< Yohani 4 >

1 Lino aVafalisayi vakapulika imhola sa Yesu kuuti ikwofugha na kuuva na vavulanisivua vinga kukila uYohana umwofughi,
Basi Yesu alipofahamu kuwa Mafarisayo wamesikia kuwa Yesu alikuwa anafuasa na kuwabatiza zaidi ya Yohana,
2 (neke uYesu jujuo naakava ikwofugha, looli avavulanisivua vaake ve vano valyale vikwofugha),
(ingawa Yesu mwenyewe alikuwa habatizi ila wanafunzi wake),
3 UYesu ye akagwile kuuti imhola saake sipulikiike, akavuuka mukighavo ikya Yudea akagomoka ku kighavo ikya Galilaya.
alitoka Judea na akaenda Galilaya.
4 Ye vigomoka ku Samalia lukavoneka kuuti kwevule uvufumbue uvwa kukilila mu kighavo ikya Samalia, pe vakakilila isila ijio.
Hivyo ilikuwa muhimu kupitia Samaria.
5 Pe vakafika mu likaaja ilya Sikali lino lyale mukighavo ikya Samalia, ilikaaja ilio lilyale piipi nu mughunda ghuno u Yakobo alyampeliile umwanake u Yosefu.
Na akafika kwenye mji wa Samaria, unaoitwa Sikari, karibu na eneo ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu.
6 Apuo pwekilyale ikitiimu kya Yakobo. UYesu akikala palubale pa kitiimu ikio kuuti apuume, ulwakuva alyakatiile nu lughendo. Unsiki ughuo ghwale ghwa kavalilo aka ntanda pamwisi.
Na kisima cha Yakobo kilikuwa hapo. Yesu alikuwa amechoka kwa ajili ya safari na akakaa karibu na kisima. Ilikuwa muda wa mchana.
7 Pe akiisa umukijuuva jumomonga uNsamalia kunegha amalenga pa kitimu kila, uYesu akam'buula akati, “Nisuuma amalenga ninyue.”
Mwanamke Msamaria alikuja kuteka maji, na Yesu akamwambia, “Nipe maji ninywe.”
8 Ulwakuva avavulanisivu vaake vakava valutile kughula ikyakulia.
Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wameenda zao mjini kununua chakula.
9 Umukijuuva jula uNsamalia akamwamula akati, “Uve uli Muyahudi, une nilinsamalia, lwandaani ghusuuma amalenga kulyune?” Alyajovile enendiki ulwakuva aVayahudi navalyale nu vuhangilanisi na Vasamalia.
Yule mwanamke akamwambia, “Inakuaje wewe Myahudi, kuniomba mimi mwanamke Msamaria, kitu cha kunywa?” Kwa sababu Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.
10 UYesu akamwamula akati, “Ghwale ukagulaghe sino uNguluve ilonda kukukupeela na kuuti nene veeni ne juno nikukusuuma amalenga, ngale usumile une, une naale nikukupeela amalenga ghano ghikuvapeela avaanhu uvwumi.”
Yesu akamjibu, “Kama ungelijua karama ya Mungu, na yule anayekuambia 'Nipe maji, ' ungelimwomba, na angelikupa maji ya uzima.”
11 Umukijuuva jula akamwamula uYesu akati, “Ghwe Ntwa uve nuli ni ndoovo ija kuneghela, kyope ikitiimu kitali. Lino ukughaagha kuughi amalenga gha vwumi?
Mwanamke akajibu, “Bwana hauna ndoo ya kuchotea, na kisima ni kirefu. Utayapata wapi Maji ya Uzima?
12 Unkuulu ghwitu uYakobo alyatupeliile ikitiimu iki, umwene na vanaake vanywile amalenga agha kitiimu ulim'baha kukila uYakovo?”
Je wewe ni mkuu, kuliko baba yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki, na yeye mwenyewe na watoto wake pamoja na mifugo yake wakanywa maji ya kisima hiki?”
