< 1 Ukorintiyawa 11 >

1 Sun lisosin limang nafo men, nafo na men din su lisosin nafo Kristi.
Niigeni mimi kama ninavyomwiga Kristo.
2 Nene in di liru mine bara na idin lizunu nin mi nan nya nimon vat tutun inin yisin gangang nan nya nadadu alenge na inani munu.
Nawapeni hongera kwa sababu mnanikumbuka na kwa sababu mnayashikilia yale maagizo niliyowapeni.
3 Nene ndinin su iyinin Kristiari unan nbu nko kame gankilime, a gakilime ubun nwani, a Kutellẹ amere unan bun nKristi.
Lakini napenda pia mjue kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, na mwanamume ni kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
4 Gakilime ka na ata nlira sa ayene ubun a litime kirno na ana litime ngongon ba.
Basi, kila mwanamume anayesali au anayetangaza ujumbe wa Mungu huku amefunika kichwa chake, huyo anamdharau Kristo.
5 Nani vat uwani ule na ata nlira sa a yene ubun sa ukirrunu litime na nà litime ngongon ba. Bara usosin imon irumere nin woru apele titime.
Na mwanamke akisali au kutangaza ujumbe wa Mungu bila kufunika kichwa chake, anamdharau mumewe; anayefanya hivyo ni sawa tu na mwanamke aliyenyoa kichwa chake.
6 Asa na uwani ma kiru litime ba, na awarin titime cot. Andi imon cingharib uwani werin sa apelu titime, nbara a kiru litime.
Mwanamke asiyefunika kichwa chake, afadhali anyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa; basi, afadhali afunike kichwa chake.
7 Naneri na gankilime wa kiru litime ba, bara na ame kuyeleri nin gongon Kutellẹ. Ame uwani ngogon ngankilimeri.
Haifai mwanamume kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na kioo cha utukufu wake Mungu; lakini mwanamke ni kioo cha utukufu wa mwanamume.
8 Bara na iwa ke gankilime unuzu kitin nwani ba, uwaneri iwa keghe unuzu kitin gankilime.
Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.
9 Na iwa ke gankilime bara uwani ba, iwana ke uwani bara gankilimeri.
Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.
10 Unere nta uwani cau ayita nin litappa tigo litime, bara nono kadura Kutellẹ.
Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.
11 Vat nin nani, kitin Cikilari, uwani sosin lisosin litime ugan nin gankilime ba, a na gankilime wang sosin lisosin litime ugan nin wani ba.
Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.
12 Nafo na uwani na dak unuzu kitin gankilime, nanare gankilime na dak unuzu kitin nwani. A imon vat unuzu kiti Kutellẹ.
Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.
13 Sun asarawe ikosu ulire nin natimine, udi dert uwani ti nlira udu kiti Kutellẹ. nin litime fwangha?
Amueni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kumwomba Mungu bila kuvaa kitu kichwani?
14 Ani na makeke litime ndurso minu nenge, asa gankilime di nin titi jakaka imon ncighari kitime,
Hata maumbile yenyewe huonyesha wazi kwamba kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu ni aibu kwake mwenyewe;
15 Ani na makeke ndurso minu nwo asa uwani di nin titi ti jakaka na imon ngogon mere ba?
lakini kwa mwanamke kuwa na nywele ni heshima kwake; nywele zake ndefu amepewa ili zimfunike.
16 Asa umon di nin mong uliru ugang nin lele, na arik dinin namong al ada ugang ba, sa nan nya niti nlira Kutellẹ wang.
Kama mtu anataka kuleta ubishi juu ya jambo hili, basi, na ajue kwamba sisi hatuna desturi nyingine, wala makanisa ya Mungu hayana desturi nyingine.
17 Nan nya nale adue, na ndin liru mine ba, bara asa izuro ligowe, na idin dazu nin nimon icine ba sai inanzan.
Nikiwa bado nawapeni maagizo haya, siwezi hata kidogo kuwapa ninyi hongera kuhusu haya yafuatayo: mikutano yenu ninyi waumini yaleta hasara zaidi kuliko faida.
