< 1 Yuhana 2 >

1 Nono kibinai nin, i yertine ile mone udu kiti mine bara iwa su kulapi. Bara nani andi umom suu kulapi, tidinin nan seru ulena adi nin Ncife, Yesu nKristi ulena adi lau kang.
Watoto wangu wapendwa, nawaandikia haya ili msitende dhambi. Lakini kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye Mwombezi kwa Baba: ndiye Yesu Kristo, Mwenye Haki.
2 Amere yisin kitik bite kitene nalaapi bit, na alapi bit cas ba. ama tutung vat nanya inye.
Yeye ndiye dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu, wala si kwa ajili ya dhambi zetu tu, bali pia kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote.
3 Bara nanere tima yinu tiyiru ghe, andi ti dofuno tidokokime.
Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.
4 Ame ulena woro, “Ayiru Kutelle,'' amini nari u dortu tidokokime, atah kinu, kigen di nanya me ba.
Mtu yeyote asemaye kuwa, “Ninamjua,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, wala ndani ya mtu huyo hamna kweli.
5 Bara nani ulena dofuno uliru me, Kidegenere nanya nitu une usu Kutelle mali ti likara kan, Nanyanenere tima yinu tidi nin ghe,
Lakini mtu yeyote anayelitii neno lake, upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kweli kweli. Katika hili twajua kuwa tumo ndani yake.
6 Ame ule na aworo adi nin Kutelle na chinu nafo naa Yesu Kristi na chinu.
Yeyote anayesema anakaa ndani yake hana budi kuenenda kama Yesu alivyoenenda.
7 Anan kibinai nin, na din nyertu tidokoki ti pesariri ba, bara nanin tidokoki ti kuseri tona ina mali lazu nin fune. Tidokoki ti kuse tone tinere ti pipin too na ina malin lanzu.
Wapendwa, siwaandikii ninyi amri mpya bali ile ya zamani, ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilosikia.
8 Vat nanin indin nyertinu minu ti dokoki ti pese, to na kidegen ghari nanya Kristi nan ghinu, bara insirte din katizu nin nanin kidegen nkanan mali chizunu.
Lakini nawaandikia amri mpya, yaani, lile neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu, kwa sababu giza linapita na ile nuru ya kweli tayari inangʼaa.
9 Ame ulena aworo adi nanya nkanan, amini nari gwana me aduu nanya sirti harnene.
Yeyote anayesema yumo nuruni lakini anamchukia ndugu yake bado yuko gizani.
10 Ame ulena adinin suu gwana me aduu nanya nkanan na imong ntiru di nanya me ba.
Yeye ampendaye ndugu yake anakaa nuruni, wala hakuna kitu chochote ndani yake cha kumkwaza.
11 Bara nani ame ulena anari gwaname aduu nanya nsirti nin chinu nanya nnsirti; na ayiru kika na ama duu ba, Bara nsirte mali tursu ghe iyizi me.
Lakini yeyote amchukiaye ndugu yake, yuko gizani na anaenenda gizani, wala hajui anakokwenda, kwa sababu giza limempofusha macho.
12 Ina nyertin minu, nono suu nin, bara alapi mine ina shawa mun kite lisa me,
Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa ajili ya Jina lake.
13 Ina nyertin udu kiti mine, acif, bara iyiru ilena adi infune. Ina nyertin minu azamang, bara ina malin katu likara nmunge. Inmi nyertin minu nono nibebene, bara iyiru ucife.
Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nawaandikia ninyi watoto wadogo, kwa sababu mmemjua Baba.
14 ina nyertin minu acif, bara iyirughe tun uchizine. In nyertin minu angyana, bara indimin nakara, nin ti pipin Kutelle suo nanya mine inani mali katu likara nmunge une.
Nawaandikia ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
15 Na iwasu ukauna iyeba sa nin nimong nanya inye. Andi umong dinisuu inye usu Kutelle chife di nanya me ba.
Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Kama mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
16 Bara ilemong na idin nanya inye in nare, usu kidawo, ushaawa nizi, nin foo figiri kinan zan na inchifari ba in nanya inyeri.
