< Malika 5 >

1 Vakafika umwamboijinge ija lisumbe, mulikaja lya Gerasi
Walikuja mpaka upande mwingine wa bahari, katika mkoa wa Gerasi
2 Nakalingi u Yesu ye ihuma mu ngalama, akisa kwa mwene umuunhu jumonga unyalipepo lilamafu akahumile ku mbiipa.
Na ghafla wakati Yesu alipokuwa akitoka nje ya mtumbwi, mtu mwenye roho chafu alikuja kwake kutoka makaburini.
3 U muumhu uu akikalagha ku mbiipa. Nakwalyale uwakunkola nabe kukundindila, nambe kukunkunga ni minyololo.
Mtu huyu aliishi makaburini. Hakuna aliyeweza kumzuia zaidi, hakuna hata kwa minyororo.
4 kekinga akapinywagha ni pingu na manyololo. akadumulagha amanyololo ni pingu akadenyagha. Nakwaliyale unyangufu ghwa kumulefia.
Alikuwa amefungwa nyakati nyingi kwa pingu na minyororo. Aliikata minyororo na pingu zake zilivunjwa. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na nguvu za kumshinda.
5 Pakilo na pamwisi akikalagha ku mbiipa na kufidunda, akakolagha na kukutemateme namavue amajodofu.
Usiku na mchana akiwa makaburini na milimani, alilia na kujikata yeye mwenyewe kwa mawe makali.
6 Ye am'bwene u Yesu pavutaali, akankimbilila na kufughama pa mwene.
Alipomwona Yesu kwa mbali, alikimbilia kwake na kuinama mbele yake.
7 Akakola ni lisio ilivaha, “Lunoghile nivombe kiki, Yesu, Mwana ghwa Nguluve juno alikukyanya fijo? Nikukusuma mulitavua lya Nguluve, uleke pikumumusia.”
Alilia kwa sauti kuu, “Wataka nikufanyie nini, Yesu, Mwana wa Mungu aliye Juu sana? Ninakusihi kwa Mungu mwenyewe, usinitese.”
8 Ulwakuva yumbulile, “Ghwe lipepo lichafu uve, huma mwa muunhu uju.”
Kwa kuwa alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe roho mchafu.”
9 Gwoope akamposia akati, “Ilitavua lyako veeve veeni?” Ghwope akamwamula, “Ilitavua lyango nene Ligioni, ul. wakuva tuliviinga.”
Naye alimwuliza, “Jina lako ni nani?” Naye alimjibu, “Jina langu ni Legion, kwa kuwa tuko wengi.”
10 Akampelepesia kange leka pikughadaga mu iisi jila.
Alimsihi tena na tena asiwapeleke nje ya mkoa.
11 Ilipugha ilivaha ilya ngube lilyale pakyana pakidunda silyale sidimua,
Sasa kundi kubwa la nguruwe lilikuwa likilishwa juu ya kilima,
12 ghoope ghokampelepesia, sikati, “Utusung'e mu ngube, mwetwingile munkate mu sene.”
nao walimsihi, wakisema, “Tutume kwa nguruwe; tuingie ndani yao.”
13 Akaghatavula; amapepo amalamafu ghakahuma mwa muunhu na pikwingila mu ngube, sope sikakimbilila pasi pa kidunda na pikwingila mulisumbe, neke ilipugha lya ngube imbilima ivili sikadwivila mulisumbe
Hivyo aliwaruhusu; roho wachafu waliwatoka na kuingia ndani ya nguruwe, nao walikimbilia chini ya kilima mpaka baharini, na karibia nguruwe elfu mbili walizama baharini.
14 Navadima ngube vakakimbila vakaluta mulikaja na mufikaja kuhumia imhola kusino sihumile na pivombeka mu likaja na mukisina. Pepano avaanhu vinga vakahuma kuta kulola kino kikahumile.
Na wale waliokuwa wakiwalisha nguruwe walikimbia na kutoa taarifa ya kilichotokea katika mji na katika nchi. Ndipo watu wengi walitoka kwenda kuona kilichotokea.
15 Pepano vakisa kwa Yesu pe vakamwagha umuunhun juno ahasiling'ine na mapepo alyale nu nsikali ikalile pasi, afwasivue, ali nuluhala lunofu, voope va koghopa.
Ndipo walikuja kwa Yesu na walimwona mtu aliyepagawa na pepo—aliyekuwa na Jeshi—amekaa chini, amevikwa, na akiwa katika akili yake timamu, nao waliogopa.
