< 2 Ukorintiyawa 1 >

1 Bulus unan kadura Yesu Kristi nin su Kutelle, nin Timintawus gwana bit, udu kutii kulau korintiyawe, nin vat nanit alau nigbirin na ikilin acaiya.
Barua hii ni kutoka kwangu mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko Akaya yote:
2 Ubolu Kutelle na uda kiti mine kibinayi kisheu unuzu KutelleUcif bite nin Cikilari Yesu Kristi.
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
3 Na mmari Kutelle nin Cif ncikilari Yesu Kristi soo, ule na amereUcif ukunekune nin Kutelle nonko nibinayi,
Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja yote.
4 Ulena adin nonkuzu nibinaiyi bite nanya piwu nibinaiyi bite arik nonko among ale na nibinaiyi mine piya nin nonku nibinai na Kutelle na ma nonku nari mun nibinaibit.
Yeye hutufariji katika taabu zetu, ili tuweze kuwafariji walio katika taabu yoyote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka kwa Mungu.
5 Bara nafo uniyu Kristi karin bara arik nenere ununkuzu nibinayi bite karin nanya Kristi.
Kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi ndani ya maisha yetu, hivyo ndivyo faraja yetu inavyofurika kwa njia ya Kristo.
6 Bara nanin tiwa se upiwu nibinaiyi usuu utucunin nin nonku nibinayi nenere. Sa i wa nonku nibinayi bite unfe unon ku nibinayari, ulena udi na uwa da lanza uniuwe nannarik.
Kama tunataabika, ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu, iwaleteayo saburi ya mateso yale yale yanayotupata.
7 Nin nayi akone bite kitife nyisina nin yiru nafo na una neu nan narik tutung nenere unonku nibinaye.
Nalo tumaini letu kwenu ni thabiti, kwa sababu tunajua kwamba kama vile mnavyoshiriki mateso yetu, ndivyo pia mnavyoshiriki katika faraja yetu.
8 Bara na ti dinin su tiso sa uyiru ba linwana mbeleng na tiwase nanya Asiya; iwa naulin nari nafo na ti wasa ti tere nibinai ba kan har tiwa nutun nibinai sa tim ati ulai.
Ndugu wapendwa, hatutaki mkose kujua kuhusu zile taabu tulizopata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo sana, kiasi cha kushindwa kuvumilia, hata tulikata tamaa ya kuishi.
9 Nin nene iwa tinari tishot inkul nati bite bara nanin i wadin yenju nati mase likara kibinai nati bite ba inmaimako kiti Kutelle ulena ana fiya abi.
Kwa kweli, mioyoni mwetu tulihisi tumekabiliwa na hukumu ya kifo, ili tusijitegemee sisi wenyewe bali tumtegemee Mungu afufuaye wafu.
10 Awa tucu nari nanyang kul nijas, ama kuru atucu nari tutun. Ti kotina ayibit kitene me tutung ama nutu nari
Yeye aliyetuokoa kwenye hatari kubwa ya kifo na atatuokoa tena. Kwake yeye tumeweka tumaini letu kwamba ataendelea kutuokoa.
11 Ama su nari nani i wa bun nari nanya nlira anit gbardan ba daduru liburi liboo iyisunu bite bara ubolsu Kutelle na ana ninari nanya nlira na nit gbardan.
Kama vile mlivyoungana kusaidiana nasi katika maombi, hivyo wengi watatoa shukrani kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka za neema tulizopata kwa majibu ya maombi ya wengi.
12 Nene ilelere ti din fo figiri mung ushaida yiru bite ule na arik wa su nin nati bite nanya yi. Tiwa su nanin bara kata yinu nin lau nin kidegere na wa nuzu kiti Kutelle na nafo kujinjin yii ulele bara nanin inuzu ballu Kutelle.
Basi haya ndiyo majivuno yetu: Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeenenda katika ulimwengu na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, katika utakatifu na uaminifu utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya kidunia bali kwa neema ya Mungu.
13 Na tidin yarti minu imonile na iwa sa ibele sa uyinin ba indi nin likara kibinai tutung.
Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma au kuyaelewa. Natumaini kwamba,
14 Nafo na ina malin yinu nari likot, lirum au lirin Cilkilari bite Yesu tina yite udalilin fizu nabanda mine nafo na anung ba yitu unbit.
kama vile mlivyotuelewa kwa sehemu, mtakuja kuelewa kwa ukamilifu ili mweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu katika siku ya Bwana Yesu.
15 Bara nan wadi nin likara kibinai nilele iwa din nin su indak kitefe nin burnu, au unan sere mbang inse na mara aba.
Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilitaka nije kwenu kwanza, ili mpate faida mara mbili.
16 Iwa di woru inlasin kit fe cindu Umakidaniya inkueu mda yene fi cin sa Unuzu Makidoniya nani fe nin tiyi ndina udu Ujudia.
Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia na kurudi tena kwenu nikitoka Makedonia, ili mnisafirishe katika safari yangu ya kwenda Uyahudi.
17 Kubi kona iwa din kpilzu nan, iwa belin kibinai fe? sa uwa yinan miu nin kibinai unitan, bara in woro fi ''ee ee” nin “babu babu”kube kurume?
Nilipopanga jambo hili, je, nilikuwa kigeugeu? Au ninafanya mipango yangu kwa hali ya mwili, ili niseme, “Ndiyo, ndiyo” na “Siyo, siyo” wakati huo huo?
18 Bara nanin nafo na Kutelle unan yinnu sa uyenu nati wasa ti woro “ee” nin “babu” ba.
Hakika kama Mungu alivyo mwaminifu, maneno yetu kwenu hayajawa “Ndiyo na Siyo.”
19 Bara gono Kutelle Yesu Kirst, ule na Silvanus Timitawus nin mi na beling naya min, na ame “ee “nin ''babu” ba bara nani ame ee wari vat kubi.
Kwa kuwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ambaye tulimhubiri kwenu: Mimi, Silvano na Timotheo, hakuwa “Ndiyo” na “Siyo,” bali kwake yeye siku zote ni “Ndiyo.”
20 Bara vat nalikawali Kutelle ''ee' wari nanya me baranani nanya me asa ti wuru uso nani udu uzazu Kutelle.
Kwa maana ahadi zote za Mungu zilizo katika Kristo ni “Ndiyo.” Kwa sababu hii ni kwake yeye tunasema “Amen” kwa utukufu wa Mungu.
21 Nene Kutelleri munu nari nanya Kristi nin narik.
Basi ni Mungu atufanyaye sisi pamoja nanyi kusimama imara katika Kristo. Ametutia mafuta
22 Ana tursu nari nin na gilet me na ni nari Ifip nanya nibinai bite minin so kulap ni mele na ama da ninari nin dandaunu.
kwa kututia muhuri wake na kutupa Roho wake mioyoni mwetu kuwa rehani kwa ajili ya kututhibitishia kile kijacho.
23 Nin nanin ina yicila Kutelle aso unan nizi iba ning bara imele na inati nan daa u Kurintiya ba bara inan unan tucu fiari.
Mungu ni shahidi wangu kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya kuwahurumia ninyi sikurudi Korintho.
24 Na bara ti di nin su wuru timiin uyenu sa uyenu b, bara na tidi katwa nin yenu sa uyenu miner, bara mmag min, nayinsin nanya yinnu sa uyenu
Si kwamba tunatawala imani yenu, bali twatenda kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kwa sababu ni kwa imani mwasimama imara.

< 2 Ukorintiyawa 1 >