< Luuka 1 >

1 kulyuve mwoghopua Tiofilo avaanhu vinga valembile imhola isa Yesu Kilisite ndavule silyavombike kulyusue.
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 valembile imhola isi ndavule tulyapangilue na vano valyalolile na maaso ghave, navano valyasipulisie kuhuma vuvutengulilo vwake.
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 ulwakuva nilondile vunono uvwakyang'haani vwa mhola sa Yesu vuhuma vuvutengulilo lino najune nivwene lunono kukulembela isi sooni muvutavike.
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 neke ulukagule ulwakyang'haani lwa mbombo sino ukavulanisivue.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 mu fighono fya Helode untwa ghwa Yudea, pwealyale untekesi jumonga juno alyale ikemelua Sakalia ughwa lukolo lwa Abia un'dala ghwake alyahumile muvaliive va Haluni, ni litavua lyake alyale ikemelua Elisabeti.
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 voni van valyale vagholofu pa maaso gha Nguluve amaghendele ghale ghasita kukuvapika mundaghilo sooni munjovele ja Mutwa.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 neke navalyale nu mwana ulwakuva uElisabeti alyale mughumba na kukavalilo akuo voni vale vaghogholofijo.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 lino lulyahumile kuuti uSakalia alyale nu Mhepo umwimike kuvutavike vwa Nguluve. akalutile nuvutavike vwa vutekesi kuhumila mu vutavike vwa ludimo lwake.
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 kwevulyale uvutavike uvwa kuvomba mu nyumba ja Nguluve veni umuunhu untekesi, veni idalikila akasalulua ikipugha akingila mu nhumba ja Mutwa akanyanya uvufumba.
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 ilipugha lyoni lya vaanhu vakava vikufunya kunji ye vinyanya uvusumba.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 unyaMhola ghwa Mutwa akamwumila na kukwiima ulubale lwa luvoko lwa ndia kufitekelelo kuno vinyanyila uvusumba.
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 uSakalia akoghopa ye alwaghile ulutetemo lulyamughwila.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 neke unyaMhola akam'bula kuuti, ulekaghe pikwoghopa Sakalia ulwakuva ulufunyo lwako lupulikike. undala ghwako uElisabeti ikukuholela umwana ilitavua lyake ghukun'kemela Yohani.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 ghuliva nu lukelo na kuhovoka, na vinga vikuhovokela kuholua kwa mwene.
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 ulwakuva iliva nu vuvaha kuhuma kwa Mutwa ujuo nanganyisaghe nambe kimonga kino kighasia. looli ingufu sa Mhepo umwimike siiva nu mwene kuhuma pano ali mulileme lwa ng'iina.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 na vaanhu vinga ava Silaeli ilikuvagomosiagha kwa Nguluve uMutwa ghwave.
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 ujuo ilikumulongolela uMutwa mu ngufu nu mwojo ndavule alyale uEliya kusambania mu ngufu sa Mhepo uMwimike neve vano navikumwoghopa vighendagha muluhala lwa vano valweli. ikuvavombela ndiki kukuvavika kwa Mutwa avaanhu vano vaghelanisivue vwimila jake.
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 uSakalia akam'bula unyaMhola, “niwesia ndani kukagula ili? ulwakuva une nili nsehe nu n'dala ghwango na maka ghake ghali minga kyongo”.
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 unyaMhola akamwamula na kumb'ula, une nene Gabilieli, nejuno nikwima pavulongolo pa Nguluve. nisung'ilue kukuvuula, kukuletela iMhola inofu iji.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 kange lolagha, nungajove kinu ghuva kimie nungawesie kujova kuhanga ikighono kila pano isi siva sihumile. ulu lwe ulwakuva ukakunilue kukwitika amasio ghango ghano mu nsiki ghiva ghavombike.
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 lino avaanhu valyale vikumughula uSakalia. valyadeghile kuuti alyale itumila unsiki mwinga ku nyumba inyimike ja kufunyila.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 neke ye ahumile kunji, akakunilue kujova navo. pe aveene vakakagula kuuti, luvonike lumonga mu nyuma inyimike neke umwene akava ihufia lumonga na mavoko. akajigha kinunu.
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 ye fisilile ifighono fyakuvomba imbombo jakilekesi ayavukile kugomoka kunyumba jake.
