< Yohani 16 >

1 Nivavulile isio kuuti namungalulekaghe ulwitiko lwinu.
Nimewaambia mambo haya ili msiweze kukwazwa.
2 Avaanhu vikuvadagha mu masinagogi ghaave, kange ghukwisa unsiki pano umuunhu angavabude umue itisagha ikum'bombela uNguluve.
Watawatoa nje ya masinagogi; hakika saa inakuja ambayo kila atakayewaua atafikiri kuwa anafanya kazi njema kwa ajili ya Mungu.
3 Vilikuvavombela isio, ulwakuva navankagwile uNhaata, kange navang'hagwile une.
Watawatendea mambo haya kwa sababu hawamfahamu Baba wala hawanifahamu mimi.
4 Nivavulile isi kuuti unsiki ughuo ghungafike, mukumbukaghe kuuti nilyavavulile. Nanilyavavulile isi ulutasi, ulwakuva nilyale palikimo numue. Sikuwaambia kuhusu mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
Nimewaambia mambo haya ili kwamba wakati ukifika wa haya kutokea, mnaweza kuyakumbuka na jinsi nilivyowaambia muweze wao. Sikuwaambia kuhusu mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 Poope nambe lino niluta kwa juno alyasung'hile une kulyumue, neke napwale nambe jumo pakate palyumue juno ikumhosia kuuti, “Ghuluta kughi?”
Japokuwa, sasa naenda kwa yule aliyenituma; lakini hakuna kati yenu anayeniuliza, “Unaenda wapi?”
6 Neke ulwakuva nivavulile isio, musukunile fiijo.
Kwa sababu nimesema maneno haya kwenu, huzuni imejaa mioyoni mwenu.
7 Nikavavuula isa kyang'haani kuuti, luuva lunofu kulyumue une nivuuke, ulwakuva ningaleke pivuuka uNtangili naangise. Looli ningalute nikunsuung'ha kulyumue.
Hata hivyo, nawaambia ukweli: ni vyema kwenu nikiondoka; kwa maana nisipoondoka, mfariji hatakuja kwen; lakini nikienda ntamtuma kwenu.
8 Untangili ujuo angiise, ikuvahufyagha avaanhu ava mu iisi uvuhosi vwave, uvugholofu nu vuhighi vwa Nguluve.
Akija, huyo mfariji ataubitisha ulimwengu kuhusiana na dhambi, kuhusiana na haki na kuhusiana na hukumu.
9 Ihufiagha uvuhosi vwave, ulwakuva navikunyitika une.
Kuhusiana na dhambi, kwa sababu hawakuniamini mimi,
10 Ikuvahufiagha uvugholofu vwango ulwakuva niluta kwa Nhaata, namulikunyaagha kange.
kuhusiana na haki, kwa sababu naenda kwa baba, na hamtaniona tena;
11 Ikuvahufyagha uvuhighi vwa Nguluve ulwakuva uNguluve amalile kukumhigha uSetano umbaha ghwa iisi iji.
na kuhusiana na hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amehukumiwa.
12 Napano nijighe naso nyinga isa kuvavuula, neke nanikuvavuula, ulwakuva unsiki ughu namungasitang'hanie.
Ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamtayaelewa sasa.
13 Looli uMhepo ughwa kyang'haani ujuo angiise, ikuvalongosiagha kuvingilila uvwakyang'haani; ulwakuva naijovagha muvuta vulilua vwake jujuo, looli ijovagha sino apuliike na kukuvavuula sino sikwisa.
Lakini, yeye, Roho wa kweli, akija, atawaongoza katika kweli yote; kwa kuwa hataongea kwa ajili yake mwenyewe; lakini yoyote atakayoyasikia, atayasema mambo hayo; na atayadhihirisha kwenu mambo yatakayokuja.
14 Umwene ihufiagha uvuvaha vwango, ulwakuva ikuvavulagha sino upiile kulyune.
Yeye atanitukuza mimi, kwa sababu atayachukua mambo yangu na atayatangaza kwenu.
15 Fyoni fino alinafyo uNhaata, fyango, fye nambe nivavulile kuuti, uMhepo ujuo ikuvavulagha sino upiile kuhuma kulyune.
Vitu vyote alivyonavyo Baba ni vyangu; kwa hiyo, nimesema kwamba Roho atachukua mambo yangu na atayadhihirisha kwenu.
16 Ghusighiile unsiki n'debe namukunyaagha kange, neke pambele unsiki n'debe kange mukunyaagha.
Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi tena, mtaniona.”
17 Vamo mu vavulanisivua vaake vakava viposania viiti, “Asi, kwe kuti kiki pano iiti, 'Ghusighile nsiki n'debe namukunyaagha, neke pambele unsiki n'debe mukunyaagha? Na pano iiti ulwakuva niluta kwa Nhaata?”
Baadhi ya wanafunzi wake wakaambizana, “Ni nini anachotuambia, “muda mfupi, na hamtaniona tena,' na, kisha, mda mfupi mtaniona,' na, 'kwa sababu naenda kwa Baba?”
