< varumi 11 >

1 pe niti, neke uNguluve alyavakanile avaanhu vake? nambe padebe. ulwakuva najune kange nili mwiSilaeli ghwa kikolo kya Abulahamu, ghwa kikolo kya Benyamini.
Basi nasema, je, Mungu aliwakataa watu wake? Hata kidogo. Kwa kuwa mimi pia ni Mwiisraeli, wa ukoo wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
2 UNguluve nalyavakanile avaanhu vake, vano alyavamanyile kuhuma mu vwandilo. pe namukagula ililembe liti kiki kuhusu uEliya, ndavule alyansumile uNguluve kyanya ja Silaeli?
Mungu hakuwakataa watu wake, aliowajua tangu mwanzo. Je hamjui andiko linasema nini kuhusu Eliya, jinsi alivyomsihi Mungu juu ya Israeli?
3 Ntua vabudile avavili vako vope vanyemwile ilitekelo lyako. nijighe ene ne mwene, vope vinoghua uvwumi vwango”.
“Bwana, wamewaua manabii wako, nao wamebomoa madhabahu zako. Mimi peke yangu nimesalia, nao wanatafuta uhai wangu.”
4 neke ulwamulo lwa Nguluve luti kiki kuveene? “nivike vwimila jango avaanhu imbilima lekela lubale vano navikumfughamila uBaali”.
Lakini jibu la Mungu lasema nini kwako? “Nimetunza kwa ajili yangu watu elfu saba ambao hawampigii magoti Baali.”
5 nambe lino unsiki ughu ghwa lino kange kwevale vano vasighile vwimila vusalusi vwa vumosi.
Hata hivyo, wakati huu wa sasa pia kuna walio salia kwa sababu ya uchaguzi wa neema.
6 neke nave vwe vumosi, sio kange kumaghendele,
Lakini ikiwa ni kwa neema, si tena kwa matendo. Vinginevyo neema haitakuwa tena neema.
7 pe kiki? imbombo jino uIsilaeli alyale ilonda nakakyaghile looli havakemelua vakakyagha, navange vakaponesevua uvusito.
Ni nini basi? Jambo ambalo Israeli alikuwa akitafuta, hakukipata, bali wateule walikipata, na wengine walitiwa uzito.
8 ndavule jilyalembilue: “'uNguluve avapelile umwoojo ghwa ghano naghilila neke valekaghe kulola, ni mbughulutu neke navangapulikaghe kuhanga umusyughi iji.”
Ni kama ilivyoandikwa: “Mungu amewapa roho ya ubutu, macho ili wasione, na masikio ili wasisikie, mpaka leo hii.”
9 ghwope uDavidi iti, “leka imesa save sive vwafu, lutengo, lubale lwa kukuvala, na kuhombekesia uluhombo kuvene.
Naye Daudi anasema, “Acha meza zao na ziwe wavu, mtego, sehemu ya kujikwaa, na kulipiza kisasi dhidi yao.
10 leka aamaso ghaponekesivue ing'iisi neke vakunue kulola. ukaghaghunamisie amasana ghave ifighono fyoni”
Acha macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona. Ukawainamishe migongo yao daima.”
11 pe nijova, “pe vakuvile nambe kughua?” nalungavisaghe nahele ifighono fyoni. pepano kwa kukunua kuveene, uvuvangi vufikile ku iisi, neke vavuo vaponekesivue uvwifu
Basi nasema, “Je, wamejikwaa hata kuanguka?” Isiwe hivyo kamwe. Badala yake, kwa kushindwa kwao, wokovu umefika kwa Mataifa, ili wao wenyewe watiwe wivu.
12 lino nave kukunua kwave vwe vumofu vwa iisi, pe kalingi pwevuli uvukamilifu kwave kukila.
Sasa ikiwa kushindwa kwao ni utajiri wa ulimwengu, na kama hasara yao ni utajiri wa mataifa, ni kiasi gani zaidi itakuwa kukamilika kwao?