13 UYesu akamwamula akati, “Umuunhu ghweni juno inyua amalenga agha kitimu iki, ikwumilua kange,
Yesu akajibu, “Yeyote anywae maji haya atapata kiu tena,
14 neke umuunhu juno inyua amalenga ghano nikumpeela ghiiva nkate mwa mwene, kiiva kindwivu kya malenga ghikumpeelagha uvwumi vuno navusila lusiku.” (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini yeye atakaye kunywa maji nitakayompa hatapata kiu tena. Badala yake maji nitakayompa yatakuwa chemchemi inayobubujika hata milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 Pe umukijuuva jula akansuuma uYesu akati, “Ghwe Ntwa, umeele amalenga aghuo, nileke pikwumilua, kange nileke pikwisa apa kunegha amalenga.”
Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, nayaomba maji hayo ili nisipate kiu, na nisihangaike kuja hapa kuchota maji.”
16 UYesu akambuula akati, “Lutagha, unkemeele umughosi ghwako, ghwise naghwo apa.”
Yesu akamwambia, “Nenda kamwite mumeo, kisha urudi.”
17 Umukijuuva jula akamwamula akati, “Une nili nsila mughosi.” UYesu akambuula akati, “Ujovile seseene kuuti, 'ulinsila mughosi,'
Mwanamke akamwambia, “Sina mume.” Yesu akajibu, “Umesema vyema, 'Sina mume;'
18 Ulwakuva ulyatolilue na vaghosi vahano, ghwope juno ghukukala naghwo lino, naghwako. Mu ulu ujovile isa kyang'haani!”
kwa maana umekuwa na wanaume watano, na mmoja ambaye unaye sasa sio mume wako. Katika hili umesema kweli!”
19 Umukijuuva jula akamwamula akati, “Ghwe Ntwa, nivona uve uli m'bili.
Mwanamke akamwambia, “Bwana naona yakuwa wewe ni nabii.
20 Avakuulu viitu valyale vikumwimika uNguluve pa kidunda iki, neke umue mwiti ku Yelusalemu kwe kuno kunoghiile kukumwimika uNguluve.”
Baba zetu waliabudu katika mlima huu. Lakini ninyi mwasema ya kuwa Yerusalemu ndiyo sehemu ambayo watu wanapaswa kuabudu.”
21 UYesu akam'buula akati, “Ghwe mukijuva uve, ghwitikaghe sino nijova, ghukwisa unsiki ghuno namukumwimikagha uNguluve uNaata pa kidunda iki nambe ku Yelusalemu.
Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu au Yerusalemu.
22 Umue mu kumwimika uNguluve juno namunkagwile, neke usue tukumwimika uNguluve juno tunkagwile, ulwakuva uNguluve ikuvapokea avaanhu kukilila ku Vayahudi.”
Ninyi watu mwaabudu kile msichokijua, lakini sisi twaabudu tunachokijua, kwa sababu wokovu watoka kwa Wayahudi.”
23 Lino unsiki ghukwisa, kange ghufikile, pano avaanhu vano vikumwitika uNguluve uNhaata mu vwakyanghaani, vikumwimikagha mutwa kulongosivua nu mhepo ghwake na vule vulungika uvwakyang'haani vwake.
Hatahivyo, wakati unakuja, na sasa upo hapa, wakati waabuduo kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli, kwa sababu Baba anawatafuta watu wa namna hiyo kuwa watu wake wanao mwabudu.
24 UNguluve ghwe mhepo, avaanhu vano vikumwimika umwene, vanoghiile kukumwimika mu ngufu isa mhepo ghwake na mu vwakyang'haani.”
Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu kwa roho na kweli.”
25 Umulijuuva jula akamwamula akati, “Nikagwile kuuti uMesiya, (juno ghwe Kilisite). Ikwisa iliva isile, ujuo ilikutuvuula sooni.
Mwanamke akamwambia, “Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote.”
26 UYesu akam'buula akati, “Une ne juno nijova nuuve, neene Mesiya.”
Yesu akamwambia, “Mimi unayesema nami ndiye.”
