelle.
Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
21 Mammal nilele, anite tirino ini nani ugo, Kutelle na nani Saul ku usaun kish, unit unuzu likuran Banyami, bara kubi nakus akut annas.
Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
22 Na kutelle nkalaghe nanya nanan tigo, a yauna Dauda ku aso nani ugo, uwaso kitene Dauda kutelle wa woro, 'Nnase Dauda usaun Jesse aso unit nayi nighe; aba su vat nile imon na ndinin su we.'
Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
23 Unuzu kuwunu nnit ule Kutelle ba da ni nonon Israila ku unan tucu, Yesu nafo na anusu alikawali nsu we.
Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
24 Uleli imone wa cizin kube, kamin Yesu dak, Yohanna wa cizin ubellun nshimtinnu ndiu kutyin, udu kiti nanit Israila vat.
Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
25 Na Yohanna wadi malizunu katuwa me, aworo, 'Anung din su meng ghari? Na mere ba, ama lanzan, umong din cinu udak kidung nighe, akwatak nabunu me na meng batin nbunku ba.'
Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
26 Linuana, nono nanya kuwunu Ibrahim, nin nanya mine na idin dortu Kutelle, kiti bitere, kadura nbellen nnan tucu iwa tuu nari mun.
Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
27 Bara inughe na iwa sosin nanyan Urushelima nan nago mine, na iwa yinin ghe ba, sa iyinin tiwui nanan nliru nnu Kutelle na isa ibelle ko ayeme assabar, ina ni na Kullo ubellu we, kadure nti Yesu unan kul.
Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
28 Vat nani na iwase imomon icaut kiti me nworu akuu ba, itirino Bilatus ku nworu amollu ghe.
Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
29 Kubi na imala vat nile imon na ina nyertu liti me itoltunghe kitene kutca, inonko ghe nanya kissek.
Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
30 Amma Kutelle wa fya ghe nanya na nan kul.
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 Anit gbardang wa yenje ghe nanya nayiri gbardang na lenge na i di ligowe nan ghe na i wa nuzun Galile ne indu Urushelima. Anit alelere iyizi naba me kiti nanite.
Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
32 Bara nani ti da minu nin liru unang imbeleng nciu nnuu ulenge na iwa su an kaa bite unin uworsu:
Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
33 Kutelle na ceo nari uciu nlirne, arik nono mine, nworu Kutelle wa fya Yesu ku kisssek.
Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
34 Ununu kidegen nworu ana fya ghe nanya na nan kul bara kidowo me wa yene ubiju, amini wa su uliru nenge, 'Mma nifi nkoli milau in nanda milau.'
Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
35 Unnare nati ana kuru abelle nan nya namong avu tutung: 'Na una yinnu unit ulau fe a yene ubiju ba.'
Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
36 Bara na kimal na Dauda wa su Kutelle katwa kubi kiyi mine gegeme kanin aku. iwa aoroghe nin na cif me, amini wa biju,
Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
37 amma ame ulenge na Kutelle wa fya Kissek na awa yene ubiju ba.
Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
38 Linuana na iyinnin ilele, unuzu nlele ina sun nari unuu nbeleng nkussu nalapi.
Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
39 Bara ame vat ule na ayinni ma se usurtu nan nye vat ule na ti tisse usurtu mun ba.
Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
40 Bara ceon nibinai kiti kirum bara imon ile na a annabawa na belin kitene i wa minu ba.
Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
41 Yeneng, anung anan nanzu nimon nafi fiu kifo minu inana. Bara meng din su katwa nayiri mine, Katwaa kango na ima yinnu mun ba andi ma umong ma belin minu ubeleng kanin.'”
'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
42 Na Bulus nin Barnabas nnyaa, anite fo nani acara nworu ikuru ida belu nani uliru urum une Asabar ncin dak.
Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
43 Na uzuru kilari nlire nmala, Ayahudawa gbardang nin namon anan salin dortu Kutelle dofino Bulus ku nin Barnabas, alenge na iwa su nani uliru i woro nani ili ubun nin cin nan nya nbolu Kutelle.
Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
44 Assabar nda duru anan kagbiri vat da zuro inan lanza uliru Ncikilari.
Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
45 Na Ayahudawa in yene ligozi nanite, ikulo nin shina isu uliru uganbalang nin nilenge na Bulus nbelle izoguzo ghe.
Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
46 Amma Bulus nin Barnabas su uliru nin nayi akone i woro, “Uso gbas i cizin ubelu anughe ku uliru Kutelle. Na iyene nworu anung nfillo unin ina nin yira ati mine na ucaun ise ulai nsa ligan ba, yeneng, tima kpillu kiti na wurmi. (aiōnios g166)
Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios g166)
47 Bara nanere Cikilari na bellin nari, aworo, 'Nna ceo minu nafo nkanan ucin du kiti na wurmi, nworo adak nin adak nin tucu nan nyan vat niti nan nya in yii vat'”
Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
48 Na Awurme nlanza nani, ilanza mmang kang izazina lissa Ncikilari. Ngbardang nalenge na ina fere nani bara ulai nsa ligang wa yinnin. (aiōnios g166)
Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios g166)
49 Uliru Kutelle wa malu kiti vat nan nya nmine.
Neno la Bwana lilienea nchi yote.
50 Amma Ayahudawa su ubeleng nawani anan ni nati alenge na idi nin nimon icine. Ileli imon ta nworu ipiziru umonlun Bulus ku nin Barnabas iko nani inutuno nani unuzu kipin mine.
Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
51 Amma Bulus nin Barnabas kotuno lidau nabunu mine liso nati mine. Inya ucindu kipin Ikoniya.
Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
52 Nono kadura wa kulo nin nayi abo a Uruhu Ulau.
Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.

< Katwa Nono Katwa 13 >