< 1 Ukorintiyawa 1 >

1 Meng Bulus, uyiculun Kristi Yisa nso unan kadura bara uyinnu Kutellẹ, a Sostanisu gwana bit,
Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
2 udu kiti na nan tortu Kutellẹ na idi in Korintus, alenge na Kristi Yisa nati nani iso lan, iwa yiwa nani iso anit alau, vat nan na lenge na idin yicu lissan Cikilari bite Yisa Kristi in ko kame kiti, Cikilari mine nini unbit.
tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
3 Na ubolu me nin lissosin lisheu unuzu kitiin Kutellẹ ucif bit a Cikilari Yisa Kristi.
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4 Ndin godu Kutelle ning ko kome kubi bara anughe, nan nyan bolu Kutellẹ na Kristi Yisa nani minu.
Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
5 Ana tti minu anan se nan nya ko lome libau, nan nya nliru nin yiru vat.
Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
6 Ana ti minu ita imon nacara, nafo na ubellee nimon liburu libo litin Kristi, na nuzu kanang nan nya mine.
kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
7 Bara nani na idiira ufilllu nruhuba, naffo na ina yita nin tok ncaa nnuzu kanang in Cikilari bite Yisa Kristi.
hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
8 Ame ni minu akara tutung udi duri imaline, bara inan so sa alapi lirin Cikilari bite Yisa Kristi.
Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 Kutellẹ di nin yinnu, ame ulenge na ana yicila minu nan nya lissosin ligo nin saunne, Yisa Kristi Cikilari bite.
Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
10 Nene ndi munu kucukusu, nuana nilime nan nishono, nan nya lissan Cikilari bite Yisa Kristi, na vat mine na yinin, na i wa se uwucu nati nati nan nya mine ba. Ndi kucukusu imunu ati umalizinu kugir kun lo ligowe nin kibinai kirum a udalili urim.
Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
11 Nani anan gan kuluwi na da tyi vet natuf nbeleng nworu uwutuzunu din piun nan nya mine.
Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
12 Nene uliru niighe ule: Ko gha mine din su, “Mengg un Bulus ari,” “Meng un Apolos” “Meng un Kefas,” sa, “Mengg un Kristi.”
Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, “Mimi ni wa Paulo,” mwingine: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine: “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine: “Mimi ni wa Kristo,”.
13 Kristẹ nkoso kidowa? iwa kotun Bulus ku kuca bara anughe? Iwa shintin munu nmyen nan nya lissan Bulussa?
Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14 Ndi nin liburi libo kiti Kutellẹ na nna shintin umon mine nmyen ba, se kiribun nin Gayus.
Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
15 Una so nani bara na umong mine man woru miyari na shintin ghe nmyen nan nya lissa ning ba.
Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
16 Ina kuru nshintino anan gan Istifanus ku. Nbanda nani, nan yiru sa nnakuru nshinto among tutung ba.
(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17 Bara ana Kristi na tuyi nshitu anitari nmyen ba nani nsu uwazi nliru ntucuari na nin nagbulan njinjin nnit ba, bara kuca nkootunu in Kristi wa so imon ihe.
Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
18 Bara kadura kuca nkotunuee tilalanghari kiti na lenge na i din nan nya nkul. Nani kitii na lenge na Kutellẹ din kacisso mine, likara Kutellẹ ari.
Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
19 Bara ina nyertin, “Meng ma malu kiti nin dadiu na yinjini” mma canu uyinnu na nan yiru.
Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali.”
20 Unit ujinjinghe din weri? Unan ni nyerte din we? Unan piziru in yinnu nko kuje din we? Na Kutellẹ na kpilya njinjin in yeh misoo tilalang ba? (aiōn g165)
Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu. (aiōn g165)
21 Bara na uyih vat nin jinjing nnin na una yinnin Kutellẹ ba, una poah Kutellẹ liburi nan nya tilalan nbellu nliru Kutelle kiti na lenge na iyinna.
Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
22 A Yahudawa wa piziru imon al'ajibi a Hilinawa pizira njinjing.
Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
23 Nani arik din uwazi nkotunu in Kristi, litala ntizuru na Yahudawa a tilalang kiti na Hilinawa.
lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
24 Kiti na lenge na Kutellẹ na yicila, a Yahudawa nin na Hilinawa, ti din su uwazi in Kristi nafo Likara nin kujinjin Kutellẹ.
lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
25 Bara tilalang Kutellẹ katin likara njinjing nanit, a usali likara Kutellẹ katina akara nanit.
Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
26 Yenen imusun in yicilue na Kutellẹ na yicila munu mun, nuana nilime nin nishono. Na gbardan mine wa di jinjing ba nan nya yenjun nanit. Na gbardang mine wadi nin gongong mbun nanit ba.
Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
27 Nani Kutellẹ wa fere imon ilalang in yih ani unit ujinjing ncin. Kutellẹ waa fere imon nsali nakara in yih ani imon nakara in yih ncin mun.
Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
28 Kutellẹ wa fere imon igugur na ina filing in yih umunu imon ile na tiyira inin nafo imon ile na arik in yira imon icinari.
Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
29 Ana su nani bara ummong wa se imon for figiri mbun me.
Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
30 Bara imon ile na Kutellẹ na su, nene i di nan nyan Kristi Yisa, Ulenge na ana so nari njinjing kiti Kutellẹ katwa kacine bite, nlau bite nin utucu bite.
Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
31 Nafo, na i nyerte nabelin, “Na ulenge na ana fo figiri na a fo nan nyan Cikilari.”
Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana.”

< 1 Ukorintiyawa 1 >