< 1 Utasalonika 1 >

1 Bulus, Silvanus nin Timothy, uchin du kuti kulau nTassulinika nanya Kutelle Uchif nin Chikilari Yesu Kristi. Nshew nin mang udu kitimine.
Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike, ninyi mlio ndani ya Mungu Baba yetu na ndani ya Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na amani.
2 Tidin nizu Kutelle ugodo bara anun ka kishi, nyan lira bit asa ti belle ubellen mine.
Siku zote tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu ninyi nyote, tukiwataja kwenye maombi yetu daima.
3 Tidin lizunu sa ligagng katah kidegen mine uniu nsuu nin ti reu kibinei bara ubun nya Chikilari Yesu Kristi unbun Kutelle nin Chif bit.
Tunaikumbuka daima kazi yenu ya imani mbele za Mungu aliye Baba yetu, taabu yenu katika upendo na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo.
4 Linwana na Kutelle dinin suuwe, tiyiru nin yichilu mine.
Ndugu zetu mpendwao na Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba Mungu amewachagua,
5 na abing amang wa da minu na tigbulang chas ba nya na kara, Ufunu ulau nin yinnu udiya vat nin yiru arik imusu na yapi anitarinya mine bara anun.
kwa sababu ujumbe wetu wa Injili haukuja kwenu kwa maneno matupu bali pia ulidhihirishwa katika nguvu na katika Roho Mtakatifu, tena ukiwa na uthibitisho kamili, kama vile ninyi wenyewe mnavyojua jinsi tulivyoenenda katikati yenu kwa ajili yenu.
6 Ina so bara arik nin Chikilari nafo na iwa seru ligulan nin nya neu nya liburi libo nfunu ulau.
Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, ingawa mlipata mateso mengi, mlilipokea lile Neno kwa furaha katika Roho Mtakatifu.
7 bara Yesu imon guru vat nyan Makaduniya nin Akaia udu alenge na idi nin kidegen.
Hivyo ninyi mkawa kielelezo kwa waumini wote katika Makedonia na Akaya.
8 Na kitimere ligulang Chikilari na nuzu ku chas ba, na Makaduniya nin Akaia ma ba - udo kiti vat na kidegen mine nya Kutelle na do-o, bara nani tiba bellu imon ba.
Kwa maana kutoka kwenu neno la Bwana limesikika, si katika Makedonia na Akaya tu, bali pia imani yenu katika Mungu imejulikana kila mahali kiasi kwamba hatuna haja ya kusema lolote kwa habari yake.
9 Bara inun na mun bellu imusin nati wa se kitimine, a nafo na anun atelle a bebene udu Kutelle lai nin kun kiden.
Kwa maana watu wa maeneo hayo wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli
10 A u chaah Ngono me na ana nuzu kitene kane ulenge na awa fya gne nya na nan kul, Yesu, ulengena adin tuchu nari tinana nayin chinu.
na ili kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu: yaani, Yesu, yeye aliyetuokoa kutoka ghadhabu inayokuja.

< 1 Utasalonika 1 >