18 Vakava viposania viiti, “Kwekuti kiki pano iiti, “Ghusighile unsiki n'debe?' Natusitang'hinie isi sino ijova.”
Kwa hiyo wakasema, “Ni kitu gani anachosema, 'Bado mda mfupi'? Hatujui asemavyo.”
19 UYesu akakagula kuuti vilonda kukumposia sino ajovile, pe akati, “Muposania sino nijovile kuuti, “Ghusighile unsiki n'debe mukunyaagha, neke pambele unsiki n'debe mukunyaagha'?
Yesu aliona kuwa walitamani kumuuliza, naye akawaambia, “Mnajiuliza wenyewe kuhusu hili, nilivyosema, 'Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi mtaniona'?
20 Kyang'haani nikuvavuula, umue mulilila na kusukunala neke avaanhu ava mu iisi vilihovoka. Mulisukunala, neke pambele ulisukunalo lwinu luluhambuka lukeelo.
Amin, amin, nawaambia, mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utashangilia, mtakuwa na huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 Umukijuuva pano ipaapa, iiva nu lusukunalo ulwakuva ali nu vuvafi. Neke angapaape, maikumbuka kange uvu vafi uvuo, ulwakuva iiva nu lukeelo ulwa kuuva nu mwana.
Mwanamke anakuwa na huzuni wakati anapokuwa na uchungu kwa sababu wakati wa kujifungua umefika; lakini anapojifungua mtoto, hakumbuki tena maumivu kwa sababu ya furaha yake kwamba mtoto amezaliwa duniani.
22 Najumue muli nu lusukunalo lino, neke nilikwisa kange kulyumue neke muliiva nu lukeelo. Nakwale juno anoghiile kuvusia ulukeelo uluo kulyumue.
Ninyi pia mna huzuni sasa, lakini nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi na hakuna atakayeweza kuiondoa furaha yenu.
23 Kange unsiki ughuo ghungafike, namulikumhosia kimonga. Kyanghaani nikuvavuula, mungansuume kimonga uNhaata mu litavua lyango, ikuvapeela.
Siku hiyo hamtaniuliza maswali. Amin, Amin, nawaambia, Mkiomba lolote kwa Baba, atawapa kwa jina langu.
24 Nambe lino namunsumile kimonga mu litavua lyango. Musumaghe mupelua, neke ulukeelo lwinu lukwilane.
Mpaka sasa hamjaomba lolote kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapokea ili kwamba furaha yenu ikamilike.
25 Nijovile isio numue mufihwanikisio, neke ghukwisa unsiki ghuno nanijovagha numue kange mu fihwanikisio. Looli nijovagha numue pa vuvalafu imhola sa Nhaata.
Nimezungumza na ninyi kwa lugha isiyoeleweka, lakini saa inakuja ambapo sitazungumza kwa lugha isiyoeleweka lakini badala yake nitawaambia waziwazi kuhusu Baba.
26 Unsiki ughuo musumagha mu litavua lyango, naniiti une nikuvasumilagha kwa Nhaata, jeeje!
Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitaomba kwa Baba kwa ajili yenu;
27 Unaata jujuo avaghanile umue ulwakuva munganile une, kange mukwitika kuuti nihumile kwa Nguluve.
Kwa kuwa Baba mwenyewe anawapenda kwa sababu mmenipenda mimi na kwa sababu mmeniamini kuwa nimetoka kwa Baba.
28 Nilyahumile kwa Nhaata, nikiisa mu iisi muno; kange nivuuka mu iisi muno, nigomoka kwa Nhaata.
Nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni; tena, naondoka ulimwenguni na ninaenda kwa Baba”.
29 Avavulanisiva vaake vakati, “Ulolile, lino ghujova pavuvalafu, naghujova mu fihwanikisio.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Unaona, sasa unaongea wazi wazi na hautumii mafumbo.
30 Lino, tukagwile kuuti uve usikagwile sooni, naghulonda umuunhu ghweni akuposiaghe lumonga. Mu uluo tukwitika kuuti ulyahumile kwa Nguluve.
Sasa, tunajua kwamba unajua mambo yote, na hauhitaji mtu yoyote akuulize maswali. Kwa sababu hii tunaamini kuwa unatoka kwa Mungu.
31 UYesu akavaposia akati, “Lino mukwitika?
Yesu akawajibu, “Sasa mmeamini?”
32 Lolagha, unsiki ghuli piipi, lweli kange seseene ghufikile, pano umue mupalasana nujunge iluta kwa mwene na kukundeka ne mwene. Neke une nanili ne mwene ulwakuva uNhaata ali palikimo nuune.
Tazama, saa inakuja, ndiyo na hakika imefika, ambapo mtatawanyika kila mmoja na kwa wa kwao mtaniacha mwenyewe. Lakini siko peke yangu kwa sababu Baba yupo nami.
33 Nikuvavuula isi kuuti muve nu lutengaano, ulwakuva muli nkate mulyune. Pa iisi apa muli ni mhumhuko, neke namungoghopaghe ulwakuva une nijilefisie iisi.”
Nawaambia mambo haya ili kwamba ndani yangu muwe na amani. Duniani mna matatizo, lakini jipeni moyo, nimeushinda ulimwengu.

< Yohani 16 >