18 Nin cizune, nna lanza au asa izuro ligowe kuti nlira, usali munu nati din nan nya mine, na nyina nin lirumine vat ba.
Awali ya yote, nasikia kwamba mnapokutana pamoja hutokea mafarakano kati yenu. Nami naamini kiasi,
19 Uso gwas na ise naissin nan nya mine, bara alenge na iyinna nin liyissin mine inan se useru nan nya mine.
maana ni lazima fikira tofauti ziweko miongoni mwenu, ili wale walio thabiti wapate kutambulikana.
20 Bara iwa zuro ligowe na idin li ujibin NCikilare ba.
Kweli mnakutana, lakini si kwa ajili ya kula chakula cha Bwana!
21 Asa idin le, kogha mine dirtinu nli ninme imonli, a amon dutu nin kukpon, a umon na yita nin kushiton ntoro.
Maana mnapokula kila mmoja hukikalia chakula chake mwenyewe, hata hutokea kwamba baadhi yenu wana njaa, na wengine wamelewa!
22 Na idi nin nilari na imali iso nan nye ba? din yassu kilari Kutellẹ ini tizza anan likimon ilanza ncingha? Nyaghari nba bellin minu? Meng nrù munua? Na nma zazun minu kitene lile imone ba!
Je, hamwezi kula na kunywa nyumbani kwenu! Au je, mnalidharau kanisa la Mungu na kuwaaibisha hao wasio na kitu? Niwaambie nini? Niwasifu? La hasha! Si kuhusu jambo hili.
23 Bara nna seru kitin Ncikilari ilenge imon na meng wang nani minu, Cikilari Yisa, nin kitike na iwa nari ame, ayauna ufungule.
Maana mimi nilipokea kwa Bwana yale maagizo niliyowaachieni: kwamba, usiku ule Bwana Yesu aliotolewa, alitwaa mkate,
24 Kimal ntin lira, apuco uni aworo, “ilele kidowo nigharidi, ka naki di bara anung, man suzun nani ilizizin ninmi”
akamshukuru Mungu, akaumega, akasema: “Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
25 Nanere tutung awa yaun kakukke kimal jibe, aworo, “kakkuk kane kan ciu nliru upese ari nannya nmī ning. Suzun nani kubi kongo na idin sonē nin kakukke inan lizino nin me.''
Vivyo hivyo, baada ya kula, akatwaa kikombe akasema: “Hiki ni kikombe cha agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu. Fanyeni hivi, kila mnapokunywa, kwa kunikumbuka.”
26 Bara vat kubi ko na ileo ufungal ulele nin kakkuk kane, idin girzunu nkul Ncikilarere udu lirin same.
Maana kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
27 Vat nlege na adin li ufungalle sa adin so kakkuk Ncikilare a ayita likara linanzang ama yitu nin kulapi kiti kidowo nin mī Ncikilare.
Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.
28 Na unit tu adumun litime, ma anin li ufungal ani sono kakukke.
Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;
29 Vat ulenge na adin li aso sa uyenun ngongong kidowo Ncikilare adin li aso usharawari litime.
maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.
30 Unnare nta among mine gbardan di nin sali nakara a tikonu, among mine wang nkuzu.
Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.
31 Bara asa ti dumuzuna atibite, iba sunari ushara ba.
Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.
32 Nani asa idin su nari ushara, ti dinse ugwaru kitin Ncikilare, bara iwa da walin nari ligowe nin yih.
Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
33 Bara nani nuana ning, asa ida zuro ligowe kiti kileowe son ncà nati.
Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana kula chakula cha Bwana, kila mmoja amngoje mwenzake.
34 Asa umon din lanzu kukpon, na ali kilari, bara iwa da zuro ligowe nan da so ushara kubi ko nan nda nma bellun minu imn ilenge na idin nbun.
Na kama kuna yeyote aliye na njaa, na ale nyumbani kwake, ili kukutana kwenu kusisababishe hukumu. Lakini, kuhusu yale mambo mengine, nitawapeni maelezo nitakapokuja.

< 1 Ukorintiyawa 11 >