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 pambele uSakalia akavuja kukaja kuhuma ku mbombo sake sakitekesi un'dala ghwake akava n'kunue, akifisa amesi ghahaano akajova.
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 “ulwakuva lwe luno uMutwa ambombile une ye andolile kulughano lwoni kukumbusikisia isoni pa maaso gha vaanhu”
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 ye ghufikile umwesi ghwa n'tanda pavukunue vwa Elisabeti uNguluve akatuma unyaMhola uGabilieli kuluta mu iisi ja Galilaya ilitavua ilinge Nasaleti,
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 kwa mhinja juno akatambulwagha Maliya. kwa mhinja juno alyatunilue nu mughosi ilitavua lyake ghwe Yosefu. umuholua mukikolo kya Davidi nilitavua lya mhinja akakemeluagha ghwe Maliya.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 unyaMhola ye afikile akati, “nikukuhungila uve ghwe juno usungukilue nu Mutwa, uMutwa alinuve;
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 amasio ghanyaMhola ghaka mangajisia kyongo mu mwojo ghwake na alyaghamanyile kiki unyaMhola ihungila hungila iji kidegho.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 unyaMhola akam'bula “nungoghopaghe Maliya ulwakuva uNguluve akusungukile.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 lolagha ghuva nu vukunue, ghupapagha umwana neke ghukun'kemelagha ilitavua ghwe Yesu.
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 iliva m'baha ikemeluagha mwana ghwa juno alikukyanya kyongo, uMutwa uNguluve neke ikumpelagha ikitengo kya vutwa kya Davidi uvuse.
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 itemagha uvutwa mu lukolo lwa Yakovo uvusila nakusila lusiku. (aiōn g165)
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
34 uMaliya akam'bula unyaMhola ili, iva ndani ulwakuva une nanighelile kuvwafuka nu mughosi ghwoghwoni?
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 unyamhola akamwamula akam'bula “uMhepo uMwimike ikwisa kulyuve. ni ngufu sa juno alikukyanya kyongo sikwisa kulyuve. pe lino umwimike juno iholua ikemeluagha mwana ghwa Nguluve.
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 lolagha ulukololuo uElisabeti alinuukunue vwa mwana mufighono fyake fya vughogholo, ughu ghwe mwesi ghwa n'tanda juno valyatile mughumba.
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 ulwakuva kwa Nguluve nakwekili kino kimuulemile”
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 uMaliya akajova akati, une nilim'baanda ghwa Mutwa neke luuleke luve luve kulyune ndavule ujovile” pe pano unyaMhola akavuka iluta.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 ye fikikile ifighono nde filingi uMaliya avuka ng'haning'habi na kuluta ku iisi jimonga jino jale nyafidunda, ija Yudea.
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 ukuo akingila mu nyumba ija Sakalia na kumwungila uElisabeti,
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 lino pe lulyahumile kuuti,” uElisabeti ye apulike uluhungilo lwa Maliya. umwana mu lileme akaomoka tomoka, neke uElisabeti ingufu isa Mhepo uMwimike sikamwisila.
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 pe akatengula pijova kungufu akati, “ufunyilue uve mukighavo kya vakijuuva najumwana juno alimulileme lyako afunyilue.
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 neke lulindani kulyune ungiina ghwa Mutwa lunoghile pikwisa kulyune?
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 ulwakuva lolagha ye lupulikike mu mbughulutu sango ilisio lya kuhungila kulyuve umwana mulileme lyango atomwike nu lukelo.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 neke afunyilue umukijuva jula juno alyitike kuuti vulyahumila uvya kyang'haani vwa sino alyavulilue kuhuma kwa Mutwa”.
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 uMaliya akati, inimbula jango jikunfunya uMutwa,
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 naghumwojo ghwango ghuvovwike mwa Nguluve umpoki ghwango.
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 ulwakuva avulolile uvukotofu vwa m'banda ghwake umhinja. lolagha kuhuma mu fisina fyoni vikughonelagha nilifunyua.
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 ulwakuva umwene unya sooni avombile sino mbaha kylyune. ni litavua lyake ilyimike.
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 uvukola vwake kuhuma ikisina ni kisina ku vano vikumwopa umwene.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 avonisie ingufu mu luvoko lyake avapalanisie vala vano vakighiniagha mu masaghe gha mooja ghave.
