< 1 Ukorintiyawa 16 >

1 Nene nbelen mapitiru pitiru nanit alau, nafo na nna bellin anan dortu Kutellẹ nati nlira in Galantiya, nanere anung wang sun.
Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
2 Liri lin cizinu nayiri kuzor, na kogha mine rafa imoimon likot ligan kayiri me. Asa nda na mapitiru pitire ma yituku ba.
Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
3 Asa nda duru, alenge na anung yinna mung, mba tu nani nin niyerti idi ni mapitiru pitiru mine in Urshalima.
Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
4 Andi uma caunu meng wang do, ima du nan mi.
Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
5 Mba dak kitime, asa nda kata in Makidoniya-bara nma katun Makidoniya.
Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia—maana nataraji kupitia Makedonia.
6 Nmoti nanghinuere mbaso udu kubin pitiru kiti, bara inan buni ncinnighe, vat kiti kanga na nma du.
Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
7 Bara na ndi nin su in yene munu nene nan nya kubiri bat ba, ndi cissu kibinayi ntinayiri gbardang nan ghinu, andi Cikilare in yinna.
Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
8 Vat nani meng ba so in Afisos nduru kubin pentecost,
Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
9 Vat nin woru katwa puni pash, a anan shina yita ku gbardang.
Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
10 Nene asa Timitawus nda, na aso nan ghinu sa fiu, bara adin su katwa in Cikilari nafo menghe.
Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
11 Na umong wa yasighe ba. Buno ghe nya shewu anan da kiti ning, bara ndin cissu iyizi in yene ghe ada ligowe nan nya linuana.
Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
12 Nengene ubelen Apolos gwana bit: Nna ghe likara kibinayi a dak kitimine nin linuana, na a yinna udake nene ba; ama dak asa ase kubi.
Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
13 Sun lissosi nca, yisinan nin nakara nan nya yinu sa uyenu mine, sun nafo nanilime, yitan nin nakara.
Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
14 Vat nimon ile na ima su sun nan nya kauna.
Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
15 Iyiru anan kilarin Istifanas, inughere anan cizinun seru nlirun tucu Akaya, inughe na ni atimine kiti katwa nanit alau. Nene ndi minu kucukusu, nuana nilime nan nishono,
Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
16 nakpan atimine kiti inmusu nanit ane, nin vat lenge na adin bunu nan nya katwa a anontizo ligowe nan ghirik.
muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
17 Ndi su liburi libo nin dakin Istifanas, Furtunatus, a Akaikus; inun kulo kika na anun duku ba.
Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
18 Bara ina da ghantini uruhu nighe nin na lele. Bara nani cau iyinni nin nimus nanit nafo alengene.
Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
19 Anan dortu Kutellẹ in Asiya din lissu minu. Akila nin Briskila din lissu nan nya NCikilari, nin nanan dortu Kutellẹ nan nya ngamine.
Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
20 Vat nuana nilime nan nishono din lissu minu. Lisson atimine nin ni lip icine.
Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
21 Meng, Bulus, nsu ile iyerte nin nilip ncara ning.
Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
22 Andi ko uyeme unit na adi nsu usun Cikalari ba, na utin nu kifo ghe. Na Cikilari bite dak!
Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA—BWANA, njoo!
23 Na ubolu Ncikilari Yisa so nan ghinu.
Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24 Usu ning so nan ghinu vat nan nya Kristi Yisa. Uso nani.
Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.

< 1 Ukorintiyawa 16 >