< Luuka 4 >

1 uYesu ye amemilue nu uMhepo uMimike, akagomwike kuhuma kukikogha ikya Jolidani, na Mhepo akamulongosia ku lihaka
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 ku fighono fijigho fine, ukuo akagheluagha nu Setano. un'siki ughua nakalile kyokyoni, nu vusililo vwa n'siki ughuo injala jikatengula.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 uSetano akam'bula akati,” ndeve uve uli mwana ghwa Nguluve, livule ilivue ili live nkate”.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 uYesu akamwamula akati, “jilembilue; “umuunhu naiva nu vwumi kulia un'kate ghwene.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 pe pano uSetano akamulongosia kukyanya kuvusililo vwa kidunda, na kukunsona uvutwa vwoni vwa iisi ku n'siki n'debe.
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 uSetano akambula akati.” nikupela uvutavulilwa vwa vutwa vwoni palikimo nu vunofu vwake”. niwesia kuvomba ndikio ulwakuva fyoni fitavulilwa kulyune, neke une nikumpela ghwoghwoni juno nighanile kukumpela.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 pe lino, ndeve ungafughame na kukunyimika, ifinu ifi fyooni fiiva fyako”.
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 neke uYesu akamwamula akati, “jilembilue kuuti, umwimikaghe uMutwa uNguluve ghwako, kange um'bombelaghe umwene mwene”.
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 pambele uSetano akamulongosia uYesu kuhanga ku Yelusalemu na kukum'bika ulubale ulwa pakyanya fiijo pa nyumba inyimike ija kufunyila na kukum'bula, “ndeve uve uli mwana ghwa Nguluve, ghujitaghe paasi kuhuma apa.
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 ulwakuva jilembilue, “ikuvalaghikisia avanyaMhola vaake vakusunge na kukulolela,
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 kange vikukutosia ku kyanya mu mavoko ghave neke kuuti, nungalemasiaghe amaghulu ghako mu livue.
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 uYesu akamwamula akati, “jijovilue, nungamughelaghe uMutwa Nguluve ghwako”.
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 uSetano ye amalile kukumughesia uYesu, akamuleka alutaghe kuhanga un'siki ughunge.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 pe pano uYesu akagomoka ku Galilaya ku ngufu sa Mhepo, ni mhola inofu sa mwene sikaluta na kupalasana mu fighavo iya vupipi fyoni.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 akavulanisie mu nyumba saave isa kufunyila na vooni vakamughinia.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 ikighono kimonga akalutile ku Nasaleti, umpulo ghuno akusungilue na kukulia. ndavule vulyale uvuatavike, akingila mu nyumba ija kufunyila. ikighono kya Sabati, akimile na kukwimba amalembe amimike.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 akapelua ikitabu kya m'bili Yesaya, pe akadindulila ikitabu na kulonda pano palembilue,
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 uMhepo ghwa Mutwa ali palikimo nune, ulwakuva akamakile amauta kudalikila iMola inou ku vakotofu anhumile kupulisia uvwavuke ku vano vali mundinde, nakukuvavomba vano naviloola vawesie kulola kange. kuvavika vwavuke vano vadidikilue,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 kukughupulisia u mwaka ghuno uMutwa ilivonesia ulusungu lwake.
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 pe baho akadinda ikitabu, akan'gomokesia umulongosi ghwa nyumba ja kukufinyila, akikala paasi. amaaso gha vaanhu vooni ghalyale pavulongolo ghikumulola umwene.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 akatengula pijova navo akati, “umusyughu ililembe ili lifikile mu mbughulutu sinu”.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 umuunhu ghweni pala akapulike kila kino akajovile uYesu, na vinga mu vanave vakadegha amasio gha vukoola ghano ghakahumagha mu mulomo ghwake. vakale viiti, “uju na ghwe n'swambe lwene ghwa Yosefu, na uluo?”
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 uYesu akavavula akati, “kyang'haani mulijova ulujovo ulu kulyune,” mughanga, ghusosie juve. kyokyoni kino kino ghwavombagha ku Kapelinaumu tupulike, vomba na pakikaja kyako”.