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 avisisie paasi avana va vatwa kuhuma mufitengo fyave ifya vutwa na kukuvatosia kukyanya vano vakotofu.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 alyavapelile avanya njala ifinu ifi nono looli avamofu avadagile na mavoko gheene.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 ahumisie uvutangilisi kwa Isilaeli um'bombi ghake, neke akumuke kuvonesia uvuhugu.
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 (ndavule alyajovile kuvanhaata vitu) kwa Abulahamu ni fisina fyake kuvusila na kusila” (aiōn g165)
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
56 uMalia alikalile nu Elisabeti hwene mesi ghatatu pepano akagomoka ku nyumba ja mwene.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 lino unsiki ghulyafikile ughwa Elisabeti kupaapa umwana un'dimi.
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 avabading'ani vake na vanyalukolo vake valyapulike ndavule uMutwa atupelanisie mu vuhugu vwake, kange vakahovoka palikimo nu mwene.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 lino kilyahumile ikighono kya lekela kwoni valisile kukivungo najumwana lulyanoghile vampele ilitavua lyake ghwe Sakalia kulwiho lwa vise.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 looli ung'ina akamula akati, “ndali” ikemelua ghwe Yohani”
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 vakam'bula napwale nambe jumo mulukolo juno itambulua ku litavua ili”
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 pe vakam'bombela ikimanyilo uvise kuuti, umwene iti ilitavua akemelue veni.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 uvise akalonda ikisegho akalemba “ilitavua ghwe Yohani” voni vakadegha ku ili
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 ku kenyemukila umulomo ghake ghukadinduka nu lumili lwake lukava vuleka akajova na kukumughinia uNguluve
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 uludwesi lukavisila voni vano valikalile pipi navoimbombo isio sikakwilana mu iisi jooni ja fidunda fya Yudea,
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 na voni vano valyaghapulike vakaghagadilila mu mwoojo ghave, vakati umwana uju ghwa ndani ndani?” ulwakuva uluvoko lwa Mutwa lulyale palikimo naghwo.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 ivise ghwa Sakalia akapeluula ingufu nu Mhepo uMwimike akatengula kuhumia uvuvili akatisagha,
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 aghinwaghe uMutwa, uNguluve ghwa Isilaeli, ulwakuva atangile kange na kukuvavanga avaanhu vake.
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 atupelile uvupoki kuhuma mu nyumba ja nyambombo ghwake u Davidi, kuhuma mukikolo kya m'bombi ghwake uDavidi.
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 ndavule alyajovile mumulomo ghwa vavili vake vano kwevalyale kuhuma kuvukuulu. (aiōn g165)
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
71 alatupoka kuhuma kuvalugu viitu na kuhuma mumavoko ghavaanhu vooni vano vikutukalalila.
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 alavomba ndiki kuvonesia ulusungu kuvanhaata vitu na kukumbuka ululaghilo lwake ulwimike.
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 ulujigho luno alayjovile kwa Abulahamu unhaata ghwitu.
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 alyajighile na kunkangasia kuuti lunoghile pikum'bombela umwene kisila vwoghofi pano tupokilue pihuma mumavoko ghavalugu viitu.
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 muvwimike na muvagholofu uvwakyang'haani pa maaso ghake ni fighono fyake fyoni.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 Ena, najuve mwana ghukemeluagha uli mb'ili ghw ajuno ali kukyanya fiijo ulwakuva alyaghendelelagha ku maaso ghwa Mutwa kuuti ikuvavonesia isila. neke kukunosekesia isila avaanhu pano ikwisagha umwene.
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 kukuvavula avaanhu vake kuuti valapyanilwagha valavuvunagha uvupoki kusila kusila ja vupoki vwa nyfi saave.
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 ili lilyahumile ulwakuva ja lusungu lwa Nguluve ghwitu ulwakuva ilijuva kuhuma kukyanya likutwisila.
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 kukutumulikila ku vano vikalile mu ng'isi nu lumwighighi ghwa vafue alavomba ndiki kulongosia amaghulu ghitu kusila ja lutengano.”
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 lino umwana jula akakula na kuva nyangufu mwa Mhepo uMwimike. alikalile kulihaka kuhanga unsiki ghuno akavonekagha ku vaSilaeli.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.

< Luuka 1 >