< Luuka 7 >

1 pe baho uYesu ye amalile kila kinu kino akale ijova kuvaanhu vano vakampulikisiagha, akingilagha ku kapenaumu.
Baada ya Yesu kumaliza kila kitu alichokuwa anasema kwa watu waliomsikiliza, akaingia Kapernaumu.
2 um'bombi jumonga ghwa Akida akale ghwa ndalama nyinga kyongo, alyale n'tamu kyongoakale pipi pifua.
Mtumwa fulani wa akida, aliyekuwa wa thamani sana kwake, alikuwa mgonjwa sana na alikuwa karibu ya kufa.
3 neke ye apulike imhola sa Yesu uAkida jula akan'sunga umulongosi ghwa kiYahudi, kun'suuma ise kumpoka um'bombi ghwake aleke pifua.
Lakini akiwa amesikia kuhusu Yesu, yule Akida alimtuma kiongozi wa kiyahudi, kumwomba aje kumwokoa mtumwa wake ili asife.
4 vakati vafikile pipi nu Yesu, vakampelepesiagha vakatisagha, “anoghile kum'bombela ndiki umwene,
Walipofika karibu na Yesu, walimsihi kwa bidii na kusema, “anastahili kwamba unapaswa kufanya hivi kwa ajili yake,
5 ulwakuva ajighanile iisi jitu, ghwe mweene akajengile inyumba jitu ija kufunyila.
kwa sababu analipenda taifa letu, na ndiye aliyejenga sinagogi kwa ajili yetu”.
6 uYesu akaghendelelagha nu vukyusi vwake palikimo na vope. akatile alutile patali ni nyumba jila, um'bha juno akavasung'a avamanyani vake kujova nu mwene kuuti,”Ntwa uleke kujikatalila ghwemwene, ulwakuva une naninoghile uve kukwingila mu nyumba jango.
Yesu akaendelea na safari yake pamoja nao. lakini kabla hajaenda mbali na nyumba, afisa mmoja aliwatuma marafiki zake kuzungumza naye. “Bwana, usijichoshe mwenyewe kwa sababu mimi sistahili wewe kuingia kwenye dari yangu.
7 ulwakuva nambe june nisaghile ne mwene kuuti, naninoghile kukwisa kulyuve ujove ilisio lyene um'bombi ghwango ye isokagha.
Kwa sababu hii sikufikiria hata mimi mwenyewe kuwa ninafaa kuja kwako, lakini sema neno tu na mtumishi wangu atapona.
8 ulwakuva na june nili muunhu juno ipulika ululaghilo lwa vavaha vango, najune nili navasikali vango. ningam'bule uju “luta” nu jjunge “ghwise” ikwisa naju m'bombi ghwango 'vomba iki ghwope ibomba”
Kwani mimi pia ni mtu niliyewekwa kwenye mamlaka na nina askari chini yangu. Husema kwa huyu “Nenda” na huenda, na kwa mwingine, “Njoo” naye huja, na kwa mtumishi wangu 'Fanya hiki', na yeye hufanya”.
9 uYesu ye apulike aghuo akadegha, pe akalisyetukila ilipugha lino likam'bingilile akati,” nikuvavula nambe mu va silaeli nanimwaghile umuunhu unya lwitiko lukome ndavule uju.
Yesu aliposikia haya alishangaa, na kuwageukia makutano waliokuwa wanamfuata na kusema.”Nawaambia, hata katika Israeli, sijawahi kuona mtu mwenye imani kuu kama huyu.
10 peepano vala vano vakasung'ilue vakagomoka kukaaja na kukumwagha um'bombi n'kafu.
Kisha wale waliokuwa wametumwa walirudi nyumbani na kumkuta mtumishi akiwa mzima.
11 pambele aghakatile ghahumile agha uYesu akava ikyulila ilikaaja lino likemhelua Naini. navavulanisivua vake vakalutagha palikimonu mwene vakahasing'anagha nilipugha lya vaanhu.
fulani baada ya haya, ilitokea kuwa Yesu alikuwa anasafiri kwenda mji ulioitwa Naini. wanafunzi wake wakaenda pamoja naye wakiambana na umati wa watu.
12 ye alipipi nu mulyango ghwa mpulo un'kome lola, umuunhu juno afwile akava apindilue, umwana ujuo alyale mwene kwa mukijuuva jula, juno alyale mfwile. ilipugha ilikome kuhuma mumpulo ghula valyale palokimo numue.