27 Unsiki ughuo avavulanisivua vaake vakagomoka, vakadegha kyongo kuvona uYesu ijova nu mukijuuva, neke nakwealyale juno alyaghelile kukumposia kuuti, “Ghulonda kiki?” nambe kuuti “Kiki ghujova naghwo?”
Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, “Unataka nini?” au “Kwa nini unazungumza naye?”
28 Umukijuuva jula akaluleka pala pala ulusaaji lwake ulwa malenga akaluta kukikaaja, akavavuula, avanu akati,
Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu,
29 “Mwise mulole umuunhu juno ambulile sooni sino nivombile. Asi umuunhu ujuo ndepoonu iiva ghwe Kilisite?”
“Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?”
30 Avaanu yepulike isio vakaluta kuno kwale uYesu.
Wakatoka mjini wakaja kwake.
31 Unsiki ughwa pamwisi avavulanisivua vaake vakam'buula uYesu vakati, “Ghwe m'bulanisi ulie ikyakulia.”
Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, “Rabi kula chakula.”
32 Umwene akavavuula akati, “Une nili ni kyakulia kino umue namukikagwile.”
lakini yeye aliwambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 Avavulanisivua vaake vakatengula kuposania viiti, 'Asi, kuli muunhu isile vwa Nhaata, juno kukumuletela ikyakulia?”
Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula,”Je walileta?”
34 UYesu akavamula akati, “Ikyakulia kyango une, kwe kuvomba isa vughane vwa Nhaata juno asung'hulile nimale imbombo jaake.
Yesu akawambia, “Chakula changu ni kufanya mapenzi yake yeye aliyenituma na kutimiza kazi yake.
35 Asi, namwamujova kuuti, “Gasighile ameesi ghahaano kupeta?” Neke une nikuvavuula niiti, lola amaghunda vule ghalivuo pano lukwiline kupeta!
Je, hamsemi, 'Bado miezi mitano na mavuno yatakuwa tayari?' Ninawambieni tazameni mashamba yalivyo tayari kwa mavuno!
36 Ghwope juno ipeta ikwupila uluhombo lwake, umpeto ve vaanhu vano vikwupila uvwumi uvwa kuvusila kusila, apuo juno ivyala na juno ipeta vooni vivisagha nu lukeelo palikimo. (aiōnios g166)
Yeye avunaye hupokea mishahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili kwamba yeye apandaye naye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 Kwelule ulujovo luno luuti, 'Jumonga ivyala ujunge ipeta ulujovo uluo lwa kyang'haani.'
Kwa kuwa msemo huu ni wa kweli, 'Mmoja apanda na mwingine avuna.'
38 Une nivasunghile umue kupeta fino namuhangajikile, Avange vakavombile imbombo inalamu, umue mupeta vwimila imbombo jaave.”
Niliwatuma kuvuna ambacho hamkukihangaikia, Wengine wamefanya kazi na ninyi mmeingia katika furaha ya kazi yao.”
39 AVasamalia vinga ava mulikaaja lila ilya sikali vakamwitika uYesu ulwakuva valyapuliike sino alyajovile umukijuuva jula kuuti, “Umuunhu ujuo ambulile sooni sino nivombile.”
Wasamaria wengi katika mji ule walimwani kwa sababu ya taarifa ya yule mwanamke aliyekuwa akishuhudia, “Aliyeniambia mambo yote niliyoyafanya.”
40 Pe aVasamalia vala vakafika pano pwale uYesu vakampelepesia kuuti ikale palikimo na veene, pe akikala mu likaaja ilio ifighono fivili.
Hivyo Wasamaria walipokuja walimsihi akae pamoja nao na akakaa kwao kwa siku mbili.
41 Avaanhu vinga fiijo vakamwitika uYesu vwimila ilisio lyake.
Na wengi zaidi wakamwamini kwa sababu ya neno lake.
42 Vakam'buula umukijuva jula vakati, “Lino nakwekuti tumwitiike umuunhu uju vwimila si sino utuvulile uve, looli tumwitike ulwakuva tupulike sino ajovile, kange tukagwile kuuti kyang'haani umuunhu uju ghwe mpoki ghwa vaanhu vooni.”
