< 1 Yuhana 1 >

1 Inlele wadi infune, elena tina mali lazu ilena tina mali yenu nin nizi bit, ilena tina mali gwinu, nin nachara bi na kifoo, kitene tipin lai.
Tunawajulisha lile lililokuwepo tangu mwanzo, lile tulilosikia, ambalo tumeliona kwa macho yetu, ambalo tumelitazama na kuligusa kwa mikono yetu, kuhusu Neno la uzima.
2 Ulaiye na ina yinin nin yenu, nin tinizi iba nin beling minu ulai sali ligang, ulena wadi nin ncife, na tina yino kiti bit. (aiōnios g166)
Uzima huo ulidhihirishwa; nasi tumeuona na kuushuhudia, nasi twawatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa pamoja na Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. (aiōnios g166)
3 Ilele na ti yene nin lanzu tima belin minu, bara usuu usujaida ligowe nin narik nin usujaida ligowe nin Ncif nin Uson, Yesu Kristi
Twawatangazia lile tuliloliona na kulisikia, ili nanyi mwe na ushirika nasi. Na ushirika wetu hasa ni pamoja na Baba na Mwanawe, Yesu Kristo.
4 Tinanin yrtine elemone bara ti timinu liburi liboo kaan.
Tunaandika mambo haya ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
5 Ulelere uliru umagulete dana tina laza tidin belin minu: Kutelle nkanan ghari nanya me na mbibit diku ba vat.
Huu ndio ujumbe tuliosikia kutoka kwake na kuwatangazia ninyi: kwamba Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza lolote.
6 Andi tibenle tidin su usujaida ligowe nin ghe tinani din chin nanya sirti tia kinu, natidin su kidegen ghe ba.
Kama tukisema kwamba twashirikiana naye huku tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatutendi lililo kweli.
7 Bara nani andi tidin chin nanya nkana ghe nafo amen in nkanan ghe, tinani dinin dimun usujaida ligowe nin kogha, nin mmii Yesu uson me kusu nari lau unu nalapi bit.
Lakini tukienenda nuruni, kama yeye alivyo nuruni, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.
8 Andi ti woro tidinin kulapi ba, tidin rusuzu atibitari na kidegen di nanya bi ba.
Kama tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe wala kweli haimo ndani yetu.
9 Bara nani anadi benle alapi bit, ame dinin kibinai kisheu ma shawu nin na lapi bite anin kusu nari lau unuzu salinlaubite.
Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha kutoka kwenye udhalimu wote.
10 Andi tibenle ti dinin na lapi ba tita ghe unan kinu, nin nani tipipin me di nanya bit ba.
Kama tukisema hatukutenda dhambi, twamfanya yeye kuwa mwongo na neno lake halimo ndani yetu.

< 1 Yuhana 1 >