Alipofika karibu na Lango la jiji tazama, mtu aliyekufa alikuwa amebebwa, na ni mtoto wa pekee kwa mama yake. aliyekuwa mjane, na umati wa wawakilishi kutoka kwenye jiji walikuwa pamoja naye.
13 akatile amwaghile uMutwa akam'belelela nu lusungu lukome akam'bula akati,” uleke pilila”
Alipomwona, Bwana akamsogelea kwa huruma kubwa sana juu yake na akamwambia, “Usilie”.
14 pe akalivelelela ilivokosi lino likapindile umfimba, akalyabasia, vano valyapindile vakiima akati, “ghwe nsoleka niti sisimuka”
Kisha akasogea mbele akaligusa jeneza ambalo walibebea mwili, na wale waliobeba wakasimama akasema “Kijana nasema amka”
15 umfue akasisimula na kukukala pasi nakutengula pijova. Peepano uYesu akampeela ung'iina umwanake
Mfu akainuka na kukaa chini na akaanza kuongea. Kisha Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
16 neke vooni vakamwoghopa vakaghendelela kukumughinia uNguluve viti, “Um'bili um'baha isile kulyusue” kange uNguluve avalolile avaanhu vake.
Kisha hofu ikawajaa wote. wakaendelea kumtukuza Mungu wakisema “Nabii mkuu ameinuliwa miongoni mwetu” na “Mungu amewaangalia watu wake”
17 imhola isa inono isa Yesu sikakwiline imbale sooni isa Yudea na mu fighavo ifya pa vupipi.
Hizi habari njema za Yesu zilienea Yudea yote na kwa mikoa yote ya jirani.
18 uYohani akavulwagha na vavulanisivua ghoni agha.
Wanafunzi wa Yohana walimwamwambia mambo haya yote.
19 pe uYohani akavakemhela avavulanisivua vake vavili, akavasung'a kwa Mutwa akati, “veve uve ghukwisa, neke kwale ujunge juno tumuhuvilaghe?
Ndipo Yohana akawaita wawili wa wanafunzi wake na kuwatuma kwa Bwana kusema “Wewe ndiye yule ajaye, au kuna mtu mwingine tumtazamie?
20 ye vafikile pipi nu Yesu ava vakati,” uYohani umwofughi atusung'ile kulyuve atile,'uve veve ghukwisa, neke kwale ujunge tumuhuvilaghe?
Walipofika karibu na Yesu hawa wakasema, “Yohana mbatizaji ametutuma kwako kusema, 'Wewe ni yule ajaye au kuna mtu mwingine tumtazamie?”
21 unsiki ghula ghula akavasosia avaanhu vinga kuhuma mu nhaamu ni mhumhuko, kuhuma ku mapepo amalamafu, na kuvaanhu vano navilola akavapelagha kulola.
kwa wakati huo aliowaponya watu wengi kutoka katika magonjwa na mateso, kutoka kwa roho wachafu, na kwa watu wenye upofu aliwapa kuona.
22 pe uYesu akavamula avene akati,” kumwande muva mulutile kuno muhumile mum'buulaghe uYohani sino musaghile na kupulika, avabofu vikwupilakulola, avakilemela vighenda, avanya buba vivalala, avanya mapule vipulika, avafue visyuka, na kuva vwumi. kange, avakotofuvivulua imhola inofu.
Yesu akajibu na kusema kwao. “Baada ya kuwa mmekwenda mlikotoka mtamjulisha Yohana mlichokiona na kukisikia. Wenye upofu wanapokea kuona na viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakasika, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na kuwa hai tena, masikini wanaambiwa habari njema.
23 nu muunhu juno nabuhila kukunyitika une vwimila mumaghendele ghango afunyilue.
Na mtu ambaye hataacha kuniamini mimi kwa sababu ya matendo yangu amebarikiwa”.
24 pambele ye vagomwike vala vano vakasung'ilue nu Yohani kuno vahumile, uYesu akatengula kujova isa Yohani ku lipugha akati,”muvele mulutile kunji kulola kiki, ililasi pano imhepo jisukania ililasi?
Baada ya wale waliotumwa na Yohana kurudi walikotoka, Yesu akaanza kusema kwa makutano juu ya Yohana, “Mlikwenda nje kuona nini, mwanzi ukiwa unatikiswa na upepo?
