< 1 Ukorintiyawa 14 >

1 Cheo ayi npiziru nsu nin filizunu Kutellẹ, bara inan se usu anaba.
Utafuteni upendo na kutamani sana karama za rohoni, zaidi sana mpate kutoa unabii.
2 Bara ulenge na adin su uliru nin long lilen na adin su uliru nin nanutari ba nin Kutelleari, na umon wasa ayininghe ba bara na adin bellu nan nya Nfip milau imon ile na inyesin.
Maana yeye anenaye kwa lugha hasemi na watu bali husema na Mungu. Maana hakuna aelewaye kwa sababu anena mambo yaliyofichika katika Roho.
3 Ulenge na adin su annabci, din liru nin nanitari atizanani ikunjo, atizanani likara, anin tizanani ayi asheu.
Lakini yeye atoaye unabii, asema na watu na kuwajenga, kuwatia moyo, na kuwafariji.
4 Ulenge na adin su uliru nin tilem din zazinu litimere, a unan sun annabci kpizina tukunan kilari Kutellẹ.
Yeye anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, lakini yeye atoaye unabii hulijenga kanisa.
5 In di nin su vat mine iwa din su uliru nin tong tilem, nin likati nane wang, usu nighari isu anabci. Ulenge na adinsuzu anabci katin unan liru nin tilem adi na unan kpilizu tileme duku ba, bara kilari nlire nan se ukunu.
Sasa natamani kwamba ninyi nyote mnene kwa lugha. Lakini zaidi ya hayo, natamani ya kwamba mtoe unabii. Yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha (labda awepo wa kutafasiri), ili kwamba kanisa lipate kujengwa.
6 Nene nuana nilime nin nishono, nwa dak kitimine nnin liru nin tong tilem, iyaghari ima se kitinighe, se de ntunun minu nliru fwang, sa uyiru, sa anabci, sa udursuzu kiti?
Lakini sasa, kaka na dada zangu, nikija kwenu na kunena kwa lugha, nitawafaidia nini ninyi? Siwezi, isipokuwa nasema nanyi kwa njia ya ufunuo, au kwa njia ya maarifa, au unabii, au kwa njia ya fundisho.
7 Andi adadu nsali tilai nafo ishirya sa abengbeng na tiwuyi mine di ngangang ba, ima ti iyinzari umon yinin iyaghari idin wulusue?
Ikiwa vitu visivyo na uhai kama filimbi au kinubi visipotoa sauti zilizo na tofauti, itatambulikanaje ni chombo gani kinachezwa?
8 Asa ipene kulantun ghe nin lon li wuyi ugan na lin likumba, umon ba ti iyinzari ayinin kubin kelu ndu likume?
Kwa maana ikiwa baragumu itatoa sauti isiyojulikana, ni jinsi gani mtu atatambua ya kuwa ni muda wa kujiandaa kwa vita?
9 Nanere di ni ghinue wang; asa idin su uliru nin ti gbulang tongo nati di kanan ba, iyizari imati umong yining imon ile na ibelle, iba liru, na umon ba yinu ba.
Vivyo hivyo na ninyi. Mkitoa kwa ulimi neno lisilo dhahiri, ni jinsi gani mtu ataelewa mnachosema? Mtakuwa mkiongea, na hakuna atakayewaelewa.
10 Tilem duku gbardang nyi, na nlong duku sa uma'na ba.
Hakuna shaka kwamba kuna lugha nyingi mbalimbali duniani, na hakuna hata moja isiyo na maana.
11 Bara nani andi na nyinno imong ile na idin belẹ nin long lilem ba, nmaso kumara kiti nnan lirẹ, ame unan lirẹ wang so kumara kitining.
Lakini ikiwa sijui maana ya lugha, nitakuwa mgeni kwake yeye anenaye, naye anenaye atakuwa mgeni kwangu.
12 Anung wang andi idin yalinu nworu iyene Nfip micine in nan nya mine yitan yakyak n kelu kutin nlira.
Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani sana kuona uthihirisho wa Roho, takeni kwamba mzidi sana kulijenga kanisa.
