< 2 Ukorintiyawa 6 >

1 nani katwa logow, idin foo minu nnacara na wa seruu ubolu Kutelle hen nani ba
Na kwa hiyo, kufanya kazi pamoja, tunawasihi ninyi msiipokee neema ya Mungu pasipo matokeo.
2 Bara na abenle “Nanya kubi ku mang inwa lanza minu, ninwe liri intucu nwa bun minu “Yeneng nenere kubi kumanghe yeneng nenere lirin tucua.
Kwa kuwa anasema, “Wakati uliokubalika nilikuwa makini kwenu, na katika siku ya wokovu niliwasaidia.” Tazama, sasa ni wakati uliokubalika. Tazama, sasa ni siku ya wokovu.
3 Na arik na ceu litalan tirzu nbun mun b, bara na tidinin su katwa bite se ulazi ba.
Hatuweki jiwe la kizuizi mbele ya mtu yeyote, kwa kuwa hatuitakii huduma yetu iletwe katika sifa mbaya.
4 Nin yenu nani, ti duro atibite nin nitwa bite vat au arike acin Kutelleari nanya nteru nibinai umin ijasi.
Badala yake, tunajihakiki wenyewe kwa matendo yetu yote, kwamba tu watumishi wa Mungu. Tu watumishi wake katika wingi wa ustahimilivu, mateso, dhiki, ugumu wa maisha,
5 utecu, nannya kuti licin ufizu nayi nin katwa kagbagba, nin salin moroninkitik nin kukpon.
kupigwa, vifungo, ghasia, katika kufanya kazi kwa bidii, katika kukosa usingizi usiku, katika njaa,
6 Nin lau uyiru, kbinai ki shau nin washalang nin fip me al, nin su nanya kibinai.
katika usafi, maarifa, uvumilivu, wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo halisi.
7 Nin ligbulang kidegen, nin likara Kutelle nin ticilak nibinai nilau ncra ulime nin cara ugule.
Tu watumishi wake katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu. Tuna silaha ya haki kwa ajili ya mkono wa kuuume na wa kushoto.
8 Ti di katwa nin ngongon nin salin ngongo, nin tizugo nin lir. I wa yicu nari anan kinu arik nin kidegene bite.
Tunafanya kazi katika heshima na kudharauliwa, katika kashfa na sifa. Tunatuhumiwa kuwa wadanganyifu na wakati tu wakweli.
9 Tidin su katwa we nafon na iwa yiru nari ba a iyiro nari lau nafo tidin kul na tiyita nin lai nafo anan burn, bara nitwa bite na nafo anan caa ukul ba.
Tunafanya kazi kana kwamba hatujulikani na bado tunajulikana vizuri. Tunafanya kazi kama wanaokufa na -Tazama! - bado tunaishi. Tunafanya kazi kama tunaoadhibiwa kwa ajili ya matendo yetu lakini sio kama waliohukumiwa hata kufa.
10 Tidi katwa nafo nin nibinai nisirne bara nani tidi nin nibinai nibo, nafo nan diru nimum tina yita mum. tina
Tunafanya kazi kama wenye masikitiko, lakini siku zote tuna furaha. Tunafanya kazi kama maskini, lakini tunatajirisha wengi. Tunafanya kazi kana kwamba hatupati kitu bali kama tunaomiliki kila kitu.
11 Tina me belin minu kidegene bite va, anan Korintiy, nibinai bite pun pas.
Tumezungumza ukweli wote kwenu, Wakorintho, na mioyo yetu imefunguka kwa upana.
12 Nati wantin minu nibinai mine b, bara nani anughere wanting ukpilizu ni binai mine
mioyo yenu haizuiliwi na sisi, bali mnazuiliwa na hisia zenu wenyewe.
13 Nene nanya kpilizu ubarabara indi liru nan ghenu nafo nono punun nibinai mine pash
Sasa katika kubadilishana kwa haki - ninaongea kama kwa watoto - fungueni mioyo yenu kwa upana.
14 Na iwa teru nibinai mine nin nanan salinyinu b, bara nanin iyanghari munu kibinai ki lau nin sali udoka? Sa iyanghari munu njana nin sirti?
Msifungamanishwe pamoja na wasioamini. Kwa kuwa kuna uhusiano gani kati ya haki na uasi? Na kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
15 Iyapin iyinari di Kristi ku nin nin Beliyar [kudodoa]? Sa uyapi uladari di unanyinu sauyenu ninnan salin yinuri.
Ni makubaliano gani Kristo anaweza kuwa nayo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na asiyeamini?
16 Nin yapin uyenuari di kuti Kutelle nin Chill? Bara na arik ati alau Kutelle unan laiyar, nafo na ana belin “in ma so nanya mine in kuru cinu nanya mine inin yita Kutelle mine, anin wang yita aniti nin.
Na kuna makubaliano gani yapo kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi ni hekalu la Mungu aliye hai, kama ambavyo Mungu alisema: “Nitakaa kati yao na kutembea kati yao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
17 nani Ucif nabelin”nuzun nanya mine iso kusari kurum.” Na iwa dudo imon inazan ile isali lau b, menbah ba timinu mahabi.''
Kwa hiyo, “Tokeni kati yao, na mkatengwe nao,” asema Bwana. “Msiguse kitu kichafu, na nitawakaribisha ninyi.
18 Menghe ma so Ucif kiti fer. Anunghe nin soo ason nin ni na shono nin “Ubenlun Ucif udia.
Nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu wa kiume na wa kike,” asema Bwana Mwenyezi.

< 2 Ukorintiyawa 6 >