25 neke muvele kunji kulola kiki, umuunhu juno afwalile vunono? loola vala vano vifwala amhenda amanono agha vutwa na kukukala mu vwumi vwa lukelo, vali muvulugu vwa vutwa.
lakini mlikwenda nje kuona nini, mtu aliyevaa vizuri? tazama watu wale wanaovaa mavazi ya kifalme na kuishi maisha ya starehe wako kwenye nafasi za wafalme.
26 neke muluta kunji kulola kiki, m'bili? Ena, nijova numue kyongo kukila um'bili.
lakini mnakwenda nje kuona nini, Nabii? Ndiyo, ninasema kwenu na zaidi sana kuliko nabii.
27 uju ghwe juno vakamulembile, 'Lola!, nukunsung'a umwomolua ghwango pavulongola pa maaso ghinu, juno itenda isila vwimila jango,
Huyu ndiye aliyeandikiwa, “Tazama, namtuma mjumbe wangu mbele ya macho yenu, atakeyeandaa njia kwa ajili yangu,
28 nijova kulyumue kuuti, “ku vala vano vaholilue nu n'dala, kusila m'baha ndavule uYohani, neke umuunhu juno asila vufumbue juno ilikukala nu Nguluve ulubale luno pwale, iliiva mb'aha kukilla uYohani”
Nasema kwenu, kati ya wale waliozaliwa na mwanamke, hakuna mkuu kama Yohana, lakini mtu asiye muhimu sana atakayeishi na Mungu mahali alipo yeye, atakuwa mkuu kuliko Yohana.”
29 avaanhu voni palikimo navasongesia songo, vakati vapulike aghuo vakapulisyagha kuuti, “uNguluve ghwe nya kyang'haani. pwevakale vano vakofughue ku lwofugho lwa Yohani.
Na watu wote waliposikia haya pamoja na watoza ushuru, walitangaza kuwa Mungu ni mwenye Haki. Walikuwepo kati yao wale waliobatizwa kwa ubatizo wa Yohana.
30 neka avafalisayi na vavulanisi va ndaghilo sa kiYahudi, vano navofughue nu mwene vakasitile ulusungu lwa Nguluve vwimila javo veene.
Lakini mafarisayo na wataalamu wa sheria za kiyahudi, ambao hawakubatizwa na yeye walikataa hekima za Mungu kwa ajili yao wenyewe.
31 kange ndeponu ihwananisia ni kiki avaanhu ava kisina kiki? vali ndavule vali ndani?
Tena naweza kuwalinganisha na nini watu wa kizazi hiki? Wakoje hasai?
32 vahwanine na vaanha vano vinena kulighuliko, vanovikukala na kukemelana jumo nu junge vijova, 'tuvapulile ifilongilongi vwinaka namulilimila jinu, neke namusejile tusukunile neke namunenile.
Wanafanana na watoto wanaocheza kwenye eneo la soko, wanaokaa na kuitana mmoja baada wa mwingine wakisema, 'Tumepuliza filimbi kwa ajili yenu, na hamkucheza. tumeomboleza na hamkulia.'
33 uYohani umwofughi alisile na akalisagha unkate nambe kunyua uluhuje na mukati, “ali nilipepo.
Yohana mbatizaji alikuja hakula mkate wala hakunywa divai, na mkasema “Ana pepo.
34 umwana ghwa Muunhu alisile mulia kyongo kange mughasi mwiti,” manyani ghwa vasongesia songo kange vanya sambi.
Mwana wa Mtu amekuja amekula na kunywa na mkasema, “Angali ni mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi!
35 neke uvukola vukagulike kuva vuli ni kyang'ani ku vaanha vake voni.
Lakini hekima imetambulika kuwa ina haki kwa watoto wake wote.”
36 umufarisayi jumonga alyansumile uYesu alute kulia palikimo numwene. pe uYesu ye ungile mu nyumba ja Falisayi, akeghamila imesa jila neke alie.
Mmoja wa mafarisayo alimwomba Yesu aende kula pamoja naye. Baada ya Yesu kuingia kwenye nyumba ya farisayo, aliegemea kwenye meza ili ale.
37 lola kwealyale un'dala jumonga mulikaaja ilio juno alyale muhosi. akamanya kuuti ikalile kwa Falisayi, akaleta isupa ja mafuta amanono ghano ghinukilila.
Tazama kulikuwa na mwanamke mmoja katika jiji hilo aliyekuwa na dhambi. Akagundua kuwa alikuwa amekaa kwa Farisayo, akaleta chupa ya manukato.