16 Vala vano vakasivwene sino sivombike kwa muunhu juno alyahassiling'ine na mapepo vakakimbila kino kikahumile kwa mwene kange vwimila ingube.
Wale waliokuwa wameona kilichotokea kwa mtu aliyekuwa amepagawa na pepo waliwaambia kilichotokea kwake na pia kuhusu nguruwe.
17 Voope vakampelepesia kuuti avuuke mu iisi jave.
Nao walianza kumsihi aondoke katika mkoa wao.
18 U Yesu ye ikwingila mu ngalava, umuunhu juno alyahasiling'ine na mapepo akampelepesiaa kuuti alutaghe palikimo nu mwene.
Na alipokuwa akiingia ndani ya mtumbwi, mtu aliyekuwa amepagawa na mapepo alimsihi kwamba aende pamoja naye.
19 U Yesu akankana, akati, “Lutagha kukaja na kuva nyalukolo vako, uvavule akuvombile u Mtwa, nulusungu luno akupelile.”
Lakini hakumruhusu, lakini alimwambia, “Nenda nyumbani kwako na kwa watu wako, na uwaambie alikufanyia Bwana, na rehema aliyokupa.”
20 Pepano akavuka na kuluta kupulisia imbaha sino am'bombili u Yesu mu Dekapoli, imhola isio sikava kidegho ku vooni
Hivyo alienda na alianza kutangaza mambo makuu ambayo Yesu amefanya kwake katika Dekapoli, na kila mmoja alistaajabu.
21 Pano u Yesu alyalovwike kange imwambo ijinge, mu ngalava, ilipugha ilivaha lika kong'ana kukunsungutila, pano alyale mulubale mulisumbe.
Na wakati Yesu alipovuka tena upande mwingine, ndani ya mtumbwi, umati mkubwa ulikusanyika kumzunguka, alipokuwa kando ya bahari.
22 Umbaha jumo ughwa va sinagogi, akatambuluagha Yairo, akisa, ye amwaghile, akaghua pa maghulu gha mwene.
Na mmoja wa kiongozi wa sinagogi, aliyeitwa Yairo, alikuja, na alipomwona, alianguka miguuni pake.
23 Akampelepesia fijo kange fijo, akati, “Mwalivango n'debe ghukova pifua. Nikusuma ghwise uvike uluvoko lwako pakyanya pa mwne ulwakuuti usoke akupele uvwumi ughendelele pikukala.”
Akamsihi zaidi na zaidi, akisema, “Binti yangu mdogo anakaribia kufa. Ninakusihi, njoo na uweke mikono yako juu yake ili kwamba aweze kupata afya na kuishi.”
24 Apunakavuka palikimo nu mwene, nalilipugha ilivaha lika m'bingililaa vaka mpitagha kukunsungutila.
Hivyo alikwenda pamoja naye, na umati mkubwa ulimfuata nao walimzonga karibu wakimzunguka.
25 Pwe alyale umumama jumonga juno alyale ihuma idanda inaaaamu ijio jilya mpumwisia amaka kijigho na gha viili.
Kulikuwa na mwanamke ambaye damu yake ilikuwa imetoka kwa miaka kumi na miwili.
26 Alya pumuike yongo kuva ghanga vinga alya vombiile ikyuma kyoni kino alyale nakyo. Neke nalyasokile nambe padebe, looli inamu jikava jifikwongelela.
Aliteseka vya kutosha chini ya matabibu wengi na alitumia kila kitu alichokuwa nacho. Hata hivyo hakusaidika kwa chochote, lakini badala yake alizidi kuwa na hali mbaya.
27 Akapulika imola isa Yesu. Pe akatengula kukwisa kughenda mumbele muno mwa mwene pano alyale ighenda pakate palipugha. ghwope akagusa umwenda ghwa mwene.
Alisikia habari kuhusu Yesu. Hivyo alikuja nyuma yake wakati alipokuwa akitembea ndani ya umati, naye aliligusa vazi lake.
28 wakuva akajovile, Nane ninga guse ghamenda ghake ni soka, niva mwumi.”
Kwa kuwa alisema, “Kama nikiyagusa mavazi yake tu, nitakuwa mzima.”
29 Ye agusile, idanda jikabuhilapihuma, akivoona mumbili ghwake asokile kuhuma munamu jila.
Alipomgusa, kutokwa damu kulikoma, na alijisikia katika mwili wake kwamba aliponywa kutoka kwenye mateso yake.