Wakamwambia yule mwanamke, “Tunaamini sio tu kwa maneno yako, kwa sababu sisi wenyewe tumesikia, na sasa twafahamu kuwa hakika yeye ni mwokozi wa ulimwengu.”
43 Ifighono fivili ye fikilile, akavuuka kiluta ku Galilaya.
Baada ya siku hizo mbili, akaondoka na kuelekea Galilaya.
44 UYesu alyoliike kuuti um'bili naikwoghopua na vaanhu ava mu kikaaja kyake.
Kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ametangaza kuwa nabii hana heshima katika nchi yake mwenyewe.
45 Avaanhu ava ku Galilaya valyamwupiile uYesu, ulwakuva valyasivwene sooni sino alyavombile ku kyimike ikya Pasaka ku Yelusalemu, kukyimike ukuo voope kwevalyale.
Alipokuja kutoka Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha. Walikuwa wameona mambo yote aliyoyafanya Yerusalemu kwenye sikukuu, kwa sababu na wao pia walikuwa wamehudhuria kwenye sikukuu.
46 UYesu akaluta kange ku kikaaja ikya Kana mu kighavo ikya Galilaya. Kukikaaja ikio kwe kuno alyahambwisie amalenga kuuva luhuuje kwe alyale umulongosi jumonga ughwa selikali ku Kapelnaumu, umulongosi ujuo umwanaake alyale ntamu.
Alikuja tena Kana ya Galilaya huko alikoyabadilisha maji kuwa divai. Palikuwa na ofisa ambaye mwana wake alikuwa ni mgonjwa huko Kapernaumu.
47 Ye apulike kuuti uYesu isile kange ku Galilaya kuhuma ku Yudea akaluta kukumpelepesia uYesu kuuti alute ku Kapelenaumu, ansosi umwanaake ulwakuva umwanaake ujuo ghulyale ghukova.
Aliposikia kuwa Yesu alitoka Judea na kwenda Galilaya, alienda kwa Yesu na kumsihi atelemke amponye mwanawe, ambaye alikuwa karibu kufa.
48 UYesu akamwamula akati, “Umue namunganyitike kisila kufyagha ifivalilo ni fidegho.
Ndipo Yesu akamwambia, “Ninyi msipoona ishara na maajabu hamwezi kuamini.
49 Umulongosi jula akamwamula akati, “Ghwe Mutwa nikukusuuma luvuke unsosie umwanango pano akyale pifua.”
Kiongozi akasema, “Bwana shuka chini kabla mwanangu hajafa.”
50 UYesu akam'buula akati, “Vujagha, umwanaako asokile.” Akitika amasio gha Yesu akavuuka ivuja.
Yesu akamwambia, “Nenda mwanao ni mzima.” Yule mtu akaamini neno alilolisema Yesu na akaenda zake.
51 Umulongosi jula ye ali mu sila ivuja, akatang'hana na vavombi vaake vakambuula vakati umwanaako asokile nkafu.
Alipokuwa akishuka, watumishi wake walimpokea na kumwambia mwana wake alikuwa mzima.
52 Pe akavaposia akati. Asokile unsiki ghuliku, “Aveene vakamwamula vakati, asooka pamihe pamwisi akavalilo aka lekela lubale.”
Hivyo akawauliza ni muda gani alipata nafuu. Wakajibu, “Jana muda wa saa saba homa ilipomwacha.”
53 Uviise ghwa mwana jula akakagula kuuti asooka unsiki ghula ghuno uYesu ajova kuuti, “Umwanaako asookile.” Pe umwene palikimo na vaanhu vooni ava munyumba jaake vakamwitika uYesu.
Ndipo baba yake akatambua kuwa ni muda ule ule Yesu aliosema, “Mwana wako ni mzima.” Hivyo yeye na familia yake wakaamini.
54 Ikidegho ikio kyale kivalilo kya vuvili kino alyavombile uYesu ku Galilaya ye ahumile ku Yudea.
Hii ilikuwa ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipotoka Yudea kwenda Galilaya.

< Yohani 4 >