38 akima nsana jake pipi na maghulu ghake kuno ilila. kange akatengula kunyopesia amaghulu ghake na masosi, na kupulusia ni linyele lwa mutu ghwake, kuno inonela amaghulu ghake na kupaka amafuta ghala ghano ghinukilila.
Alisimama nyuma yake karibu na miguu yake huku akilia. Tena alianza kulowanisha miguu yake kwa machozi, na kuifuta kwa nywele za kichwa chake, akiibusu miguu yake na kuipaka manukato.
39 umfalisayi jula huno alyale amughongolile uYesu ati avwene ndikio, akasagha jujuo akati, “nave umuunhu uju asavisagha m'bili, ale ikagula uju ghwe veni kange ghwe n'dala ghwa ndani juno ikumwabasia, kuuti ghwe nya sambi.
Na yule farisayo aliyekuwa amemwalika Yesu alipoona hivyo, akawaza mwenyewe akisema, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua huyu ni nani na ni aina gani ya mwanamke anayemgusa, ya kuwa ni mwenye dhambi.
40 uYesu akamwamula na kukum'bula, “simoni nili ni kinu kwa kukuvula, “akati, kijove mbulanisi'
Yesu akajibu na kumwambia, “Simoni nina kitu cha kukuambia. “Akasema” “Kiseme tu mwalimu!”
41 uYesu akaati, “kwevalyale avaanhu vavili vano valyale visighilua ihela kwa jumonga juno alyavakopile. jumo asighiluagha idinali ifilundo fihaano nu ghwa vuvili asighiluagha idinali fijigho fihaano.
Yesu akasema “Kulikuwa na wadaiwa wawili kwa mkopeshaji mmoja. Mmoja alikuwa anadaiwa dinari mia tano na wa pili alidaiwa dinari hamsini.
42 avaanhu ava ye va kunilue kuhomba, juno alyavakopile akavasaghila. lino mu avuo vano vano vakasaghilwagha, “aliku kya ikumughana kyongo?
Na walipokuwa hawana pesa ya kumlipa aliwasamehe wote. Sasa ni nani atampenda zaidi?
43 uSimoni akamwamula akati, “nivona juno asaghilue kyongo”. uYesu akambula kuuti, “uhighile sesene”.
Simoni akamjibu na kusema, “Nadhani aliyesamehewa zaidi.”Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
44 uYeu akansyetukila umukijuva na kujova kwa Simoni, “ghukumwagha umukijuva uju. ye ningile mu nyumba jako. numelile amalenga vwimila amaghulu ghango, neke uju, ku masosi ghake, ofwighe amaghulu ghango na kupulusia ni linyele lyake.
Yesu akamgeukia mwanamke na kusema kwa Simoni, “Unamwona huyu mwanamke. Nimeingia kwenye Nyumba yako. Hukunipa maji kwa ajili ya miguu yangu, lakini huyu, kwa machozi yake, alilowanisha miguu yangu na kuifuta kwa nywele zake.
45 nukaninonile, neke umwene, kuhuma ikwingila muno nakalekile kukughanonela amaghulu ghango.
Hukunibusu, lakini yeye, tangu alipoingia humu hakuacha kunibusu miguu yangu.
46 nukapakile amafuta mu maghulu ghango, neke apakie amaghulu ghango amafuta amanono ghano ghinukila.
Hukuipaka miguu yangu kwa mafuta, lakini ameipaka miguu yangu kwa manukato.
47 ku ulu nikukuvula kuuti alyale nu vuhosi vwinga kange asaghilue kukila, kange akanoghile kyongo. neke juno asaghilue padebe, ighana padebe lwene.”
Kwa jambo hili, nakwambia kwamba alikuwa na dhambi nyingi na amesamehewa zaidi, na pia alipenda zaidi. Lakini aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo tu.”
48 pe pano uYesu akam'bula umukijuuva jula akati, “upyanilue infivi saako”.
Baadaye akamwambia mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa”
49 neke vala vano vakikalile pa mesa palikimo nu mwnene vakatengula kukuposesania vavuo ku vavuo, “uju ghweveni kuhanga ipyanilua inyivi?
Wale waliokaa mezani pamoja naye wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani mpaka anasamehe dhambi?”
50 apuo uYesu akam'bula kange umukujuuva jula akati, “ulwitiko lwako lukupokile. ulutaghe nu lutengano”.
Na Yesu akamwambia mwanamke, “Imani yako imekuokoa. Enenda kwa amani”

< Luuka 7 >