30 Unsiki ghughuo u Yesu akivona mu m'bili ghwake sihumile ingufu. Akyasyetuka imbale soni mulipugha pe akaposia, “Ghwe veeni juno abasisie u mwenda ghwango?”
Na ghafla Yesu aligundua ndani yake mwenyewe kwamba nguvu zimemtoka. Na aligeuka huku na huku katika umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyeligusa vazi langu?”
31 Avavulanisivua vaake vaka mwamula, “Ulivwene ilipugha ilili likikupita lisyungutile, najuve ghuti, ghweveeni juno ikukwabasia?
Wanafunzi wake walimwambia, “Unaona umati huu umekusonga ukikuzunguka, nawe wasema, 'Ni nani aliyenigusa?'”
32 Looli u Yesu akava ifilolesia ulwakuuti ankagule juno amwabasisie.
Lakini Yesu alitazama huku na huku kuona ambaye aliyekuwa amefanya hili.
33 Umukijuuva, akakagula lunoluhumile kwa mwene, akoghopa na pihilila. Akalukagula pe akaghua pasi pamwene akolelela sooni sino sivombike.
Mwanamke, akijua kilichotokea kwake, aliogopa na kutetemeka. Alikuja na alianguka chini mbele yake na kumwambia ukweli wote.
34 Akajova kwa mwene, “Mwalivango usokile vwimila ulwitiko lwako. Ulutaghe nulutangano inamu jako jisoke lwoni
Alisema kwake, “Binti, imani yako imekufanya uwe mzima. Enenda kwa amani na uponywe kutoka kwenye ugonjwa wako.”
35 Pano alyale ijova, valisile avaanhu vamo kuhuma kwa ngoyo wa Sinagogi, vakaati, “Umwalivo afuile. Kiki ghuku n'gasia um'bulanisi?”
Alipokuwa akizungumza, baadhi ya watu walikuja kutoka kwa kiongozi wa Sinagogi, wakisema, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua mwalimu?”
36 Looli u Yesu ye akipulike kino valyajovile, akambula um'baha ghwa sinagogi, “Uloghopagha. Itikagha.”
Lakini Yesu aliposikia ambacho walikisema, alimwambia kiongozi wa Sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
37 Akavakana vooni kulutania naghwope, looli akantoola u Petro, Yakobo, nu Yohana navanyalukolo va Yakobo.
Hakumruhusu yeyote kuongozana naye, isipokuwa Petro, Yakobo, na Yohana, ndugu yake Yakobo.
38 Vakisilepakaja pa m'baha ghwa va sinagogi ghwope akalivona ili batu, kukola na kulila.
Walikuja nyumbani kwa kiongozi wa Sinagogi naye aliona vurugu, kulia kwingi na kuomboleza.
39 Ye ingile mu nyuma, akavaposia akati, “Kiki musukunile kange kiki mulila? Umwana nahwile looli ighona.”
Alipoingia nyumbani, aliwaambia, “Kwa nini mmesikitika na kwa nini mnalia? Mtoto hajafa bali amelala.”
40 Vakanseka, looli umwene akavahumia vooni kunji, akavatola ava pafi nava vulanisivua vala, kingila munkaate muno mwealyale u mwana.
Walimcheka, lakini yeye, aliwatoa wote nje, alimchukua baba wa mtoto na mama na wale waliokuwa pamoja naye, na aliingia ndani alimokuwa mtoto.
41 Akankola uluvoko lwa mwana akati, “Talitha koum,” kwekuuti, “Ggwe minja uve nikukuvula, simuka.”
Aliuchukua mkono wa mtoto na alimwambia, “Talitha koum,” ambayo ni kusema, “Binti mdogo, nakuambia, amka.”
42 Unsiki ghughuo umwana jula akasimuka na na pighenda (ulwakuva alyale na maka kijigho na ghaviili). nakalinga vakakoluo ni nganighani na nuludegho luvaha.
Ghafla mtoto aliamka na kutembea (kwa kuwa alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Na ghafla walishikwa na mshangao mkubwa.
43 Akavakana ku ngufu kuuti nalunoghile umuunhu ghweni akagule imbombo jino jivombika apa. Akavavuula kuuti vampele uminja jula ikyakulia.
Aliwaamuru kwa nguvu kwamba hakuna yeyote anapaswa kujua kuhusu hili. Na aliwaambia wampatie yule binti chakula.

< Malika 5 >