Kwa maana kila kitu kilichomo ulimwenguni, yaani tamaa ya mwili, tamaa ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na Baba bali hutokana na ulimwengu.
17 Uye nin nimong suu kibinai di katuzu. Bara nanin ule na adin suu unufi Kutelle ama suu sa ligang. (aiōn g165)
Nao ulimwengu unapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu milele. (aiōn g165)
18 Nono ni bebene, kubi kun ni malin ghari. Nafo na imali lanzu unan nivira Kristi di cinu, nene ma anan nivira Kristi mali dak, bara nanere ti yino kubi kuni malin ghari.
Watoto wadogo, huu ni wakati wa mwisho! Kama mlivyosikia kwamba mpinga Kristo anakuja, hivyo basi wapinga Kristo wengi wamekwisha kuja. Kutokana na hili twajua kwamba huu ni wakati wa mwisho.
19 Ina nuzzu kusaei bit, bara na idi nan gharik ba. Bara andi idi nanghari ima li bung nngharik. Bara bara kubi kona inuzu, nanin nuna nainin di nanghari ba.
Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu hasa. Kwa maana kama wangelikuwa wa kwetu, wangelikaa pamoja nasi, lakini kutoka kwao kulionyesha kwamba hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kwetu.
20 Bara nani anin dini shapewe unuzu kiti le na adi Lau, inani yiru kidegen gye.
Lakini ninyi mmetiwa mafuta na yeye Aliye Mtakatifu, nanyi nyote mnaijua kweli.
21 Nanyertin minu, bara na iyiru kidegen ba, bara iyiru barana kinu di degen gye ba.
Siwaandikii kwa sababu hamuijui kweli, bali kwa sababu mnaijua, nanyi mnajua hakuna uongo utokao katika kweli.
22 Ghari unan kinue amere ule na anari Yesu ku amere Kristi? Ule unitere unan ni vira nin Kristi, bara na anari Ucif.
Je, mwongo ni nani? Mwongo ni mtu yule asemaye kwamba Yesu si Kristo. Mtu wa namna hiyo ndiye mpinga Kristo, yaani, yeye humkana Baba na Mwana.
23 Ulena anari Usaun na adinin Ncife ba. Vat ulena ayina nin Usaun adini Ucife tutung.
Hakuna yeyote amkanaye Mwana aliye na Baba. Yeyote anayemkubali Mwana anaye na Baba pia.
24 Bara anughe, elemong na ina lanza nin cizine soo nanya mine, inani mayitu nanya in Saun ne nin Cife.
Hakikisheni kwamba lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu. Kama lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana na ndani ya Baba.
25 Lo likawaire ana ni nari: ulai unsali ligang. (aiōnios g166)
Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani, uzima wa milele. (aiōnios g166)
26 Imalu nyertinu minu kitene nale na ima wultunu minu.
Nawaandikia mambo haya kuhusu wale watu ambao wanajaribu kuwapotosha.
27 Bara anunghe, ushapewe na ina malin seru kiti me suu nanya mine, nin naanin idinin suu umong da dursuzo minu ba. Bara ushapi me ma dursu minu imong vat nin gidegen na kinu ba, nafo na amlin dursuzu minu uworu, suu nanya me.
Nanyi, upako mlioupata kutoka kwake unakaa ndani yenu, wala ninyi hamna haja ya mtu yeyote kuwafundisha. Lakini kama vile upako wake unavyowafundisha kuhusu mambo yote nayo ni kweli wala si uongo, basi kama ulivyowafundisha kaeni ndani yake.
28 Nin nene nono nayi nin, suu nanya me, bara kubi kona ada, tima yitu nin chin in daki me ba.
Sasa basi, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake wakati wa kuja kwake.
29 Andi iyirughe adi lau, iyiru vat ulena adi cin gigime ina marighe kiti mere.
Kama mkijua kuwa yeye ni mwenye haki, mwajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.

< 1 Yuhana 2 >