< 2 Ukorintiyawa 1 >

1 Bulus unan kadura Yesu Kristi nin su Kutelle, nin Timintawus gwana bit, udu kutii kulau korintiyawe, nin vat nanit alau nigbirin na ikilin acaiya.
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo, tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho, na watu wote wa Mungu kila mahali katika Akaya.
2 Ubolu Kutelle na uda kiti mine kibinayi kisheu unuzu KutelleUcif bite nin Cikilari Yesu Kristi.
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
3 Na mmari Kutelle nin Cif ncikilari Yesu Kristi soo, ule na amereUcif ukunekune nin Kutelle nonko nibinayi,
Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye huruma na Mungu mwenye kuleta faraja yote.
4 Ulena adin nonkuzu nibinaiyi bite nanya piwu nibinaiyi bite arik nonko among ale na nibinaiyi mine piya nin nonku nibinai na Kutelle na ma nonku nari mun nibinaibit.
Yeye hutufariji sisi katika taabu zetu zote, ili nasi tupate kuwafariji wengine katika kila taabu kwa faraja hiyohiyo tunayopokea kutoka kwa Mungu.
5 Bara nafo uniyu Kristi karin bara arik nenere ununkuzu nibinayi bite karin nanya Kristi.
Naam, kadiri mateso ya Kristo yanavyozidi ndani yetu, ni kadiri hiyohiyo tunazidi kufarijiwa naye.
6 Bara nanin tiwa se upiwu nibinaiyi usuu utucunin nin nonku nibinayi nenere. Sa i wa nonku nibinayi bite unfe unon ku nibinayari, ulena udi na uwa da lanza uniuwe nannarik.
Ikiwa tunapata taabu, basi ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu. Tukifarijika, ni kwa ajili ya kuwafariji ninyi na kuwaunga mkono mpate nguvu ya kustahimili mateso yaleyale tunayoteseka sisi.
7 Nin nayi akone bite kitife nyisina nin yiru nafo na una neu nan narik tutung nenere unonku nibinaye.
Tena, matumaini tuliyo nayo kwa ajili yenu ni imara; tunajua kwamba mkishiriki mateso yetu, mtashiriki pia faraja yetu.
8 Bara na ti dinin su tiso sa uyiru ba linwana mbeleng na tiwase nanya Asiya; iwa naulin nari nafo na ti wasa ti tere nibinai ba kan har tiwa nutun nibinai sa tim ati ulai.
Ndugu, tunataka kuwajulisheni taabu zilizotupata kule Asia; taabu hizo zilitulemea kupita kiasi, hata tukakata matumaini yote ya kuendelea kuishi.
9 Nin nene iwa tinari tishot inkul nati bite bara nanin i wadin yenju nati mase likara kibinai nati bite ba inmaimako kiti Kutelle ulena ana fiya abi.
Naam, tulikuwa kama watu waliohukumiwa kuuawa, ili tufundishwe kumtegemea Mungu mwenye kuwafufua wafu, badala ya kutegemea nguvu zetu sisi wenyewe.
10 Awa tucu nari nanyang kul nijas, ama kuru atucu nari tutun. Ti kotina ayibit kitene me tutung ama nutu nari
Yeye alituokoa katika hatari kubwa ya kifo, na anaendelea kutuokoa; sisi tumemwekea tumaini letu kwamba atatuokoa tena,
11 Ama su nari nani i wa bun nari nanya nlira anit gbardan ba daduru liburi liboo iyisunu bite bara ubolsu Kutelle na ana ninari nanya nlira na nit gbardan.
ninyi mkiwa mnatuunga mkono kwa kutuombea. Hivyo neema tutakazokuwa tumepata kutokana na maombi ya watu wengi hivyo, ziwe sababu ya watu wengi zaidi kumshukuru Mungu kwa ajili yetu.
12 Nene ilelere ti din fo figiri mung ushaida yiru bite ule na arik wa su nin nati bite nanya yi. Tiwa su nanin bara kata yinu nin lau nin kidegere na wa nuzu kiti Kutelle na nafo kujinjin yii ulele bara nanin inuzu ballu Kutelle.