13 Ame ule na adin liru nin long lilem na asu nlira ase ukpiliuwe.
Hivyo, yeye anenaye kwa lugha na aombe apewe kutafasiri.
14 Bara nwa ti nlira nin long lilem, uruhu nghari di nlire a na kibinayi ni nnin mara imon icine ba.
Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
15 Nyaghari meng basu? Mba su nlira nin ruhu ning, nkquru nsu nlira nin kibinayi ning tutung. Mba su avu nin ruhu nin, nkuru su avu nin kibinayi nin tutung.
Nifanye nini? Nitaomba kwa roho yangu, lakini pia nitaomba kwa akili zangu. Nitaimba kwa roho yangu, na nitaimba kwa akili zangu pia.
16 Andi na nani ba, uwa su liru Kutellẹ nin ruhu ame ule na adin lanzu timap feba ti inyizari aworo ''usonani'' andi udin nakpu ngudiya, a na ame yiro imon ilenge na fe din belue ba?
Vinginevyo, ukimsifu Mungu kwa roho, yeye aliye mgeni ataitikaje “Amina” utoapo shukurani, akiwa hayajui usemayo?
17 Fe nnaKpa ugudiyẹ fe gegeme kang, na ulele in nin setikunang nan nya ba.
Maana ni kweli wewe washukuru vema, lakini yule mwingine hajengwi.
18 Ngode Kutellẹ nworu nkatin minu vat nin su nliru nin tilem ngangang.
Namshukuru Mungu kwa kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote.
19 Ukatin mengku nworu nbelin agbulang ataun nan nya kuti Nlira nin yinnu ning nnan kele among, nnin woru nenge nbelin agbulang amui nin tilem likure a na umong lanza ba.
Lakini katika kanisa ni heri ninene maneno matano kwa ufahamu wangu ili nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.
20 Nuana nilime ni nishono, na iwa su ukpilizu tinonoba. Kitene nimon inanzang, son nafo nono, nan nya kpilizu mine yitan awasara.
Kaka na dada zangu, msiwe watoto katika kufikiri kwenu. Badala yake, kuhusiana na uovu, iweni kama watoto wachanga. Lakini katika kufikiri kwenu mkawe watu wazima.
21 Nan nya sharawe ina yertin, “Kiti nanit tilem tilem nin tinu namarari nma liru nin nanit alele; vat nin nani na ima lanzui ba,” Ubellun Ncikilari.
Imeandikwa katika sheria, “Kwa watu wa lugha nyingine na kwa midomo ya wageni nitasema na watu hawa. Wala hata hivyo hawatanisikia,” asema Bwana.
22 Bara nani tileme alamar, na kiti na nan dortu Kutellẹ ba, se kiti na nan salin dortu Kutellẹ. U anabci na kulapari kiti na nan ṣali dortu Kutellẹ ba se kiti na nan dortu Kutellẹ.
Hivyo, ndimi ni ishara, sio kwa walioamini, bali kwa wasioamini. Lakini kutoa unabii ni ishara, sio kwa wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio.
23 Andi bara nanere, vat anan dortu Kutellẹ nwa dazuro isu uliru nin tilem, anan das nin nanan salin dortu Kutellẹ nin da pira, na iba woru tidi nin nilazaba? ag,
Haya, ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja na wote wanene kwa lugha, na wageni na wasioamini wameingia, je hawawezi kusema kwamba mna wazimu?
24 Iwa din woru vat mine di nan nya annabci kunan das sa unan salin dortu Kutellẹ nin da pira, amase uyinnu vat nile imon na alanza, ame kpilizu nin litime imon irika na alanza idin belue.
Lakini ikiwa wote mnatoa unabii na asiyeamini au mgeni akaingia, atashawishiwa na yote asikiayo. Atahukumiwa na yote yasemwayo.
25 Imon liyeshin kibinayi me ba nuzu kanang anin diu nin muro me a su Kutellẹ usujada a durso kanang Kutellẹ nan nya mine.
Siri za moyo wake zingefunuliwa. Matokeo yake, angeanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu. Angekiri ya kwamba Mungu yu kati yenu.
