< 2 Utasalonika 3 >

1 Nene, linuana, sun nlira bara arik, bara ligbulan Cikilari nyaa mas nin zazinu, nofonalidi nin na nun,
Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
2 tinan se tinuzu nachara na nan na buri asirne nin na nit ananzan, na vatari dinin kidegen ba.
Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
3 Cikilari di nin kidegen, abatunu minu anin kuru ayenje minu unuzu na charan nnit unanzan.
Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
4 Arik yinna nin Cikilari ndellen mine, iba su ili ubun su ni le imon nati kpada minu.
Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
5 Nlirari Cikilari durso nibinei mine uchindu usuu Kutelle nin teru kibinei Kristi.
Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
6 Nene, tikpada minu, linuna nya lisan Cikilari bite Isa Kristi, ichin vat gonni ulenge na a sosin sa atanda ale na ina seru kitibite.
Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
7 Anun yiru iyizyari iba so nofo arik. Natiwa su nofo agballa nya mine ba.
Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
8 Tutung na tiwa li imonli mmong sa nlira ba. Nworu nani, nya kataa nin nieu tiwa su kataa kitii nin liyirin, bara tiwa umon mine kutura.
hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
9 Na ti dira akara ri ba, bara ti so-oh imon yenu kitimine, anun nan so bara arik.
Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
10 Kubi na tiwa di nan ghinu, tiwa kpada minu, “Asa umon nari usu kataa, naawa li ba.”
Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, “Mtu asiyefanya kazi, asile.”
11 Tina lanza amon nya mine di nin mon su ba. Na idin sukataa ba ama agballari nrusuzu nanit.
Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
12 Nene imus nalele tikpada nin nakara nya Cikilari Isa Kristi, nya kutik na isu kataa ili imonli mine.
Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
13 Anun, linuana, yenjen iwa chin usu ni mon ichine nya nibinei mine.
Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
14 Asa umon nari ligbulan bit nyan niyert ilele, yenjen nani na imomon wa munu minu ba nan na nin ba, bara ina lanzan chin.
Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
15 Na iwa yene gne nofo unan liburi lisirne ba, wunun gne kutuf nofo gwana.
Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16 Na Cikilari mmang litime niminu mmang vat nabi nya tibau mine. Cikilari so nan na nun vat.
Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
17 Ilelere ilip nin, Bulus, nin na chara nin, udursuari vat nya niyert na nna yertin.
Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
18 Na nshew Cikilari Isa Kristi sonan a nun vat.
Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< 2 Utasalonika 3 >