13 na lino nijova numue mwevaanhu va pa iisi. ulwakuva muli vasung'ua va vaanhu va iisi isinge, nikujighinia mu mbombole jango inofu.
Na sasa naongea nanyi watu wa Mataifa. Kwa kuwa nimekuwa mtume kwa watu wa Mataifa mengine, najivunia huduma yangu.
14 ndeponu nikuvaponia uvwifu ku vano valim'bili ghumo nune. pamo ndeponu tukuvapoka vamonga.
Labda nitawatia wivu walio mwili mmoja na mimi. Labda tutawaokoa baadhi yao.
15 ulwakuva nave kukanilua kwave ghe mapuling'ano gha pa iisi, pe luvisagha ndani kukwupilua kwave, looli vwumi kuhuma ku vafue?
Maana ikiwa kukataliwa kwao ni maridhiano ya dunia, kupokelewa kwao kutakuwaje ila uhai toka kwa wafu?
16 nave imheke isa kwanda sa kuvikilisia, pe jilivuo inonge ja vutine. nave ghuvikilisia amalela na gha matafi vulevule.
Kama matunda ya kwanza ni akiba, ndivyo ilivyo kwa donge la unga. Kama mzizi ni akiba, matawi nayo kadhalika.
17 neke nave amatafi ghadumulivue ndavule uve, ilitafi lya museituni ghukavwalilue mu vamonga, nave ulyavombile palikimo na vavo mu malela gha vumofu vwa mseituni,
Lakini kama baadhi ya matawi yamekatwa, kama wewe, tawi pori la mzeituni, ulipandikizwa kati yao, na kama ulishiriki pamoja nao katika mizizi ya utajiri wa mzeituni,
18 nungajighiniaghe ku matafi neke nave ghukughinia na veve ghwejuno ghukughatanga amalela, looli amalela ghikukutanga uve.
usijisifu juu ya matawi. Lakini kama unajisifu, si wewe ambaye unaisaidia mizizi, bali mizizi inakusaidia wewe.
19 pe ghuliti, “amatafi ghakadumulivue neke nipate uvwalua mu limela”.
Basi utasema, “Matawi yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika shina.”
20 lino pe lweli vwimila kuleka kukwitika kwave vakadumulivue, neke uve ukimile ku lukangafu lwa lwitiko lwako. nungajisaghile juve ghwemwene mu lywa kwighinia kyongo, looli oghopagha.
Hiyo ni kweli. Kwa sababu ya kutoamini kwao walikatwa, lakini wewe ulisimama imara kwa sababu ya imani yako. Usijifikirie mwenyewe kwa hali ya juu sana, bali ogopa.
21 ulwakuva nave uNguluve nakaghalekila amatafi gha vutengulilo kange nailikusaghila najuve.
Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, hatakuhurumia wewe pia.
22 lola himbe amaghendele amaagholofu nu vukali vwa Nguluve. ku lubale lumo, uvukali vulyisile kyanya ja vaYahudi vano valyaghwile. neke kulubale ulunge uvugholofu vwa Nguluve vukwisa kulyuve, nave ghukukala mu vugholofu vwake. nave na uluo najuve vikukubudila kutali.
Angalia, basi, matendo mema na ukali wa Mungu. Kwa upande mmoja, ukali ulikuja juu ya Wayahudi ambao walianguka. Lakini kwa upande mwingine, wema wa Mungu huja juu yako, kama utadumu katika wema wake. Vinginevyo wewe pia utakatiliwa mbali.
23 nave avene navighendelela kuleka kukwitika vivyalilila kange. ulwakuva uNguluve aliningufu sa kuvwavyala kange.
Na pia, kama hawataendelea katika kutoamini kwao, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
24 ulwakuva nave umue mukadumulivue kunji ndavule umseituni ghwa mulisoli ughwa muvutengulilo, pe kusyetuka na kuvyalua mumseituni ghuno nono, nakwekukila kyongo ava Yahudi, vano hwene matafi gha muvutengulilo ghano ndeponu ghivwalua kange nkate ja mseituni gwave vene?