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 kange akati,” kyang'haani nikuvavula umue, nakwale um'bili juno vikumwitika ku isi jake”
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 neke nikuvavula umue ikyang'haani kuuti, kwevalyale avafwile vinga ku Silaeli mu n'siki ghwa Eliya pano kukyanya kukadindilue nakungavisaghe ni ula ku maka ghatatu na mesi ntanda, unsiki ghuno kulyane ni njala ing'ome mu isi jooni.
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 neke uEliya nakasung'ilue kwa muunhu ghweni, neke kwa mfwile jumo juno ikalagha ku Sarepapipi nu mpulo ghwa Sidoni.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 kangekulyale na vakoma mufighono fya m'bili Elisha Isilaeli neke nakwealyale nambe jumo mu vanave juno akasosilue, looli u Naamani umuunhu ghwa ku Silia.
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 avaanhu voni vano valyale mu nyumba ija kufunyila ye vapulike aghuo vakava ni ng'alasi.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 vakiima na kukumwumia kunji kulikaaja lyave, nakukumulongosia kuhanga kuvusililo vwa kidunda kya likaaja pano umpulo ghujengilue nkyanya jake,
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 neke vantaghe paasi. neke akakila vunono pakate pavo na kuluta.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 pambele akikagha ku Kapenaumu, mulikaaja ilya Galilaya. Isabati jimonga jilyale jivulanisia avaanhu mu nyumba ija kufunyila.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 vakadegha imbulanisio sake, ulwakuva akavulanisie kuvutavulua.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 lino ikighono ikio mun'kate mu nyumba ija kufunyila, kulyale nu muunhu juno alyale ni lipepo ililamafu, akakoola kyongo,
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 tuli ni kiki nuve? ghwe Yesu mu Nasaleti? ghwisile kukututipula? nikagula uve veve veni! uve veve mwimike ghwa Nguluve”
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 uYesu akalidalikila ilipepo akati,” jigha kimie, na uhume kwa muunhu uju!” ilipepo lila lyati lin'taghile umuunhu jula pasi pakate javo, likahuma kwa muunhu jula kisila kumulemasia.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 avaanhu vooni vakadegha na kughendelela kuku n'jovela ku ilio. vakatisagha,” ghe masio maki agha? akughadaga amapepo amalamafu ku vutavulua ni ngufu ghope ghivuka?
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 pe lino imhola inofu isa Yesu sikaghenda imbale sooni sino sisyunguta mukighavo ikio.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 uYesu akavuka mulikaaja ilio pe akingila ku nyumba ja Simoni. lino un'kwivw gha Simoni akale ivavua imungu kyongo, vakampelepesia uYesu ansosie.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 peeano uYesu akam'belelela akajidalikila imungu jila jikamulekesia, akima na kutengula kuvatengelela.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 ilijuva ye lisema, avaanhu voni valyale na vatamu avanga anmu sinosilipinga vakan'twalilagha uYesu. akavikagha amavoko pa kyanya pave, akavasosia voni.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 kange amapepo ghakavahuma, vinga vakalilagha ku lisio na kuuti, “uve veve mwana ghwa Nguluve”. uYesu alyaghadalikila amapepo ghaleke pivoja. ulwakuva vakakagwile kuuti, umwene alyale ghwe Kilisite.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 unsiki ghuno ye kukile, akaluta ulubale luno lusila vaanhu, ilipugha lya vaanhu valyale vikumulonda vakisa ku lubale luno pweakale umwene. vakaghela kukunsigha nangalutaghe kutali na vene.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 neke akavavula akati,” lunoghile kange kudalikila imhola inofu sa vutwa vwa Nguluve mu makaaja aghange aminga. ulyakuva uluo lwe lwene nikasungilue apa.
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 pe pano akaghendelela kudalikila mun'kate mu nyumba ijakufunyila ku vaYahudi voni.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luuka 4 >