26 N'yaghari tutung nuana nilime nin nishono? Iwa da zuro ligowe, umon dinin na sem, umon udursuzu kiti, umon upuzunu nimon, umon uliru nin tilem, sa ukpilizu tilem. Na tisu imon vat ti nan se tikunant kuti Nlira.
Nini kifuatacho basi, kaka na dada zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana Zaburi, mafundisho, mafunuo, lugha au tafsiri. Fanyeni kila kitu ili kwamba mlijenge kanisa.
27 Asa umon lira nin lon lilem, na ise anit naba sa natat, nan nya mine, ise umon unan kpilizu nimon ile na ibelle.
Kama yeyote ananena kwa lugha, wawepo wawili au watatu, na kila mmoja katika zamu. Na mtu lazima atafasiri kilichosemwa.
28 Asa na unan kpiliu dukuba, kogha mine min tik nan nya kilari nlire, na ana su uliru nin litime usanme a Kutellẹ.
Lakini kama hakuna mtu wa kutafasiri, basi kila mmoja wao akae kimya ndani ya kanisa. Basi kila mmoja aongee peke yake na kwa Mungu.
29 Na a annabawa naba sa natat su uliru, na among anan lanzẹ nin dumun ulire na ibelle.
Na manabii wawili au watatu wanene, na wengine wasikilize kwa kupambanua kilichosemwa.
30 Andi ujinjin duku nan nya lissosin mine na ayinno, na ame ulenge na ayita nlire ti tik.
Lakini aliyeketi akifunuliwa jambo katika huduma, yule ambaye alikuwa ananena na anyamaze.
31 Andi kogha mine nsu u annabnaci nalalarum bara kogha mine nan se likara nibinayi.
Kwa kuwa kila mmoja wenu anaweza kutoa unabii mmoja baada ya mwingine ili kwamba kila mmoja aweze kujifunza na wote waweze kutiwa moyo.
32 Bara ti ruhu na anabawa, inung a anabawere nin nati mine din dortu mun.
Kwa kuwa roho za manabii ziko chini ya uangalizi wa manabii.
33 Bara na Kutellẹ. di Kutellẹ. ku shogolog ba, kun lisosin limanghari. Nafo na nitin nlira nanit alauwe di.
Kwa kuwa Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani. Kama ilivyo katika makanisa yote ya waumini,
34 Na awani mizin tik nan nya niti nlira. Bara na iyina nani isu uwiliru ba, na inughe yita nin ni nati, nanere uduke din belu.
imewapasa wanawake wakae kimya katika kanisa. Kwa kuwa hawaruhusiwi kuzungumza. Badala yake, wanapaswa kuwa katika unyenyekevu, kama pia sheria inavyosema.
35 Andi imoimon duku ile na idin konu nani ayi inyinnuẹ na itirin ales mine nilari. Bara imon ncinghari uwani su uliru nan nya kilari nlira.
Kama kuna chochote wanatamani kujifunza, basi wawaulize waume zao nyumbani. Kwa kuwa ni aibu kwa mwanamke kuongea katika kanisa.
36 Uliru Kutellẹ na nuzu kiti minere? Anughere una duru kiti mine cassa?
Je neno la Mungu lilitoka kwenu? Je limewafikia ninyi tu?
37 Asa umon din pillu ame annabiari sa unit unan ruhu, na a belu nenge imon ile na ina nyertin minu uduka Ncikilariari.
Kama mtu akijiona kuwa ni nabii au wa rohoni, inampasa ayatambue mambo ninayowaandikia ya kwamba ni maagizo ya Bwana.
38 Asa umon nari ule ulire na iwa yinin ninghe. ba.
Lakini asipotambua haya, mwacheni asitambuliwe.
39 Bara nani linuana, piziran usu nworu isu u ananbci, nani na iwa wanting uliru nin tilem ba.
Hivyo basi, kaka na dada zangu, takeni sana kutoa unabii, na msimzuie mtu yeyote kunena kwa lugha.
40 Bara nani na tisu imon vat nan nyan kanang nin libau dert licine gegeme.
Lakini mambo yote yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.

< 1 Ukorintiyawa 14 >