Kwa maana ikiwa ninyi mlikatwa nje kwa ulio kwa asili mzeituni mwitu, na kinyume cha asili mlipandikizwa katika mzeituni ulio mwema, si zaidi sana hawa Wayahudi, ambao ni kama matawi ya asili kuweza kupandikizwa tena ndani ya mzeituni wao wenyewe?
25 ulwakuva vanyalukolo nanilonda muleke kukagula sino sifisime neke kuuti namungavisaghe vakoola kwa kusagha kwinu jumue. ulufiso ulu kwe kuuti ulutalamu luhumile ku Isilaeli kuhanga kukamilika kwa iisi kyale kwisile.
Kwa maana ndugu sitaki msijue, kuhusiana na siri hii, ili kwamba msiwe na hekima katika kufikiri kwenu wenyewe. Siri hii ni kwamba ugumu umetokea katika Israeli, hadi kukamilika kwa mataifa kutakapokuja.
26 lino avasilarli voni vilipokua ndavule jalembilue, “kuhuma ku saYuni ilikwisa uMpoki ivusia uvuhosi kuhuma ku Yakovo.
Hivyo Israeli wote wataokoka, kama ilivyoandikwa: “Kutoka Sayuni atakuja Mkombozi. Atauondoa uovu kutoka kwa Yakobo.
27 nili liiva lipuling'ano palikimo navo, unsiki ghuno kyale nikusivusia isambi save”.
Na hili litakuwa agano langu pamoja nao, wakati nitakapoziondoa dhambi zao.”
28 ku lubale lumo kujova isa livangili vwimila jinu. ku lubale ulunge kuhumilanila nu vutavusi vwa Nguluve, vaghanilue vwimila avaghogholo,
Kwa upande mmoja kuhusu injili, wanachukiwa kwa sababu yenu. Kwa upande mwingine kutokana na uchaguzi wa Mungu, wamependwa kwa sababu ya mababu.
29 ulwakuva ilitekelo nuvukemelo lwa Nguluve nalubadilika.
Kwa kuwa zawadi na wito wa Mungu haubadiliki.
30 ulwakuva muvwasio umue mulyamuhokile uNguluve, neke lino mwupile ulusungu vwimila uvuhosi kwave.
Kwa kuwa awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmeipokea rehema kwa sababu ya kuasi kwao.
31 ku sila jijijio lino avayahudi ava vahokile. amahumile ghake kwekuuti kuhumila mulusungu luno mulyapelilue umue ndeponu kange mukwupila ulusungu,
Kwa njia iyo hiyo, sasa hawa Wayahudi wameasi. Matokeo yake ni kwamba kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi wanaweza pia kupokea rehema.
32 ulwakuva uNguluve avapinyile avaanhu vooni ku vuhosi neke awesie kukuvasaghila voni. (eleēsē g1653)
Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi, ili aweze kuwahurumia wote. (eleēsē g1653)
33 ndavule silivuo mbaha uvomofu nu vukoola nu luhala lwa Nguluve! nasiloleka inyigho sake na kusila sa mwene nasiloleka!
Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hazichunguziki hukumu zake, na njia zake hazigunduliki!
34 ulwakuva ghwe veni juno ikagula uvufumbue vwa Mutwa? nambe ghwe veni umuvungi ghwake?
“Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani amekuwa mshauri wake?
35 neke ghweveni juno ampelile kimonga uNguluve, neke ahombue kange?
Au ni nani kwanza aliyempa kitu Mungu, ili alipwe tena?”
36 ulwakuva kuhuma kwa mwene, na ku sila ja na kwamwene, ifinu fyoni kwefile. kwamwene kwevule uvwimike kusiala na kusila. Ameni. (aiōn g165)
Kwa maana kutoka kwake, na kwa njia yake na kwake, vitu vyote vipo. Kwake uwe utukufu milele. Amina. (aiōn g165)

< varumi 11 >