Sisi tunajivunia kitu kimoja: dhamiri yetu inatuhakikishia kwamba tumeishi ulimwenguni hapa, na hasa kati yenu, kwa unyenyekevu na unyofu tuliojaliwa na Mungu; hatukuongozwa na hekima ya kibinadamu bali neema ya Mungu.
13 Na tidin yarti minu imonile na iwa sa ibele sa uyinin ba indi nin likara kibinai tutung.
Tunawaandikia ninyi mambo mnayoweza kuyasoma na kuyaelewa. Ninatumaini kwamba mtaelewa vizuri kabisa,
14 Nafo na ina malin yinu nari likot, lirum au lirin Cilkilari bite Yesu tina yite udalilin fizu nabanda mine nafo na anung ba yitu unbit.
maana mpaka sasa mmenielewa kiasi fulani tu. Tunajua kwamba katika ile Siku ya Bwana Yesu mtaweza kutuonea sisi fahari kama nasi tunavyowaonea ninyi fahari.
15 Bara nan wadi nin likara kibinai nilele iwa din nin su indak kitefe nin burnu, au unan sere mbang inse na mara aba.
Nikiwa na matumaini hayo, nilikusudia kuja kwenu hapo awali ili mpate baraka maradufu.
16 Iwa di woru inlasin kit fe cindu Umakidaniya inkueu mda yene fi cin sa Unuzu Makidoniya nani fe nin tiyi ndina udu Ujudia.
Nilikusudia kupita kwenu nikiwa safarini kwenda Makedonia, na wakati wa kurudi pia, ili nipate msaada wenu kwa safari yangu kwenda Yudea.
17 Kubi kona iwa din kpilzu nan, iwa belin kibinai fe? sa uwa yinan miu nin kibinai unitan, bara in woro fi ''ee ee” nin “babu babu”kube kurume?
Je, mnadhani nilipopanga hivyo nimekuwa kama mtu asiye na msimamo? Je, mnadhani kwamba ninafanya uamuzi wangu kwa fikira za kibinadamu na kwamba nasema “Ndiyo” na “Siyo” papo hapo?
18 Bara nanin nafo na Kutelle unan yinnu sa uyenu nati wasa ti woro “ee” nin “babu” ba.
Mungu ni ukweli mtupu; basi, kile tulichowaambia ninyi si jambo la “Ndiyo” na “Siyo”.
19 Bara gono Kutelle Yesu Kirst, ule na Silvanus Timitawus nin mi na beling naya min, na ame “ee “nin ''babu” ba bara nani ame ee wari vat kubi.
Maana Kristo Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye mimi, Silwano na Timotheo, tulimhubiri kwenu, hakuwa mtu wa “Ndiyo” na “Siyo”; bali yeye daima ni “Ndiyo” ya Mungu.
20 Bara vat nalikawali Kutelle ''ee' wari nanya me baranani nanya me asa ti wuru uso nani udu uzazu Kutelle.
Maana ndani yake ahadi zote za Mungu zimekuwa “Ndiyo”. Kwa sababu hiyo, “Amina” yetu husemwa kwa njia ya Kristo kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
21 Nene Kutelleri munu nari nanya Kristi nin narik.
Mungu mwenyewe ndiye mwenye kutuimarisha sisi na ninyi pia katika Kristo, na ndiye anayetuweka wakfu;
22 Ana tursu nari nin na gilet me na ni nari Ifip nanya nibinai bite minin so kulap ni mele na ama da ninari nin dandaunu.
ndiye aliyetutia mhuri wa kuwa mali yake yeye na kutujalia Roho mioyoni mwetu kama dhamana ya mambo yote ambayo ametuwekea.
23 Nin nanin ina yicila Kutelle aso unan nizi iba ning bara imele na inati nan daa u Kurintiya ba bara inan unan tucu fiari.
Mungu ndiye shahidi wangu—yeye anajua moyo wangu! Mimi sikuja tena Korintho, kwa sababu tu ya kuwahurumieni.
24 Na bara ti di nin su wuru timiin uyenu sa uyenu b, bara na tidi katwa nin yenu sa uyenu miner, bara mmag min, nayinsin nanya yinnu sa uyenu
Hatutaki kutumia mabavu juu ya imani yenu; ninyi mko imara katika imani yenu. Wajibu wetu ni kufanya kazi pamoja kwa ajili ya furaha yenu.

< 2 Ukorintiyawa 1 >